Hotuba ya Rais ya Kikwete kwenye baraza la Idd-Mawazo yangu

Hakuna amabe hajafanya biashara ya utumwa, na usitake kusema ni waarabu tu walijikita katika biashara ya utumwa. hao weuzi walioko kontinenti jipya, walipelekwa na Waarabu?

Biashara ya Utumwa ilifanywa na Waafrika na Waarabu na Wazungu hakuna ambae hajaifanya na usijidanganye kuwa biashara ya utumwa imekwisha, ina sura mpya tu. na ushahidi ni huu hapa:

What is modern slavery?

Millions of men, women and children around the world are forced to lead lives as slaves. Although this exploitation is often not called slavery, the conditions are the same. People are sold like objects, forced to work for little or no pay and are at the mercy of their 'employers'.

Source: Anti-Slavery - What is modern slavery

Kwa kukujuza tu, kanisa lilihusika direct na utumwa wa zamani na mpaka papa akaomba msamaha kwa kanisa kujihusisha na utumwa. Na ushahidi upo wa kanisa kuomba msamaha kwa hilo. Hayo mafundisho yako ya kuwa ni waarabu pekee waliojikita kwenye biashara ya utumwa hayana mshiko kwangu, na uwadanganye wengine.

Kuhusu mashule, ikiwa historia inafutwa makusudi unategemea utakuta nini kilichobakishwa cha waarabu baada ya kuingia wazungu kwa miaka kadhaa?

Historia ya wazungu na ukoloni hapaka kwetu haikuanzia kwa wajerumani na waingereza pekee, naona umewasahau wareno. Jee, hujui kwamba wareno kilichowaeta huku ni krusedi? na wajerumani huelewi ni kina nani wali resist (vita vya majimaji) kuingia mjerumani? hali kadhalika kwa waingereza?

Wazungu walipoingia hapa walikuta kuna nyumba za ghorofa Kilwa, walikuta kuna nyumba zinapakwa rangi wakati wao walikuwa hawajui rangi ni nini, walikuta watu wa kilwa wanasarafu zao za dhahabu wakati kwao ilikuwa hakuna, walikuta watu wa Kilwa wanafanya biashra na India na Uchina, wakati wao hata njia ya kufika huko walikuwa hawaijui. Kama kulikuwa hakuna elimu hayo yote yalipatikanaaje.

Unaonesha wewe historia yako umejifunza upande mmoja tu na zinatokana na haohao wazungu, ambao mpaka sasa wakichora picha ya Yessu wanamchora mzungu na wakichora picha ya sheta wanamchora mweusi. Huo ndio ujinga waliokujaza. Funguka na utazame ukweli.

Miaka nenda miaka rudi ya wazungu hapa kwetu ni nini walichokifanya zaidi ya kututia ujinga na kujitajirisha makwao? unafikiri utajiri wa Uingereza na Ujerumani umetokea wapi? Hao waarabu unaowasema wewe, hawana zaidi ya kuhamishia hata makao yao makuu kuwa hapahapa (Zanzibar), kama ni mali waliibakisha hapahapa.

Tanganyika inapata Uhuru baada ya Wareno, Wajerumani na Waingereza kukaa hapa zaidi ya miaka na vikaka walikuwacha na madaktari wangapi wa kiafrika? majaji wangapi? ma engineer wangapi? wasomi wangapi? mashuduuu. Kinyume na hayo, 90% ya madakatari, ma engineer, majaji, waalimu waliowaacha Waarabu Zanzibar walikuwa ni Wazanzibari, hiyo tu itakuonesha ni vipi tofauti ya hawa watawala wakiarabu na kizungu.
Aiseee............! Kweli FaizaFoxy a.k.a mbwa mwitu jike ni zaidi ya umjuavyo!
 
Niliwahi kuandika humu hapo nyuma lakini watu wakajitia uziwi kama kawaida! CCM haijawahi kuwa pamoja na maslahi ya Waislamu tangu ianzishwe na hilo halitegemei kubadilika karibuni. Makanisakwa support CHADEMA kwenye uchaguzi 2010, they were only making a statement!

Losers kwenye hili ni makundi haya mawili: WAISLAMU sasa hawana pa kukimbilia kwa maana wametumiwa na JK kwa malengo ya kisiasa na sasa hawahitaji tena!

CHADEMA nao ni losers wengine katika hili., ni wazi Waislamu wataanza tena kuichukia CCM na jamii ya kikristo itarudi kuisupport CCM kimaslahi kama zamani! Ile support CDM ilikuwa ina pata toka jamii ya kiktisto ndio mwisho wake huo! 2015 political landscape itakuwa imebadilika sana, just wait and see!

You are deadly WRONG! Wakristu hatuwezi kushabikia CCM ati kwa sababu tu JK amesema waislamu wakajenge mahakama yao ya kadhi. Na hatujawahi kushabikia CDM ati kwa sababu mmoja kati ya viongozi wakuu aliwahi kuwa kasisi. Ukristu Tanzania sio itikadi ya kisiasa kama unavyojaribu kuiweka. Ama hujui kuwa kuna mamia ya waislamu amabao nao wameunga mkono hotuba ya JK? Achana na masheikh ubwabwa wanaotangaza maandamano. Wapo wanazuoni wanaosema kama serikali ikianzisha mahakama ya kadhi, wao hawatakubali kuwa sehemu yake kwa kuwa serikali siyo ya kiislamu. Kwa hiyo, msimamo wa JK kama ni wa serikali nzima basi unatuweka katika win-win situation kwa sababu mahakama ya kadhi hatuitaki. Je, tutamwamini mtu huyu aliyewahadaa waislamu wenzake hata tufikie hatua ya kuipenda sana CCM? Hapana, kajipoange upya uje na uchambuzi makini na sio kutaka kutukosanisha wakristu na waislamu. Waache waislamu wanaoipenda CCM waendelee na wanaopenda vyama vingine pia uwaache. Pia uwaache wakristu wanaopenda vyama mbalimbali waendelee na mapenzi yao bila kuhusianisha na hoja za JK na kadhi wake.
 
Hapo kwenye red; ndio maana hata serikali imewashtukia kwa udini, ubinafsi, na agenda zenu zisizoeleweka. Sikutegemea kejeli kwa wengine; sawa wanaabudu miungu hata mia, ni imani yao waache. Msidhani imani yenu ni superior kushinda zingine. Hamjapata mnaleta matusi, mkipata si ndio mtakata watu vichwa hadharani?

Kama udini unamaanisha Uislaam, basi mtaupinga sana na ndio unazidi kushamiri duniani, wala hatuna shaka nalo hilo.
 
Foxy, mkuu wangu mnakosea sana mnapotazama vitu kwa ujumla wake. JK ni rais wa nchi yetu kama marais waliotangulia na kuna makosa makubwa yamefanyika ambayo hayakutakiwa kutolewa majibu rahisi kama ya JK ktk hotuba yake. Pengine wewe umeyatazama haya kama vile JK ni mfadhili fulani ambaye anaweza kutoa majibu kihuni kama alivyopfanya JK..

Kwanza ni lazima utambue ya kuwa CCM wamekuwa wakicheza karata mbaya sana ya Udini toka Nyerere ameondoa madarakani. Na hili swala la mahakama ya kadhi limeondolewa wakati wa Nyerere lakini kwa shinikizo la waislaam wenyewe wakati huo mwanasheria mkuu nadhani akiwa Sheikh Amri Abeid Karuta..Na wala tusitake kujidanganya kuwa haya maswala ya ndoa, mirathi, wakfu na kesi nyingine za madai zinaweza kutolewa hukumu kirahisi na chombo ambacho hakitambuliwi na serikali ati kwa kufananisha na mpira wa kwenye vumbi..

Pengine wewe na utawala wa JK hamfahamu haswa sababu ya Waislaam kuomba mahaka aya kadhi kiasi kwamba ndio maana mnatoa majibu ya kipuuzi kama mpira wa vumbi usiohitaji refa. Foxy nikukumbushe tu kwamba madai yote ya ndoa, mirathi wakfu yanaweza kutolewa ufumbuzi hata msikitini tu na yakaisha bila hata ya kuwa na mahakama ya Kadhi, isipokuwa kilichotokea ni pale anapotokea mtu mkorofi ambaye hakubaliani na sheria za kidini isipokuwa zile za serikali at his/her advantage.

Huyu mtu huweka madai yake ktk mahakama za serikali ambazo pengine zinapingana ktk maamuzi na sheria za dini, mathlan masharti ya utoaji talaka, kugawana mali, mirathi na kadhalika sasa inapofikia hapo hukumu ya serikali ambayo yaweza kuwa pizani na ile ya Kidni ndio sababu haswa Waislaam wametaka mahakama ya kadhi kwa kuwa kesi nyingi za kiislaam zimehukumiwa kinyume cha mafundisho ya dini...Sasa inapotokea Waislaam wengi wanaitaka mahakama hii ujue pengine kuna sheria kweli ktkmahakama zetu ambazo zinawakinza Waislaam wake kwa waume na tunaweza vipi kuzitatua..

Sasa unaposema huu ni mpira wa vumbini mkuu wangu nashindwa kuwaelewa wewe na JK kama mnaelewa vizuri uzito wa swala hili kwa sababu huwezi kusema mahakama ya kadhi ni suala la waislaam ili hali mahakama za kawaida zinaweza kuingilia maamuzi ya mahakama ya kadhi na ndio kitu kilichosababisha waislaam kuomba mahakama ya kadhi inayotambulika ili kuondoa migogoro ya kimaamuzi baina ya sheria za dini na sheria za binadamu.

