Hotuba ya Rais Karume kwenye Sherehe za Mapinduzi Zanzibar:The Best Ever!

- Mkuu vipi hapo kweli pamekaa sawa? Mbona habari za ground zero zinasema tofauti? kwa jinsi anavyohaha!

Respect

FMEs!
Mkuu FMEs, ni kweli ndio maana nimebold 'kwa mujibu wa katiba', hiyo katiba siyo Masahafu.

Ila pia I'm an interested party naomba msaada wako kwa hizo za ground zero. Nitaku PM.
 
Uwe unasoma vizuri posts kuna mtu kasema Zanzibar haipo Zanzibar ipo kama ninavyoweza kusema Mbeya ipo, mimi nimesema hakuna kitu kinachoitwa NCHI YA ZANZIBAR mna jeshi nyie mtaitwaje nchi hata UN hamtambuliki hamna kiti kule JK anakiti chake lakini Karume hana labda akasimame, ukweli ndo huo.
Mwaka 2010 kuna uchaguzi wa Rais wa JMT. Hivi Wazanzibari (wapiga kura) kule mathalan waharibu kura zao na huyo JK awe amechaguliwa kwa kura nyingi lakini ni za upande huu wa pili (Tanganyika tu) atakwenda kukalia hicho kiti huko UN.
 
Ningependa sana nione Zanzibar inavuna mafuta yake na jinsi gani yatawafaidisha wanzanzibari ili iwe fundisho kwa serikali ya bara ya kutuuzia nchi na dhahabu yote kutokomea nayo kisha kutuachia mahaandaki na umaskini wa mwisho, hongera wazanzibari.
 
Mwaka 2010 kuna uchaguzi wa Rais wa JMT. Hivi Wazanzibari (wapiga kura) kule mathalan waharibu kura zao na huyo JK awe amechaguliwa kwa kura nyingi lakini ni za upande huu wa pili (Tanganyika tu) atakwenda kukalia hicho kiti huko UN.

Pakacha, sheria yetu ya uchaguzi, haisemi kama rais wa muungano hajachaguliwa na kura hata moja ya upande pili ndio sio rais. Kama mnaweza hebu jaribisheni. Jumbe alijaribu na kina Dourado, yaliyomkuta sote tunayajua. Mkimyima kura JK, cha moto mtakiona, mwanzo mmekuwa mkitawaliwa kwa siasa, sasa nadhani mnataka bakora mkatafute pa kulilia........................................................................................................Wasomi wazuri wa geolojia wana uthibitisho Zanzibar ilimeguka toka bara miaka milioni kadhaa iliyopita. Alipokuja Sultan Seyyid Said akaitwaa Zanzibar kama sehemu yake, mpaka leo vizalia vya waarabu vinafikiri Zanzibar mali yao na babu zao!. No, Nyerere alilijua hilo, Zanzibar ni sehemu ya muungano, tena chokochoko zikizidi, tutaigeuza Mkoa na waarabu wajirudie kwenye asili yao, tena mbona kule mafuta kibao?......................................................................................................Tanzania yetu!, Zanzibar pia yetu! Umoja ni wetuMuungano udumu milele!.
 
Mwaka 2010 kuna uchaguzi wa Rais wa JMT. Hivi Wazanzibari (wapiga kura) kule mathalan waharibu kura zao na huyo JK awe amechaguliwa kwa kura nyingi lakini ni za upande huu wa pili (Tanganyika tu) atakwenda kukalia hicho kiti huko UN.

Badala ya kusema wazanzibari waharibu kura zao, tuseme wampigie kura mtu wao na wale wapiga kura wa bara wampigie mwingine. Hivi unadhani nani atakuwa rais? Kura zenu wote hazifikii idadi ya wasukuma kwa hiyo ukweli ni kuwa katika demokrasi kama yetu, wasukuma wana umuhimu zaidi kuliko wazanzibari! Na hata kama wazanzibari wote watagoma kupiga kura bado rais atakayechaguliwa na machogo bado atakuwa legitimate na atakuwa rais wa JMT. Sasa tuseme machogo wote wagome kupiga kura na rais achaguliwe na kura za wazanzibari peke yao, unadhani ataweza kweli kujiita rais wa JMT na kuhamia Ikulu Dar es Salaam? Ndio ukweli ulivyo, mpende, msipende.

