Hongera Prof Tibaijuka kwa 2009 Göteborg Award

Ngareni3

Member
Dec 4, 2006
31
2
Wana JF
Itatoa furaha kubwa pale ambapo watanzania wenzetu wanang'ara katika anga za kimataifa. Si michezo tu (Hasheem) ila sasa katika anga za kitaaluma ambapo Mama yetu, Mwalimu wetu Prof Ana Tibaijuka naye ameteuliwa miongoni mwa washindi wa Nobel Prize katika mazingira inayotolewa na Goteborg University Huko Sweden.
Twampongeza sana, na kwa waliosoma Chuo Kikuu Dar, enzi hizo akiwa Economic Research Bureau (ERB) tunamkumbuka sana.
Mwenyezi Mungu aendelee kufungua nyota zetu katika anga za juu.

Mama Hongera. Naambatanisha Taarifa yenyewe, usiseme nimeizusha....

UN-HABITAT’s Executive Director Mrs. Anna Tibaijuka has been named one of three winners of the 2009 Göteborg Award, the prestigious “Nobel Prize in Environment”.

The G öteborg Award now celebrating its tenth year, conferred its jubilee prize of one million Swedish Kroner (USD 126,775) to be shared equally between Mrs. Tibaijuka, Mr. Enrique Peñalosa, the former mayor of Bogotá, Colombia, and Mr. Sören Hermansen, of Samsö, Denmark who was named by Time Magazine as a 2008 Hero of the Environment. Last year’s winners included Mr. Al Gore the former US Vice-President and global environment champion.

“We are thrilled to award our jubilee prize to these brilliant visionaries, strategists and system transformers,” said Mr. Stefan Edman, Chairman of the Award Jury since its conception in 2000. The Award was established by the City of Göteborg and several interested companies in 1999 to “stimulate further positive developments and recognize strategic work for national and international sustainable development”.

Mrs. Anna Tibaijuka thanked Mr. Stefan Edman and the members of the jury. "I am honored to be given this award. I accept it with humility and on behalf of all of my colleagues. This recognition comes at an opportune time. With over 50% of humanity now living in urban areas, the award highlights the urgent need for sustainable urbanization for the future of the planet," said Mrs. Tibaijuka, who was launching UN-HABITAT's campaign on sustainable urbanization in the Pacific region when she heard the news.

The award is funded by the City of Göteborg together with the Second Swedish National Pension Fund, Carl Bennet AB, Elanders AB, Eldan Recycling, Folksam, Götaverken Miljö, Handelsbanken, Nor*dea, Peab, Schenker AB and SKF.

The Jury panel said in its announcement of the 2009 winners: “Each one comes from a separate continent and they are, locally and globally, knowledgeable, engaged and impatient doers. They are ambassadors for one of the most decisive factors for humanity – the battle for sustainable development in the cities and towns around the globe.”

The Award winners will receive their prize at a prize ceremony on the 26th of November in Göteborg. For details and the citations
 
Hongera mama unastahili hiyo tuzo, nasubiria haters hapa sijui watoka na lipi...Kuhani et al na Dilunga et al...
 
Finally we have a laureate, tutatoka tu mwaka huu.

ABA, hongera Tibaijuka.
 
Hongera mama. Lakini hii sio Nobel Prize ndo maana wakaiweka kwenye " ". Yaani its considered the "Nobel Prize" of the environment, thread title ina miss-lead.
 
Thanks Kang for straightening up,hata mimi hapa nilitaka kushangaa, nafikiri labda hizi ni sub-nobel za mazingira--labda!!!!!!


Any way hongera mama Tibaijuka, but what the role model did you play for your country on urbanising our poor Villages as top head of HABITAT. we better ask ourselves pamoja na kwamba tunatoa Hongera nyingi kwa huyu mama
 
Haya mambo ya kumsifia mtu kwa sababu tu kashinda kitu fulani yamebaki tu kwa watz;nchi zingine huwa scholars wanasifiwa kwa kila walichoifanyia jamii inayowazunguka!

Mama Tibaijuka kawa na nafasi nzuri sana kwenye UN hasa ile ya huduma za makazi;kitengo chenye miradi lukuki UN lkn alifanya nini kuwasadia japo watz wachache wenye matatio ya makazi?Si ni huyu Mama aliyepeleka miradi mingi ya makazi ya UN Kenya?
Nasisitiza tuache kusifia sura,tusifie kwa yale waliyotufanyia!mama huyu na mwenzake mama Migiro wote ni sifuri na nitashangaa kama mtazidi kuwasifia,tuzo yake aipambe nyumbani kwake hana faida na sisi!
 
Hongera Sana Mama.

Kuna kipindi hapa petu alikuwa na harakati za kuanzisha "Baraza za wanawake" sijui kama kulikuwa na mizengwe. Au ndo hivyo tena kuwa "Nabii Hakubaliki Nyumbani"?
 
Hongera mama. Lakini hii sio Nobel Prize ndo maana wakaiweka kwenye " ". Yaani its considered the "Nobel Prize" of the environment, thread title ina miss-lead.