Sote tunaweza ku argue kwamba inatakiwa sheria moja kwa watu wote lakini come to think of that ni sheria gani itumike?. maanake sheria nyingi za madai ktk mahakama zetu zimejengwa ktk misingi ya Kikristo na tamaduni za nchi za magharibi ambao hakuna makosa wala dhambi kutembea nje ya ndoa wala hata kuzaa nje ya ndoa isipokuwa ni swala la wana ndoa wenyewe. Sasa ni vigumu sana kuweza kupata maamuzi yenye haki ikiwa wananchi wenyewe wametawaliwa na sheria nyingi tofauti na zinaweza kuchezewa at ones advantage.. Maskini wengi wamekosa haki zao kutokana na kukosa nguvu ama kuwa na imani ya dini lakini mahakama za serikali zikawanyima haki hizo kutoana na makosa ya tamaa zetu wenyewe.

Huko ndiko tulipotokea mkuu wangu hadi mahakama ya kadhi zikaombwa na Waislaam, sasa ni jukumu la JK na utawala wake kutafuta mbinu ambayo itaweza kutumika kuondoa dosari hizi dhidi ya wanandoa Waislaam waliofunga ndoa wakaweka vows zao ndani ya misingi ya kiislaam lakini siku ya siku ya talaka au mirathi mmoja wao anaenda korti za serikali ambazo zina mtazamo tofauti kabisa na mafundisho ya dini.

Kwa hiyo huwezi sema ni bora kuwa independent wakati hujui tumeshindwa kuwa independent kutokana na sheria za serikali kuwa pinzani na zile za kiislaam hivyo kutoa hukumu kinyume cha mafundisho ya Kiislaam laa sivyo haya maswala yangekuwa yakimalizwa nyumbani au hata miskitini tu...Hili ni tatizo dogo sana ukilitazama at face value lakini ni kero kubwa sanakwa waislaam na hasa Bakwata ambao hupokea malalamishi kila siku kutoka kwa Waumini wake, pia kwa upande wao wameshindwa kuelewa kwamba sisi Waislaam wenyewe ni wanafiki wa imani ya dini yetu wenyewe. Kwa matatizo mengi yanayotokana na kutopata suluhisho hutokana na uzinifu, talaka ambazo bwana kapata kitu kimpya, urithi wa mtoto wa nje ya ndoa na kadhalika ili mradi huwezi kutoa kuhumu ya haki pale Waislaam wenyewe wamepindisha mafundisho ya dini..


JK hakutakiwa kuwaahidi waislaam lolote mwaka 2005 or 2010, hili ndio kosa lake kubwa sana na hayomajibu yake ya kebehi hayawezi kuondoa makosa yaliyotangulia kwa rais kuwadanganya waislaam... HE LIED which makes him a LIAR! Alipowaahidi Waislaam mahakama ya kadhi hali akijua fika kwamba hatawapa wala haiwezekani kuwapa ndilo kosa lake kubwa acha kabisa habari ya kusema ukweli ambao aliuficha miaka yote iliyopita. na hakika anapowaambia waislaam kwamba swala la mahakama ya kadhi ni suala la Waislaam yaonyesha kwamba JK hajui kilichotokea huko nyuma kwa sababu hata siku moja haikuwa mahakama ya kadhi sii swala la waislaam.


Pili, mkuu wangu JK kama rais wa nchi huwezi kuwaambia Waislaam ati wamechelewa wapi kuja nao kuomba mkataba kama wa MoU.. Ule mkataba ni makosa makubwa yalifanywa na Mh. Mwinyi kwa sababu huwezi kuongoza nchi kwa kugawa makundi. Huwezi kufanya mkataba na dini moja ukitegemea wengine wakija utafanya nao pia mkataba hali kazi ya serikali ni kujenga policy ambayo vyombo, taasisi na jumuiya zote wanatakiwa kuwa obliged to na sii kimakundi. Sasa kama kesho waislaam wataenda kuweka mkataba, kesho kutwa watafuata Baniani, Ismailia, Budha - why not have One policy for all?..

Hapa JK na utawala wake wanacheza karata mbaya sana za kujenga udini na kesho wakristu watataka kuona Waislaam wamepewa nini ktk mkataba wao, wahindi vile vile na kuendeleza kujenga matabaka baina ya wananchi wake. Halafu kama ameshindwa kuwapa Mahakama ya kadhi alowaahidi na kuapa una uhakika gani atawapa mkataba wa MoU pengine atasema tena mkataba mnaoutaka ni suala la Waislaam!..The guy is a liar!

Believe me, JK ktk hotuba zake hakunifurahisha hata kwa moja.. The only hotuba nilomvulia kofia JK ni ile ya kwanza bungeni na kichekesho ni kwamba kashindwa kukamilisha hata MOJA la hotuba ile..

Mkuu Mkandara , Nimejaribu kufuatilia post kwenye hii thread hasahasa za waislam lakini naona nazidi kuwa confused . Hivi waislam mnataka nini?. Mkuu hivi ninavyokuandikia naangalia habari hapa ITV. Usiku wa kuamkia leo huko Tanga kuna vijana wamejaribu kuchoma makanisa…waliweza kumwaga petroli na kuwasha moto lakini bahati nzuri waamini walifanikiwa kuuzima moto. Kwa sasa wanaendelea na vitisho.kwa wakristu. Naona ndiyo hotuba ya Kikwete inaanza kufanya kazi.

Turudi kwenye mada…mimi naona hata wewe mwenyewe upo confused na sidhani kama unafahamu kitu unachokitaka kina maana gani kwa wananchi wote wa TZ wa madhehebu mengine na wasio na madhehebu.
Mfano….Unasema kikwete hawezi kuwaambia waislam ati wamechelewa wapi kuja nao kuomba mkataba kama wa MoU kwa sababu ule mkataba ni makosa . Unasema MoU ni kugawa nchi kwa makundi….eti waislam , baniani, Budha nk wanaweza kudai MoU pia. Unasema kuhusu one policy for all.
Sasa kama unatazama MoU kwa jicho hilo kwanini usiitazame mahakama ya Kadhi kwa jicho hilohilo? Nina maana kwani hizo dini nyingine na zenyewe haziwezi kufuata mkumbo huo huo na kutaka sheria zao dini zisimamiwe na serikali?
Halafu kitu kingine sikielewi kabisa…unasema mmekuwa mnafuatilia kuhusu uanzishwaji wa mahakama ya kadhi kwa sababu sheria zenu za mirathi ,ndoa nk zinapingana na zile za serikali lakini wakati huhuo unasema kikwete alikosea kuwaahidi waislam mahakama ya kadhi kwenye uchaguzi 2005 na 2010. Sasa hapa sijui kama asingewaahidi kitu chochote ndiyo mngekuwa mmetulia tu hamdai tena au….?
Halafu wengi wenu hamuitambui BAKWATA , mnasema ni kama vile chombo cha serikali ……..Ila mnadhani kama Kadhi ikisimamiwa na serikali itakuwa chombo cha waislam wote.Yeah BAKWATA na Kadhi ni vitu viwili tofauti lakini mimi naona ni confusion tu.
Mkuu ngoja niwaache mparurane …mimi imetosha!
 
Kama udini unamaanisha Uislaam, basi mtaupinga sana na ndio unazidi kushamiri duniani, wala hatuna shaka nalo hilo.

Muhula wa Nyerere - waislamu kimya
Muhula wa Mwinyi - waislamu na OIC
Muhula wa Mkapa - waislamu kimya
Muhula wa Kikwete - waislamu na mahakama ya kadhi

mwenye akili haambiwi tazama..........utatoa tafsiri yako mwenyewe ya udini.
 
Muhula wa Nyerere - waislamu kimya
Muhula wa Mwinyi - waislamu na OIC
Muhula wa Mkapa - waislamu kimya
Muhula wa Kikwete - waislamu na mahakama ya kadhi

mwenye akili haambiwi tazama..........utatoa tafsiri yako mwenyewe ya udini.

mapinduzi yanakuja, waislamu watajitenga.

thumbnail.aspx
 
@FaizaFoxy
Hakuna amabe hajafanya biashara ya utumwa, na usitake kusema ni waarabu tu walijikita katika biashara ya utumwa. hao weuzi walioko kontinenti jipya, walipelekwa na Waarabu?
Soma majibu yangu vizuri. Nimesema waarab walijikita zaidi kwenye biashara ya utumwa. Wote wameshiriki kwenye biashara ya utumwa but others did leave something else behind - shule. Waarab waliacha nini? then rudi kwenye hoja yako ya msingi ya ukoloni na fursa za elimu kwa waislam.

Kuhusu mashule, ikiwa historia inafutwa makusudi unategemea utakuta nini kilichobakishwa cha waarabu baada ya kuingia wazungu kwa miaka kadhaa? Historia inaonesha jamii ya waislam hawakuwekeza kwenye elimu i.e kwa kujenga shule nyingi kama wakristo. Na kwa kurudia maneno yako Faiza ni kwamba waislam wengi hawakupeleka watoto kwenye shule zilikuwepo wakati huo (nyingi zikiwa chini ya umiliki wa wakristo) kwa 'kuhofia' ...

Historia ya wazungu na ukoloni hapaka kwetu haikuanzia kwa wajerumani na waingereza pekee, naona umewasahau wareno. Jee, hujui kwamba wareno kilichowaeta huku ni krusedi? na wajerumani huelewi ni kina nani wali resist (vita vya majimaji) kuingia mjerumani? hali kadhalika kwa waingereza? - Katika hoja yangu niliweka wakoloni katika makundi mawili: wakristo (wakiwemo missionaries) na waislam (waarabu). Na nilijaribu kukuonesha kuwa pamoja na kuwa haya makundi yalikuwa na one thing in common (unyonyaji) kundi la wakoloni wakristo liliacha a relatively stronger leagacy kwenye elimu. Na nilijaribu kukuuliza kwa nini unakwepa kuchambua mchango wa waarab katika kuelimisha wale waliowatala? Hii ya wareno or any other group you can remember haibadilishi the fact that,historically at least sehemu kubwa ya jamii ya kiislam imekuwa very casual when it comes to elimu dunia.

