Mkodoleaji
JF-Expert Member
- Apr 27, 2008
- 458
- 138
Nimesoma kwenye magazeti na kusikiliza kwenye vyombo vya habari. Kwa kweli wengi wamemsifia kwamba ametoa hotuba nzuri. Lakini mimi kwa kweli nimekuwa na mtazamo tofauti. Naomba niseme wazi kwamba Raisi Kikwete amekuwa mean with the truth kwenye hii hotuba yake. Kwanza kwenye suala la Mahakama ya Kadhi, ni yeye na CCM yake ambao waliwaahidi waislamu mwaka 2005 kuwa watalipatia ufumbuzi.
Sasa kwa waislamu wengi ufumbuzi ilikuwa serikali itaanzisha hiyo Mahakama. Lakini cha ajabu nadhani mwaka 2008, Kikwete huyo huyo mbele ya Maaskofu wa KKKT alikanusha kuhusika na suala la mahakama ya kadhi. Akasema lilianzishwa na Mrema na Sheikh Ramia. Kwa maana nyingine yeye asiulizwe.
Leo anasema kuwa ni suala la waislamu wenyewe lakini hapo hapo anakiri kuwa Waziri Mkuu anaratibu. Waziri Mkuu ataratibu vipi suala la ibada. Kwangu mimi nadhani Kikwete angekiri walipoteleza na kueleza kuwa walifanya makosa kuingiza suala la dini kwenye siasa.
Suala la pili ni kuhusu suala la MOU ambapo waislamu wamelalamika kuwa wakristo wanapewa fursa zaidi. Kikwete amesema kwa sababu wao hawaombi. Hapa kwa kweli panatia shaka. Kikwete kama mara mbili akiwa kwenye mikutano na viongozi wakristo alinukuliwa akitoa takwimu kuonyesha pesa ambazo taasisi za kikristo wamepata kutoka serikalini.
Hivi alishindwa nini kutoa takwimu kuonyesha ni kiasi gani taasisi za kiislamu zinapokea kutoa serikalini? Kwa nini hakutoa hata mfano kuwa Muslim University kilitolewa na serikali? Je pia alishindwa kuonyesha kuwa hizo shule za makanisa kama zinazuia kusoma watu wa dini nyingine? Na pia kwa sababu alikuwa Waziri wakati Mzee Mwinyi atakuwa anajua kwanini MOU ilisainiwa, je alishindwa nini kutoa hiyo institutional memory ili kuondoa upotoshaji unaoendelea.
Alichozalisha hapa ni kuonyesha kuwa wakristu wamekuwa wakipendelewa kwa sababu wanaomba na waislamu wamenyimwa kwa sababu hawaombi kitu ambacho nadhani si sahihi. Kama kwenye wamenyimwa serikali haitakiwi kusubiri hadi kuombwa, kwani Nyerere aliombwa na nani kutaifisha shule?
Kwa kweli kwangu nadhani ni hotuba inayopalilia udini badala ya kuumaliza.
NAWASILISHA
Sasa kwa waislamu wengi ufumbuzi ilikuwa serikali itaanzisha hiyo Mahakama. Lakini cha ajabu nadhani mwaka 2008, Kikwete huyo huyo mbele ya Maaskofu wa KKKT alikanusha kuhusika na suala la mahakama ya kadhi. Akasema lilianzishwa na Mrema na Sheikh Ramia. Kwa maana nyingine yeye asiulizwe.
Leo anasema kuwa ni suala la waislamu wenyewe lakini hapo hapo anakiri kuwa Waziri Mkuu anaratibu. Waziri Mkuu ataratibu vipi suala la ibada. Kwangu mimi nadhani Kikwete angekiri walipoteleza na kueleza kuwa walifanya makosa kuingiza suala la dini kwenye siasa.
Suala la pili ni kuhusu suala la MOU ambapo waislamu wamelalamika kuwa wakristo wanapewa fursa zaidi. Kikwete amesema kwa sababu wao hawaombi. Hapa kwa kweli panatia shaka. Kikwete kama mara mbili akiwa kwenye mikutano na viongozi wakristo alinukuliwa akitoa takwimu kuonyesha pesa ambazo taasisi za kikristo wamepata kutoka serikalini.
Hivi alishindwa nini kutoa takwimu kuonyesha ni kiasi gani taasisi za kiislamu zinapokea kutoa serikalini? Kwa nini hakutoa hata mfano kuwa Muslim University kilitolewa na serikali? Je pia alishindwa kuonyesha kuwa hizo shule za makanisa kama zinazuia kusoma watu wa dini nyingine? Na pia kwa sababu alikuwa Waziri wakati Mzee Mwinyi atakuwa anajua kwanini MOU ilisainiwa, je alishindwa nini kutoa hiyo institutional memory ili kuondoa upotoshaji unaoendelea.
Alichozalisha hapa ni kuonyesha kuwa wakristu wamekuwa wakipendelewa kwa sababu wanaomba na waislamu wamenyimwa kwa sababu hawaombi kitu ambacho nadhani si sahihi. Kama kwenye wamenyimwa serikali haitakiwi kusubiri hadi kuombwa, kwani Nyerere aliombwa na nani kutaifisha shule?
Kwa kweli kwangu nadhani ni hotuba inayopalilia udini badala ya kuumaliza.
NAWASILISHA