Hivi Hosea si alisema Ph.D yake alifanyia USA? Au aliacha kule na kuja kuanza upya UDSM.
Maelezo aliyoyatoa kwenye tuhuma zake huenda yana utata.
Jamaa ana Ph.D ya rushwa TZ na bado mambo ya rushwa yanamgonga, hapo tatizo sio elimu, tatizo ni watu wenyewe waliopewa hayo majukumu.
Hosea atunukiwa PhD
2007-11-25 12:38:28
Na Godfrey Monyo
Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Dk. Edward Hosea, ametunikiwa shahada ya juu ya udaktari (PhD) katika fani ya sheria.
Alifanya utafiti kwenye eneo hilo la mapambano dhidi ya rushwa nchini Tanzania: Nguvu ya ushahidi wa mazingira.
Dk. Hosea ni miongoni mwa wanachuo 3,739 wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, waliotunukiwa shahada mbalimbali na Mkuu wa Chuo Balozi Flugence Kazaura,katika mahafali ya 37 yaliyofanyika jana chuoni hapo. Takwimu zinaonyesha kuwa idadi ya wanawake waliohitimu walikuwa 1,376.
Akizungumza muda mfupi baada ya kutunukiwa shahada hiyo Mkurugenzi wa TAKUKURU alisema elimu aliyopata itamuongezea kiwango cha ujuzi na maarifa katika utendaji kazi.
Alisema pamoja na kupanua uelewa amekuwa na zana kamilifu za kitaaluma za kupambanua mambo na kufanya kazi kwa viwango vya juu kiufanisi na kwa umahiri.
``Nashukuru kupata shahada lengo langu ni kuwatumikia wananchi kikamilifu. Lakini pia hatua hii iwe changamoto kuwa kusoma hakuna mwisho unaweza kujiendeleza hata ukiwa kazini� tusichoke kusoma,`` alisema Dk. Hosea aliyechukua miaka mitatu kukamilisha PhD yake.
Alipata shahada ya kwanza ya Sheria katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na ya pili aliichukulia nchini Canada.
Katika shehere hiyo ya mahafali Chuo Kikuu kilitangaza mkakati wa kuboresha elimu pamoja na shughuli zinazoendeshwa na taasisi hiyo ya elimu ya juu kwa kuunda kitengo maalumu cha kuhakiki na kudumisha viwango vya ubora.
Makamu Mkuu wa Chuo Profesa Rwekaza Mukandala, alisema katika hotuba yake kuwa kitengo hicho kitakachoanzishwa hivi karibuni kitadumisha viwango vya ubora katika kufundisha, kutafiti na kutoa huduma za kijamii.
``Moja ya majukumu muhimu ya kitengo ni kuhakikisha kuwa viwango vya elimu vinaboreshwa, ufundishaji unaangalia upya namna ya kuboresha programu zao mara kwa mara ili zilingane na viwango na taratibu zinazokubalika kimataifa,``alisema Makamu Mkuu wa Chuo.
Aliwaambia wahitimu na wageni mbalimbali kuwa lengo kuu la kuangalia upya progamu hizo mara kwa mara ni kuhakiki, kuboresha na kudumisha ubora wa progamu zinazofundishwa.
``Kitengo hiki kitafanya kazi bega kwa bega na wakuu wa vitivo na idara ili kuiwezesha menejimenti ya chuo kuwa na taarifa wakati wote juu ya changamoto zinazokabili ubora wa utendaji kazi kila zinapotokea ili kuchukua hatua za haraka kukabiliana nazo,\"alisema Profesa Mukandala.
Profesa Mukandala alisema Baraza la chuo hicho limeidhinisha sera mpya ya uhakiki wa ubora kwa ajili ya chuo kikuu, sera ambayo iko mbioni kutumika.
Katika tukio hilo, Makamu Mkuu wa Chuo alimtangaza Profesa Pius Yanda kuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel.
Alisema: ``Mwaka huu mmoja wetu Profesa Yanda alishiriki katika paneli juu ya mabadiliko ya hali ya hewa duniani ambapo yeye na wenzake akiwemo Makamu wa Rais wa zamani wa Marekani Bw. Al-Gore wamepata Tuzo ya Nobel,``alisema Profesa Mukandala na kumpongeza kwa dhati kwa ushindi huo ulioipa heshima Tanzania.
Alizungumzia suala la udahili na kuongeza kuwa nia si kupunguza idadi ya udahili bali pia kuweka mikakati ya maendeleo ya muda mrefu.
``Mkakati huu utajumuisha kuongeza kasi ya upanuzi wa udahili katika baadhi ya programu za mafunzo na katika viwango fulani na wakati huo huo kuongeza au kupunguza idadi ya wanafunzi katika fani nyingine, `` alisema.
Alisema mjadala wa namna ya kupunguza wanafunzi katika fani fulani na kutekeleza mkakati huo yanaendelea.
Akizungumza uhaba wa walimu na jitihada za kuongeza wanataaluma wa kufundisha sekondari na shule za msingi Profesa Mukandala alisema Chuo Kikuu kitatoa kipaumbele katika programu ya shahada ya kwanza kwa kupanua udahili katika fani ya elimu na kuboresha programu nyingine zinazofungamana na ualimu.
``Pia tunahitaji kuzipa umuhimu fani za sayansi, teknolojia na biashara kutokana na umuhimu wake katika maendeleo ya nchi na uhitaji wa taaluma hizo katika soko la ajira.``
SOURCE: Nipashe
Maelezo aliyoyatoa kwenye tuhuma zake huenda yana utata.
