Hospitali kutoa service muda wa usiku huku customer care level mbovu!

bg_dg_dy

JF-Expert Member
Feb 27, 2009
603
488
Hivi nini maana ya kuwepo na 24Hrs service kwenye hospital na wakati mida ya usiku kuna kuwa na poor customer care level,

Nilienda juzi mida ya saa tano usiku nilimpeleka mgonjwa hospitali ya hubert kairukii memorial , kuingia tu main entrance nikawakuta manurse na doctors (if not medical assistants) wanapiga soga tu kwenye bench la kuchukulia namba, kusonga mbele nikakutana na kidada kimoja reception hicho kiko busy chazungumza na simu huku anachukua maelezo ya mgonjwa wangu then akatuelekeza kwenda chumba cha kuonana na daktari ambae kwa wakati huo hakuwepo. Tumesubiria nusu saa katokea cjui alikokuwepo (imagine kwa mfano km mgonjwa angekuwa seriously ill?)

Hivi kweli ni haki kwa hospitali kuweka masaa 24 huku kukiwa na huduma kwa wateja mbovu?

Hubert Kairuki memorial hospital pamoja na hospitali zingine please jirekebisheni, Uongozi wa kila hospitali ufatilie huduma itolewayo na wafanyakazi wa shift za usiku, msiruhusu majina na hadhi nzuri za hospitali zenu ziharibiwe na hawa wazembe.
 
Mkuu hospitali za Bongo usiku kama mgonjwa wako hajazidiwa sana wala usijisumbue,hata akizidiwa afadhali mpeleke Muhimbili toa chai kidogo( sipendi lakini nifanyeje) atahudumiwa vizuri.Private zote watatuliza maumivu/labda kumlaza na shughuli yote itaanza asubuhi.
Nenda Nairobi ndio utajua namna 24hrs inavyofanya kazi hadi raha,daktari anaitwa saa 8 usiku na anafanya upasuaji muda huo.
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom