Hotuba ya Rais Kikwete kwa watanzania mwezi Septemba 2011

.............Wakuu tuwe wazi kabisa,mbona inatia hasira? wapi mambo yafuatayo?
  1. Kupanda gharama za maisha...
  2. Kupanda kwa bei ya mafuta kila siku....
  3. Malipo ya Dowans na mikataba mengine feki...
  4. Ajali za kila siku(hili sio kificho,kila siku watu wanakufa hii nchi kwa ajali)
  5. Matatizo ya umeme yasiyokwisha....tulidanganywa kuwa mwezi wa 9 mgao utapungua,badala yake makali ndio yanaongezeka..
Yani hotuba nzima imejaa safari ya marekani wakuu,full kujisifia sifa zisizo na tija wala manufaa kwa watanzania? Ndio maana watu wengi wameacha kusoma au kusikiliza hotuba za huyu jamaa...Kuna nini hapo cha kuleta matumaini? Jamani huyu jamaa tumfanyaje?

Najutia muda wangu niliokaa kumsikiliza na kusoma hotuba hii....
Hayo mambo wakiyasema wapinzani utasikia wazushi wakati yalitakiwa kuwa addressed na rais mwenyewe ili kuondoa hisia potofu.
 
Hapooo! good night friends and may GOD bless you and your family,girl or boy friends and concubines!

The BIBLE may help to explain the presidas speech: Read Jacob 5:1-7.
 
Hotuba nzuri sana, amejitahidi kuelezea juu ya uraia wa nchi mbili kitu ambacho kimekuwa kikisumbua sana wananchi. Nadhani baada ya hii hotuba watu watakuwa wameshapata majibu ya matatizo yao mbalimbali.

Wanaoishi nje ya nchi ni watoto wa matajiri, watanzania masikini hawana maji, madawa, umeme, sukari, chakula nk. Hajagusia yote haya zaidi ya sifa za kijinga!
 
Hii siyo hotuba ya rais, nashindwa kuamini kabisa. DACOTA na uraia wa nchi mbili unawhusu watu asilimia ngapi ya wa Tanzania. Watanzania wengi sasa wanakabiliwa na matatizo mengi sana ambayo halitakiwa hayatolee maelezo.
 
Pili, niliwataka wasisahau nyumbani kwao. Wametoka huku nyumbani kwenda nje kuchuma ili wajiletee maendeleo. Wakumbuke kujenga nyumba nzuri kwao ili wawe na mahali pazuri pa kufikia. Wakati mwingine kukosa mahali pazuri pa kufikia kunawafanya wasije nyumbani au wakija waishie mjini kwa sababu nyumbani kwao hakuwafai kwa viwango vyao. Aidha, niliwataka wasaidie kuwaendeleza wazazi na ndugu zao kwa elimu au hata kwa misaada mingine ya kuwaendeleza kiuchumi na kuwapatia kipato.

Yaani hapa RAIS wa nchi Dr. Dr. Kanali JK anahutubia TAIFA!!!!!
 
Ukiangalia gharama ya safari ya JK kwenda na kurudi Marekani na haya anayowaeleza wananchi ktk "hotuba" yake inatia hasira. nakubaliana na massenberg its like a ripoti ya matukio latest na si hotuba
 
Huyo ndie kikwete raisi wa ovyo kuliko maraisi wote waliowahi kuongoza nchi hii, msanii, sharobaro, hayo aliozungumza kwa upeo wake anadhani ndio tunayotaka kusikia ushuzi mtupu.

Sasa napata picha kikwete ni mdini namba wani,ameshindwa kukemea matamshi ya bakwata dhidi ya CHADEMA?Badala yake anatoa vitisho kwakuwa anajeshi na polisi vinamlinda,kikwete unajidanganya sana.

Kama unafikiri kuna watu wanakuogopa ww ibeni kura Igunga. Kikwete co wote tunaoshindia ubwabwa na chips. Jaribu sasa uone! Tumekuchokaaaaaaaa!
 
