Fixed Point
JF-Expert Member
- Sep 30, 2009
- 11,304
- 12,744
Mi nawaombeni akina mama ishini vizuri na hawa wafanyakazi wa ndani maana wanabeba dhamana kubwa ya nyumba zenu wengi wenu mnawanyanyasa kana kwamba hana kwao au hana wazazi waleeni kama mnavyo walea watoto wenu vilevile mjitahidi kuwathamini haya yote mabaya wanayo fanya ni kutokana na ukatili wa akina mama wenye nyumba.
Poleni sana wafiwa wa Moro.
Ni kweli Fidel80 uliyosema, lakini cha kushangaza sana wadada wengi ambao wananyanyaswa sana na waajiri wao ndo wanakaa muda mrefu na wanachapa kazi sana. na mara nyingi ukikaa na mdada kama mtoto wako (hasa hawa wadada wa siku hizi) anaona wewe huwezi bila yeye kwa hiyo atakunyanyasa mpaka ujisikie. kuna kipindi cha miaka kama 3 iliyopita nilikuwa nabadilisha sana wadada, na sio kwamba wanataka kuondoka, ila mimi nakuwa uvumilivu umenishinda, nawarudisha kwao maana siwezi kabisa kutesa mtoto wa mtu. kuna kama 2 walishakuja kuomba warudi kwangu na kusema walikuwa wanakaa vizuri sana ila utoto ndo uliwaponza, maana kwingine walikoenda wanasema ni balaa.