Wazungu walipoingia hapa walikuta kuna nyumba za ghorofa Kilwa, walikuta kuna nyumba zinapakwa rangi wakati wao walikuwa hawajui rangi ni nini. Hapa kuna utata. Natambua mikoa ya kusini hasa Mtwara na Lindi kuna aina ya miti ikichemshwa hutoa rangi na wenyeji wamekuwa wanatumia katika mambo mbalimbali. Hata leo hii wanatumia kubadilisha rangi za ukili wa kutengeneza makapu i.e black. Kitu ambacho ni disputable hapa Faiza ni hii revelation yako kwamba wazungu hawakujua rangi hadi walipofika Kilwa? In other words rangi iligunduliwa na watu wa Kilwa? Ni mwaka gani huo? Ningefurahi sana kama kweli hili kweli but I have a feeling unaongelea maendeleo ya Kilwa (kwa wakati huo) ni isolation!

Miaka nenda miaka rudi ya wazungu hapa kwetu ni nini walichokifanya zaidi ya kututia ujinga na kujitajirisha makwao? - Nani kawaleta?

Tanganyika inapata Uhuru baada ya Wareno, Wajerumani na Waingereza kukaa hapa zaidi ya miaka na vikaka walikuwacha na madaktari wangapi wa kiafrika? majaji wangapi? ma engineer wangapi? wasomi wangapi? mashuduuu. Kinyume na hayo, 90% ya madakatari, ma engineer, majaji, waalimu waliowaacha Waarabu Zanzibar walikuwa ni Wazanzibari, hiyo tu itakuonesha ni vipi tofauti ya hawa watawala wakiarabu na kizungu. -

Then what happened? Unataka kusema waarab waliacha madaktari, ma-engineer majaji, walima wengi kuliko ilivyo sasa? Kwa bahati I know a thing or two about the history of Zanzibar na utawala wa Sultan. Unaelewa historia ya Wagoa, Wahindi au jamii ya Zorostian Zanzibar wakiwemo wazazi wa Fariq (wengi mnafaham kama Freddy Mercury - mwanamzuki aliyehamia Uk, sasa ni marehemu)? Sultan alikuwa ana -import skilled labour from India, Pakistan and Persia. Wamatumbi walikuwa kwenye mashamba ya karafuu! So, let's leave it there.

Na huku Tanganyika mwarab aliacha wataalam wangapi? Na kwa maoni yako unataka waarab warudi ndio waislam wapeleke watoto shule? What exactly is your point here Faiza kwa kuzingatia hoja inayozungumzwa?
 
Mkuu Mkandara , Nimejaribu kufuatilia post kwenye hii thread hasahasa za waislam lakini naona nazidi kuwa confused . Hivi waislam mnataka nini?. Mkuu hivi ninavyokuandikia naangalia habari hapa ITV. Usiku wa kuamkia leo huko Tanga kuna vijana wamejaribu kuchoma makanisa…waliweza kumwaga petroli na kuwasha moto lakini bahati nzuri waamini walifanikiwa kuuzima moto. Kwa sasa wanaendelea na vitisho.kwa wakristu. Naona ndiyo hotuba ya Kikwete inaanza kufanya kazi.

Turudi kwenye mada…mimi naona hata wewe mwenyewe upo confused na sidhani kama unafahamu kitu unachokitaka kina maana gani kwa wananchi wote wa TZ wa madhehebu mengine na wasio na madhehebu.
Mfano….Unasema kikwete hawezi kuwaambia waislam ati wamechelewa wapi kuja nao kuomba mkataba kama wa MoU kwa sababu ule mkataba ni makosa . Unasema MoU ni kugawa nchi kwa makundi….eti waislam , baniani, Budha nk wanaweza kudai MoU pia. Unasema kuhusu one policy for all.
Sasa kama unatazama MoU kwa jicho hilo kwanini usiitazame mahakama ya Kadhi kwa jicho hilohilo? Nina maana kwani hizo dini nyingine na zenyewe haziwezi kufuata mkumbo huo huo na kutaka sheria zao dini zisimamiwe na serikali?
Halafu kitu kingine sikielewi kabisa…unasema mmekuwa mnafuatilia kuhusu uanzishwaji wa mahakama ya kadhi kwa sababu sheria zenu za mirathi ,ndoa nk zinapingana na zile za serikali lakini wakati huhuo unasema kikwete alikosea kuwaahidi waislam mahakama ya kadhi kwenye uchaguzi 2005 na 2010. Sasa hapa sijui kama asingewaahidi kitu chochote ndiyo mngekuwa mmetulia tu hamdai tena au….?
Halafu wengi wenu hamuitambui BAKWATA , mnasema ni kama vile chombo cha serikali ……..Ila mnadhani kama Kadhi ikisimamiwa na serikali itakuwa chombo cha waislam wote.Yeah BAKWATA na Kadhi ni vitu viwili tofauti lakini mimi naona ni confusion tu.
Mkuu ngoja niwaache mparurane …mimi imetosha!
Thank U nashukuru sana unapokuja na swali lenye msingi mzuri na sii matusi yako nayoyasoma humu ukitukana waislaam kwa kuzaana kama wanyama na kadhalika..Yaani unajiona keki kama redneck with white supremacy au niseme Christian supremacy!

Kwanza lazima ufahamu kwamba serikali yetu haina dini na kama haina dini serikali haiwezi kuweka mkataba na dini moja ikaacha dini nyingine kwa sababu ati hawajaomba. hapo unaondoa tayari sababu ya kuwa na sheria moja au sio?.. Sasa nimesema toka mwanzo binafsi siafiki Mahakama ya kadhi na hao waislaam wameomba mahakama ya kadhi kwa sababu ndio mfumo wa serikali yetu kila dini iombe kama wakristu walivyoomba Mkataba na wakapewa. Ndipo walislaam nao wakaomba kwanza mahakama ya kadhi, OIC, benki isiyokuwa na riba kwa sababu wenzano wakiomba hupewa!

Lakini kwa sababu swala la Waislaam ni gumu sana kukubalika (na wakristu) wakati wote wa serikali ya Mwinyi, Mkapa na hata JK kuwapa waislaam mahakama ya kadhi au OIC, CCM ikanunua muda kwa kuwapa ahadi ya UONGO..Ndio maana nikasema JK hakutakiwa kuwapa hata ahadi hiyo kwa sababu haya ni makosa juu ya makosa yanafanyika kuingiza madhehebu ya dini ktk siasa. na ndio maana nimesema Mkataba wa MoU ulikuwa makoosa na kwa uhakika unatakiwa kuvunjwa kwa sababu yote yaliyoombwa ndani ya mkataba huo ni maswala ya Kikristu kama lilivyo swala la Mahakama ya kadhi..

Pili, pengine pale nilipokuchanganya nadhani ni wakati nazungumzia sababu za Waislaam kuomba mahakama ya kadhi ni kutokana na historia ya sheria zetu hazikidhi madai ya Waislaam wengi kiasi kwamba hukumu zinazotolewa huwa ni kinyume cha mafundisho ya dini hivyo walichokitaka wao Waislaam wapewe mahakama yao. Na ukiniuliza mimi nitakwambia kwamba hakuna sababu ya kuweka mahakama ya kadhi ( ni kosa jingine) na nimewahi kulizungumzia hili hapa JF kwamba serikali inaweza kutazama sheria za kiislaam na kuzitumia pale inaposwihi kwani ndani ya sheria za ndoa serikali imezitambua ndoa zote kwa makundi yake. Ndoa ya Kikristu inatambuliwa pamoja na kwamba vows zake zinasema hawataachana hadi kifo!. Pia zipo za kiislaam, za Baniani na hata zipo ndoa za Kienyeji na Halmashauri ya jiji..

Na ukienda kuisoma katiba ktk baadhi ya sheria utakuta sheria zetu pia zimetambua ndoa hizi kwa kueleza vifungu kulingana na imani ya dini husika hivyo sioni tatizo kuongezea baadhi ya sheria ktk hukumu ya ndoa hizi ulizozitambua tofauti..ndoa inayowahusu Waislaam au hata Wakristu ktk ndoa, mirathi na kadhalika kwa sababu sheria tangulizi zimejali imani za dini. Huwezi kuamua sawa kwa mkristu anayeruhusiwa kuoa mke mmoja sawa na Muislaam au ndoa za asili zenye wake zaidi ya mmoja..Labda wewe nambie utaweza vipi kuandika sheria moja hali watu hawa wanaruhusiwa kuoa wake kwa idadi tofauti!./... sheria ipi moja ifuatwe! NAOMBA KTK MAJIBU YAKO UNIJIBU HILI KWANZA!

Kisha mara zoote nimesisitiza WATU na MAZINGIRA kuwa kioo cha utunzi wa sheria na mikakati inayoweza kuwajenga jamii hiyo hivyo hatuwezi kutumia sheria za Muingereza au Marekani ambao Uhuru wao umepatikana kupitia Ukristu na ndio maana sheria zao zimechukua sehemu kubwa ya canon law, au tukafuata Arabuni ambao asilimia 98 kama sio 100 ni waislaam tukazitumia kwetu. Tanzania ni nchi pekee yenye mgawanyiko karibu sawa wa Waumini wa Kiislaam, Kikristu na wenye dini za kiasili hivyo sheria zetu ni lazima ziwalinde wananchi wake wote ktk imani zao na sii kuegemea upande mmoja... na katika kulinda huko huwezi kupendelea upande ama kusema kila upande uwakilishe kero zao isipokuwa unatazama sheria inayoweza tumika kwa jamii nzima bila kupoteza ibada za wahusika.

Mkuu wangu jaribu kutumia akili zaidi ujnapozungumzia swala la Bakwata na Kadhi kwa sababu leo wewe mwenyewe ktk madai yako unamsifia JK ili hali huipendi CCM... sasa hapo tu unajikanyaga acha nikikuuliza kama jaji mkuu nchini naye hana tofauti na CCM?..nakuomba uelewe kwamba Bakwata ni chama kama kilivyo CCM na huwezi kunambia kina Mnauye, Makamba na Mukama wana akili sana kuwa viongozi wa CCM kuliko Jaji mkuu au huoni tofauiti baina ya jaji mkuu na CCM. Kaa tafakari kisha rudi tena na hoja yenye mshiko!