Nawachukia wale wote wanaosema eti tunasherekea miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania/Tanzania Bara. Ni wa kuogopwa kama UKOMA.

wewe ndio wa kuogopwa kama ukoma. wewe hujui kwamba tulipata uhuru toka kwa mwingereza tokea tisa desemba 1961
 
TBC-Televisheni ya Taifa inapotoa tangazo, halifanyiki na hawatoi ufafanuzi tuwaeleweje?Sisi kama watanzania tunaihitaji sana hiyo hotuba, tena hotuba inayotoa ufafanuzi wa matatizo ya wananchi na sio kuwatuhumu watu au vyama juu ya vitu fulani.

Ndugu pambana kutafuta ufumbuzi wa matatizo yako, nani wa kutoa hotuba ya kupatia ufumbuz wa matatizo yanayoikabili nchi hii??hapo anaeleza tu jinsi alivyorandaranda huko USA, tena hajasema safari yake kwenda kukutana na 50 Cent, nadhani kasahau tu.

Tushazoea anataja yalopita badala ya kueleza mikakati ya kutukwamua kiuchumi, umeme shida, maji shida, mafuta shida, gas shida, mkaa shida, usafiri shida, msongamano shida,sukari shida, mahusiano shida, chakula shida, kipi sasa kinachotatuliwa na hii serikali mungu wangu?

Dah!! haela hakuendeki na dunia haikaliki basi ilimradi tu.
 
Hii siyo hotuba ya rais, nashindwa kuamini kabisa. DACOTA na uraia wa nchi mbili unawhusu watu asilimia ngapi ya wa Tanzania. Watanzania wengi sasa wanakabiliwa na matatizo mengi sana ambayo halitakiwa hayatolee maelezo.
Jaman mi nadhani tunakuwa wepesi mno kusahau, Rais alisha sema yeye mwenyewe hajui kwanini Tanzania ni maskin, sasa kama Rais hajui tatizo la nchi yake, mnadhani atatatua tatizo gani hapo wakati haelewi tatizo ni nini?

So tusitegemee ufumbuzi wa tatizo lolote kutoka kwa JK mana haelewi tatizo nini. Yani kimsingi anashangaa kwanini watu wake mmepigika wakati nchi ina mito inayobubujisha asali na maziwa.
 
Umeme wa uhakika utapatikana DICOTA sijui? kwenye eneo linalohusu kuchakachua na kulazimisha sifa kwa CCM wasizostahili wanakuwa wa kwanza kutolea maelezo na mikwara lakini mambo ya maana yanayomgusa kila mtanzania ya kila siku kama kutokuwa na huduma za uhakika za maji safi,umeme,kupanda kwa bei za bidhaa mbali mbali,kushuka kwa thamani ya shilingi na mambo mengine ya maana huwasikii wakiyatolea maelezo.

Nahisi dhumuni la hii hotuba ya leo ilikuwa kupiga mkwara wa Igunga basi lakini hayo mengine hayamhusu moja kwa moja Mtanzania anayeishi Kasulu,Mwembetogwa,Marangu au Loliondo.Nchi hii ina safari ndefu sana kufikia matumaini ya kweli,miaka 4 natamani iishe haraka! Hakika Mungu atatupigania na kama taifa tutatoka katika mambo haya ya sifa za kijinga jinga za tuzo na vitu visivyo na maana kabisa!

Hivi mtu wa kasulu ana matatizo kibao unamwambia uraia wa nchi mbili ili iwe nini? angeyafanya hayo kimya kimya tu basi.aaaaaaaaaaaaaaaaaah

Huna cha kusema? soma hapa kuhusu jitihada za umeme wa uhakika, ambapo hakuna Rais yoyote tangu tupate Uhuru anaejitahidi kwa dhati kutatua tatizo la umeme zaidi ya Kikwete: Home
 
Back
Top Bottom