Jamaa ana Ph.D ya rushwa TZ na bado mambo ya rushwa yanamgonga, hapo tatizo sio elimu, tatizo ni watu wenyewe waliopewa hayo majukumu.
Hosea atunukiwa PhD
2007-11-25 12:38:28
Na Godfrey Monyo
Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Dk. Edward Hosea, ametunikiwa shahada ya juu ya udaktari (PhD) katika fani ya sheria.
Alifanya utafiti kwenye eneo hilo la mapambano dhidi ya rushwa nchini Tanzania: Nguvu ya ushahidi wa mazingira.
Dk. Hosea ni miongoni mwa wanachuo 3,739 wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, waliotunukiwa shahada mbalimbali na Mkuu wa Chuo Balozi Flugence Kazaura,katika mahafali ya 37 yaliyofanyika jana chuoni hapo. Takwimu zinaonyesha kuwa idadi ya wanawake waliohitimu walikuwa 1,376.
Akizungumza muda mfupi baada ya kutunukiwa shahada hiyo Mkurugenzi wa TAKUKURU alisema elimu aliyopata itamuongezea kiwango cha ujuzi na maarifa katika utendaji kazi.
Alisema pamoja na kupanua uelewa amekuwa na zana kamilifu za kitaaluma za kupambanua mambo na kufanya kazi kwa viwango vya juu kiufanisi na kwa umahiri.
``Nashukuru kupata shahada lengo langu ni kuwatumikia wananchi kikamilifu. Lakini pia hatua hii iwe changamoto kuwa kusoma hakuna mwisho unaweza kujiendeleza hata ukiwa kazini� tusichoke kusoma,`` alisema Dk. Hosea aliyechukua miaka mitatu kukamilisha PhD yake.
Alipata shahada ya kwanza ya Sheria katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na ya pili aliichukulia nchini Canada.
Katika shehere hiyo ya mahafali Chuo Kikuu kilitangaza mkakati wa kuboresha elimu pamoja na shughuli zinazoendeshwa na taasisi hiyo ya elimu ya juu kwa kuunda kitengo maalumu cha kuhakiki na kudumisha viwango vya ubora.
Makamu Mkuu wa Chuo Profesa Rwekaza Mukandala, alisema katika hotuba yake kuwa kitengo hicho kitakachoanzishwa hivi karibuni kitadumisha viwango vya ubora katika kufundisha, kutafiti na kutoa huduma za kijamii.
``Moja ya majukumu muhimu ya kitengo ni kuhakikisha kuwa viwango vya elimu vinaboreshwa, ufundishaji unaangalia upya namna ya kuboresha programu zao mara kwa mara ili zilingane na viwango na taratibu zinazokubalika kimataifa,``alisema Makamu Mkuu wa Chuo.
Aliwaambia wahitimu na wageni mbalimbali kuwa lengo kuu la kuangalia upya progamu hizo mara kwa mara ni kuhakiki, kuboresha na kudumisha ubora wa progamu zinazofundishwa.
``Kitengo hiki kitafanya kazi bega kwa bega na wakuu wa vitivo na idara ili kuiwezesha menejimenti ya chuo kuwa na taarifa wakati wote juu ya changamoto zinazokabili ubora wa utendaji kazi kila zinapotokea ili kuchukua hatua za haraka kukabiliana nazo,\"alisema Profesa Mukandala.
Profesa Mukandala alisema Baraza la chuo hicho limeidhinisha sera mpya ya uhakiki wa ubora kwa ajili ya chuo kikuu, sera ambayo iko mbioni kutumika.
Katika tukio hilo, Makamu Mkuu wa Chuo alimtangaza Profesa Pius Yanda kuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel.
Alisema: ``Mwaka huu mmoja wetu Profesa Yanda alishiriki katika paneli juu ya mabadiliko ya hali ya hewa duniani ambapo yeye na wenzake akiwemo Makamu wa Rais wa zamani wa Marekani Bw. Al-Gore wamepata Tuzo ya Nobel,``alisema Profesa Mukandala na kumpongeza kwa dhati kwa ushindi huo ulioipa heshima Tanzania.
Alizungumzia suala la udahili na kuongeza kuwa nia si kupunguza idadi ya udahili bali pia kuweka mikakati ya maendeleo ya muda mrefu.
``Mkakati huu utajumuisha kuongeza kasi ya upanuzi wa udahili katika baadhi ya programu za mafunzo na katika viwango fulani na wakati huo huo kuongeza au kupunguza idadi ya wanafunzi katika fani nyingine, `` alisema.
Alisema mjadala wa namna ya kupunguza wanafunzi katika fani fulani na kutekeleza mkakati huo yanaendelea.
Akizungumza uhaba wa walimu na jitihada za kuongeza wanataaluma wa kufundisha sekondari na shule za msingi Profesa Mukandala alisema Chuo Kikuu kitatoa kipaumbele katika programu ya shahada ya kwanza kwa kupanua udahili katika fani ya elimu na kuboresha programu nyingine zinazofungamana na ualimu.
``Pia tunahitaji kuzipa umuhimu fani za sayansi, teknolojia na biashara kutokana na umuhimu wake katika maendeleo ya nchi na uhitaji wa taaluma hizo katika soko la ajira.``
SOURCE: Nipashe