Kinyambiss
JF-Expert Member
- Dec 2, 2007
- 1,374
- 72
watugee buku mbili kila mwananchi tu tie vocha tuu kama vipi..lol
You made my day!!!watugee buku mbili kila mwananchi tu tie vocha tuu kama vipi..lol
Na Nyerere aliwahi kusema hivi, Umaskini wa ni mbaya lakini umaskini wa akili ni mbaya sana sana.Hapo ndo viongozi wetu na sisi hatujui tunaomba nini au tunataka tusaidie
Huyu kijana anafanyabiashara na baba yake na kuusaka ubunge ilikuwa ni njia moja wapo ya kuwekeza!! Unapowekeza ,unatarajia kupata zaidi ya kile ulichowekeza na hivyo ndivyo ilivyotokea kwa huyu kijana; matumizi yake akiwa mbunge kwa yote aliyoainisha na asioainisha ni kidogo ukilinganisha na mapato aliyopata kwa kutumia influence ya ubunge pamoja na marupurupu ya ofisi hiyo! Mfanyabiashara yeyote hasa muhindi hawezi kutumia pesa yake mahala ambapo hanufaiki. Huyu kijana anawazuga hao wanyaturu kwa kuwahongahonga unga na khanga/fulana wakati wa uchaguzi halafu ukimalizika uchaguzi huyo anarudi maskani yake Oysterbay Dsm; sidhani kama hata ana makazi ya kudumu huko Singida zaidi ya maduka aliyopamga National Housing!!
ubunge wa namna hii haufai kabisa. wananchi wanatakiwa wasidiwe katika kutatua matatizo yao ya kudumu na sio kuwajaza mapesa mifukoni mwao. hizo pesa anazozitoa kazitoa wapi? kama sio hizihizi za kwetu. pili ikiwa kila mbunge atafanya hivyo katika jimbo lake itajuwaje kwa wabunge ambao hawana fedha kama za huyu mweshimiwa. kununua tractor sio tija ndio maana wanachi hawalitumii hapa alikosa ushauri angepigania kutafuta masoko ya mazao ya jimbo lake wananchi wangenunua matractor yao baada ya kupata pesa nyingi. hii style ya mimi nimefanya hiki na kile ni usanii tu. tungemwelewa kama angefanya hayo alipojuwa sio mbunge, hapa anaonekana kama vile ubunge ni sehemu ya kuficha madhambi yao. mwana falasa PLATO aliwahi kusema viongozi wazuri hawapandi kuongoza na viongozi wabaya wanajipendekeza kupewa uongozi hapa tunaona kila dalili ya kujipendekeza tu kuongoza.
Hivi kazi (wajibu) wa Mbunge ni kutoa misaada?...hivi hizo shule na misaada ya elimu kila kata huoni kama ni zaidi ya msaada wa kawaida,hiyo ni investment kubwa sana kwa hao wanyaturu na mungu sijui awape nini? kanunua tractor wewe unataka awatafutie masoko,kwani wengine wanafanya nini? mbona mnataka kufanyiwa kila kitu na hata shukrani hamna,kama kafanya hiki na kile na ni kweli sioni ubaya wowote akiongea wazi na hakuna usanii wowote lazima watu wajue,maana mafisadi kama nyie mnapenda ku distort records za watu na kuwaita wezi,nyie watu lazima mjifunze kuwa na shukrani mnaposaidiwa na sio kila kitu ni siasa,kama jamaa anaficha kitu hiyo ni topic nyingine na unaweza kuileta hapa(doubt kama una chochote zaidi ya majungu) ila its obvious aliyoyafanya kwa wanyaturu ni ya kumsifu sio kumtukana
...halafu returns za pesa zako zinarudi vipi katika haya mazingira ya kumulikana na kutafutana uchawi kila kukicha?
BTN huyu na ROSTAM inaonekana huyu kafanya mazito zaidi
Nothing wrong kuonyesha kuwa kafanya
Jiulizeni mbona Wabunge wengine hawasemi washafanya nini?
Mi nataka kumn'goa.. suggestions please!