HOTUBA ya Seif Sharrif na Majibu yake kuhusu Maridhiano Zanzibar!

Nahitaji sana kujua historia zbar...kwa undani zaidi kama alivyoanzisha Maalim....naomba kupatiwa links nisome historia nzima....
 
1. Tangu lini Anno Domini imekuwa KABLA ya kuzaliwa Kristu?

2. Hauwezi ukazungumzia historia ya Zanziba bila kuzungumzia utumwa. Hao mnaosema kuwa wenyeji walishiriki watuambie ni kabila gani walikuwa na soko la watumwa ambako binadamu walikuwa wakipigwa mnada kama mbuzi? Watuambie ni kabila gani lilikuwa likiwahasi wale waliowateka vitani? Watuambie ni kabila gani ambalo lili m-dehumanise binadamu mwenzao kama walivyofanya hawa waarabu na wazungu? Msitake kuandika historia upya kwa kutaka kujikomba kwa hao mnaoona wamewazidi. Angalau wazungu wameosha utu wa kujutia biashara hii haramu na dhalimu. Kwa mtu anayejiita mmoja wa viongozi wakuu wa kisiasa Zanziba kuinyamazia ni incomprehensible.

Amandla.........

kama kutanguliza utumwa basi hii leo Obama asigelikuwa Raisi wa Dunia wacheni Fitna za utumwa leo hii jitizame nani anakuumiza?
 
Nimeitoa hapa;http://en.wikipedia.org/wiki/Street_light



kutoka hapa:http://genealogytrails.com/ill/adams/history/aqesl.htm



Kutoka hapa:http://www.zanzibar-holiday.com/brief_history.html

Hizo taa za stimu anazozingumzia Maalim ziliwekwa lini? Kama ni baada ya 1883, New York tayari walikuwa nazo tangu 1880.

Wawindaji wakubwa wa nyangumi kihistoria walikuwa watu wa Norway, Iceland n.k. Wamerekani wawaache wote hao waje kununua mafuta ya nyangumi Zanziba kuwashia taa za mitaani kwao? Zanziba ambao hawakuwa na historia ya kuwinda nyangumi!

Nchi gani hizo ambazo Zanziba ilikuwa ikizidai na ni kiasi gani ilikuwa ikidai? Zanziba ingedaiwaje wakati uwezo wa kukopa kama nchi kutoka nchi nyingine hakikuwa nao? Kwani leo wanadaiwa kiasi gani na NCHI ipi ya kigeni?

Amandla........
huna la kusema Amandla katafute gazeti la UHURU usome huelimishiki na hutoelimishika.
 
Hizo takwimu nilizoquote kwa rangi nyekundu ndio vichekesho japo hazina nambari lakini zinabaki kuwa ni takwimu kwa vile umetumia neno wengi(majority). hivi nikuulize ni nchi gani ambayo kunatokea mauwaji watu wasikimbilie nchi jirani? hii ni sheria ya kimaumbile na huwezi kuchukulia hiki kama ni kigezo cha ukarimu wa wabara kwa wazanzibari.(Mungu awalinde)lakini hata nyinyi mkianza kuuwana basi mtakimbilia zanzibar na kenya hivyo hii haiwezi kuwa ni hoja.

Chukua mfano huu hapa unaweza kufanana na hoja yako hii.Ireland walitawaliwa,kuonewa na kukandamizwa sana na waingereza lakini raia wa kawaida walikimbilia kwa hao hao madhalimu wao wa kiingereza kutafuta usalama wao na huku wakijua kwamba muingereza ndio adui yao.Hivyo wazanzibari kukimbilia bara kwenye matatizo haiondoi uhalisi wa kwamba bara hawezi kuwa adui yetu.

Hoja ya wahindi: hapa naona unajichanganya tena,kwenye mabandiko yako mengine,wahindi na waarabu unawatoa kwenye uzanzibari lakini hapa unawatamka kama wazanzibari kwakuwa tu wamekimbilia bara,tukamate lipi?

Kuhusu kesi ya Okello, ndugu ifatilie tena kesi ya okello kukimbizwa na nyerere usiuzuge umati wa JF. Soma tena mapinduzi ya Zanzibar.

Nakubaliana na wewe kwamba Karume aliungana na bara kwa kupata ulinzi, lakini baada ya kifo chake nini kiliendelea?

Kama Nyerere hakuupenda muungano je kulikuwa na haja gani ya kuunganisha vyama? Au utatwambia kwamba na vyama alitaka jumbe viunganishwe? acheni siasa za shule ,tuongeleeni uhalisi wa mambo jamani!

Wengi haina maana ya kuwa majority. Ningesema wengi "wa" hapo ungeweza kusema ninazungumzia majority. Wengi ni "many" na sio "most". Kuna wahindi (katika hawa nawajumuisha wale tunaowaita magoa) ambao walikimbia kuepuka mabinti zao kuolewa. Kuna wengine walikimbia kwa sababu nyingine.

