Mpita Njia
JF-Expert Member
- Mar 3, 2008
- 6,997
- 1,163
Nadhani Mod atarekebisha title ye thread hii
Kama tujuavyo, tulitenga shilingi bilioni moja kwa kila mkoa wa Tanzania Bara na shilingi milioni 100 kwa kila mkoa kwa mikoa minne ya Zanzibar na milioni 200 kwa mkoa wa Mjini Magharibi, Unguja. Tulikubaliana kuwa mikopo hiyo itatolewa na Benki za CRDB na NMB na asasi ndogo za fedha kama vile Benki ya Posta, PRIDE, SELF n.k.
Taarifa zinaonyesha kuwa hadi Novemba 30, 2008 jumla ya shilingi bilioni 39 zimekopeshwa na NMB (16.1bn/=) na CRDB (22.9bn/=) na watu 48,339 wamenufaika pamoja na SACCOS 192 na vikundi 137. Benki na asasi nyingine 12 zimeshakopesha SACCOS 236 na shilingi 4.6 bilioni zimetumika katika wilaya 46 za Tanzania Bara.
Mwalimu naomba unisaidie hesabu kidogo..
hesabu zangu hazipandi.. where am I messing it up?
kuna zaidi ya billion 15 haijulikani ilikotoka kwani haikuwepo kwenye kiasi kilichotengwa na pia haijulikani ni nani wamepewa si ndiyo hivyo?
otherwise walioandika hotuba wamerikoroga na Mkuu mwenyewe hana time.
Sikilizeni hotuba yake redioni, pengine dosari hiyo itakuwa imerekebishwa. Mlio ughaibuni sikilizeni RADIO MARIA mtandaoni. Kuna tetesi kuwa Radio Maria itarusha hewani live hotuba hiyo.
Mwalimu naomba unisaidie hesabu kidogo..
hesabu zangu hazipandi.. where am I messing it up?
Mwalimu naomba unisaidie hesabu kidogo..
hesabu zangu hazipandi.. where am I messing it up?
Mpaka sasa ni nyimbo za RC. Bado tumetega misikio. Thanks
MAGAZIJUTO:
Mikoa ya Tanzania Bara:
1. Dar-es-Salaam = Bilioni 1 za Bwana Fulani
2. Mwanza = Bilioni 1 za Bwana Fulani
3. Arusha = Bilioni 1 za Bwana Fulani
4. Manyara= Bilioni 1 za Bwana Fulani
5. Dodoma= Bilioni 1 za Bwana Fulani
6. Singida= Bilioni 1 za Bwana Fulani
7. Rukwa= Bilioni 1 za Bwana Fulani
8. Ruvuma= Bilioni 1 za Bwana Fulani
9. Mbeya= Bilioni 1 za Bwana Fulani
10. Pwani= Bilioni 1 za Bwana Fulani
11. Morogoro= Bilioni 1 za Bwana Fulani
12. Tanga= Bilioni 1 za Bwana Fulani
13. Kilimanjaro= Bilioni 1 za Bwana Fulani
14. Tabora= Bilioni 1 za Bwana Fulani
15. Kigoma= Bilioni 1 za Bwana Fulani
16. Mtwara= Bilioni 1 za Bwana Fulani
17. Lindi= Bilioni 1 za Bwana Fulani
18. Iringa= Bilioni 1 za Bwana Fulani
19. Shinyanga= Bilioni 1 za Bwana Fulani
Jumla = Bilioni 19 za Bwana Fulani
Salio= Bilioni 10 za ?
Kwa nini sasa Mara na Kagera hawamo kwenye mgawo?