Amandla.......
 
Mwaka 2010 kuna uchaguzi wa Rais wa JMT. Hivi Wazanzibari (wapiga kura) kule mathalan waharibu kura zao na huyo JK awe amechaguliwa kwa kura nyingi lakini ni za upande huu wa pili (Tanganyika tu) atakwenda kukalia hicho kiti huko UN.

Kwani Zanzibar mko wangapi? na waliompigia kura Kikwete ni wangapi? hawafiki hata laki mbili sawa na idadi ya wapiga kura wa wilaya tu ya Shinyanga vijijini tunahitaji kura zenu ili mujione ni part ya watanzania msibaki wapweke kura za bara zinamtosha ati.
 
Kwani Zanzibar mko wangapi? na waliompigia kura Kikwete ni wangapi? hawafiki hata laki mbili sawa na idadi ya wapiga kula wa wilaya tu ya Shinyanga vijijini tunahitaji kura zenu ili mujione ni part ya watanzania msibaki wapweke kura za bara zinamtosha ati.

Eti umemaliza darasa la saba?
 
Sisi huku Zanzibar hatuna uchaguzi safari hii, Maalim Seif keshasema kama uchaguzi ufanyike baada ya miaka 2 ijayo...period!

Nyie mrudisheni tuu huyo JK apate kufanya ufisadi na muzidi kufa mafukara :D
 
Sisi huku Zanzibar hatuna uchaguzi safari hii, Maalim Seif keshasema kama uchaguzi ufanyike baada ya miaka 2 ijayo...period!

Nyie mrudisheni tuu huyo JK apate kufanya ufisadi na muzidi kufa mafukara :D
Katoa rai tu...! Ni jukumu la baraza la wawakilishi wananchi na wanachama wa vya vyote kuridhia ushauri huo, ili kuweza kubadili katiba kwa manufaa ya maridhiano.

Usijaribu kupindisha ukweli hapa....
 
Katoa rai tu...! Ni jukumu la baraza la wawakilishi wananchi na wanachama wa vya vyote kuridhia ushauri huo, ili kuweza kubadili katiba kwa manufaa ya maridhiano.

Usijaribu kupindisha ukweli hapa....

Huo ndio msimamo wa CUF kuwa uchaguzi upelekwe mbele, na iko wazi kabisa uchaguzi kwa kusimamiwa na katiba zilizopo ni kuleta vurugu tuu visiwani humo.

Kwenda kwenye uchaguzi na ZEC iliopo sasa, kutafuta mvutano mwengine.Ni jambo la busara hilo kuepuka huo uchaguzi, na kurekebisha hizo katiba.

Au unasemaje mkuu?Au huu umoja wanao hubiri hawa viumbe wawili, unatia kitumbua chako mchanga?
 
Huo ndio msimamo wa CUF kuwa uchaguzi upelekwe mbele, na iko wazi kabisa uchaguzi kwa kusimamiwa na katiba zilizopo ni kuleta vurugu tuu visiwani humo.

Kwenda kwenye uchaguzi na ZEC iliopo sasa, kutafuta mvutano mwengine.Ni jambo la busara hilo kuepuka huo uchaguzi, na kurekebisha hizo katiba.

Au unasemaje mkuu?Au huu umoja wanao hubiri hawa viumbe wawili, unatia kitumbua chako mchanga?
Kitumbua gani au kireja gani... (ta'dabu)! Umeshasema huyo ni msimamo wa CUF, awali ulitoa kauli tofauti na hiyo kwamba hakuna uchaguzi. Kumbuka kuwa Maalimu kapendekeza kuongezwa kwa muda, aidha kazi hiyo itafanywa na vyombo husika, na ni baada ya kuridhika kama kuna umuhimu huo.

Sasa unapokuja hapa na kupotosha ukweli ni kwa faida ya nani hasa? Au wewe ndio wale vidudu mtu anaowazungumzia Maalim?
 
Sisi huku Zanzibar hatuna uchaguzi safari hii, Maalim Seif keshasema kama uchaguzi ufanyike baada ya miaka 2 ijayo...period!

