sixlove
JF-Expert Member
- Dec 20, 2011
- 549
- 372
Habarini za maisha kwa ujumla. Hivi karibuni nilipokea ujumbe kutoka kwa mtu fulani akihitaji tuwe marafiki kupitia facebook, sikusita kumkubalia kwani ndivyo urafiki unavyoenea. Siku zikaendelea huku tukiendelea kuwasiliana kupitia e-mail, ndipo siku moja alinitumia email akidai yeye ni mkimbizi na sasa anaishi dakar- senegal kwenye kambi ya wakimbizi, hivyo basi anahitaji kupata partiner ili imsaidie kupata viza za kuja bongo: Kabla sijamjibu akatuma nyingine akidai marehemu baba yake aliweka kiasi fulani cha fedha kwenye akaunti yake kabla hajafa, hivyo aliniomba nimsaidie kufanya transaction kutoka kwenye hiyo benk kwenda kwenye akaunti yangu. Alinitumia anuani za benki kisha akanitaka niwasiliane nao ili wajue kuwa tupo serious na suala hilo. Nilifanya hivyo, kisha bank walitumia email wakitaka niwatumie taarifa zangu, zikiwemo anuani zangu,account no, pamoja na kitambulisho. Nikaingia mkenge nikatuma.
Kama ilivyo sema usikike, nikampa story msela wangu mmoja, si ndo akanifumbua macho. Akaniambia kuwa huyo mtu ni miongoni mwa watu wezi duniani wanaojulikana kama,,"scammers" hivyo niachane naye. Niliachana nae,
wanajamvi naomba mnisaidie, nitawaepuka vp watu hawa ukizingatia, wana tarifa zangu zote kikiwemo kitambulisho changu. Nifanye nini?
1.nifunge akaunti zangu, je itasaidia?
Ushauri wa kina unahitajika.....
Kama ilivyo sema usikike, nikampa story msela wangu mmoja, si ndo akanifumbua macho. Akaniambia kuwa huyo mtu ni miongoni mwa watu wezi duniani wanaojulikana kama,,"scammers" hivyo niachane naye. Niliachana nae,
wanajamvi naomba mnisaidie, nitawaepuka vp watu hawa ukizingatia, wana tarifa zangu zote kikiwemo kitambulisho changu. Nifanye nini?
1.nifunge akaunti zangu, je itasaidia?
Ushauri wa kina unahitajika.....