Amanikwenu
Senior Member
- Dec 1, 2009
- 187
- 0
Kwangu mimi moja ya sasabu kuu ya kumfanya Kikwete akubali suala la kuwa na katiba mpya ni fedheha ya kusubiri kupewa maelekezo na Bunge nini Serikali inapasa kufanya kuhusu suala la kuwa na katiba mpya. Kitendo cha John Mnyika kupeleka hoja binafsi katika ofisi za Bunge kutaka Bunge litoe muongozo kuhusu uundaji wa katiba Mpya naamini kimechangia sana kumfanya Kikwete akubali suala la kuwa na Katiba Mpya japo kwa shingo upande vinginevyo angebaki peke yake. Kwa hili nampongeza sana Mbunge John Mnyika kwa kile alichokifanya kwa faida ya Watanzania.