Hotuba ya mbowe mazishi ya Makani imebeba uzito stahiki unaofikirisha

Candid Scope

JF-Expert Member
Nov 8, 2010
11,886
6,883

SAM_2537.JPG


Mbowe apasua jipu kwenye mazishi ya Makani

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, amewaonya wanasiasa wanaopenda kutumia propaganda chafu za udini kwa manufaa ya muda mfupi ya kisiasa ya vyama vyao kwa gharama ya kuwagawanya Watanzania na kulibomoa taifa lao.

Amesema kuwa amekuwa akishangazwa na unyenyekevu, ukaribu na ushirikiano unaooneshwa baina ya wanasiasa na viongozi mbalimbali wa kiserikali wakati wa misiba, lakini huonekana kusahahu kila kitu mara baada ya misiba na kuendekeza propaganda za udini na ukabila, badala ya kuweka mbele utaifa.

Akizungumza wakati wa kutoa salaam za rambimrambi kwa niaba ya Chadema mara baada ya mazishi ya mmoja wa wanasiasa wa chama hicho, Bob Mkani Makani, jana katika kijijini Ukenyenge, wilayani Kishapu, Mbowe alisema marehemu alikuwa mtu mzuri aliyejitoa kwa hali na mali kwa ajili ya Watanzania.

“Kwa ujumla niseme tu kuwa siwezi kutumia dakika tano hizi kumaliza kuzungumzia sifa za Bob, lakini niseme kuwa nimekuwa nashangazwa na unyenyekevu huu unaooneshwa wakati wa misiba pekee, wakati wa misiba kunakuwa na ukaribu na ushirikiano wa hali ya juu, lakini tunakuwa wepesi sana tunasahau punde tu…baada ya msiba tunarudi kunyukana tena kwa kutumia na kutanguliza propaganda mbalimbali zikiwemo za udini,” alisema na kuongeza:

“Mathalani leo wengine hapa walijua Bob ni Mkristo, kumbe Bob ni Mwislamu, lakini tumekuwa tunatumia propaganda nyepesi za udini tunaharibu historia makusudi kwa maslahi yetu mafupi ya kisiasa bila kujua kuwa wakati huo huo tunalibomoa taifa letu katika misingi ya udini.”

“Leo tumekaa wote hapa, watu wa dini mbalimbali, tuna viongozi wetu hapa wa dini mbalimbali, tumekaa pamoja kabisa tumevumiliana, wapo watu wa makabila mbalimbali…hakuna tatizo lolote kabisa, kwa sababu sisi hatupaswi kutambulishwa kwa makabila wala dini zetu bali tunatambulishwa kwa utaifa na Utanzania wetu basi,” aliongeza.

“Napenda kutoa hii rai leo kwa viongozi wa dini zote walioko mahali hapa, kwa viongozi wote wa vyama vya siasa na kwa viongozi wa serikali, vyama hivi vya siasa ni vitu vya kupita, tusibomoe utaifa wetu kwa bendera za vyama vyetu. Vyama vyote hivi Chadema na CCM vitapita, lakini Watanzania na nchi yao watabaki,” alisema Mbowe huku waombolezaji wakishindwa kujizuia kumpigia makofi mengi.

Mbowe alisema kuwa Hayati Bob alijitoa kwa hali na mali kwa ajili ya Watanzania akitolea mfano namna alivyojitolea nyumba yake maeneo ya Sea View, Dar es Salaam kuwa mahali pa vikao vya mwanzo kabisa kuanzisha chama hicho cha siasa.

“Wakati watu wengi wakiogopa kujihusisha na vyama vya upinzani Bob hakujali, kwa sababu Bob was a guy of courage (mtu jasiri). Hakuogopa. Akadiriki kuruhusu nyumbani kwake kuwa mahali pa vikao. Mzee wenu amewatumikia Watanzania kupitia Chadema kwa miaka 21 mfululizo bila malipo. Leo hapa tujiulize wangapi tunaweza kufanya hivyo,” alisema.

Mzee Bob Makani alizikwa jana katika Kijiji cha Ukenyenge, Tarafa ya Negezi, wilayani Kishapu, eneo la makaburi alipozikwa Baba yake, marehemu Ali Makani na ndugu zake wengine.​
 
Binafsi nakubaliana na kauli ya Mbowe, kwani ukweli mara zote huzungukwa na kupanda propaganda, ya moyoni yanayomwumiza ameyaanika, kwani ni dalili ya propaganda tofauti na wanavyoonekana misibani, hapa napata picha kuwa viongozi na wanasiasa unafiki una kipaumbele kuliko ukweli.
 
Hivi mzee wa usingizi alikuwepo? Kumbe naye ni mwanzilishi wa cdm. Njaa mbaya sana, itachukuwa muda kuamini kuwa kumbe mzee wa usingizi anafahamu mchanganyiko wa watu waloanzisha cdm bado naye anatoka mapovu kukomalia issue za udini chadema.
Nimeipenda hii kauli ya mbowe, bendera za vyama vyetu visibomoe msingi wa utaifa wetu.
 