Binafsi siwaungi mkono Bakwata na siwapendi kabisa... lakini kutoipenda kwangu hakuondoi mamlaka waliyokabidhiwa na serikali kama ndicho chombo cha Waislaam. Vile vile siwapendi CCM lakini ndio chama kilichopewa dhamana ya kutuongoza chini ya kiongozi wake ni JK..Ni juzi tu Bakwata chini ya Mufti huyo Makamba wetu ameamrisha sikukuu ya Eid el Fitr isherehekewe siku ya Jumatano badala ya siku ya Jumanne na hakuna sababu zaidi ya nguvu alopewa Mufti.

Leo hii ni dunia ya kisayansi mwezi unapoonekana Mombasa bila shaka hata wakazi wa Dar na Tanzania nzima mnatakiwa kuuona na haswa ukitazama mzunguko mzima wa mwezi utafahamu karama za Mwenyezi Mungu ktk kuumba ulimwengu huu ya kwamba mzungumko wa sayari zake hauna kukisia isipokuwa unakwenda kwa vipimo na kufuata kalenda kama ilivyoainishwa ndani ya Kuran.. Usipouona mwezi wewe haina maana mwezi haupo, kuna watu wengine sehemu nyinge watauona kwa sababu mwezi upo! hukuuona pengine kutokana na mawingu, ozone layer ama sababu za mazingira na sii kwamba mwezi haukuandama..

Mwisho mkuu wangu sisi waislaam hatyuna siri kama ilivyo katika makanisa na Vatican, unaweza kuchimba na kupata undani wa Bakwata na isiwe kosa lolote isipokuwa chombo hiki kimeletwa na serikali na kinalindwa na serikali kwa sababu wapo watu waliojaribu kukivunja leo hii hawapo nasi.. Serikali inakilinda chombo hiki jkwa nguvu na sisi wengine hatufahamu sababu isipokuwa kuamini kuna mkono wa mtu.
 
Niliogopa kujibu kabla sijatazama hotuba nzima

Nimeshangaa sana kuona FORUM iliyosheheni mashabiki wa CHADEMA ambao kila kukicha hawaishi kumtukana JK matusi ya kia aina wameamua kumsifia kwa kila sifa

Kumbe alichokifanya JK ni kwenda Dom

1. Kawakandia waislam kuulizia kulikoni kuhusu MOU

2. Kawaambia wasithubutu kuomba shule kama wakristo kwani wamechelewa

3. Kawaambia kuwa alikutana na viongozi wa Kanisa (ambao walimpa hotuba ya siri juu ya mustakbali wa Nchi)

4. Na katika mambo ambayo yaliyoku(walimpa instructions ) ni hili la WAISLAM na MAHAKAMA ya KADHI

5. Amekutana na waislam kisha kawaambia kuwa serikali imekubaliana na matakwa ya viongozi wa Kanisa (kama walivyomwambia kwenye hotuba yao)

Couple of things labda JK ningemkumbusha:

A) BAKWATA ni just another NGO kama vile klabu ya Yanga, Namisado, Blackwizard, Mama na Mwana, Mtoto kwa mtoto, zoma zoma evalengicals etc


B) BAKWATA haiwakilishi maoni ya waislam wote Tanzania


C) MAJORITY ya waislam kisheria za dini ya kiislam ni HARAM kuongozwa na viongozi ambao hawana QUALIFICATION za kueleweka kama the likes of Mufti etc


D) JK asisahau kuwa kuna MISTRUST toka kwa Waislam kwa serikali ambayo in almost 50 years imekuwa ikiwakandamiza systematically waislam na haikutaka kuwasilkiliza kwa lolote mpaka Rais Mstaafu Mkapa alipoamua kulia approcah hili jambo kwa undani na kukaa nao chini na alikubali kuwa kulikuwa na uhuni uliofanywa na zealots walioposerikalini

E) Waislam HAWANA ugomvi na Kanisa wala wakristoi ila tatizo la waislam ni mfumo kristo



Waislam na hoja ya Shule:

Ni kweli Nyerere aliamua ku taifisha shule zote za kidini mwaka 1969 lakini kuna baadhi ya mambo manne makuu lazima niyaweke wazi kwa hiyo kijana aliyemwandikia JK hii speech.

1. kati ya mwaka 1961-1969 Nyerere huyo huyo ambaye JK juzi alimsifia kule Dom ndiye aliyekuwa kinara wa kupinga utaifishajiwa hizi shule za kidini na hasa za kikiristo. Hili lilitokana na ukweli kuwa waislam walikuwa nyuma sana kielimu sasa kutatua tatizo la waislam na elimu akaona bora kufanya short cut ya kutatua tatizo la waislam na Nyerere alitoa order kuwa shule za wakristo zisitaifishwe ila serikali ijenge zingine ili ziwa accommodate waislam

Kama mnataka ushahidi someni kkitabu kilichoandikwa na David Westerbud Ujamaa na Udini : A study of some aspects of society and religion in Tanzania-soma ukurasa 122.


2 Kabla ya uhuru mpaka mwaka 1969 shule zote za kanisa zilikuwa zinaitegemea serikali kipesa na hii ilithibithishwa na kauli ya Father Robinson wa TEC ambaye alisema kuwa serikali ikithubutu kutoa misaada basi hizi shule zote zitafungwa au zitakufa. Na pesa hizi ambazo wa kristo walikuwa wanapata zilitokana na KODI za waislam! Infact asilimia 66 ya bajeti ya kuendesha shule hizi ilikuwa ni grant toka serikalini.


3. Baada ya kutaifisha hizi shule za Kanisa, bado shule hizi zilikuwa zinaendelea kuendeshwa na watu wale wale! yaani effectiveness ya hii policy ya utaifishaji katika operational level was largely dependent on the goodwill ya wale wale waliokuwa wanapinga huu utafishaji kwa nguvu zote in the first place. No wonder almost 50 yrs baada ya uhuru JK, policy advisor's wake, speech writers wake na maaskofu aliokutana nao wanaona taabu kukubali na kusema wazi kuwa if anything Muslims are far worse today than Christians.

4. Kwa wanaojua historia ya Tanzania ni kuwa ukweli usiopingika ni kuwa by 1969 serikali ya Nyerere ilijaa wakristo na haikuwa na nia ya kukaa na kuangalia namna ya kutatua issues zinazohusu waislam. Baada ya hapo (KAMA ALIVYOAGIZA JK juzi kule Dodoma) waislam wakaamua kujitegemea kwa nguvu zao (japo leo wanakebewa kuwa hawana self efforts) na kuunda jumuiya yao chini ya East Africa Welfare Sosiety (EAWS) ambayo ilikuja kupigwa marufuku na Nyerere baada ya kupewa instructions na viongizi wa kanisa (Msome Sivalon 1992) na baada ya hapo Nyerere akaja kuunda chombo kinachoitwa BAKWATA mwaka 1968!


BAKWATA hii iliyoundwa na Nyerere na ambayo juzi JK kaongea nao iliundwa kwa KATIBA ya TANU na kilichoondolewa kwenye ile katiba ni neno TANU na kuingizwa BAKWATA! na viongozi wa waislam waliopinga kuundwa na Bakwata walitiwa ndani na Nyerere na kuundwa kwake ilikuwa ni kuwa onyesha waislam kuwa anajaribu kutatua matatizo yao wakati huo huo mwaka 1969 Nyerere huyo huyo aliyekuwa anapinga zoezi la kubinafsisha shule za kanisa akawa bize kuzitaifisha kama vile kupinguza ile hasira za waislam kwa kuwaonyesha kuwa hana udini na anataifisha shule za Kanisa!

MOU:

JK anasema waislam wakitaka waende na MOU yao lakini huko nyuma kasahau kuwa jumuia za kanisa zilizosign MoU ndizo zilikuwa vinara wa kupinga na kufanikiwa waislam kupata misaada toka OIC kwa kudai kuwa OIC ni jumuia ya kidini! (Tazama tamko la baraza la kanisa la Pentecostal tar 9 September 2000)


Ukweli ni kuwa baada ya kusign MoU kanisa wamekuwa wakipata misaada direct toka serikali za nje na bila kusahau personnel na hakuna aliyedai kuwa kuna udini ndani yake ambao juzi JK aliamua kuwashushua waislam.

Cha kujiuliza ni why should the churches set conditions kwenye mambo ya waislam na serikali? Je kuna kipengele gani kwenye katiba kinachowapatia wao haki zaidi ya waislam na wasio wakristo?


Je JK anavyosema waislam waende na MoU yao serikali je atatuhakikishia vipi kuwa hayatowakuta yaliyowakuta ile asisi ya MIDECE kule Mtwara?
 
Hili swala la MOU na wakristo naona bado linaonekana kama 'msaada wa wakristo' lakini mtu akiweka ukristo & uislam pembeni anaweza kupata tafsiri tofauti. Ni hivi: Serikali ya Tanzania haina uwezo (capacity & capability) ya kutoa huduma za jamii kwa watanzania wote kama inayotakikana. Kwa mfano kwenye huduma za afya, serikali haina hospotali za kutosha kila eneo la nchii hii, na wala haina uwezo wa kununua dawa za kutosha na wala hawana madaktari wa kutosha. Ziko taasisi/mashirika ya dini wanaotoa huduma na hapa wakristo kama taasisi wanatoa huduma za afya i.e hospitali ya KCMC ni ya KKKT. Na hata bila ya msaada wa serikali KKKT wana uwezo wa kuendesha KCMC. Lakini kama KKKT wangeachwa kugharamia kila kitu peke yake basi ujue mteja (mgonjwa) angetakiwa ailipie huduma anayopewa kwa gharama za juu.- very simple.