Wapi nilipowatoa wahindi na wengine katika uzanzibari? Ninapozungumzia uarabu, ushihiri, uhindi, ungazija hizi ni identities ambazo zinatumika na zimekuwa zikitumika Zanzibar. Kwa watu wa nje, watu wote waliokuwa wakiishi Zanzibar walionekana kama wazanzibari. Lakini miongoni mwenu hadi leo mnajuana nani ni mngazija na nani ni muarabu. Hivi karibuni tumeona juhudi zikifanywa kuwanyang'anya haki wangazija za kuwa wazanzibari. Sio mimi, bali ni nyinyi ambao mnakataana.

Unazungumzia Ireland bila kuelewa historia yake. Waliokuwa wakigandamizwa ni wakatoliki na wengi walikimbilia Marekani, Canada, Australia n.k. hasa baada ya Great famine (an Gorta Mór) ya 1845-1852.
Usisahau vilevile kuwa waingereza wahamiaji walikuwepo kibao Ireland na hasa Ireland Magharibi wao walikuwa ndiyo majority. Wengine wao baada ya njaa kali bila shaka walirudi kwao. Hivi karibuni wa-irish wamekuwa wakihamia uingereza kuganga njaa. Wa-Irish waliohamia uingereza hata hivyo waliendelea kubaguliwa. Hii ni tofauti na wazanzibari waliohamia bara wakati wa utawala wa Karume I. Hawa hawakubaguliwa bara bali walikubaliwa kama watanzania wengine. Ingawa wengine walihamia bara kuganga njaa bado wapo wengi waliokimbia utawala wa kidhalimu wa mzanzibari mwenzao tofauti na wa-Irish waliokimbia utawala dhalimu wa wageni. Labda utuambie kuwa hao ndugu zako walikimbilia bara kukimbia utawala dhalimu wa watu wa bara! Utufahamishe vile vile ni lini watu wa bara wametawala Unguja!

Mimi nimesoma historia ya Zanzibar (pamoja na mchango wa Okello) na nimeweka tafsiri yangu. Wewe kama unaelewa tofauti basi weka tafsiri yako badala ya kutoa maagizo ya kipuuzi ya ati niisome upya. Unashindwa nini kuiweka hapa unavyoielewa?

Nani amesema Nyerere hakupenda Muungano? Nyerere alikuwa na ndoto ya kuunganisha Afrika nzima acha hako ka-Zanzibar. Nyerere ali-ofa kusogeza mbele uhuru wa Tanganyika ili tuweze kuungana na Kenya na Uganda. Nyerere aliupenda sana Muungano kinadharia lakini hakuuhitaji kama alivyouhitaji Karume. Baada ya kuungana na kuona mambo yaliyokuwa yakiendelea Zanzibar ndiyo akapendekeza vyama viungane.Waulize waliokuwa Zanzibar wakati wa utawala wa Karume I watakueleza hali ilivyokuwa. Haikuwa tu televisheni ya rangi (na viwanja vya michezo) alivyozungumzia Maalim.

Unataka kujua nini kiliendelea baada ya kifo cha Karume I? Waulizie wakina Ussi, Hanga na wengine! Hawa nao walinyongwa na Nyerere?

Amandla.......
 
Sasa mie nauliza this so called Baba wa Taifa amefariki, sasa taifa limekuwa yatima?

P:S
**Kwani Tanganyika hakuna wamasai, wamekonde, wazaramu???
 
si mlimpa cheo kisicho rasmi cha ubaba wa taifa au? labda nikuulize alikuja kufanya nini kwenye kamati ya dharura ya pale kiswandui kabla kutangazwa matokeo ya urais?,mkitaka msitake mguu wa tanganyika unaiathiri sana zanzibar!

Nyerere hakuwa na jeshi wala polisi. Alikuja kama raia. Jeshi na polisi wote walikuwa chini ya Mzanzibari mwenzenu. Sasa kama hao wazanzibari waliokuwa kwenye hicho kikao hawakuafikiana nae walishindwa nini basi kukataa mchango wake?

Nimewauliza, bara wanawazuia nini kuendeleza bandari zenu na viwanja vyenu vya ndege? Bara inawazuia nini kuendeleza zao lenu la karafuu? Mlilia bandari mmeachiwa na hadi sasa hamja fanya kitu. Mlianzisha benki yenu imewashinda. Wote mkawa mnafungua akaunti kwenye benki za bara. Mnadhani benki yenu ingeendelea vipi bila nyinyi wenyewe kuweka hela zenu mle? Mkaanzisha viwanda vya soda n.k. vimewashinda! Mnakosa umeme si kwa sababu bara hawaletei umeme bali kwa sababu mmeshindwa kuwekeza kwenye distribution network yenu! Lakini bado hamuoni kuwa nyinyi ndiyo wenye matatizo mnabaki kuilamu bara. Huo mguu wa bara uko wapi? Mbona Hong Kong walitawaliwa na uingereza lakini walipata maendeleo. Nyie mnadhani siasa ndiyo zitawakomboa badala ya kubadilika tabia na kuweka juhudi katika maendeleo yenu! Matumaini ya wengine wenu ni kuwa mkijitoa kwenye Muungano basi ma-ankal kutoka Oman watawamwagia mapesa! Acheni kulalama. Ukombozi wenu uko mikononi mwenu na hakuna anayewazuia isipokuwa nyinyi wenyewe!

Amandla.....
 
