Hotuba Ya JK: Tafsiri Yangu


:frusty::frusty::A S 114::A S 114::blah: You Maggid, ww kazi yako si Journalist wa Siasa, bakia Global publishers, UDAKU fits you best, acha kuandika

usichojua, koma, kaandike nani KAFUMANIWA,na GUEST GANI, Nani na nani wanatoka kungonoka etc, hii ndio kazi yako, umbea Journalism
& kujua Ubongo wako how low u r, ETI JANA JK KAFANYA JAMBO KUBWA SANA.....!!!!!!!!!!???? :frusty::frusty: :smash::smash: hii njaa hii, mbaya sana,
hasa unapokuwa na njaa ya akili, kwani nani alianzisha hoja ya katiba mpya? hata hujui unaandika nini, na TUNATAKA TUME HURU IUNDWE NA BUNGE na Dowans mbona hujamuuliza
hajasema chochote?, nadhani umeelewa why i said ww UMBEA, UDAKU, Upaparazzi unakufaaaaa, hivi have you even Graduated F4? Kaandike Amani, Ijumaa, Uwazi, Risasi usiingilie kuandika Siasa, get out, hata hufanani na Kinyonga wala Bendera fuata upepo, shame on you, hufaiiiii period
Kweli bwana anaudhi:angry::frusty:
 
Maggid hii ni fani yake..... kwahiyo we expect more from his analysis..... simjui vizuri kwahiyo siwezi kusema huko nyuma aliyoandika lakini kwa hili... very dissapointing.

You defeat someone's analysis by analysing either the same issue, or his analysis to show where he is wrong or disappointing.

Most u r comments show u r KIHIYO as Maggid, arrogance dominates u r mind, you never say the truth, hatutaki Kiongozi of copying & pasting, pure & simple

Hata kama ni Kihiyo, bado ametoa hoja yake, iwe ya kweli au kakosea. Hoja yako kuidefeat ya kwake iko wapi. Hoja hupingwa kwa hoja kama huna hoja kaa kimya sio kutusi.
 
You defeat someone's analysis by analysing either the same issue, or his analysis to show where he is wrong or disappointing.



Hata kama ni Kihiyo, bado ametoa hoja yake, iwe ya kweli au kakosea. Hoja yako kuidefeat ya kwake iko wapi. Hoja hupingwa kwa hoja kama huna hoja kaa kimya sio kutusi.

Go & read what is Definition of Hoja, POINTLESS is not hoja is Kiroja, na kiroja hakijibiwi, mjinga hutoa kiroja.
u r of the same type, hiding what is right exposes ur stupidity especially when we know
where the truth lies.
 
Go & read what is Definition of Hoja, POINTLESS is not hoja is Kiroja, na kiroja hakijibiwi, mjinga hutoa kiroja.
u r of the same type, hiding what is right exposes ur stupidity especially when we know
where the truth lies.


Onyesha hoja yako na kiroja cha Maggid. Kama ni kumkoma nyani giladi basi wewe ndio mwenye viroja.
 
Mzee Mwanakijiji said:
somebody please shoot me!! yaani he is now a hero? really?
somebody wont shoot you... but will hilariously potrays JK's image as hero despite initial motives from his Gov to reject the idea!!
 
Lakini hili wazo ni la Kikwete au nani huko serikalini? Maana labda I missed something lini CCM walibadilisha ajenda yao au ilani yao au sasa imekuwa Rais ni kama mfalme fulani ambaye anaweza kutoa tamko lolote hususana kwenye jambo kubwa kama hili bila kupitia vikao halali vya chama chake.

Hivi akija baadaye na kuamua kuanzisha mjadala ya kuvunja Muungano kuna mtu anataweza kumuuliza?
 