Kilichofanyika ni kwa serikali kuunganisha nguvu ili kumpunguzia gharama mgonjwa. Kwa maneno mengine MOU sio msaada kwa maana msaada ila ni subsidy ili ili kushusha gharama au kufanya humuda ya afya ipatikane kwa watu wake kirahisi. Kama ilivyo kwenye pembejeo za kilimo na hata kwenye umeme kwamba serikali inatoa ruzuku ili kufanya bei halisi isiwe juu. Na hapa serikali walikuwa na option mbili. Ama wajenge hospitali na kutoa huduma wenyewe, jambo ambalo bado ni gumu kama nilivyoeleza hapo juu, au waunganishe watumie gharama ndogo nakuunganisha nguvu na taasisi ambazo tayari zinatoa huduma hiyo. Tukumbuke hapa the ultimate goal ni kufanya huduma imfikie mwananchi regardless ni wa dini gani, kabila gani au jinsia ipi. Na hata leo hii serikali inaweza kuvunja hii MOU na bado huduma zikaendelea ila watanzania wanaopata huduma hiyo watatakiwa walipe zaidi.

Sasa kuhusu hoja kwamba kama wakristo wana MOU kwa nini waislam wasipate MOU kwenye kuendesha mahakama ya kadhi? Kwa uelewa wangu Mahakama ya kadhi ni matakwa ya kidini (kiroho) yaani utoaji wa haki kwa kutumia mafundisho ya dini ya kiislma. Kwa maneno rahisi ni sehemu ya ibada. Huduma kama hospitali sio za kiimani mtu yeyote anaweza kuugua. Wakristo wanaugua kama ambavyo waislam wanaugua. Hali kadhalika, watu wasio na dini nao wanaugua. Na huwezi kuficha maradhi, kama hukupata huduma za afya unaweza kufa na watu wengi wamekufa na bado wanaendelea kufa kwa kukosa huduma hii muhimu ya afya.

Serikali haiendeshi ibada na wala hata kikatiba hairusiwi kujikita kwenye mambo ya dini. Lakini serikali katika majukumu yake makuu ni pamoja na kuhudumia wananchi wake i.e kujenga hospotali, kununua dawa. Kwa ligha ya kiimani ni kwamba serikali haifanyi kazi za kiroho, inajishughulisha na kazi za kimwili. Na ndio maana serikali inashirikiana na taasisi ziwe za dini au zozote pale wanapotoa huduma za kimwili na sio kiroho. Hatujasiki serikali inatoa ruzuku kujenga kanisa au msikiti au temple. Na ukienda kwenye pale KCMC kwa mfano utakuta wagonjwa wa dini zote. Binafsi ndugu zangu wengi waislam wamekuwa wanapata huduma pale as far as I can remember. Na wanaenda hapo kwa sababu ya gharama nafuu. Na maisha yanaendelea bado ni waislam safi.

Mimi ningefurahi kama ningesikia serikali ime-sign MOU na hospitali ya Abdallah bin Wahid inayomilikiwa na Masjid Magharib huko Mafia, au Makete, au hata Korogwe au kwengine popote. Likes for likes. Lakini habari kwamba kama wewe unapata ruzuku za kununulia asprin basi na mimi nataka ruzuku ya kuendesha ibada yangu nadhani sio sahihi. Wakatoliki wana mahakama lakini wala huusikii maana wanajua hayo ni mambo ya watu wanaoamini katika Kanisa katoliki peke yake. Lakini MOU ni kwa ajili ya vitu kama hospitali na hizi hospitali zipo, zinaonekana kwa macho na watu wote wapagani na wanaomini kwenye hizi modern religions wanapata huduma.

Mwisho, lawama kwa Hayati Mwl Nyerere. Ni zaidi ya miaka 20 tangu Mwl Nyerere aachie ngazi na zaidi ya miaka 10 tangu kifo chake. He is not alive today sasa sijui kwa nini bado anaonekana ndio kikwazo. Hata kama mtu atasema ni mfumo, mbona wameondoa Azimio la Arusha (tena akiwa bado hai) kwa nini wasiondoe huu mfumo (kama kweli upo?). Mimi nadhani kuna mtu anawaaongoza vibaya waislam, badala ya kuwaambia namna ya kuboresha mambo yeye anawasimulia hadithi. Kuna mtoa hoja mmoja hapa alisema hii saga ni sawa na yale madai kwamba sisi ni maskini kwa sababu ya wakoloni!!!
 
Thank U nashukuru sana unapokuja na swali lenye msingi mzuri na sii matusi yako nayoyasoma humu ukitukana waislaam kwa kuzaana kama wanyama na kadhalika..Yaani unajiona keki kama redneck with white supremacy au niseme Christian supremacy!

Kwanza lazima ufahamu kwamba serikali yetu haina dini na kama haina dini serikali haiwezi kuweka mkataba na dini moja ikaacha dini nyingine kwa sababu ati hawajaomba. hapo unaondoa tayari sababu ya kuwa na sheria moja au sio?.. Sasa nimesema toka mwanzo binafsi siafiki Mahakama ya kadhi na hao waislaam wameomba mahakama ya kadhi kwa sababu ndio mfumo wa serikali yetu kila dini iombe kama wakristu walivyoomba Mkataba na wakapewa. Ndipo walislaam nao wakaomba kwanza mahakama ya kadhi, OIC, benki isiyokuwa na riba kwa sababu wenzano wakiomba hupewa!

Lakini kwa sababu ni swala la Waislaam ni gumu sana kukubalika wakati wote wa serikali ya Mwinyi, Mkapa na hata JK kuwapa waislaam mahakama ya kadhi au OIC, CCM ikanunua muda kwa kuwapa ahadi ya UONGO..Ndio maana nikasema JK hakutakiwa kuwapa hata ahadi hiyo kwa sababu haya ni makosa juu ya makosa yanafanyika kuingiza madhehebu ya dini ktk siasa. na ndio maana nimesema Mkataba wa MoU ulikuwa makoosa na kwa uhakika unatakiwa kuvunjwa kwa sababu yote yaliyoombwa ndani ya mkataba huo ni maswala ya Kikristu kama lilivyo swala la Mahakama ya kadhi..

Pili, pengine pale nilipokuchanganya nadhani ni wakati nazungumzia sababu za Waislaam kuomba mahakama ya kadhi ni kutokana na historia ya sheria zetu hazikidhi madai ya Waislaam wengi kiasi kwamba hukumu zinazotolewa huwa ni kinyume cha mafundisho ya dini hivyo walichokitaka wao Waislaam wapewe mahakama yao. Na ukiniuliza mimi nitakwambia kwamba hakuna sababu ya kuweka mahakama ya kadhi ( ni kosa jingine) na nimewahi kulizungumzia hili hapa JF kwamba serikali inaweza kutazama sheria za kiislaam na kuzitumia pale inaposwihi kwani ndani ya sheria za ndoa serikali imezitambua ndoa zote kwa makundi yake. Ndoa ya Kikristu inatambuliwa pamoja na kwamba vows zake zinasema hawataachana hadi kifo!. Pia zipo za kiislaam, za Baniani na hata zipo ndoa za Kienyeji na Halmashauri ya jiji..

Na ukienda kuisoma katiba ktk baadhi ya sheria utakuta sheria zetu pia zimetambua ndoa hizi kwa kueleza vifungu kulingana na imani ya dini husika hivyo sioni tatizo kuongezea baadhi ya sheria ktk hukumu ya ndoa hizi ulizozitambua tofauti..ndoa inayowahusu Waislaam au hata Wakristu ktk ndoa, mirathi na kadhalika kwa sababu sheria tangulizi zimejali imani za dini. Huwezi kuamua sawa kwa mkristu anayeruhusiwa kuoa mke mmoja sawa na Muislaam au ndoa za asili zenye wake zaidi ya mmoja..Labda wewe nambie utaweza vipi kuandika sheria moja hali watu hawa wanaruhusiwa kuoa wake kwa idadi tofauti!./... sheria ipi moja ifuatwe! NAOMBA KTK MAJIBU YAKO UNIJIBU HILI KWANZA!

Kisha mara zoote nimesisitiza WATU na MAZINGIRA kuwa kioo cha utunzi wa sheria na mikakati inayoweza kuwajenga jamii hiyo hivyo hatuwezi kutumia sheria za Muingereza au Marekani ambao Uhuru wao umepatikana kupitia Ukristu na ndio maana sheria zao zimechukua sehemu kubwa ya canon law, au tukafuata Arabuni ambao asilimia 98 kama sio 100 ni waislaam tukazitumia kwetu. Tanzania ni nchi pekee yenye mgawanyiko karibu sawa wa Waumini wa Kiislaam, Kikristu na wenye dini za kiasili hivyo sheria zetu ni lazima ziwalinde wananchi wake wote ktk imani zao na sii kuegemea upande mmoja... na katika kulinda huko huwezi kupendelea upande ama kusema kila upande uwakilishe kero zao isipokuwa unatazama sheria inayoweza tumika kwa jamii nzima bila kupoteza ibada za wahusika.

Mkuu wangu jaribu kutumia akili zaidi ujnapozungumzia swala la Bakwata na Kadhi kwa sababu leo wewe mwenyewe ktk madai yako unamsifia JK ili hali huipendi CCM... sasa hapo tu unajikanyaga acha nikikuuliza kama jaji mkuu nchini naye hana tofauti na CCM?..nakuomba uelewe kwamba Bakwata ni chama kama kilivyo CCM na huwezi kunambia kina Mnauye, Makamba na Mukama wana akili sana kuwa viongozi wa CCM kuliko Jaji mkuu au huoni tofauiti baina ya jaji mkuu na CCM. Kaa tafakari kisha rudi tena na hoja yenye mshiko!

Binafsi siwaungi mkono Bakwata na siwapendi kabisa... lakini kutoipenda kwangu hakuondoi mamlaka waliyokabidhiwa na serikali kama ndicho chombo cha Waislaam. Vile vile siwapendi CCM lakini ndio chama kilichopewa dhamana ya kutuongoza chini ya kiongozi wake ni JK..Ni juzi tu Bakwata chini ya Mufti huyo Makamba wetu ameamrisha sikukuu ya Eid el Fitr isherehekewe siku ya Jumatano badala ya siku ya Jumanne na hakuna sababu zaidi ya nguvu alopewa Mufti.