Nyerere hakuwa na jeshi wala polisi. Alikuja kama raia. Jeshi na polisi wote walikuwa chini ya Mzanzibari mwenzenu. Sasa kama hao wazanzibari waliokuwa kwenye hicho kikao hawakuafikiana nae walishindwa nini basi kukataa mchango wake?

Nimewauliza, bara wanawazuia nini kuendeleza bandari zenu na viwanja vyenu vya ndege? Bara inawazuia nini kuendeleza zao lenu la karafuu? Mlilia bandari mmeachiwa na hadi sasa hamja fanya kitu. Mlianzisha benki yenu imewashinda. Wote mkawa mnafungua akaunti kwenye benki za bara. Mnadhani benki yenu ingeendelea vipi bila nyinyi wenyewe kuweka hela zenu mle? Mkaanzisha viwanda vya soda n.k. vimewashinda! Mnakosa umeme si kwa sababu bara hawaletei umeme bali kwa sababu mmeshindwa kuwekeza kwenye distribution network yenu! Lakini bado hamuoni kuwa nyinyi ndiyo wenye matatizo mnabaki kuilamu bara. Huo mguu wa bara uko wapi? Mbona Hong Kong walitawaliwa na uingereza lakini walipata maendeleo. Nyie mnadhani siasa ndiyo zitawakomboa badala ya kubadilika tabia na kuweka juhudi katika maendeleo yenu! Matumaini ya wengine wenu ni kuwa mkijitoa kwenye Muungano basi ma-ankal kutoka Oman watawamwagia mapesa! Acheni kulalama. Ukombozi wenu uko mikononi mwenu na hakuna anayewazuia isipokuwa nyinyi wenyewe!

Amandla.....
Mbona unaongelea matatizo ya umeme zanj. kama vile bara umeme upo? aagh! bara wameshindwa kuleta umeme vijijini na mjini wanaweza kuwasaidia wazenj acheni unafiki hapa

Waachie zanz. na mambo yake..wakishindwa wakiweza sawa tu...si nchi yao wht is the problem...?
 
Wengi haina maana ya kuwa majority. Ningesema wengi "wa" hapo ungeweza kusema ninazungumzia majority. Wengi ni "many" na sio "most". Kuna wahindi (katika hawa nawajumuisha wale tunaowaita magoa) ambao walikimbia kuepuka mabinti zao kuolewa. Kuna wengine walikimbia kwa sababu nyingine.

Wapi nilipowatoa wahindi na wengine katika uzanzibari? Ninapozungumzia uarabu, ushihiri, uhindi, ungazija hizi ni identities ambazo zinatumika na zimekuwa zikitumika Zanzibar. Kwa watu wa nje, watu wote waliokuwa wakiishi Zanzibar walionekana kama wazanzibari. Lakini miongoni mwenu hadi leo mnajuana nani ni mngazija na nani ni muarabu. Hivi karibuni tumeona juhudi zikifanywa kuwanyang'anya haki wangazija za kuwa wazanzibari. Sio mimi, bali ni nyinyi ambao mnakataana.

Unazungumzia Ireland bila kuelewa historia yake. Waliokuwa wakigandamizwa ni wakatoliki na wengi walikimbilia Marekani, Canada, Australia n.k. hasa baada ya Great famine (an Gorta Mór) ya 1845-1852.
Usisahau vilevile kuwa waingereza wahamiaji walikuwepo kibao Ireland na hasa Ireland Magharibi wao walikuwa ndiyo majority. Wengine wao baada ya njaa kali bila shaka walirudi kwao. Hivi karibuni wa-irish wamekuwa wakihamia uingereza kuganga njaa. Wa-Irish waliohamia uingereza hata hivyo waliendelea kubaguliwa. Hii ni tofauti na wazanzibari waliohamia bara wakati wa utawala wa Karume I. Hawa hawakubaguliwa bara bali walikubaliwa kama watanzania wengine. Ingawa wengine walihamia bara kuganga njaa bado wapo wengi waliokimbia utawala wa kidhalimu wa mzanzibari mwenzao tofauti na wa-Irish waliokimbia utawala dhalimu wa wageni. Labda utuambie kuwa hao ndugu zako walikimbilia bara kukimbia utawala dhalimu wa watu wa bara! Utufahamishe vile vile ni lini watu wa bara wametawala Unguja!

Mimi nimesoma historia ya Zanzibar (pamoja na mchango wa Okello) na nimeweka tafsiri yangu. Wewe kama unaelewa tofauti basi weka tafsiri yako badala ya kutoa maagizo ya kipuuzi ya ati niisome upya. Unashindwa nini kuiweka hapa unavyoielewa?

Nani amesema Nyerere hakupenda Muungano? Nyerere alikuwa na ndoto ya kuunganisha Afrika nzima acha hako ka-Zanzibar. Nyerere ali-ofa kusogeza mbele uhuru wa Tanganyika ili tuweze kuungana na Kenya na Uganda. Nyerere aliupenda sana Muungano kinadharia lakini hakuuhitaji kama alivyouhitaji Karume. Baada ya kuungana na kuona mambo yaliyokuwa yakiendelea Zanzibar ndiyo akapendekeza vyama viungane.Waulize waliokuwa Zanzibar wakati wa utawala wa Karume I watakueleza hali ilivyokuwa. Haikuwa tu televisheni ya rangi (na viwanja vya michezo) alivyozungumzia Maalim.