Lakini hili wazo ni la Kikwete au nani huko serikalini? Maana labda I missed something lini CCM walibadilisha ajenda yao au ilani yao au sasa imekuwa Rais ni kama mfalme fulani ambaye anaweza kutoa tamko lolote hususana kwenye jambo kubwa kama hili bila kupitia vikao halali vya chama chake.

Hivi akija baadaye na kuamua kuanzisha mjadala ya kuvunja Muungano kuna mtu anataweza kumuuliza?

Tunahitaji Katiba mpya, liwe wazo la CJ, AG, REDET, SYNOVATE, CHADEMA, CCM. Maadam ni public demand, Rais anatakiwa alifanyie kazi.

Suala la Muungano lipo ndani ya Katiba so akitaka kuvunja Muungano itabidi avunje kwanza Katiba, au Katiba mpya itakayoruhusu kuvunjwa kwa Muungano ipatikane.
 
Hivi mbona idadi ya Watanzania ambao ni bendera fuata upepo inaongezeka kwa kasi? Tangia lini Kikwete and Co wakawa ma-championi wa kudai Katiba mpya? Sifahamu kama JK anakunywa mvinyo but typically jana usiku his state of mind was not the same!

kikwete hanywi pompe, labda umesahau mkapa ndio alikuwa anaoga, NASIKIA HARUFU YA UDINI HAPA
 
Lakini hili wazo ni la Kikwete au nani huko serikalini? Maana labda I missed something lini CCM walibadilisha ajenda yao au ilani yao au sasa imekuwa Rais ni kama mfalme fulani ambaye anaweza kutoa tamko lolote hususana kwenye jambo kubwa kama hili bila kupitia vikao halali vya chama chake.

Hivi akija baadaye na kuamua kuanzisha mjadala ya kuvunja Muungano kuna mtu anataweza kumuuliza?


Angetaa lolote kuhusu katiba ungesema nini? ulitaka akatae uandike? sio lazima uandike makala kuhusu katiba unaweza kuandika issue nyingine au kuendelea kutoa mawazo constructive kwenye hii move na sio upupu huu wa kuonesha chuki binafsi
 
doooh!
Majjid kuna mengi umenena na sijakubaliana nayo.
Kwamba jk ametumia busara, sidhani kama uko sahihi - shinikizo ni kubwa kwa sasa (watu wana mwamko).
Kwamba jk si mwendawazimu, labda uko sahihi - ila mbona alikuwa anaongea kimajungu sana juu ya watu wanaotaka kusababisha vurugu? Kama rais wa nchi amewashindwa wafanya vurugu nani atawaweza? (hapo namaanisha kuwa mleta vurugu namba moja ni yeye)
kwamba jk amefocus miaka 50 ijayo, si kweli - angeanza na kuisafisha system

i have a strong feeling of hatred towards my president.. Yes, i said so!


hama nchi yeye ndio rais utaugua ugonjwa wa moyo, nasikia harufu ya udini hapa



 
Maana, JK kama binadamu, kuna mazuri na mabaya aliyoyafanya katika utendaji wake wa kazi maishani mwake. Na katika hili la Uona Mbali juu ya Katiba yetu, basi, kama JK atafanikiwa kuongoza juhudi hizi za Watanzania kupata Katiba iliyofanyiwa marekebisho makubwa, sina shaka yeyote, kuwa ataacha legacy kwa maana ya haiba. Katiba Mpya itakuwa moja ya jambo kubwa atakalokumbukwa nalo.


Mkuu katika hiyo red nataka unikumbushe mazuri aliyofanya labda nimesahau kidogo! maana sie binadamu huwa tunasahaugi mazuri na kukumbuka mabaya tu! ila to be honest there is nothing to ring the bells for me to recall anything good from him apart from bringing and paying football Managers for our Taifa stars, and i really appreciate this but i am lost about anything positive from this president! i am sorry if i am missing something here.


Kwenye red naona kama mpingano! yapo mengi ila likiwemo la wewe kuongea hapa kwa uhuru , nasikia HARUFU YA UDINI HERE AGAIN
 
Akubali kuundwa kwa tume ya kuchunguza mchakato ulio muweka madarakani ili ni msifie vizuri.........
 
Kila jambo na tafsiri yake. Tafsiri yangu ya kilichoongewa jana na JK imeleta tafsiri nyingine. Ni jambo jema. Lililo kubwa hapa ni mjadala wa Katiba. Nimekumbushia kwa ufupi tulikotoka. Inahusu historia yetu, kuipitia historia yetu kunatusaidia kujitambua.

Kwa hili vuguvugu la madai ya vyama vingi na katiba ni miaka 20 iliyopita. Nilikuwa na umri wa kufuatilia haya ya mchakato wa demokrasia yetu na hata kuandika, mbali ya kupiga picha.

Kuna mengi nimejifunza, na bado najifunza. Tukumbuke, hata la vyama vingi lilikuwa jambo geni sana miaka 20 iliyopita. Na kawaida yetu wanadamu tunaogopa mabadiliko. Si ni hata tunapokuwa kwenye chumba cha giza. Mara taa zikiwaka ghafla, mboni za macho zinauma ( Fotofobia). Kisha macho nayo yanauzoea mwanga. Inakuwa ni kawaida.

Hivi ni kijana gani leo atakuelewa ukianzisha mjadala wa ama kuwa na chama kimoja au vyama vingi? Na kuna wajukuu zetu wataotushangaa, watakaposoma maandiko yetu na kubaini, kuwa babu zao tulikaa na kujadiliana juu ya ama tuifanyie marekebisho makubwa katiba yetu ya mwaka 1977 au ibaki kama ilivyo? Ndio, kila jambo na wakati.

Naamini, kuwa waliookuwa kwenye mamlaka miaka hiyo walihofia vyama vingi. Waliruhusu mfumo wa vyama vingi kwa shingo upande. Na mpaka hii leo tunalipa gharama ya hofu hiyo ya tangu miaka 20 iliyopita.

Hata sasa, mwaka 2011, bado kuna walio kwenye mamlaka wanaoona kuwa upinzani ni uadui, ni jambo baya. Na jamii nayo imelishwa propaganda hiyo. Katika nchi yetu kuna wahanga wa siasa za vyama vingi. Kuna ambao biashara zao zimekufa kwa vile wameonyesha hadharani mapenzi kwa vyama vya upinzani. Kuna hata hii leo, wakulima wanyonge wanaonyimwa mbolea za ruzuku kwa vile wanajihusisha na siasa za upinzani.

Na juzi hapa nikauliza; Je, uhuru= hakuna upinzani? Labda sasa kuna wanaoliona jibu la swali hilo. Ndio, moja ya tafsiri za uhuru yaweza kuwa marufuku ya kuwepo kwa upinzani wakati wachache wakila matunda ya uhuru!

Na je, kuna mnaokumbuka, kuwa Augustino Mrema, enzi hizo akiwa Waziri wa Mambo ya Ndani, alitamka nini pale zilipofika habari, kuwa Oscar Kambona alikuwa njiani kurudi nyumbani kutoka uhamishoni Uingereza?
 
Ndio, tumeumaliza mwaka jana na mjadala wa Katiba mpya. Tunaingia mwaka 2011 na mjadala wa Katiba Mpya. Hili ni jambo jema. Na lililo muhimu kabisa katika mjadala wowote uwao ni kujiuliza; nini shabaha na malengo yetu? Nionavyo, shabaha na leo letu liwe kudumisha Umoja wetu wa Kitaifa, amani na utulivu tulio nao. (CCM)




kujenga taifa lenye amani, maendeleo, demokrasia, hadhi na heshima kwa raia wote.
 
Mbona mimi sioni chochote alichoandika huyu Majidi au mimi kiswahili kinanichenga jamani?
 
Hiyo thread nahisi kama ameandika jk mwenyewe. Kama siyo, basi ni mwanawe. Haina mashiko. Ni upuuzi tu wa kutughiribu.
 
somebody please shoot me!! yaani he is now a hero? really?

Nadhani Maggid ameliangalia jambo hili wa mtazamo wa haraka bila mizania. Kumwita kikwete shujaa au mtu katika historia sikubaliani nako. Kikwete amekuwepo katika Serikali kwa miaka zaidi ya 20. Marekebisho mengi na vikao vingi vilivyozunguzia katiba alikuwepo. Hakuna mahali aliponukuliwa akionyesha ''vision'' yake kuhusu hilo. Hata plae Mwanasheria mkuu Jaji Warioba alipopinga katiba mpya Kikwete alikuwa kimya.
Wapinzani walidai katiba mwaka 2005 alikaa kimya akijua iliyopo itampeleka 2015. Leo kuna pressure kutoka katika umma ambayo imemlazamisha kukubaliana na matakwa ya wananchi, tumwite shujaa? Mbona Kombani alipotoa kauli si Ikulu wala rais aliyekemea. Mbona Werema alipobwata rais hakukemea! Hawa si wateule wake? Walizungumza kama msimamo wa Kikwete. Leo CUF na Chadema wameanza kuandamana JK anaitwa shujaa, kwa lipi.
Na sijui tumwamini vipi JK, maana mambo yote aliyowahi kusema yamezikwa. Tume ya kuchunguza EPA, Madini, orodha ya majambazi na wauza unga n.k. Leo ni miaka 3 serikali yake haijatumbia Richmond, Kagoda, meremeta ni nini. Leo hajatuambia nani anamiliki Downs, leo hatujui Radar walishiriki akina nani. Yote haya yametokea JK akiwa kiongozi wa serikali za awamu zote, Sijui hili la katiba nitamuamini kwa kutumia busara gani. Alichokifanya ni kushusha joto la matatizo yanayomwandama, sasa tusubiri dana dana, tume itakabidhi taarifa June 2015, na mabadiliko yataanza Januari 2016. Tume ni njia rahisi ya JK kuwapooza Watanganyika, amefanya hivyo mara nyingi na kufanikiwa. Jiulize tume ya AG, IGP na PCCB imeishia wapi kama si usanii tu.
Kama historia itakuwa sahihi basi JK ataingia kwa kulea wizi, ubadhirifu na marafiki waharibifu. Itamhukumu JK kwa kuliingiza taifa kwenye grand corruption, his cronies, allies and culprits get away with it.
Kiongozi anyefanya kazi kwa mashinikizo hana vision wala ushujaa.
 
Nimesoma maelezo mengi ya Majjid lakini sijaona ni wapi JK kafanya maajabu au kuandika historia.

1. Suala la Katiba Mpya halijawahi kuwa suala la CCM wala Serikali yake. Sasa hivi maji yamezidi unga hana choice.

2. Katika Kampeni CHADEMA walilibeba kama agenda kuu. In some occassion CUF walilimention kiaina

3.Kuna uwezekano kuwa CUF walitonywa kupitia ndoa yao na CCM Zanzibar kuwa JK atalizungumzia katika hotuba hii, wakafanya maandamano ya kudai katiba mpya huku wakipeleka rasimu ambayo haijibu mahitaji yote ya Katiba. Hii ilikuwa ni kugain-popularity

4. Chimbuko la NCCR lilikuwa ni vuguvugu la vyama vingi na Katiba mpya. Niko aware Dr. Mvungi kwa kupitia research mbalimbali anayo draft ya "Katiba Mpya" ambayo ina-address mahitaji yote ya sasa na baadaye.

5. Njia sahihi: Mchakato huu ni vema uanzie ndani ya Bunge. Hili si suala la serikali ni la Wananchi ambao wawakilishi wao wako Bungeni.
 
Back
Top Bottom