Leo hii ni dunia ya kisayansi mwezi unapoonekana Mombasa bila shaka hata wakazi wa Dar na Tanzania nzima mnatakiwa kuuona na haswa ukitazama mzunguko mzima wa mwezi utafahamu karama za Mwenyezi Mungu ktk kuumba ulimwengu huu ya kwamba mzungumko wa sayari zake hauna kukisia isipokuwa unakwenda kwa vipimo na kufuata kalenda kama ilivyoainishwa ndani ya Kuran.. Usipouona mwezi wewe haina maana mwezi haupo, kuna watu wengine sehemu nyinge watauona kwa sababu mwezi upo! hukuuona pengine kutokana na mawingu, ozone layer ama sababu za mazingira na sii kwamba mwezi haukuandama..

Mwisho mkuu wangu sisi waislaam hatyuna siri kama ilivyo katika makanisa na Vatican, unaweza kuchimba na kupata undani wa Bakwata na isiwe kosa lolote isipokuwa chombo hiki kimeletwa na serikali na kinalindwa na serikali kwa sababu wapo watu waliojaribu kukivunja leo hii hawapo nasi.. Serikali inakilinda chombo hiki jkwa nguvu na sisi wengine hatufahamu sababu isipokuwa kuamini kuna mkono wa mtu.
Ndugu yanga Mkandara, mimi naona bado unazidi kunichanganya tu maana na madai mengine tena yanaanza kuongezeka. Mimi naona nyinyi waislam hata mkipewa kitu mtabadilisha madai na kudai tena ..na kudai na kudai tena na tena. Siwaelewi kabisa.
Unasema wakristu walipoomba mkataba walipewa kwa hiyo na nyinyi mkiomba Kadhi mpewe! Tuachane na Kadhi kwanza twende kwenye MoU.

Kikwete aliwauliza mashehe pale Dodoma kama waliomba mkataba(MoU) halafu wakanyimwa.. Aliwaambia wasilalamike kama hawajaomba na kama wameomba wakanyimwa wapeleke madai yao kwenye vyombo husika yatashughulikiwa. Kikwete anaona MoU ya wakristu na serikali ni kitu kizuri na anawashauri waislamu wenzake wafuate huo mfano lakini waislam hamtaki. Sasa sijui mnataka nini?. Kila kitu kifanywe na serikali ndiyo kutakuwa na usawa? Kwani hizo shule, vyuo , mahospitali , visima n.k vinahudumia wakristu tu? Mbona vinahudumia watu wote bila ubaguzi wa dini!

Mimi naona kwamba tatizo lenu waislam ni mmejikita sana kwenye kuendeleza imani ya kiislam lakini siyo kwenye mambo mengine ya maendeleo nje ya imani kama shule, vyuo nk. Ni kwamba hakuna balance kati ya mambo ya kiimani na shughuli za maendeleo kama vile kwa wakristu. Ndiyo maana kila kitu mnataka kifanywe na serikali.
Unakumbuka haya maneno ya Kikwete “Believe in being part of the solution” ..wakati unapinga maandamano marekani? Kwa nini mpaka leo hii mmekosa initiative ya kufanya kitu ambacho wakristu wamefanya miaka karibu 20 iliyopita?mnabaki kulalamika tu.

Kuhusu Mahakama ya Kadhi mkuu , mimi msimamo wangu ni uleule kama wa Kikwete.
Naomba wana JF wajaribu kuitafuta ripoti ya hiyo tume iliyopendekeza mahakama ya kadhi ifanywe na waislam wenyewe. Hii tume iliongozwa na muislam bingwa wa sheria za kiislam kwa hiyo inaweza ikawa na mambo mazuri tu ambayo sisi labda hatuyajui mpaka sasa.

Mkuu narudia tena..ILE HOTUBA YA KIKWETE ILIKUWA NJEMA …na kwa kusema hivyo haimaanishi ninamshangilia na kusahau uchovu na udhaifu wake. Stance yangu bado haijabadilika.

Mkuu mimi sibandiki post tena hapa maana naona na argue na watu ambao mindset zao zimekaa kivingine na hawataki kufunguka na kuona ukweli. Kwa heri!
 
Hata kama hatukubaliani na Kikwete kuna ukweli mwingi kuhusu aliyosema.

1. Kadhi ni swala la waislamu pekee na watu wa dini nyingine haliwahusu. Kama waislamu wanaamua kufanya mahakama yao basi ni lazima wakubali wenyewe na isiwe sheria za nchi kwani nchi yetu ina dini mbalimbali. Vilevile Tanzania kuna uhuru wa kidini lakini tunafata katiba kwa mahakama hivyo kama sheria za kidini zibakie kwenye misikiti.

Vilevile hakuna Mtanzania anatakiwa kulazimishwa kufuata hizo sheria hata kama ni mwislamu ni lazima akubali kutumia hizo mahakama za dini. Mfano mimi ni mkatoliki lakini hatuwezi kuanzisha mahakama yakufuata sheria ya kikatoliki halafu ikawa ya nchi nzima kwani Tanzania ni nchi yenye dini tofauti.

Kitu ambacho kila mtu anaweza kufuata ni mahakama za sasa za chini ya katiba lakini dini ziwe za dini. Wakatoliki wa wakistro kwa mfano wanaenda kujadili na mapadre na wachungaji matatitizo ya ndoa lakini ni kwa hiani yao na serikali haihusiki kwa hilo. Vilevile kama mtu anaona hatendewi haki anaweza kwenda kwenye mahakama ya kawaida.

Ndoa vilevile ni mfano mwingine zinafungwa makanisani na misikitini lakini vilevile unaweza kufuta sheria na kufunga ndoa kiserikali na kufuata taratibu za kisheria na katiba.

2. Kuhusu elimu sijui kama Waislaamu wananyimwa na vilevile ni lazima tuwe wakweli ili uweze kupata hii misaada ya vyuo na shule ni lazima ufikie kiwango fulani cha standard. Mimi siamini kama Agha Khan university itanyimwa pesa kama wakianzisha chuo! kwani ni chombo cha dini ya kiislam lakini wana fiki kiwango cha juu kabisa kwenye shule na hata chuo watakachofungua.

Lakini ukweli ni kwamba kuna shule nyingi sana za kiislaamu ambazo zinafelisha watoto kila siku! na bado ziko wazi wakati huohuo Agha Khan watu wanagombea kuingia bila kujali dini kwasababu wana kiwango cha juu.

Vyuo vyote vya dini ni lazima vipewe pesa au grants kutokana na kufia kiwango kilichowekwa kwani bila kufanya hivyo Tanzania itakuwa inarudisha nyuma watoto wetu. Hakuna sababu yeyote ya mtoto yeyote Tanzania kupewa elimu duni! bila kujali dini

Ndugu zetu Waislaamu mimi ningeshauri waache kulaumu kila jambo na kusimama pamoja kuimarisha elimu. Kuna shule nyingi tu za kiislaamu za sekondari zinazofanya vibaya sana lakini sijawahi kusikia malalamiko wakati shule zinatoa Div 4 na 0 kila siku!

Bado tunaruhusu watoto waende kwenye shule ambazo zinafelisha kila mwaka nenda rudi!.Agha Khan ni mfano mzuri wa shule iliyoanzishwa kwa dini lakini tunaona watu wanavyokimbilia kuanzia shule, hospitali na hata ukumbi wa diamond!.


Nitajie sheria za kikatoliki ni zipi, na kama hazipo kwenye katiba na sheria zingine za nchi.
 
Nitajie sheria za kikatoliki ni zipi, na kama hazipo kwenye katiba na sheria zingine za nchi.


Loh! Unaingia kwenye anga zingine. Full text ya sheria za Kanisa Katoliki hizi hapa: Code of Canon Law

Niruhusu ninukuu kipengele kimoja tu kuhusu (ndoa) talaka:


CASES OF SEPARATION OF SPOUSES

Can. 1692 §1. Unless other provision is legitimately made in particular places, a decree of the diocesan bishop or a judicial sentence can decide the personal separation of baptized spouses according to the norm of the following canons.

§2. Where an ecclesiastical decision has no civil effects or if a civil sentence is not contrary to divine law, the bishop of the diocese of the residence of the spouses, after having weighed the special circumstances, can grant permission to approach the civil forum.

§3. If a case concerns only the merely civil effects of marriage, the judge, after having observed the prescript of §2, is to try to defer the case to the civil forum from the start.

Can. 1693 §1. Unless a party or the promoter of justice requests the ordinary contentious process, the oral contentious process is to be used.

§2. If the ordinary contentious process has been used and an appeal is proposed, the tribunal of second grade, observing what is required, is to proceed according to the norm of ⇒ can. 1682, §2.

Can. 1694 The prescripts of ⇒ can. 1673 are to be observed in what pertains to the competence of the tribunal.

Can. 1695 Before accepting the case and whenever there is hope of a favorable outcome, the judge is to use pastoral means to reconcile the spouses and persuade them to restore conjugal living.

Can. 1696 Cases concerning the separation of spouses also pertain to the public good; therefore the promoter of justice must always take part in them according to the norm of ⇒ can. 1433.

Hebu onesha ni kwa vipi serikali za nchi zinatakiwa kuhusishwa kwenye implementation ya hiyo sheria ya talaka. Kila kitu ni huko huko kanisani na asiye mkatoliki wala hatakaa ajue kwamba kuna sheria kama hiyo - kwa ufupi haiwahusu wasio wakatoliki.

Hebu na wewe tuwekee za kwenu isije kuwa mnataka kukata watu vichwa au kutupiga kwa mawe. Kwa ajenda za ajabu, hamuaminiki nyie watu.
 
mbona hamuulizi MIDECE walifanyiwa nini kule Mtwara?