Unataka kujua nini kiliendelea baada ya kifo cha Karume I? Waulizie wakina Ussi, Hanga na wengine! Hawa nao walinyongwa na Nyerere?

Amandla.......

Nyerere hakuwa na jeshi wala polisi. Alikuja kama raia. Jeshi na polisi wote walikuwa chini ya Mzanzibari mwenzenu. Sasa kama hao wazanzibari waliokuwa kwenye hicho kikao hawakuafikiana nae walishindwa nini basi kukataa mchango wake?

Nimewauliza, bara wanawazuia nini kuendeleza bandari zenu na viwanja vyenu vya ndege? Bara inawazuia nini kuendeleza zao lenu la karafuu? Mlilia bandari mmeachiwa na hadi sasa hamja fanya kitu. Mlianzisha benki yenu imewashinda. Wote mkawa mnafungua akaunti kwenye benki za bara. Mnadhani benki yenu ingeendelea vipi bila nyinyi wenyewe kuweka hela zenu mle? Mkaanzisha viwanda vya soda n.k. vimewashinda! Mnakosa umeme si kwa sababu bara hawaletei umeme bali kwa sababu mmeshindwa kuwekeza kwenye distribution network yenu! Lakini bado hamuoni kuwa nyinyi ndiyo wenye matatizo mnabaki kuilamu bara. Huo mguu wa bara uko wapi? Mbona Hong Kong walitawaliwa na uingereza lakini walipata maendeleo. Nyie mnadhani siasa ndiyo zitawakomboa badala ya kubadilika tabia na kuweka juhudi katika maendeleo yenu! Matumaini ya wengine wenu ni kuwa mkijitoa kwenye Muungano basi ma-ankal kutoka Oman watawamwagia mapesa! Acheni kulalama. Ukombozi wenu uko mikononi mwenu na hakuna anayewazuia isipokuwa nyinyi wenyewe!

Amandla.....

for the sake of argument acha nikubaliane na wewe yote hayo uliosema. naomba nikuulize masuali madogo sana ambayo hayahitaji uchambuzi.
1)kabla ya muungano na baada ya muungano ni wapi zanzibar ilikuwa na nguvu za kiuchumi na wapi ilikufa kiuchumi?
2)naomba unijibu yes or no, je nyerere hakuwa na athari yoyote katika uendeshaji wa nchi baada ya kung'atuka kwake?
3)nini kinachowapelekea watanganyika kuung'ang'ania muungano wakati zanzibar ni mzigo kwao?
4)ccm kiswandui wanapompendekeza dr.bilal kuwa rais wa zanzibar na ccm dodoma wanapompitisha amani karume.Je hapa huoni kama wazanzibari tumetawaliwa? au hili unalichukuliaje?
yapo masuali mengi yanayonitatiza lakini tuanze na hayo.Guu la tanganyika lipo zanzibar,huu ndio ukweli wenyewe.
 
Mutake musitake, haiwezekani kwenye dunia ya leo ati ukapindue jeshi kwa upanga kama alivyo fanya Okello.

Huyo Okello na watanganyika wenzake walikuwa ni watu wa Nyerere walikwenda Zanzibar kupindua.Hii ndio theory ambayo inaingia akilini mwangu, lakini najua itapingwa sana, na badala yake itakuwa Okello na gurupu la watanganyika wenzake wote walikuwa ni wazanzibari walipinduana.

Hizi theory za kuwa ati Nyerere hakutaka kabisa Zanzibar, alikuwa anatamani aisogeze huko mbali ndani ya visiwa vya Hindi...hizi theory ni bora mukaendelea kudanganyana huko huko Mbagala.

Huku kwetu haziingii akilini, na mtu yoyote mwenye akili timamu hawezi kubali ati nchi yenye jeshi na silaha ilipinduliwa kwa upanga wa Okello!...Hata huyo Rambo pia hupewa angalau bastola ndio akashinda!!

Sasa vyovyote iwanvyo, Tanganyika iko bizzi sana na Zanzibar.Kila uchaguzi ni lazima jeshi sijuwi kama si nusu hupelekwa visiwani.Mara ya mwisho nafikiria 2005 Unguja yote ilibidi itekwe....au pia Mkapa ni mzanzibari kama alivyokuwa Mwinyi?

Na huyo Mkapa ajitahidi sana asije akafa kabla Zanzibar haijapata kiongozi mwenye uchungu...lakini akiwacha mwanya basi ajue ana kesi The Hague ya kuuwa wazanzibari huko Pemba.
 
Mutake musitake, haiwezekani kwenye dunia ya leo ati ukapindue jeshi kwa upanga kama alivyo fanya Okello.

Huyo Okello na watanganyika wenzake walikuwa ni watu wa Nyerere walikwenda Zanzibar kupindua.Hii ndio theory ambayo inaingia akilini mwangu, lakini najua itapingwa sana, na badala yake itakuwa Okello na gurupu la watanganyika wenzake wote walikuwa ni wazanzibari walipinduana.