Ni hotuba iliyokidhi vigezo,tena yenye kuonesha ukomavu wa kisiasa na uzalendo
 
Amesema kuwa amekuwa akishangazwa na unyenyekevu, ukaribu na ushirikiano unaooneshwa baina ya wanasiasa na viongozi mbalimbali wa kiserikali wakati wa misiba, lakini huonekana kusahahu kila kitu mara baada ya misiba na kuendekeza propaganda za udini na ukabila, badala ya kuweka mbele utaifa.

Hili ndilo jibu kwa Mukama Katibu mkuu wa CCM aliyeanza ukabila bale kwenye maombolezo ya Makani
 
Duh! Mbowe huwa namkubali si kwa bure tu! Huyu jamaa ni Jembe la Uhakika!
 

“Mathalani leo wengine hapa walijua Bob ni Mkristo, kumbe Bob ni Mwislamu, lakini tumekuwa tunatumia propaganda nyepesi za udini tunaharibu historia makusudi kwa maslahi yetu mafupi ya kisiasa bila kujua kuwa wakati huo huo tunalibomoa taifa letu katika misingi ya udini.”

“Leo tumekaa wote hapa, watu wa dini mbalimbali, tuna viongozi wetu hapa wa dini mbalimbali, tumekaa pamoja kabisa tumevumiliana, wapo watu wa makabila mbalimbali…hakuna tatizo lolote kabisa, kwa sababu sisi hatupaswi kutambulishwa kwa makabila wala dini zetu bali tunatambulishwa kwa utaifa na Utanzania wetu basi,” aliongeza.

“Napenda kutoa hii rai leo kwa viongozi wa dini zote walioko mahali hapa, kwa viongozi wote wa vyama vya siasa na kwa viongozi wa serikali, vyama hivi vya siasa ni vitu vya kupita, tusibomoe utaifa wetu kwa bendera za vyama vyetu. Vyama vyote hivi Chadema na CCM vitapita, lakini Watanzania na nchi yao watabaki,” alisema Mbowe huku waombolezaji wakishindwa kujizuia kumpigia makofi mengi.

Mbowe alisema kuwa Hayati Bob alijitoa kwa hali na mali kwa ajili ya Watanzania akitolea mfano namna alivyojitolea nyumba yake maeneo ya Sea View, Dar es Salaam kuwa mahali pa vikao vya mwanzo kabisa kuanzisha chama hicho cha siasa“
.
[/QUOTE]


Mbowe kanifurahisha sana, hii ni msg nzito sana
 
Magwanda bwana, hukua anachukuwa misaada kutoka vyama vya siasa vya kidini huku Mbunge wake anasema anataka Taifa la kanda ya kaskazini, huku anasimaa kudanganya watu wamuone kuwa yeye sio mdini wala mkabila. Huu ndio unafik wa kisiasa.

Angeanza kwa kuachana misaada ya kisiasa kutoka vyama vya kidini. Angeanza kwa kukemea kanisa lililowatenga waumini kwa kuwa tu waliipigia kura CCM. Angeanza kwa kumkemea na kumchukulia hatua za kinidhamu Nassari ambae anataka Taifa la kaskazini. Angeanza kwa kuwa na uwiano sawa wa wabunge wa kupendekezwa badala ya asilimia kubwa ni Wakristo na waliotoka Kaskazini.

Mbowe huu mimi nauita unafik.
 
Magwanda bwana, hukua anachukuwa misaada kutoka vyama vya siasa vya kidini huku Mbunge wake anasema anataka Taifa la kanda ya kaskazini, huku anasimaa kudanganya watu wamuone kuwa yeye sio mdini wala mkabila. Huu ndio unafik wa kisiasa.

Angeanza kwa kuachana misaada ya kisiasa kutoka vyama vya kidini. Angeanza kwa kukemea kanisa lililowatenga waumini kwa kuwa tu waliipigia kura CCM. Angeanza kwa kumkemea na kumchukulia hatua za kinidhamu Nassari ambae anataka Taifa la kaskazini. Angeanza kwa kuwa na uwiano sawa wa wabunge wa kupendekezwa badala ya asilimia kubwa ni Wakristo na waliotoka Kaskazini.

Mbowe huu mimi nauita unafik.

Acha hizo, mbona alishakemea siku nyingi. wewe hukusikia anmwambia Nasary "this is childish"
 
"vyama hivi vya siasa ni vitu vya kupita, tusibomoe utaifa wetu kwa bendera za vyama vyetu. Vyama vyote hivi Chadema na CCM vitapita, lakini Watanzania na nchi yao watabaki,”

Ni kauli ya busara sana hii.
 

SAM_2537.JPG


Mbowe apasua jipu kwenye mazishi ya Makani

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, amewaonya wanasiasa wanaopenda kutumia propaganda chafu za udini kwa manufaa ya muda mfupi ya kisiasa ya vyama vyao kwa gharama ya kuwagawanya Watanzania na kulibomoa taifa lao.

