Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Rais Mkapa aliwahutubia wananchi katika mwaka mpya 2005, Januari 31. Hotuba ile ningeipa jina la "Uaminifu na maadili ya Taifa" ilinivutia wakati ule na niliipenda. Ukweli wake bado ni kweli hata leo hii. Kama ingetolewa na mtu mwingine basi bila ya shaka ingekuwa ni mojawapo ya hotuba zenye kugusa fikra na hisia za watu kwa mantiki yake, hoja zake na mahitimisho yake... Jisomee mwenyewemsisitizo ni wangu)
Ndugu Wananchi,
Katika salamu zangu za mwaka huu mpya kwenu, pamoja na mambo mengine, nilijenga hoja kuwa wakati umefika Watanzania tuweke mkazo mpya, na umuhimu unaostahili, kwenye maadili ya kitaifa. Maadili ya kitaifa, yanayotutambulisha kama Watanzania, yanayotupa sifa ya U-Tanzania, ni ya aina nyingi. Mwezi uliopita nilizungumzia zaidi maadili ya kisiasa na kiutawala, nikawalaumu zaidi viongozi wa kisiasa na kiutawala kwa dalili za mmomonyoko wa maadili yetu ya asili. Nilikuombeni, Ndugu Wananchi, mniunge mkono kuwakatalia viongozi wa kisiasa, kidini na kiutawala ambao, kwa kauli zao au vitendo vyao, wanachangia kumomonyoa sifa za U-Tanzania, ikiwemo maadili ya uhuru, umoja, amani, utulivu, upendo, kuvumiliana na mshikamano. Nilikuombeni tusaidiane kuwaambia HAPANA viongozi wanaotuletea mambo ya udini, ukabila, umajimbo, ubaguzi, visasi, chuki na fujo, maana mambo hayo kwa hakika ni kinyume kabisa cha U-Tanzania wetu.
Leo nitaelekeza maneno yangu kwa wale wananchi wenzetu wachache ambao, kwa tabia na mienendo yao, nao wanahatarisha sifa za kijamii za Watanzania, ambazo nazo ni sehemu muhimu ya U-Tanzania wetu sote. Na leo nitazungumzia sifa moja tu ya maadili ya UAMINIFU. Maana, huko tulikotoka, Watanzania kwa ujumla tulisifika kwa uaminifu, hasa tukilinganishwa na mataifa mengine barani Afrika. Ingetazamiwa wengine wajifunze uaminifu kutoka kwetu. Lakini naona wapo baadhi ya Watanzania ambao sasa wanataka kutufikisha mahali ambapo na sisi tutaonekana hatuna tofauti na hao wengine.
Ukweli ni kuwa sifa ya U-Tanzania si sifa itokanayo na maadili ya kisiasa na kiutawala peke yake; ni sifa itokanayo pia na tabia za raia, na maadili mengine ya kijamii, ikiwemo uaminifu. Kamusi ya Kiswahili Sanifu inaeleza kuwa Uaminifu ni tabia ya mtu kuweza kuaminika, kama vile mtu kupewa amana za watu aziweke mpaka watakapokuja kuzitaka.
Ndugu Wananchi,
Katika miaka ya 1970 na 1980, nchi yetu iliwekeza sana mikopo, misaada, rasilimali, amana na akiba za taifa letu katika mashirika ya umma. Zipo sababu nyingi zilizofanya mashirika hayo yadhoofu kiutendaji, na hatimaye mengi kufa kabisa. Lakini mojawapo ya sababu hizo ni kukosa uaminifu kwa baadhi ya wenzetu tuliowakabidhi kazi ya kusimamia na kuendesha mashirika hayo, yaani wenzetu tuliowakabidhi amana za taifa letu. Kweli, wengine walikuwa na elimu au ujuzi usiotosha, na pengine mazingira ya kibiashara na kiutawala wakati huo hayakuwa mazuri sana. Lakini, kwa baadhi yao, ukosefu wa uaminifu nao ulikuwa mojawapo ya sababu ya kudhoofika na hatimaye kufa kwa mashirika ya umma.