Hizi theory za kuwa ati Nyerere hakutaka kabisa Zanzibar, alikuwa anatamani aisogeze huko mbali ndani ya visiwa vya Hindi...hizi theory ni bora mukaendelea kudanganyana huko huko Mbagala.

Huku kwetu haziingii akilini, na mtu yoyote mwenye akili timamu hawezi kubali ati nchi yenye jeshi na silaha ilipinduliwa kwa upanga wa Okello!...Hata huyo Rambo pia hupewa angalau bastola ndio akashinda!!

Sasa vyovyote iwanvyo, Tanganyika iko bizzi sana na Zanzibar.Kila uchaguzi ni lazima jeshi sijuwi kama si nusu hupelekwa visiwani.Mara ya mwisho nafikiria 2005 Unguja yote ilibidi itekwe....au pia Mkapa ni mzanzibari kama alivyokuwa Mwinyi?

Na huyo Mkapa ajitahidi sana asije akafa kabla Zanzibar haijapata kiongozi mwenye uchungu...lakini akiwacha mwanya basi ajue ana kesi The Hague ya kuuwa wazanzibari huko Pemba.

Well said,

Tanganyika u=inatumia resources nyingi za nchi kwa ajili ya mambo ya wazanziba ...ni aibu na ujinga...waache wazenj wafanye watakavyo finito.
 
for the sake of argument acha nikubaliane na wewe yote hayo uliosema. naomba nikuulize masuali madogo sana ambayo hayahitaji uchambuzi.
1)kabla ya muungano na baada ya muungano ni wapi zanzibar ilikuwa na nguvu za kiuchumi na wapi ilikufa kiuchumi?
2)naomba unijibu yes or no, je nyerere hakuwa na athari yoyote katika uendeshaji wa nchi baada ya kung'atuka kwake?
3)nini kinachowapelekea watanganyika kuung'ang'ania muungano wakati zanzibar ni mzigo kwao?
4)ccm kiswandui wanapompendekeza dr.bilal kuwa rais wa zanzibar na ccm dodoma wanapompitisha amani karume.Je hapa huoni kama wazanzibari tumetawaliwa? au hili unalichukuliaje?
yapo masuali mengi yanayonitatiza lakini tuanze na hayo.Guu la tanganyika lipo zanzibar,huu ndio ukweli wenyewe.

Sasa unataka nikupeleke shule? Sasa kama haya ni maswali madogo unaniulizia nini? Majibu si unayo tayari? Hata hivyo:

1.Kabla ya Muungano uchumi wa Zanzibar ulitegemea sana karafuu na kabla ya hapo utumwa. Baada ya Muungano, wenye mashamba ya karafuu wengi walikimbia nchi. Waliorithi hawakuwa na uwezo wa kuyaendeleza. Vile vile kazi ya uvunaji na utunzaji wa mashamba hayo ni ngumu na awali ilikuwa ikifanywa na watumwa na watu kutoka bara waliokuwa wako tayari kuifanya kwa ujira mdogo. Kama vile ilivyokuwa kwa zao la katani, baada ya uhuru watu waliokuwa tayari kufanya kazi hiyo walipungua sana. Ubora wa zao uliathirika na kule kwenye soko kubwa (Indonesia n.k.) nao wakaanza kulima karafuu na badala ya kuwa wanunuzi wakawa washindani. Baada ya Muungano, vile vile badala ya kuwekeza kwenye vitega uchumi, SMZ ikawekeza kwenye maeneo yasiyo na tija kama televisheni ya rangi n.k. Uzembe huu unaendelea hadi leo.
2. Hatuko mahakamani kuniambia nikujibu yes or no. Hata hivyo sioni athari yeyote ambayo Nyerere angeweza kuileta baada ya kung'atuka kwake.
3. Watanganyika hawang'ang'anii Zanzibar. Usichanganye viongozi wachache na watanganyika kama jamii. Wanaotaka Muungano uendelee wengi wanafanya hivyo kutokana na sentimental reasons kutotaka kuwaangusha waliouanzisha hata kama hawapo. Kama vile ilivyo na kuhamia Dodoma.
4. Hayo ya kisiwandui ni ya CCM. Hata kama palikuwa pendekezo kutoka upande mmoj, walipokutana Dodoma ni lazima masuala ya CCM kitaifa yaliangaliwa na ndio yaliopelekea uamuzi wa kuona Karume anafaa kuliko Bilal. Ukweli unabaki kuwa Zanzibar ni sehemu ya Muungano na uamuzi wowote ni lazima uangalie hatma ya Muungano kabla ya yote. CCM sera yao ni Muungano kwa hiyo wasingeweza kuweka mtu ambae wanaona angeweza kuhatarisha sera yao. Ubaya ingekuwa kama wangewawekea mtu kutoka bara. Hawakufanya hivyo. Ule ulikuwa uamuzi wa CCM. Wazanzibari wasingeafikiana nao basi wasingempigia kura waliyebambikiwa. Au huyo aliyeona amedhulumiwa angesema wazi. Hawakufanya hivyo. Kosa lao.Ndiyo demokrasi.