Its easy kusimama majukwaani na kuwaambia waislama wandae MoU zao huku tunajua fika kuwa yaliowakuta MIDECE walipotaka kufanya hivyo kule Mtwara
 
Ndugu yanga Mkandara, mimi naona bado unazidi kunichanganya tu maana na madai mengine tena yanaanza kuongezeka. Mimi naona nyinyi waislam hata mkipewa kitu mtabadilisha madai na kudai tena ..na kudai na kudai tena na tena. Siwaelewi kabisa.
Unasema wakristu walipoomba mkataba walipewa kwa hiyo na nyinyi mkiomba Kadhi mpewe! Tuachane na Kadhi kwanza twende kwenye MoU.

Kikwete aliwauliza mashehe pale Dodoma kama waliomba mkataba(MoU) halafu wakanyimwa.. Aliwaambia wasilalamike kama hawajaomba na kama wameomba wakanyimwa wapeleke madai yao kwenye vyombo husika yatashughulikiwa. Kikwete anaona MoU ya wakristu na serikali ni kitu kizuri na anawashauri waislamu wenzake wafuate huo mfano lakini waislam hamtaki. Sasa sijui mnataka nini?. Kila kitu kifanywe na serikali ndiyo kutakuwa na usawa? Kwani hizo shule, vyuo , mahospitali , visima n.k vinahudumia wakristu tu? Mbona vinahudumia watu wote bila ubaguzi wa dini!

Mimi naona kwamba tatizo lenu waislam ni mmejikita sana kwenye kuendeleza imani ya kiislam lakini siyo kwenye mambo mengine ya maendeleo nje ya imani kama shule, vyuo nk. Ni kwamba hakuna balance kati ya mambo ya kiimani na shughuli za maendeleo kama vile kwa wakristu. Ndiyo maana kila kitu mnataka kifanywe na serikali.
Unakumbuka haya maneno ya Kikwete "Believe in being part of the solution" ..wakati unapinga maandamano marekani? Kwa nini mpaka leo hii mmekosa initiative ya kufanya kitu ambacho wakristu wamefanya miaka karibu 20 iliyopita?mnabaki kulalamika tu.

Kuhusu Mahakama ya Kadhi mkuu , mimi msimamo wangu ni uleule kama wa Kikwete.
Naomba wana JF wajaribu kuitafuta ripoti ya hiyo tume iliyopendekeza mahakama ya kadhi ifanywe na waislam wenyewe. Hii tume iliongozwa na muislam bingwa wa sheria za kiislam kwa hiyo inaweza ikawa na mambo mazuri tu ambayo sisi labda hatuyajui mpaka sasa.

Mkuu narudia tena..ILE HOTUBA YA KIKWETE ILIKUWA NJEMA …na kwa kusema hivyo haimaanishi ninamshangilia na kusahau uchovu na udhaifu wake. Stance yangu bado haijabadilika.

Mkuu mimi sibandiki post tena hapa maana naona na argue na watu ambao mindset zao zimekaa kivingine na hawataki kufunguka na kuona ukweli. Kwa heri!
Sweke,
Mkuu wangu mimi nilidhani nyie wakristu ni wasomi wazuri kumbe wagumu sana wa kuelewa!... mbona nimeeleza kila kitu tena kwa kirefu na inachosha hata kusoma bado hunielewi?..

Nitarudia tena kwa utaratibu..

1. Serikali yetu ambayo haina dini haitakiwi kuegemea upande wowote! - niko sawa?
2. Serikali iliingia mkataba na kanisa ktk mkataba wa MoU - hili ni kosa la kuvunja kanuni ya kwanza - Sawa!
3. Kwa maana hii policy ya serikali inatoa fursa kwa vyombo vya dini kuingia mkataba na serikali kuhusiana na maswala yanayozihusu dini husika.
4. Bakwata na Waislaam kwa kuelewa uwepo wa policy hii nao wakaomba mahakama ya kadhi na OiC - Wakanyimwa!
5. Wakatoa mfano wa Mkataba wa MoU, jibu lake wao hawajaomba mkataba kama wa MoU, meaning - Waislaam wanatakiwa kuomba kile kilichoombwa na Wakristu tu kama kero zao na sii wao kuja na kero zao tofauti...

Kwa hiyo nachozungumza mimi ni kuwepo makosa ktk mfumo wa serikali kiutawala (Sera - Policy) ambazo CCM wanashirikiana na kanisa Katoliki kuondoa kero zao (mfumo kristo) lakini sii kwa Waislaam na madhehebu mengine. Na kero zetu haziwezi kufanana na zenu kutokana na imani na muundo tofauti ya dini hizi. Halafu unaposema shule za wakristu zinahudumia watu wote - This is cheap bro! haya ni makosa bado kwa sababu zilipokuwa chini ya serikali zilikuwa zikihudumia pia watu wote, kwa nini zilirudishwa mikononi mwa kanisa? wewe nipe sababu ya kurudishwa mikononi mwa Kanisa kwa sababu sii kweli serikali ilishindwa kuziendesha, sisi wote tulisoma shule hizo na watoto wetu wamesoma shule hizo iweje leo serikali ilishindwa kuziendesha itumie kodi zetu kuyasaidia makanisa kuendesha shule hizo hizo...

Privatization ni Ufisadi unaofanyika nchini, kwani Elimu na Afya ni investment isiyokuwa na gharama kubwa sana.. ni vitu vidogo lakini muhimu na endelevu kwa jamii ambavyo vinaweza kushughulikiwa (hudumiwa) na serikali - Tazama sera na ilani za Chadema! It's only CCM members wanaamini it's impossible. Leo shule za makanisa ni ghali kuliko hata private schools za watu binafsi hali wanapewa ruzuku za walipa kodi kuziendesha bado unashangaa ati kwa nini Waislaam hawakufanya kama nyie?. Operation KCMC ni ghali kuliko kupeleka mgonjwa India!.. acha hizo habari za upambaji wa FJM utafikiri advocate wa Kanisa kutazama upande mmoja wa shilingi. Tunazubngumza hapa kama Watanzania na sii Wakristu vs waislaam..

Swali kubwa la wakristu na mahakama ya kadhi ni serikali kutumia kodi zetu lakini wanashindwa kuelewa kwamba hata katika Muafaka wao wa MoU serikali inatumia kodi zetu kuendesha shule hizo. Kumbuka sisi wote hapa tulilalamika kuhusu mkataba wa serikali na shirika la India kuendesha shirika la reli - TRA au IPPTL ambapo serikali ndiyo inalipa mishahara na gharama zote za maitanance (ukarabati) ili hali hao RITES wana asilimia kubwa ya shareholder bila kuingiza mtaji ktk ushirika wao..Kwa hiyo, hatuwezi kusema serikali haina makosa kwa sababu reli inawahudumia watu wote na sio Wahindi pekee isipokuwa mkataba wakie ndio mbovu na haukutakiwa...

Again nachosema mimi sii kuwalaumu Wakristo sijui Wakristu, isipokuwa serikali ya CCM ambayo inaingia mkataba na taasisi za dini jambo ambalo linafungua milango kwa madhehebu mengine kutaka wapewe fursa kama hizo kinyume cha muundo wa katiba yetu ambayo inaitaka serikali kutojihusisha na maswala ya ibada isipokuwa policy yake inatoa fursa sawa kwa madhehebu yote ya dini kuendesha ibada zao.
Halafu mkuu wangu kwa nini unatazama vitu kwa sura ya Kikristu?.. sii lazima waislaam kuanzisha shule na zahanati hii sio kazi ya dini (imani ya roho) ni kazi ya serikali. Muundo wa kikristu ktk dini ni wa kibiashara wakati Uislaam dini haiwezi kuingiliana na serikali ktk maendeleo yake. Ya Kaizali tunamwachia Kaizali lakini siku hizi Ukristu hakuna cha Kaizali wala kanisa mnafanya vyote na ndio tofauti ya Uislaam na Ukristu wa leo..

halafu naona kaa unachanganya vitu vile, hutenganishi vitu kuhusiana na Sera - Policy ( serikali) tofauti na Sheria - Law (mahakama). Kwa sababu napozungumzia hukumu za maswala ya wananchi waumini wa dini nazungumzia SHERIA (law) inayotoa hukumu kulingana na kesi yenyewe. Muislaam atakuhumiwa kutokana na mkataba wa ndoa yake ya kiislaam na Mkristu atahukumiwa kesi yake kutokana na mkataba wake wa ndoa ya Kikristu (Watu na Mazingira). Wewe unalichukua hili toka mahakamani na kulipeleka sawa na muundo wa serikali ktk sera zake..

Huwezi kuwa na sheria moja ktk kesi za madai ya ndoa na mirathi ikiwa Mkristu haruhusiwi kuoa mke zaidi ya mmoja, ili hali Muislaam na waumini wa kiasili wanaruhusiwa kisheria kuoa wake zaidi ya mmoja.. Mke wa pili wa Muislaam/Asilia akiachika ktk ndoa utaweka sheria gani ambao itakuwa sawa na ya Mkristu ambaye haruhusiwi kuoa mke wa pili?.. Nilikuuliza ni sheria gani moja itumike? - HUKUNIJIBU - HUJANIJIBU na HUTANIJIBU.
 
@Mkandara, naomba nitoe mchango kwa uelewa wangu.

1. Serikali yetu ambayo haina dini haitakiwi kuegemea upande wowote! - niko sawa? - Sawa kabisa

2. Serikali iliingia mkataba na kanisa ktk mkataba wa MoU - hili ni kosa la kuvunja kanuni ya kwanza - Sawa! - Hapana, maelezo yangu No. 3

3. Kwa maana hii policy ya serikali inatoa fursa kwa vyombo vya dini kuingia mkataba na serikali kuhusiana na maswala yanayozihusu dini husika. - MOU kwa mambo ambayo ni 'exclusive ya dini' - hapana. Mambo ya jamii yooooote yanaruhusiwa, kama KCMC na Bugando Hospital.

