'House girl' amnyonga mtoto, ajinyonga

Mi nawaombeni akina mama ishini vizuri na hawa wafanyakazi wa ndani maana wanabeba dhamana kubwa ya nyumba zenu wengi wenu mnawanyanyasa kana kwamba hana kwao au hana wazazi waleeni kama mnavyo walea watoto wenu vilevile mjitahidi kuwathamini haya yote mabaya wanayo fanya ni kutokana na ukatili wa akina mama wenye nyumba.
Poleni sana wafiwa wa Moro.

Ni kweli Fidel80 uliyosema, lakini cha kushangaza sana wadada wengi ambao wananyanyaswa sana na waajiri wao ndo wanakaa muda mrefu na wanachapa kazi sana. na mara nyingi ukikaa na mdada kama mtoto wako (hasa hawa wadada wa siku hizi) anaona wewe huwezi bila yeye kwa hiyo atakunyanyasa mpaka ujisikie. kuna kipindi cha miaka kama 3 iliyopita nilikuwa nabadilisha sana wadada, na sio kwamba wanataka kuondoka, ila mimi nakuwa uvumilivu umenishinda, nawarudisha kwao maana siwezi kabisa kutesa mtoto wa mtu. kuna kama 2 walishakuja kuomba warudi kwangu na kusema walikuwa wanakaa vizuri sana ila utoto ndo uliwaponza, maana kwingine walikoenda wanasema ni balaa.
 
Mara nyingi wanakuwa abused, oppressed, repressed, and suppresed. Underpaid, overworked, caged, molested, uneducated, impregnated, talked-down, raped, muzzled... akichoka ananyonga katoto kako anaanza.
wala sio wote wanafanyiwa hvo wengine wanapendwa wankuwa sehemu ya familia ila bado wanafanya maajabu sisi mam aliwahi kumbamba Hg anatuwekea dawa kwenye chakula sasa cjui ilikuwa anatuwekea kila siku? ila hatukujua so aliondolewa siku hyo hiyo na wakati alikuwa kama mma yetu maana amenilea mimi na wadogo zetu kila kitu cha nyumabni anajua na tulimpenda sana ila mmh! baadae akatuma barua kuwa kaokoka anataka tumsamehe maana alikuwa anatuchawia kabla hajaokoka wakati yupo hapa nyumbani loooh! tulichoka ila tulimsamehe na yakapita so kama wameamua wnafanya lolote sio mpka wateswe
 
Mimi bora niajiri mtu wa kuniangalizia mtoto kuliko kuajiri mtu wa kunisaidia kazi za nyumbani. Hakuna kazi ya nyumbani ambayo siiwezi na kama sina muda wa kutosha basi nitatengeneza muda.

Unapomtumikisha mtu (kufua nguo, kupiga pasi, kusafisha nyumba, kupika, kumwangalia mtoto na kadhalika) itafika mahali huyo mtu ataanza kuona ananyanyaswa kitu ambacho kinaweza kumfanya afanye yasiyopaswa kufanywa.

Niangalizie mtoto wangu nikirudi kutoka kazini unaanza....

wamama wakibongo hawawezi haya NN, Tumezoea kuagiza na kugomba kama wahindi,
 
wamama wakibongo hawawezi haya NN, Tumezoea kuagiza na kugomba kama wahindi,

Mimi nawaoneaga huruma sana hawa 'wasaidizi wa kazi za ndani'. Manyanyaso wanayoyapata hayasemeki. Utakuta mama mwenye nyumba anamgombeza tu bila sababu ya msingi. Sasa ukute msaidizi mwenyewe ni msichana mdogo ambaye hawezi hata kujisimamia mwenyewe anabaki kuinamisha kichwa na kulia.

Mimi hapana kabisa. Siwezi siwezi kuajiri mtu wa kunisaidia kazi za nyumbani. Kazi za nyumbani kwangu ni jukumu langu mimi mwenyewe. Mtu mzima kama mimi nimpe msichana mdogo nguo zangu anifulie? Oh hell to the muthafuckin' no....I'll do my own damn washing. I'll cook my own damn food and I'll clean my own damn house.

Siwezi mimi kumnyanyasa mtu kwa namna hiyo. Roho yangu hairuhusu kabisa.

I'm glad I wasn't a 'houseboy' coz for sure I don't take shit like that from no one. No carcass can degrade, humiliate, and put me down like that. I'll swing and we'll go rounds and I'll make sure I beat your ass to a fuckin' pulp.
 
Natoa pole kwa walioondokewa na mtoto (Familia zote mbili)

Wamama wamekuwa na tabia ya manyanyaso sana kwa hawa wasaidizi wa ndani...Wanawapiga sana bila sababu za msingi.... Wanawakata mishahara yao ikitokea wamekosea kidogo hata wakiunguza mboga tu... Wanawaamsha asubuhi sana na pia hawawapi nafasi ya kupumzika
Matusi ndio zimekuwa nyimbo kwa hawa wamama... Tena wanadiriki kuwambia "shida zako ndo zilikuleta"

Wamama msipobadilika tutasikia mengi sana juu ya hao wasaidizi wa ndani.
 