Bahati mbaya siko hapa kutoa shule kwa hiyo sitaweza kujibu maswali yako mengine. Nakushauri tumia mtandao na waulize waliokutangulia, watakufahamisha.

Amandla.......
 
Sasa unataka nikupeleke shule? Sasa kama haya ni maswali madogo unaniulizia nini? Majibu si unayo tayari? Hata hivyo:

1.Kabla ya Muungano uchumi wa Zanzibar ulitegemea sana karafuu na kabla ya hapo utumwa. Baada ya Muungano, wenye mashamba ya karafuu wengi walikimbia nchi. Waliorithi hawakuwa na uwezo wa kuyaendeleza. Vile vile kazi ya uvunaji na utunzaji wa mashamba hayo ni ngumu na awali ilikuwa ikifanywa na watumwa na watu kutoka bara waliokuwa wako tayari kuifanya kwa ujira mdogo. Kama vile ilivyokuwa kwa zao la katani, baada ya uhuru watu waliokuwa tayari kufanya kazi hiyo walipungua sana. Ubora wa zao uliathirika na kule kwenye soko kubwa (Indonesia n.k.) nao wakaanza kulima karafuu na badala ya kuwa wanunuzi wakawa washindani. Baada ya Muungano, vile vile badala ya kuwekeza kwenye vitega uchumi, SMZ ikawekeza kwenye maeneo yasiyo na tija kama televisheni ya rangi n.k. Uzembe huu unaendelea hadi leo.
2. Hatuko mahakamani kuniambia nikujibu yes or no. Hata hivyo sioni athari yeyote ambayo Nyerere angeweza kuileta baada ya kung'atuka kwake.
3. Watanganyika hawang'ang'anii Zanzibar. Usichanganye viongozi wachache na watanganyika kama jamii. Wanaotaka Muungano uendelee wengi wanafanya hivyo kutokana na sentimental reasons kutotaka kuwaangusha waliouanzisha hata kama hawapo. Kama vile ilivyo na kuhamia Dodoma.
4. Hayo ya kisiwandui ni ya CCM. Hata kama palikuwa pendekezo kutoka upande mmoj, walipokutana Dodoma ni lazima masuala ya CCM kitaifa yaliangaliwa na ndio yaliopelekea uamuzi wa kuona Karume anafaa kuliko Bilal. Ukweli unabaki kuwa Zanzibar ni sehemu ya Muungano na uamuzi wowote ni lazima uangalie hatma ya Muungano kabla ya yote. CCM sera yao ni Muungano kwa hiyo wasingeweza kuweka mtu ambae wanaona angeweza kuhatarisha sera yao. Ubaya ingekuwa kama wangewawekea mtu kutoka bara. Hawakufanya hivyo. Ule ulikuwa uamuzi wa CCM. Wazanzibari wasingeafikiana nao basi wasingempigia kura waliyebambikiwa. Au huyo aliyeona amedhulumiwa angesema wazi. Hawakufanya hivyo. Kosa lao.Ndiyo demokrasi.

Bahati mbaya siko hapa kutoa shule kwa hiyo sitaweza kujibu maswali yako mengine. Nakushauri tumia mtandao na waulize waliokutangulia, watakufahamisha.

Amandla.......

unaonekana sana ulivyo mgeni na masuali ya zanzibar na hata mimi sikukusudia kukuuliza zaidi kwani haya niliyokuuliza na ulivyoyajibu tayari yananionesha kwamba tuna uelewa tafauti wa mambo! Mtu mwenye upeo wa mambo hata siku moja huwezi ukasema eti watanganyika hawautaki muungano lakini wachache wa serikali ndio wanautaka!au ukasema nyerere hakuwa na athari katika serikali baada ya kung'atuka kwake na ukazungumzia kuporomoka soko la karafuu bila kuhusisha uchumi mbadala wa utalii zanzibar n.k hapa nadoubt u great thinker wako! anyway kama alivyoshauri ndugu tumain hapo juu,nadhani mngetuachia wazenji na maamuzi yetu,naamini hatuko mbali na ukweli halisi. tuvumilianeni mpaka pale mtakapoamua kuutuwa huu mzigo wa zanzibar!
elewa tu kwamba nje ya muungano zanzibar itakuwa na:
sarafu yake
benki kuu yake
balozi kuu za nchi za nje
uhuru wa kujiunga na jumuia za kimataifa
itapokea misaada 100% na itapokea direct.
na kadhalika na kadhalika!
mimi nafikia hapa kwa leo.kila la heri ndugu.
 
Under-Age!

unaonekana sana ulivyo mgeni na masuali ya zanzibar na hata mimi sikukusudia kukuuliza zaidi kwani haya niliyokuuliza na ulivyoyajibu tayari yananionesha kwamba tuna uelewa tafauti wa mambo!

Majibu kama ulikuwa nayo uliniulizia nini? Yaani kweli ulitegmea majibu yangu yataunga mkono uelewa wako?

Mtu mwenye upeo wa mambo hata siku moja huwezi ukasema eti watanganyika hawautaki muungano lakini wachache wa serikali ndio wanautaka!