Hayo yalikuwa mashirika ya umma, na yalipokufa waliopata hasara kwa kweli ni ninyi wananchi. Leo uchumi wetu, siku hadi siku, unazidi kuwa wa soko, na hivyo unakuwa uchumi wa ushindani. Ni uchumi utokanao na uwekezaji wa sekta binafsi, wa amana za watu binafsi. Serikali haiwekezi tena kwenye viwanda, huduma za kibiashara, makampuni, mabenki na asasi za fedha. Wanaow
HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO
WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM
MKAPA, KWA WANANCHI, 31 JANUARI 2005
Ndugu Wananchi,
Katika salamu zangu za mwaka huu mpya kwenu, pamoja na mambo mengine, nilijenga hoja kuwa wakati umefika Watanzania tuweke mkazo mpya, na umuhimu unaostahili, kwenye maadili ya kitaifa. Maadili ya kitaifa, yanayotutambulisha kama Watanzania, yanayotupa sifa ya U-Tanzania, ni ya aina nyingi. Mwezi uliopita nilizungumzia zaidi maadili ya kisiasa na kiutawala, nikawalaumu zaidi viongozi wa kisiasa na kiutawala kwa dalili za mmomonyoko wa maadili yetu ya asili. Nilikuombeni, Ndugu Wananchi, mniunge mkono kuwakatalia viongozi wa kisiasa, kidini na kiutawala ambao, kwa kauli zao au vitendo vyao, wanachangia kumomonyoa sifa za U-Tanzania, ikiwemo maadili ya uhuru, umoja, amani, utulivu, upendo, kuvumiliana na mshikamano. Nilikuombeni tusaidiane kuwaambia HAPANA viongozi wanaotuletea mambo ya udini, ukabila, umajimbo, ubaguzi, visasi, chuki na fujo, maana mambo hayo kwa hakika ni kinyume kabisa cha U-Tanzania wetu.
Leo nitaelekeza maneno yangu kwa wale wananchi wenzetu wachache ambao, kwa tabia na mienendo yao, nao wanahatarisha sifa za kijamii za Watanzania, ambazo nazo ni sehemu muhimu ya U-Tanzania wetu sote. Na leo nitazungumzia sifa moja tu ya maadili ya UAMINIFU. Maana, huko tulikotoka, Watanzania kwa ujumla tulisifika kwa uaminifu, hasa tukilinganishwa na mataifa mengine barani Afrika. Ingetazamiwa wengine wajifunze uaminifu kutoka kwetu. Lakini naona wapo baadhi ya Watanzania ambao sasa wanataka kutufikisha mahali ambapo na sisi tutaonekana hatuna tofauti na hao wengine.
Ukweli ni kuwa sifa ya U-Tanzania si sifa itokanayo na maadili ya kisiasa na kiutawala peke yake; ni sifa itokanayo pia na tabia za raia, na maadili mengine ya kijamii, ikiwemo uaminifu. Kamusi ya Kiswahili Sanifu inaeleza kuwa Uaminifu ni tabia ya mtu kuweza kuaminika, kama vile mtu kupewa amana za watu aziweke mpaka watakapokuja kuzitaka.
Ndugu Wananchi,
Katika miaka ya 1970 na 1980, nchi yetu iliwekeza sana mikopo, misaada, rasilimali, amana na akiba za taifa letu katika mashirika ya umma. Zipo sababu nyingi zilizofanya mashirika hayo yadhoofu kiutendaji, na hatimaye mengi kufa kabisa. Lakini mojawapo ya sababu hizo ni kukosa uaminifu kwa baadhi ya wenzetu tuliowakabidhi kazi ya kusimamia na kuendesha mashirika hayo, yaani wenzetu tuliowakabidhi amana za taifa letu. Kweli, wengine walikuwa na elimu au ujuzi usiotosha, na pengine mazingira ya kibiashara na kiutawala wakati huo hayakuwa mazuri sana. Lakini, kwa baadhi yao, ukosefu wa uaminifu nao ulikuwa mojawapo ya sababu ya kudhoofika na hatimaye kufa kwa mashirika ya umma.
Hayo yalikuwa mashirika ya umma, na yalipokufa waliopata hasara kwa kweli ni ninyi wananchi. Leo uchumi wetu, siku hadi siku, unazidi kuwa wa soko, na hivyo unakuwa uchumi wa ushindani. Ni uchumi utokanao na uwekezaji wa sekta binafsi, wa amana za watu binafsi. Serikali haiwekezi tena kwenye viwanda, huduma za kibiashara, makampuni, mabenki na asasi za fedha. Wanaow