............Kila siku habari mbaya za hawa wasaidizi wa kazi nyumbani hadi inatisha:shock:, mbona zamani haikuwa hivi? Mie nililelewa muda mwingi na HG mbona walikuwa watu wazuri tu.........sijui pepo gani limewaingia hawa HG wa siku ni vituko kila kukicha.

Mie nimeshakata tamaa kuwa na hawa watu nafuu mtoto nimpeleke kwa mama yangu kunilelea kuliko HG maana sina matumaini nao kabisa.
 
Yaani wasichana wa ndani wananyanyasika sana nimeshuhudia.
Wengine wanaambiwa wasile chakula pamoja na watoto wa boss wengine wanalishwa makombo chakula walicho bakiza maboss wengine wanakula msosi tofauti na maboss wao yaani anaanda misosi miwili tofauti yaani manyanyaso wengine hata TV marufuku kugusa yaani utafikiri sio binadamu. Fikiria ww ndo uwe unafanyiwa hivyo utajisikiaje?

Fidel mie nadhani wengi wanaonyanyasa mahouse girl huwa ni malimbukeni wa maisha, au wanaroho mbaya tu hata kwa watu wengine kama vile ndugu nk.Pia kwa upande mwingine pia hata baadhi ya mahousegirl hawanashukurani utamfanyia kilakitu lakinibado haeleweki. Yaani ni shida tupu mimi nimeapa sitokaa na house girl nawaogopa sana kutokana na experience niliyopata kutoka nyumbani kwetu mama alikuwa anawatreat kama watoto wake but kila mtu na tabia alizotoka nazo kwao. ni kazi sana solution ni daycare tu ukitoka kazini unapitia mtoto wako basi ndo tunakoelekea mambo ya mahouegirl yataisha huko tunakoelekea.

 
Ni kweli Fidel80 uliyosema, lakini cha kushangaza sana wadada wengi ambao wananyanyaswa sana na waajiri wao ndo wanakaa muda mrefu na wanachapa kazi sana. na mara nyingi ukikaa na mdada kama mtoto wako (hasa hawa wadada wa siku hizi) anaona wewe huwezi bila yeye kwa hiyo atakunyanyasa mpaka ujisikie. kuna kipindi cha miaka kama 3 iliyopita nilikuwa nabadilisha sana wadada, na sio kwamba wanataka kuondoka, ila mimi nakuwa uvumilivu umenishinda, nawarudisha kwao maana siwezi kabisa kutesa mtoto wa mtu. kuna kama 2 walishakuja kuomba warudi kwangu na kusema walikuwa wanakaa vizuri sana ila utoto ndo uliwaponza, maana kwingine walikoenda wanasema ni balaa.

Yani Fixed point your right kabisa huwa naona dada yangu anavyohangaika na mahouse girl wake dada yangu mwenyewe mpole kama nini.
 
naona niwe babysitter sasa....

roselyn mie naona uanzishe daycare, muda wa kuleta watoto kuanzia saa 12 asubuhi na kuja kuwachukua saa 12 jioni siku nzima. umri kuanzia miezi 3 teh teh.Hivi centre kama hizi bongo zipo kweli manake naona daycare nyingi ni kindergarten sasa wanaandika daycare sijui wanamaanisha nini hapo.
 
Nilipoanzisha kale ka thread ka HG katembea na mwanangu, kweli sikujua kuwa hawa ndugu zetu wana roho ya ajabu hivi, nimeumia sana, by the way, wazazi nilazima tusimame katika nafasi zetu kama wazazi na sio kuwaachia HGs watulelee watoto na sisi
 
kwa mujibu wa taarifa ya habari ya ITV binti ndo kwanza alikuwa na mwezi mmoja tu katolewa kijijini mvomero, alikuwa ameomba aende home kusalimia akaambiwa asubiri mum akiwa off ndo aende. majirani nao wlitoa ushahidi wao kwamba hakukuwa na kutokuelewa kati yao hapo ndo nilipopata kigugumizi kabisa mie.
 
roselyn mie naona uanzishe daycare, muda wa kuleta watoto kuanzia saa 12 asubuhi na kuja kuwachukua saa 12 jioni siku nzima. umri kuanzia miezi 3 teh teh.Hivi centre kama hizi bongo zipo kweli manake naona daycare nyingi ni kindergarten sasa wanaandika daycare sijui wanamaanisha nini hapo.

nisaidieni basi capital :smilez::smilez:
mie nimechoka kubeba boksi huku,
ningekuwa na hela ningerudi kuanzisha hio biashara,
inaonekana iko viable!!:dizzy:
 
Yani Fixed point your right kabisa huwa naona dada yangu anavyohangaika na mahouse girl wake dada yangu mwenyewe mpole kama nini.

Mama Brian, mimi nimeshuhudia wamama wengi ambao wakali sana kwa maHG huwa wanakaa sana na hao wadada
 
nisaidieni basi capital :smilez::smilez:
mie nimechoka kubeba boksi huku,
ningekuwa na hela ningerudi kuanzisha hio biashara,
inaonekana iko viable!!:dizzy:

roselyne ngoja shule ziishe,tutatafutana tuanzishe hii kitu aisee nadhani itakuwabomba.
 
Back
Top Bottom