Amesema kuwa amekuwa akishangazwa na unyenyekevu, ukaribu na ushirikiano unaooneshwa baina ya wanasiasa na viongozi mbalimbali wa kiserikali wakati wa misiba, lakini huonekana kusahahu kila kitu mara baada ya misiba na kuendekeza propaganda za udini na ukabila, badala ya kuweka mbele utaifa.

Akizungumza wakati wa kutoa salaam za rambimrambi kwa niaba ya Chadema mara baada ya mazishi ya mmoja wa wanasiasa wa chama hicho, Bob Mkani Makani, jana katika kijijini Ukenyenge, wilayani Kishapu, Mbowe alisema marehemu alikuwa mtu mzuri aliyejitoa kwa hali na mali kwa ajili ya Watanzania.

“Kwa ujumla niseme tu kuwa siwezi kutumia dakika tano hizi kumaliza kuzungumzia sifa za Bob, lakini niseme kuwa nimekuwa nashangazwa na unyenyekevu huu unaooneshwa wakati wa misiba pekee, wakati wa misiba kunakuwa na ukaribu na ushirikiano wa hali ya juu, lakini tunakuwa wepesi sana tunasahau punde tu…baada ya msiba tunarudi kunyukana tena kwa kutumia na kutanguliza propaganda mbalimbali zikiwemo za udini,” alisema na kuongeza:

“Mathalani leo wengine hapa walijua Bob ni Mkristo, kumbe Bob ni Mwislamu, lakini tumekuwa tunatumia propaganda nyepesi za udini tunaharibu historia makusudi kwa maslahi yetu mafupi ya kisiasa bila kujua kuwa wakati huo huo tunalibomoa taifa letu katika misingi ya udini.”

“Leo tumekaa wote hapa, watu wa dini mbalimbali, tuna viongozi wetu hapa wa dini mbalimbali, tumekaa pamoja kabisa tumevumiliana, wapo watu wa makabila mbalimbali…hakuna tatizo lolote kabisa, kwa sababu sisi hatupaswi kutambulishwa kwa makabila wala dini zetu bali tunatambulishwa kwa utaifa na Utanzania wetu basi,” aliongeza.

“Napenda kutoa hii rai leo kwa viongozi wa dini zote walioko mahali hapa, kwa viongozi wote wa vyama vya siasa na kwa viongozi wa serikali, vyama hivi vya siasa ni vitu vya kupita, tusibomoe utaifa wetu kwa bendera za vyama vyetu. Vyama vyote hivi Chadema na CCM vitapita, lakini Watanzania na nchi yao watabaki,” alisema Mbowe huku waombolezaji wakishindwa kujizuia kumpigia makofi mengi.

Mbowe alisema kuwa Hayati Bob alijitoa kwa hali na mali kwa ajili ya Watanzania akitolea mfano namna alivyojitolea nyumba yake maeneo ya Sea View, Dar es Salaam kuwa mahali pa vikao vya mwanzo kabisa kuanzisha chama hicho cha siasa.

“Wakati watu wengi wakiogopa kujihusisha na vyama vya upinzani Bob hakujali, kwa sababu Bob was a guy of courage (mtu jasiri). Hakuogopa. Akadiriki kuruhusu nyumbani kwake kuwa mahali pa vikao. Mzee wenu amewatumikia Watanzania kupitia Chadema kwa miaka 21 mfululizo bila malipo. Leo hapa tujiulize wangapi tunaweza kufanya hivyo,” alisema.

Mzee Bob Makani alizikwa jana katika Kijiji cha Ukenyenge, Tarafa ya Negezi, wilayani Kishapu, eneo la makaburi alipozikwa Baba yake, marehemu Ali Makani na ndugu zake wengine.​
Wakuu mnaona sasa watu na cheap propoganda kumbe hata waanzilishi wa CHADEMA si wote walikuwa Wachaga wala Wakristo, (Mzee Bob Makani na Mzee Mtei waanzilishi wa CHADEMA) hii ni aibu kwa wote wa siasa za udini na kabila!!! Kumbe Mzee Bob hakuwa Mkristo wala Mchaga, yeye alikuwa Msukuma na Mwislamu safi, watokee kina siasa uchwala za dini na ukabila sasa!!!!!

 
Acha hizo, mbona alishakemea siku nyingi. wewe hukusikia anmwambia Nasary "this is childish"

Sasa kusema "childish" ndio kachukuwa hatua stahiki? unanifurahisha kweli kweli, hiyo si kumsifia tu, maana mtoto anaweza fanya lolote akaachiwa tu, si mtoto! Sasa Nassari ni mtoto?

Na kuchukuwa misaada vyama vya siasa vya kidini? na kuchaguwa wabunge wa upendeleo asilimia kubwa (zaidi ya 80%) wakristo na waliotoka Kaskazini? kama si udini na ubaguzi wa ukabila ni nini? aache unafik.

Ukiona mtu anajitangaza na kujipamba kwenye jambo fulani, basi mtazame sana huyo, "guilty conscious" inamuhangaisha.
 
17 Reactions
Reply
Back
Top Bottom