Nimesema wapi kuwa watanganyika wengi hawataki Muungano? Wengi wa watanganyika could not care less kama Muungano upo hau haupo. Au unadhani wale waliodai serikali tatu walitoka Zanzibar? Na unajua lakini hatma ya serikali tatu? Ulikuwa ndiyo mwanzo wa kuuvunja Muungano maana hakuna Rais wa tanganyika ambae angekubali hali ilivyo sasa hivi. Na huyo Rais wa JMT angekuwa hana uwezo mbele ya Rais wa Tanganyika. Mwisho ingekuwa kila mtu kuchuku chake na kujiondokea.

au ukasema nyerere hakuwa na athari katika serikali baada ya kung'atuka kwake na ukazungumzia kuporomoka soko la karafuu bila kuhusisha uchumi mbadala wa utalii zanzibar n.k hapa nadoubt u great thinker wako!

Mara ngapi nimetaja sehemu ya utalii katika uchumi wa Zanzibar? Nimezungumzia jinsi kutelekezwa kwa viwanja na ndege na bandari vinavyoathiri sekta ya utalii. Sasa ulitaka niseme nini, wewe Great Thinker?

Aliyekuambia mimi Great Thinker nani? Au ulijiunga na hii Forum ili na wewe uwe mmoja wao? Sijawahi, sitawahi kujiita Great Thinker sasa hizo doubt zako zitani-affect vipi?

tuvumilianeni mpaka pale mtakapoamua kuutuwa huu mzigo wa zanzibar!
elewa tu kwamba nje ya muungano zanzibar itakuwa na:
sarafu yake
benki kuu yake
balozi kuu za nchi za nje
uhuru wa kujiunga na jumuia za kimataifa
itapokea misaada 100% na itapokea direct.
na kadhalika na kadhalika!
mimi nafikia hapa kwa leo.kila la heri ndugu

Yale yale. Mnategemea mtabebwa na ankal kwa asili mia 100! Kwa mawazo kama haya hamyakuja kujiengua kamwe kutokana na umaskini wenu.

Kuwa kwanza pengine ndipo utaelewa vizuri hstoria ya hapo kwenu.

Amandla.......
 
elewa tu kwamba nje ya muungano zanzibar itakuwa na:
sarafu yake
benki kuu yake
balozi kuu za nchi za nje
uhuru wa kujiunga na jumuia za kimataifa
itapokea misaada 100% na itapokea direct.
na kadhalika na kadhalika!
mimi nafikia hapa kwa leo.kila la heri ndugu.


Sasa ndugu under age ukiwa na vitu ulivyovitaja ndio maendeleo au ni kitu gani maana umevitaja tu hukuvitolea melezo. Ninavyojua mimi unaweza kuwa na vitu vyoote hivyo na bado ndio matatizo yanazidi zaidi ya wakati ulipokuwa hunavyo.
 
Na unajua lakini hatma ya serikali tatu? Ulikuwa ndiyo mwanzo wa kuuvunja Muungano
Sasa hapa unajizonga zonga, u dont care less but you dont wanna let it go.Kumbe Zenji tamu, kila mtanganyika hataki kuvunja muungano kwa alivyokolea marashi ya karafuu :D

Sasa ndugu under age ukiwa na vitu ulivyovitaja ndio maendeleo au ni kitu gani maana umevitaja tu hukuvitolea melezo. Ninavyojua mimi unaweza kuwa na vitu vyoote hivyo na bado ndio matatizo yanazidi zaidi ya wakati ulipokuwa hunavyo.

Sasa ngoja nizungumze serious and straight to the point, where exactly we are going wrong on the union matter.

Kama walivyosema wahenga umoja sio tatizo, hii dhana ya Nyerere ya umoja au muungano ni nguvu ni kweli kabisa.Kinachokosekana ni mfumo mbadala wa kutengeneza muungano.Mifano ipo ya watu walioungana na kila mtu anafanya shughuli zake bila ya kuingiliana maungoni.

Mifano hiyo ni kama EU, UK, UAE hii yote ni mifano ya watu walioungana.Sasa mukisha tizama hiyo mifumo, halafu azeni kufananisha na mfumo wa muungano wa TZ.Hapo ndio utaanza kuona makosa yako wapi na nini kinahitajika kirekebishwe.

Kwa ufupi, Tanganyika au wabongo wanapenda kujifanya ni wajanja.Mwisho wake ndio wanajikuta wao wako mstari wa mbele kutengeneza mabomu na lawama kutoka visiwani.Hapa tukumbuke chimbuko la kelele zote, makosa yako kwenye vitu fulani fulani...ambavyo vyote hivyo vinalenga makombora kwenye makosa ya muungano.Nani alitengeneza makosa ay matobo hayo?..itategemea mapenzi yako, mie naona kama watanganyika hujifanya wajanja na kuleta ujanja mwingi.Mfano mmoja ni mafuta, yameingizwa kinyemela nyemela...

Au utaona JK anakimbia hoja za msingi na kuanza kutengeneza vikundi nje ya bunge anajadili kero za muungano.Hivi unamdanganya nani mwananchi au nafsi yako?Kero za muungano ni mijadala mizito ambapo mimi mwananchi nawakilishwa na wabunge, sasa unampa mpini Pinda animalize sio?