Thanks Kang kwa kuweka hili sawa... "The Nobel Prize" na "The Göteborg Award" ni vitu viwili tofauti jamani mbona tunaleteana mauza uza na hizi heading kama za magazti ya porojo..!!!

Kwa wasiofahamu; Nobel Prize imeanzishwa 1895 na hii aliyoshinda Mama yetu Tibaijuka imeanzishwa 1999.

Hongera Prof Tibaijuka kwa mafanikio haya.

---------------------------------------------------------------------

Kwa wale wanaomlaumu Prof Tibaijuka kwamba hajafanya maendeleo Tanzania hawajui walisemalo. Huyu Mama miaka 95 alikuwa anaongoza Umoja wa Wanawake (jina limenitoka) Serikali ilimpa kasheshe sana, pamoja na kuzushiwa kasfa kibao....yote hayo tunajua yalikuwa na sababu za "kisiasa". Hilo ndilo tunalolijua Tanzania, kila kitu ni siasa, siasa, siasa.

Tanzania ina wataalamu wengi sana ndani na nje lakini sio wote wanaotaka kujiingiza kwenye CCM au chama chochote. Wanataka wabakie kuwa Walimu, Washauri, Ma-engineer, Madaktari n.k lakini watumie ujuzi wao kuleta maendeleo Tanzania. Wanakwamishwa kila kukicha na wajinga wajinga wasiojua kitu lakini wana vyeo vya kisiasa. Vyeo vyenyewe walivipata kwa uchaguzi ulioshikisha 30% ya wapiga kura wote waliojiandikisha....upuuzi mtupu.
 
Hongera Mama Tibaijuka!!! Ndugu zangu huyu anayo stahili kabisa na haki ya kupata tunu hio. Sio kweli amenufaisha Kenya kwa miradi ya UN Habitat. Makao makuu ya UN Habitat yako Nairobi. Kwa wale tunaofanya kazi sekta ya nyumba, ardhi na makazi, (housing, lands and human settlement) tunafahamu Tanzania imenufaika vipi na kazi za Mama. Miradi ya kuraslimisha ardhi kwenye makazi yasiyo maalumu, ya kuboresha makazi holela ( mifano ni mingi, kule darajani Arusha, pale Manzese Dar, kule Kilimani Mbeya nk), semina na mihadhara mingi ihusiyo sekta zetu imepata ufadhili mkubwa kutoka UN Habitat na hasa katika miradi kama ile ya pro-pool land tools. Upande wa mazingira sio tu kwenye makazi holela hata kwenye miji, amesaidia sana kubuni miradi ya kusaidia nchi zinazoendelea kuwa na miji endelevu. Mifano nayo ni mingi.

Watanzania tufikie wakti wa kumtuza yule anayefanya mema na mazuri kama mama huyu, na sio lawama hata pale tusipokuwa na elimu au taarifa ya kina cha kutosha. Hujafanya utafiti, huna ruhusa ya kuzungumza. Nawasilisha Mkuu
 
Haya mambo ya kumsifia mtu kwa sababu tu kashinda kitu fulani yamebaki tu kwa watz;nchi zingine huwa scholars wanasifiwa kwa kila walichoifanyia jamii inayowazunguka!

Mama Tibaijuka kawa na nafasi nzuri sana kwenye UN hasa ile ya huduma za makazi;kitengo chenye miradi lukuki UN lkn alifanya nini kuwasadia japo watz wachache wenye matatio ya makazi?Si ni huyu Mama aliyepeleka miradi mingi ya makazi ya UN Kenya?

Nasisitiza tuache kusifia sura,tusifie kwa yale waliyotufanyia!mama huyu na mwenzake mama Migiro wote ni sifuri na nitashangaa kama mtazidi kuwasifia,tuzo yake aipambe nyumbani kwake hana faida na sisi!


Watanzania tunatia huruma.
 
Hongera mama. Lakini hii sio Nobel Prize ndo maana wakaiweka kwenye " ". Yaani its considered the "Nobel Prize" of the environment, thread title ina miss-lead.



We don't have a laureate after all!

Jamani doublecheck your story kabla ya kupost.Mimi nilitaka kumu exonerate huyu mama kwa heshima ya Nobel, nikajua Nobel asingeweza kupewa kama ana mushkeli, kumbe hata Nobel siyo?

Nilishaona tumewajibu Wakenya na yao ya mama Waathari, nikashangaa kidogo kwamba zawadi hizi hutolewa kijiografia pia itakuwaje east africa tushinde kimpigo mpigo hivi? kumbe safari bado ndefu.

Jamani a Nobel is something else na hizi habari za Nobel za uchochoroni hazifai hata kuitwa hivyo kwenye mabano.

Ama sivyo na mi nitajiita Nobel laureate wa kimanzichana institute of ramli.
 
Hongera sana mama, umeweza, na umetuinua watanzania katika anga za kimataifa! ufike mbali mama.
 
Nasikia Prof ananyemelea kajimbo ka Masilingi. Yeye akiwa pamoja na yule mstaafu kamishna wa kanda maalum ya dar.
 
Back
Top Bottom