Nyie mrudisheni tuu huyo JK apate kufanya ufisadi na muzidi kufa mafukara :D

1. Kwani uchaguzi Zanzibar ni kwa ajili ya rais wenu peke yake na Baraza lenu la Mapinduzi.
2, Kwani Maalim ndiye CUF? Kama alivyokueleza Kibunango, ni lazima apate ridhaa ya wanachama wenzake ndiyo uamuzi huo uwe halali. Na wanachama hao wanatoka pande zote za Muungano. Au mmeishaamua kuwa CUF ni Zanzibar peke yake?
3. Ingawa pengine CCM na CUF kisheria wanaweza kufanya uamuzi juu ya hatma ya uchaguzi wao wenyewe bila kuhusisha vyama vingine vya siasa kwa kutumia wingi wao katika BMZ watafungua mlango wa kuburuzwa mahakamani kwa kuwakosesha wenzao nafasi ya kushiriki katika uchaguzi.

Amandla.......
 
Eti umemaliza darasa la saba?

[Kwani Zanzibar mko wangapi? na waliompigia kura Kikwete ni wangapi? hawafiki hata laki mbili sawa na idadi ya wapiga kula wa wilaya tu ya Shinyanga vijijini tunahitaji kura zenu ili mujione ni part ya watanzania msibaki wapweke kura za bara zinamtosha ati.]quote]


sawa mkuu nime-edit unajua sisi watu wa Mara hatuna tofati ya l na r lakini natumaini ujumbe wangu ulifika
 
Kitumbua gani au kireja gani... (ta'dabu)! Umeshasema huyo ni msimamo wa CUF, awali ulitoa kauli tofauti na hiyo kwamba hakuna uchaguzi. Kumbuka kuwa Maalimu kapendekeza kuongezwa kwa muda, aidha kazi hiyo itafanywa na vyombo husika, na ni baada ya kuridhika kama kuna umuhimu huo.

Sasa unapokuja hapa na kupotosha ukweli ni kwa faida ya nani hasa? Au wewe ndio wale vidudu mtu anaowazungumzia Maalim?

You guys got no sense of humor, thats all i can see for now.By the way you didnt provide your opinions on the subject though.Hopefully you did that on purpose, didnt you?

I wanted to hear wether you think the election in Zanzibar is more important than the so called "maridhiano/muafaka"..

P:S
**Have fun....by the way, the original post had some humor in it when I said there is no election in Zanzibar according to Seif.
 
P:S
**Have fun....by the way, the original post had some humor in it when I said there is no election in Zanzibar according to Seif.
Hebu soma hapa

Naelewa mwenyewe juzi katika hotuba yake ya kilele cha sherehe za Mapinduzi amesema kwamba anakamilisha kipindi chake na Katiba ya Zanzibar hairuhusu kipindi cha tatu. Nakubaliana naye na sipendekezi kuondolewa kwa ukomo wa vipindi viwili kwa mtu anayeshikilia madaraka ya Urais wa Zanzibar . Ila namuomba sana akubaliane na matakwa ya Wazanzibari walio wengi kama yalivyokwisha oneshwa kupitia taarifa na kauli mbali mbali kwamba kipindi chake cha pili tukiongeze muda kidogo ili tusiipoteze fursa ya kihistoria ambayo ameianzisha yeye.

Ukishafahamu hapo, soma hapa chini

Natoa wito kwa wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wa pande zote mbili, Serikali na Upinzani, kulitafakari hili na kutupa Wazanzibari kile tunachokitaka.

Kwenye issue muhimu usipende kuweka dhihaka mbele! Zanzibar sasa ipo katika hatua moja kubwa mno, ambayo haitaji watu aina yako.
 
Kwenye issue muhimu usipende kuweka dhihaka mbele! Zanzibar sasa ipo katika hatua moja kubwa mno, ambayo haitaji watu aina yako.

Mimi nafahamu vizuri Zanzibar iko wapi na inahitaji nini, na humor wala sio dhihaka.Hivyo ni vitu tofauti kabisa.

Mie nafahamu uzuri hatua iliopo Zanzibar.Lakini na umuhimu wote huo hainipelekei kuwa na boring conversation with no sense of humor.

Juu ya hapo bado hujatoa maoni yako juu ya hiyo hatua muhimu unayoililia kama muda uongezwe au tujikite na uchaguzi.?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom