Dingswayo
JF-Expert Member
- May 26, 2009
- 4,019
- 2,923
http://www.habarileo.co.tz/kitaifa/?n=3699
MTOTO wa Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, Profesa Juma Kapuya, hajulikani alipo, kajificha ili wananchi wasimdhuru.
Kijana huyo aliyetajwa kwa jina la Baraka aliwatoroka wananchi wenye hasira muda mfupi baada ya mlinzi katika hoteli ya baba yake kudaiwa kumuua mwanafunzi kwa kumpiga risasi kwenye ukumbi wa disko Jumapili usiku.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tabora, Emson Mmari,amesema,walitaka kumshambulia mlinzi huyo, akawatoroka, walipomkosa wakataka kumshambulia Baraka, akakimbia kujikoa na hadi sasa haijulikani yupo wapi.
"Huyu Baraka kwa taarifa nilizozipata, wananchi baada ya kumkosa mlinzi wake, walimsaka na kurusha mawe kwenye dirisha la chumba chake, lakini aliwatoroka na kuingia kwenye gari na kukimbia," amesema Mmari jana.
Amesema,wameshindwa kupata thamani ya hasara kwa vile wenye jengo hilo hawapo,kwa sababu Baraka angewasaidia kuwaeleza thamani ya vitu hivyo haijulikani aliko.
"Sisi huyu hatumtafuti ila amekimbia hasira za wananchi ambao walitaka kumdhuru," amesema.
Kwa mujibu wa Mmari, Polisi wa Tabora walizuia wananchi hao wasiichome moto hoteli ya Millennium inayomilikiwa na Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana,Profesa Juma Kapuya, Jumapili usiku,imefahamika.
Wananchi walipandwa na jazba baada ya mlinzi wa hoteli hiyo kudaiwa kumuua mwanafunzi aliyekuwa anacheza disko kwenye ukumbi wa hoteli hiyo wakataka kuichoma moto hoteli hiyo.
Amesema jana kuwa, baada ya mwanafunzi huyo kuuawa, wananchi walipandwa na jazba, wakavunja viti, vyombo vya muziki, na vioo vya madirisha ya hoteli hiyo ili kulipiza kisasi.
Mmari amesema, hata magari yaliyokuwa eneo hilo, pikipiki, na baiskeli viliharibiwa,maduka yaliyopo kwenye jengo hilo yalivunjwa,na kwamba wanachi hao walipora vitu vilivyokuwa humo.
Amesema,baada ya uharibifu huo, baadhi ya wananchi waliandaa mpango wa kuliunguza jengo hilo, lakini kwa bahati nzuri polisi waliwahi kufika na kuvuruga mpango huo.
"Polisi waliitwa na walipofika eneo hilo waliwatawanya wananchi hao wenye hasira, lakini kuna uharibifu mkubwa umefanywa na watu hao na wengine walishaandaa mafuta wakitaka kulichoma jengo hilo maarufu kama Millennium House," amesema Mmari.
Amesema, polisi wameendelea kuweka ulinzi kwenye hoteli hiyo ili yasitokee madhara zaidi.
"Tumeweka ulinzi kuzuia hasara zaidi," alisema na kuongeza kuwa bado hajajua hasara iliyopatikana kutokana na uharibifu huo.
Akielezea chanzo cha vurugu ndani ya disko hilo, Mmari alisema ni msuguano kati ya mlinzi na baadhi ya vijana waliokuwa kwenye disko na katika ugomvi huo, baadhi ya vijana walijaribu kumnyang'anya silaha.
Amesema, mlinzi huyo alipofyatua risasi na kumpata kijana mmoja na ndipo wananchi wakapandisha hasira na kumfanya mlinzi huyo akimbie.
Hata hivyo, Kamanda Mmari amesema, mlinzi huyo amekamatwa mjini Tabora, yupo polisi.
Mwanafunzi aliyeuawa kwenye tukio hilo anatajwa kwa jina la Majuto aliyekuwa anasoma katika sekondari ya Ushokola mjini Kaliua na alizikwa Jumatatu.
Kamanda Mmari amesema,polisi wanafanya uchunguzi wa awali kuhusu mauaji ya mwanafunzi huo,utakapokamilika watamfikisha mahakamani mlinzi kumfungulia mashitaka ya mauaji.
MTOTO wa Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, Profesa Juma Kapuya, hajulikani alipo, kajificha ili wananchi wasimdhuru.
Kijana huyo aliyetajwa kwa jina la Baraka aliwatoroka wananchi wenye hasira muda mfupi baada ya mlinzi katika hoteli ya baba yake kudaiwa kumuua mwanafunzi kwa kumpiga risasi kwenye ukumbi wa disko Jumapili usiku.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tabora, Emson Mmari,amesema,walitaka kumshambulia mlinzi huyo, akawatoroka, walipomkosa wakataka kumshambulia Baraka, akakimbia kujikoa na hadi sasa haijulikani yupo wapi.
"Huyu Baraka kwa taarifa nilizozipata, wananchi baada ya kumkosa mlinzi wake, walimsaka na kurusha mawe kwenye dirisha la chumba chake, lakini aliwatoroka na kuingia kwenye gari na kukimbia," amesema Mmari jana.
Amesema,wameshindwa kupata thamani ya hasara kwa vile wenye jengo hilo hawapo,kwa sababu Baraka angewasaidia kuwaeleza thamani ya vitu hivyo haijulikani aliko.
"Sisi huyu hatumtafuti ila amekimbia hasira za wananchi ambao walitaka kumdhuru," amesema.
Kwa mujibu wa Mmari, Polisi wa Tabora walizuia wananchi hao wasiichome moto hoteli ya Millennium inayomilikiwa na Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana,Profesa Juma Kapuya, Jumapili usiku,imefahamika.
Wananchi walipandwa na jazba baada ya mlinzi wa hoteli hiyo kudaiwa kumuua mwanafunzi aliyekuwa anacheza disko kwenye ukumbi wa hoteli hiyo wakataka kuichoma moto hoteli hiyo.
Amesema jana kuwa, baada ya mwanafunzi huyo kuuawa, wananchi walipandwa na jazba, wakavunja viti, vyombo vya muziki, na vioo vya madirisha ya hoteli hiyo ili kulipiza kisasi.
Mmari amesema, hata magari yaliyokuwa eneo hilo, pikipiki, na baiskeli viliharibiwa,maduka yaliyopo kwenye jengo hilo yalivunjwa,na kwamba wanachi hao walipora vitu vilivyokuwa humo.
Amesema,baada ya uharibifu huo, baadhi ya wananchi waliandaa mpango wa kuliunguza jengo hilo, lakini kwa bahati nzuri polisi waliwahi kufika na kuvuruga mpango huo.
"Polisi waliitwa na walipofika eneo hilo waliwatawanya wananchi hao wenye hasira, lakini kuna uharibifu mkubwa umefanywa na watu hao na wengine walishaandaa mafuta wakitaka kulichoma jengo hilo maarufu kama Millennium House," amesema Mmari.
Amesema, polisi wameendelea kuweka ulinzi kwenye hoteli hiyo ili yasitokee madhara zaidi.
"Tumeweka ulinzi kuzuia hasara zaidi," alisema na kuongeza kuwa bado hajajua hasara iliyopatikana kutokana na uharibifu huo.
Akielezea chanzo cha vurugu ndani ya disko hilo, Mmari alisema ni msuguano kati ya mlinzi na baadhi ya vijana waliokuwa kwenye disko na katika ugomvi huo, baadhi ya vijana walijaribu kumnyang'anya silaha.
Amesema, mlinzi huyo alipofyatua risasi na kumpata kijana mmoja na ndipo wananchi wakapandisha hasira na kumfanya mlinzi huyo akimbie.
Hata hivyo, Kamanda Mmari amesema, mlinzi huyo amekamatwa mjini Tabora, yupo polisi.
Mwanafunzi aliyeuawa kwenye tukio hilo anatajwa kwa jina la Majuto aliyekuwa anasoma katika sekondari ya Ushokola mjini Kaliua na alizikwa Jumatatu.
Kamanda Mmari amesema,polisi wanafanya uchunguzi wa awali kuhusu mauaji ya mwanafunzi huo,utakapokamilika watamfikisha mahakamani mlinzi kumfungulia mashitaka ya mauaji.
Last edited by a moderator: