Housegirl kufanya kila kitu

Olumolongez

JF-Expert Member
Dec 19, 2015
818
294
Habarini za jioni wandugu. Kuna baadhi ya familia unakuta beki 3 anafanya kazi zote za ndani kwa 99.9% na unakuta Mama mwenye nyumba yupo, hatukatai kua kuna wamama wenye nyumba hua wanatoka asbh na kurudi jioni kama waume wao cha ajabu akifika nyumbani utamkuta yuko busy na simu na beki 3 ndiye anapanda na kushuka.Haya mazoea si mazuri ni sawa goalkeeper kuliacha goli wazi wakati mpira unaendelea yeye anaenda pembeni kupiga story.
 
Hao wanao mwachia beki Tatu kila kitu wamezidi loh mi hata msosi wa beki Tatu sili wao sijui wanawaamini vipi beki wenyewe washirikina, uelewa mdogo wachafu kwenye kupika wengine hutia had m.... In my life sipendi beki Tatu aisee sema MTU ukiwa na majukumu no way out ila sio kupika aiseee
 
Mimi wife kashaniambia yeye binafsi hahitaji beki tatu, familia ya watu wawili plus one child haimshindi kulea.
Nikasema asante Mungu, mimi niliona kama vile kazi zinamuwia nyingi akasema anazimudu bila shida.
Mkeo anafanya kazi?
 
Binafsi mi sina dada wa kazi mpk ss coz nimeolewa na sina mtt. Ila ukishapata mtt na uko kazini dada lazima. Na wanaume lzm mjiongeze na mpunguze utemi. Haiwezekani nikipata mshahara unasema tushee majukumu. Tunatoka kazini pamoja unataka niingie jikoni. Km ni hvy basi mshahara wako ndo uhudumie nyumba. Kuna post nlioka mkaka analalamika humu mkews hatoi pesa na ana mshahara. Ukimuuliza kama yy anafua au kupika atakwambia sio kazi yake. Kwa nn mnawaonea wanawake hvy?
 
Ungekuja na solution nini kifanyike! Mim naiona serikali ifike mahali mtoto wa kike alazimishwe kusoma hata kama akifail ni lazma arudie shule
 
Kuna wengine wanawaona hao beki 3 kama watumwa vile....kiukweli kama umeajiriwa angalau ule muda wa jioni jishughulishe basi kwa kupika chakula cha familia na pia siku za w.end fanya usafi na kupanga mazingira mkiwa na beki 3 utaelewa mapungufu ya nyumba yako pamoja na kuieweka safi.....
 
kwann mnaita binadam km nyie beck 3? kuweni na utu na ustaarabu! ....kila siku mnahangaika mikoani kutafuta hawa dada zetu watusaidie kazi majumbani sa hv kila mtu anajifanya anawachukia..roho mbaya sana muache! hawa wadada ni muhimu kuwaheshimu na wakati huo huo kusaidiana nao kazi za nyumbani awe baba ama mama!
 
Niliwahi kuishi na uncle enzi nasoma, uncle alikuwa mfanya biashara mkubwa hapa mjini, so walikuwa bize sana na mambo yao na mkewe aunt.
Kitu nilichokuwa nashangaa nikiwa teenager ni utaratibu aliojiwekea yule aunt kwenye familia yake.
Yaani jioni tu akilejea home basi ana take over all domestic duties akiwa na stori na uncle wangu.
Kwakuwa nilikuwa teeneger sikuelewa msimamo wa aunt na alikuwa akimwambia hg apumzike ataendelea na mambo yake siku inayofata.
Hao wanao mwachia beki Tatu kila kitu wamezidi loh mi hata msosi wa beki Tatu sili wao sijui wanawaamini vipi beki wenyewe washirikina, uelewa mdogo wachafu kwenye kupika wengine hutia had m.... In my life sipendi beki Tatu aisee sema MTU ukiwa na majukumu no way out ila sio kupika aiseee
 
Kuna wengine wanawaona hao beki 3 kama watumwa vile....kiukweli kama umeajiriwa angalau ule muda wa jioni jishughulishe basi kwa kupika chakula cha familia na pia siku za w.end fanya usafi na kupanga mazingira mkiwa na beki 3 utaelewa mapungufu ya nyumba yako pamoja na kuieweka safi.....
Wengine mkuu usafi, kupika, sijui kupangilia vitu home hawajui wanajificha nyuma ya beki tatu.
 
Binafsi mi sina dada wa kazi mpk ss coz nimeolewa na sina mtt. Ila ukishapata mtt na uko kazini dada lazima. Na wanaume lzm mjiongeze na mpunguze utemi. Haiwezekani nikipata mshahara unasema tushee majukumu. Tunatoka kazini pamoja unataka niingie jikoni. Km ni hvy basi mshahara wako ndo uhudumie nyumba. Kuna post nlioka mkaka analalamika humu mkews hatoi pesa na ana mshahara. Ukimuuliza kama yy anafua au kupika atakwambia sio kazi yake. Kwa nn mnawaonea wanawake hvy?
Mimi ndo nilietoe hiyo post kwamba mke wangu hafanyi kitu wakati ana mshahara ,maana yangu haikuwa tugawane majukumu nusu kwa nusu sivyo wala haiwezekani kwa sababu mimi ndo nilie oa,nilichokuwa namaanisha ni kwamba ,mwanamke inatakiwa achangie kwenye mambo madogomadogo ,mfano unakuta mimi sipo nyumbani na labda sukari imeisha ,unaporudi kazini anakuambie sukari imeisha naomba hela nikanunu wakati yeye kapata mshahara Jana ,hapa ndipo ninapoahangaa iweje aniombe mimi pesa ya kitu kidogo kama hicho wakati mshahara anao?
 
Wengine mkuu usafi, kupika, sijui kupangilia vitu home hawajui wanajificha nyuma ya beki tatu.
Hahahaha kweli mkuu kuna wanawake wanajua kutoa maagizo kufanya wao hapana...hawapendi kujishughulisha ....kwa upande wangu kuwa na beki 3 hata kama unamlipa sijisiki kumwachia kila jambo hata kama nimechoka unamsaidia hata kutenga chakula mezani ajione naye ni mtu katika familia
 
Mimi ndo nilietoe hiyo post kwamba mke wangu hafanyi kitu wakati ana mshahara ,maana yangu haikuwa tugawane majukumu nusu kwa nusu sivyo wala haiwezekani kwa sababu mimi ndo nilie oa,nilichokuwa namaanisha ni kwamba ,mwanamke inatakiwa achangie kwenye mambo madogomadogo ,mfano unakuta mimi sipo nyumbani na labda sukari imeisha ,unaporudi kazini anakuambie sukari imeisha naomba hela nikanunu wakati yeye kapata mshahara Jana ,hapa ndipo ninapoahangaa iweje aniombe mimi pesa ya kitu kidogo kama hicho wakati mshahara anao?
Na kweli ni ww uliandika.
 
Mkiishi wawili naona hamna haja ya dada,ila mkizid hapo na mama anafanya kazi dada ni muhimu
 
Back
Top Bottom