Sasa watanzania na waafrika kwa ujumla tufungue akili zetu na tuache ubinafsi.Muungano ni kitu chema, lakini isiwe kila Zanzibar inachotaka kufanya basi hairuhusiwi...kisa utaambiwa katiba.Sasa hii katiba ni mas-haf au biblia?

Tubadili mfumo tueke serekali 3, kila mtu adili na uchumi wake.Na tukihitajika kujadili masuala ya muungano, wajumbe wa muungano wanajadili masuala hayo.Au tuvunje, tukutane kwenye meza ya EA...ambapo naona kama ndio njia mbadala zaidi na yenye gharama ndogo kwa hizi nchi mbili.

Maana hiyo ya serekali 3 nayo ina mbinde zake, huenda gharama za uendashaji zikaongezeka.Au tukubali 2 Tanganyika na Zanzibar, na masuala ya muungano yawekwe wazi ni yepi...ikihitajika vikao vya muungano, serekali 2 hizo zinakutana na kujadili.

Sio huu mfumo uliopo sasa haijulikani suala la Tanganyika wala Tanzania, basi vurugu tupu!

Hebu tieni pressure huko kwenye serekali yenu na viongozi wenu huko bara wabadili mfumo wa muungano na wasiwe na woga wa mabadiliko.Wakubali yatatokea tuu, kama ni leo au kesho.Lakini huwezi kuzuia mabadiliko, kuyazuia ni kujitafutia gharama kubwa huko baadae.

Kuendelea kutumia nguvu za kijeshi kupindisha demokrasia Zanzibar, gharma zake ni roho za watu....na baadae ni kesi The Hague!

Nawasilisha...
 
Wapendwa wanaJF mimi kwa mtazamo wangu naona mwenendo wa Seif Sharif Hamad na Karume ni mwanzo mzuri ktk kuiletea maendeleo ya kiuchumi na kisiasa.

Nacho jiuliza ni kwa nini CCM hawataki kurekebisha katiba ya zanzibar ili karume aendeshe serikali ya mpito kwa miaka 2 ili kwa kushirikiana na CUF waandae tume mpya ya uchaguzi na baada ya hapo uchaguzi ufanyike mwaka 2012 ambao utaruhusu kila chama chenye wabunge kushiriki ktk uundaji wa serikali ya mseto.

Kama alivyosema balozi wa marekani mbona USA Obama ameteua watu kutoka Republicans ktkserikali yake? Kwa nini hii ishindikane zanzibar/Tanzania?

Naomba nihitimishe kwa kusema watanzania tuwaunge mkono wazanzibari ili wawe mwanzo mpya wa zanzibar na tanzania mpya yenye serikali za mseto zinazo shirikisha vyama vyote vyenye wabunge ktk kuunda serikali.

CCM siyo chaguo la kila mtanzania!!
 
Hoja ya msingi hapa ni kuwa Zanzibar/Tanzania siyo mali ya CCM bali ni mali ya Wazanzibari na watanzania kwa ujumla. Hata biblia kuna agano la kale na agano jipya, hii ni baada ya marekebisho fulani, je, ni kwa nini kurekebisha katiba za tanzania huwa ni kama kufanya dhambi??
 
Shida hapa ni kwamba kwanini wanaanzisha mambo haya this late?

Kwa miaka yote walikuwa wapi?..matokeo yake inaleta hisia kwamba kuna uroho wa madaraka unataka kujiinua, ambapo hawa jamaa wanataka kutumia mgongo wa vitu kama serikali ya mseto, ili kuendelea kutawala.

Kimsingi wazo ulilosema la serikali ya mseto ni la msingi sana, na ni wakati muafaka lije, Lakini Karume a'step aside, amwachie mwingine asongeshe jambo hilo, maana si la kufanya overnight!

Thats my take!
 
Shida hapa ni kwamba kwanini wanaanzisha mambo haya this late?

Kwa miaka yote walikuwa wapi?..matokeo yake inaleta hisia kwamba kuna uroho wa madaraka unataka kujiinua, ambapo hawa jamaa wanataka kutumia mgongo wa vitu kama serikali ya mseto, ili kuendelea kutawala.

Kimsingi wazo ulilosema la serikali ya mseto ni la msingi sana, na ni wakati muafaka lije, Lakini Karume a'step aside, amwachie mwingine asongeshe jambo hilo, maana si la kufanya overnight!

Thats my take!

Siasa ni mchakato na CUF baada ya kuona CCM hawataki kutekeleza muafaka kupitia kamati zilizo undwa wakajaribu kupitia kwa Karume mwenyewe.

Mkuu ktk siasa hakuna kuchelewa na ndio maana hata balozi wa marekani anasema kurekebisha katiba ni issue unweza kufanyika ktk mwezi mmoja kama pande zote zina nia ya dhati.

Kusema karume atoke hapo ndio kuna tatizo kwa sababu mazungumzo aliyafanya yeye na hakuwashirikisha CCM bara kwa sababu ndo wenye choko choko za kutaka kuitumiazanzibar kwa manufaa yao.

Tumechoka kusikia mara mabomu mara mtu kachinjwa zanzibar, let the zanzibaris decide on what they want, CCM siyo chakula kwamba wasipokubaliana na CCM watakufa.
 
Back
Top Bottom