[h=2]Mkuchika aiandikia NEC kuitisha uchaguzi wa Madiwani Arusha[/h]
NA JOHN NGUNGE
5th November 2011
B-pepe
Chapa
Maoni
Hatimaye Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, (Tamisemi),George Mkuchika
Hatimaye Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, (Tamisemi), ameandika barua rasmi kwa Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kumuagiza aitishe
uchaguzi kwa viti vitano vya madiwani wa Arusha ambao walifukuzwa na chama chao Agosti 6, mwaka huu.
Katibu wa Chadema Mkoa wa Arusha, Amani Golugwa, alisema jana kuwa amepokea nakala ya barua toka kwa Waziri Mkuchika iliyotumwa kwa Katibu Mkuu wa Chadema taifa, Dk. Wilbrod Slaa, ikimtaarifu kuwa ametambua kufukuzwa kwa madiwani hao.
Alisema barua hiyo ya Mkuchika ina mtaarifu Mwenyekiti wa NEC kwamba nafasi za viti vya udiwani katika kata tano za madiwani hao zipo wazi na anatakiwa kuitisha uchaguzi.
Nimetumiwa nakala ya barua ya Waziri Mkuchika toka kwa Katibu Mkuu Taifa wa Chadema ambayo nimeipata jana, barua hiyo iliandikwa Oktoba 6, mwaka huu, kwenda kwa Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi akitangaza kwamba kata za madiwani hao zipo wazi na atangaze tarehe ya uchaguzi, alisema. Baada ya kufukuzwa uanachama, madiwani hao walifungua kesi Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Arusha, wakipinga hatua iliyochukuliwa na Kamati Kuu ya Chadema iliyokutana katika Mkutano wa Dharura, mjini Dodoma, Agosti 6, mwaka huu, ya kuwafukuza uanachama.
Licha ya kufukuzwa kwao, madiwani hao bado walikuwa wakitambuliwa na serikali na kwa wakati mwingine walikuwa wakilipwa posho hadi pale mahakama ilipotupilia mbali kesi yao.
Madiwani waliofukuzwa na kata zao kwenye mabano ni Estominh Mallah,(Kimandolu), Charles Mpanda (Kaloleni), Ruben Ngowi (Themi), John Bayo(Elerai)na Rehema Mohammed (Viti Maalum).
CHANZO: NIPASHE
0 Maoni | Kuwa wa kwanza kutoa maoni
Inakuwaje NEC inapokea amri kutoka kwa serikali kwa ajili ya kuitisha uchaguzi ? shouldn't NEC be an independent organ from any govt. interference ? inakuwaje NEC imemtangaze mtu kuwa diwani lakini haina mamlaka ya kutangaza uwazi wa nafasi inapotokea ?? serikali ndio inatangaza kuwepo au kutokuwepo kwa uchaguzi shouldn't be the part of NEC responsibilities??? what will happen if the Govt. refuses to call for election for political reasons ?? NA JOHN NGUNGE
5th November 2011
B-pepe
Chapa
Maoni
Hatimaye Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, (Tamisemi),George Mkuchika
Hatimaye Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, (Tamisemi), ameandika barua rasmi kwa Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kumuagiza aitishe
uchaguzi kwa viti vitano vya madiwani wa Arusha ambao walifukuzwa na chama chao Agosti 6, mwaka huu.
Katibu wa Chadema Mkoa wa Arusha, Amani Golugwa, alisema jana kuwa amepokea nakala ya barua toka kwa Waziri Mkuchika iliyotumwa kwa Katibu Mkuu wa Chadema taifa, Dk. Wilbrod Slaa, ikimtaarifu kuwa ametambua kufukuzwa kwa madiwani hao.
Alisema barua hiyo ya Mkuchika ina mtaarifu Mwenyekiti wa NEC kwamba nafasi za viti vya udiwani katika kata tano za madiwani hao zipo wazi na anatakiwa kuitisha uchaguzi.
Nimetumiwa nakala ya barua ya Waziri Mkuchika toka kwa Katibu Mkuu Taifa wa Chadema ambayo nimeipata jana, barua hiyo iliandikwa Oktoba 6, mwaka huu, kwenda kwa Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi akitangaza kwamba kata za madiwani hao zipo wazi na atangaze tarehe ya uchaguzi, alisema. Baada ya kufukuzwa uanachama, madiwani hao walifungua kesi Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Arusha, wakipinga hatua iliyochukuliwa na Kamati Kuu ya Chadema iliyokutana katika Mkutano wa Dharura, mjini Dodoma, Agosti 6, mwaka huu, ya kuwafukuza uanachama.
Licha ya kufukuzwa kwao, madiwani hao bado walikuwa wakitambuliwa na serikali na kwa wakati mwingine walikuwa wakilipwa posho hadi pale mahakama ilipotupilia mbali kesi yao.
Madiwani waliofukuzwa na kata zao kwenye mabano ni Estominh Mallah,(Kimandolu), Charles Mpanda (Kaloleni), Ruben Ngowi (Themi), John Bayo(Elerai)na Rehema Mohammed (Viti Maalum).
CHANZO: NIPASHE
0 Maoni | Kuwa wa kwanza kutoa maoni
ingekuwaje endapo mkuchika mwenyewe angekuwa diwani and for some reason he is supposed to declare his position open against his will?? in my opinion NEC should have total authority to run the election without govt calling the shot. what is yours ??