4. Bakwata na Waislaam kwa kuelewa uwepo wa policy hii nao wakaomba mahakama ya kadhi na OiC - Wakanyimwa! - Bakwata (au mtu toka Bakwata) na waislam walielewa sivyo. Policy ya serikali ni kushirikiana na taasisi mbalimbali zikiwemo za dini katika kutoa huduma za jamiii. Mahakama ya kadhi ni matakwa ya ibada kama ilivyo mahakama ya wakatoliki. Shule, kisima cha maji, hospitali inahudumia watu wooote na serikali inatakiwa itoe huduma hii kwa wananchi wake hata kama hawana dini. Kitu kikubwa cha kuelewa hapa ni mahitaji ya kiimani (ibada) au mahitaji ya kidunia. Na nakubaliana na wewe kuwa serikali isijiingize kwenye mambo ya dini kama ilivyowekwa kwenye katiba, na ndio maana mahakama ya wakatoliki inagharamiwa na sadaka (sadaka) za wakatoliki.

5. Wakatoa mfano wa Mkataba wa MoU, jibu lake wao hawajaomba meaning - Waislaam wanatakiwa kuomba kile kilichoombwa na Wakristu kama kero zao na sii wao kuja na kero zao. Partly right. Pia copy & paste inaruhusiwa lakini cha muhimu ni kujua framework ya hii policy anayosema Rais Kikwete kwamba ni mambo ya jamii na sio ya dini. Very easy really.

Kwa hiyo nachozungumza mimi ni kuwepo makosa ktk mfumo wa serikali kiutawala (policy) ambazo
wanashirikiana na makanisa kuondoa kero zao lakini sii kwa Waislaam kwa sababu kero zetu haziwezi kufanana kutokana na miundo tofauti ya dini hizi.

Watu wote, wapagani, baniani, wakristo, waislam na watema mate wana matakwa yanayofanana: chakula, malazi, na afya bora. Unaweza kuishi vizuri kabisa bila kuwa na dini yoyote na wapo watu wengi wasio amini kuwa mungu yupo (athesist). Na pia unaweza kuishi bila mahakama ya kanisa au kadhi. Lakini huwezi kuishi bila maji au chakula. Msingi wa serikali katika hii MOU ni kwenye latter - mahitaji ya msingi ya kibinadamu. Bakwata na waislam kwa ujumla watakapoweza ku-grasp the guiding principles kwenye hili basi wataanda maombi yao kwa spirit yenye tija.

Hapo kwenye blue specifically: KCMC na Bugando hazipo kuondoka kero za wakristo. Ila zipo kuondoka kero za binadam wanaomini mungu na ambao hawaamini mungu. Sasa hivi ukienda KCMC utakuta wagonjwa wa dini tofauti. Na given the option wagonjwa wengi wangetaka waende moja kwa moja KCMC na sio Mawenzi (KCMC ni hospitali ya rufaa). Lakini kwenye mahakama ya kadhi kama mimi ni baniani na ninashauri langu kuhusu ndoa (talaka) siwezi kwenda kwenye mahakama ya kadhi! all you need to know ni basic needs za binadamu na kwa hakika mahakama ya kadhi sio basic need. Inaelekea wakristo waligundua hili mapema. Leo hii kwa taarifa yako Arusha, more than 40% ya huduma za jamii zinatolewa na kanisa (40%plus). Shule, hospitali, maji. Wakifunga virago Arusha kutakuwa mgogoro. Can you tell me ni kijiji kipi waislam ndio wanaongoza kutoa huduma kuu muhimu za jamii? Ukitazama kwa undani hili jambo Mkandara ni kama kuna u-selfish fulani hivi. Kwamba Wakristo wanaomba msaada kutoa huduma kwa watu wa dini zote lakini waislam wao wanataka msaada kwa mambo yao tu! Incredible!

Halafu unaposema shule za wakristu zinahudumia watu wote haya ni makosa bado kwa sababu zilipokuwa chini ya serikali zilikuwa zikihudumia pia watu wote na kwa nini zilirudishwa mikononi mwa kanisa?
Serikali ilikuwa inashindwa kama ambavyo ilivyoshindwa kuendesha JKT hili wala halina ubishi. tofauti ni kuwa hakukuwa na mtu au taasisi ya kusaidia JKT kama ambavyo kanisa lilikuwa tayari kusaidia kwenye elimu. Hivi kile chuo kikuu cha Morogoro kingekuwa kimepewa wakristo hii nchi ingekalika kweli? Na mbali na chuo kikuu cha morogoro ni viko wapi vyuo vikuu vingine chini ya BAKWATA? Ni hivi karibuni tu kulikuwa na harambee ya KKKT ya kujenga chuo kikuu mwenge!

Kumbuka sisi wote hapa tulilalamika kuhusu mkataba wa serikali na shirika la India kuendesha shirika la reli - TRA au IPPTL ambapo serikali ndiyo inalipa mishahara na gharama zote za maitanance (ukarabati) ili hali hao RITES wana asilimia kubwa ya shareholder bila kuingiza mtaji ktk ushirika wao..Kwa hiyo, hatuwezi kusema serikali haina makosa kwa sababu reli inawahudumia watu wote na sio Wahindi pekee isipokuwa mkataba wakie ndio mbovu na haukutakiwa...
Did RITES perform? Hicho ndicho kiini cha matatizo. Kama RITES wangefanya vizuri kama ambavyo tulikuwa tumeambiwa sidhani kama wananchi wangelalamika. Lakini ujio wa RITES was hell kwa watumiaji wa treni hasa kwenda bara. Na serikali iliingilia kati ikifikiri RITES management walikuwa wanahitaji a bit of help lakini pamoja na msaada wa serikali bado RITES waliendelea kuwa na bad performance. Mbeleko ikakatika!

Again nachosema mimi sii kuwalaumu Wakristo sijui Wakristu, isipokuwa serikali ya CCM ambayo inaingia mkataba na taasisi za dini jambo ambalo linafungua milango kwa madhehebu mengine kutaka wapewe fursa kama hizo kinyume cha muundo wa katiba yetu ambayo inaitaka serikali kutojihusisha na maswala ya ibada isipokuwa policy yake inatoa fursa sawa kwa madhehebu yote ya dini kuendesha ibada zao.
Mimi nadhani serikali imefikiria vema kwenye haya mambo ya MOU. Nategemea kusoma . Abadallah bin Wahid Hospital...coming soon near you! courtsey of Masjid Magharib & the United Republic of Tanzania:)

Now Mkandara, I must admit that this is my favourite part. ON THE GREEN.
sii lazima waislaam kuanzisha shule na zahanati hii sio kazi ya dini (imani ya roho) ni kazi ya serikali. Muundo wa kikristu ktk dini ni wa kibiashara wakati Uislaam dini haiwezi kuingiliana na serikali ktk maendeleo yake. Ya Kaizali tunamwachia Kaizali lakini siku hizi Ukristu hakuna cha Kaizali wala kanisa mnafanya vyote na ndio tofauti ya Uislaam na Ukristu wa leo..
Mkandara between me & you sadaka zenu mnapeleka wapi? Hivi OIC ilikuwa ni mahesabu ya kulipia bili zenu au?
Lakini swali kubwa ambalo nataka unijibu ni hili waislam wa Tanzania wanaujua uislam kuliko Iran, Saudi Arabia, UAE, Malaysia na Pakistan? Kama hoja yako itakubalika kuwa waislam hawajakaa kibiashara kama wakristo sasa inabidi ueleze OIC wao wamepataje hela? Allah anatuma ndege moja kwa moja kwao zikiwa zimejaa maburungutu ya noti au inakuwaje. And dont tell me hizo nchi zina mafuta na maana ili mafuta yawe na manufaa someone has to transact something right?

Mimi nashauri Mkandara angalieni upya mfumo wa sadaka!
 
FJM,
Mkuu wangu katika majibu yako yote, naomba ibara au kifungu cha sheria kinayoruhusu uliyoyasema.
Halafu unazungumzia mambo ya Sadaka, hivi wewe kinachofanyika kanisani ndio unataka kifanyike Msikitini?.. sadaka zetu zinakwenda kwa maskini watu wasiojiweza na sio kuendesha shule na zahanati, mkuu kila dini ina mpango wake na haya ni maswala yanatanguliwa na imani ya kiroho unapohusisha makanisa au misikiti .. again kwa mfano wako Ndoa na urithi sio swala la kiroho ila la swala la jamii.. Mimi siwezi kukuuliza wewe mshahara wako unakwenda wapi - Hii akili kweli mkuu wangu?..kwani wewe mipango yako iwe sawa na yangu kwa sababu tu sote ni binadamu au mimi nimefanikiwa ktk swala fulani basi lazima nawe ufuate yangu!.. mbona mnachosha wakuu zangu ktk kufikiria kwenu.

It is wrong kwa serikali kuingia mkataba na Kanisa hakuna sababu yeyote inayoweza kuhalalisha hili..CCM ilikiua chombo cha kiislaam kwa sababu hizo hizo na sheria kuundwa ktk Azimio la Arusha, hakuna mahala popote sheria ile imerekebishwa kukidhi ama kuwapa wakristu ruzuku na kodi za wananchi pasipo ridhaa zao - HAKUNA - Ubinafsishaji hautoi nafasi ya makanisa kupewa ruzuku ya kodi zetu kwa sababu ati zinahudumia watu wote.Kwani hayo mashirika mengine au taasisi ktk private sectors hawahudumii watu wote! Serikali ilishindwa kwa sababu sera zake ni mbovu na mbaya haihusiani kabisa na sababu zilizopelekea shule zile kurudishwa kwa makanisa na wapewe ruzuku toka kodi zetu. Ni mpango maalum unaolalamikiwa kuwa mfumo kristo!
Wee nionyesha mahala panaposema hivyo tumalize mzozo huu.
 
Endeleeni kutofautiana, ila tu msisahau kuwa kuna mwisho unaoutuhitaji twende muelekeo mmoja kwa maslahi ya Jamii yetu.
Mkimaliza mtuambia
 
Back
Top Bottom