Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,460
- 39,928
Anusurika kifo akidhaniwa albino
* Wavuvi waliomvamia wauawa na wananchi
* Mwingine anaswa na mifupa ya binadamu
NA PETER KATULANDA, MWANZA (Uhuru)
MWANAFUNZI wa darasa la kwanza, katika Shule ya Msingi Nyamatongo, wilayani Sengerema, Martha Hussein (10), amejeruhiwa kwa kukatwa panga sehemu ya jicho, baada ya kuvamiwa akidhani albino.
Mbali na hilo, polisi mkoani Mwanza wanamshikilia mwanamke anayetuhuma kukutwa na mifupa inayodhaniwa kuwa ya binadamu.
Martha alivamiwa Machi 12, mwaka huu, saa 12.00 asubuhi, ambapo waliomvamia waliuawa na wananchi.
Tukio hilo lilithibitishwa na serikali ya kijiji cha Nyamatongo na Kaimu Kamanda wa Polisi, Elias Kalinga.
Ofisa Mtendaji wa kijiji cha Nyamatongo, Lucas Mashinge, alisema Martha alikumbwa na mkasa huo, baada ya watu wawili waliodaiwa kuwa wavuvi kumvamia wakidhani ni albino kutokana na weupe wake.
Alisema wavuvi hao wakiwa na mapanga walimshambulia Martha alipokuwa akielekea shule.
Mashinge alisema Martha aliokolewa na yowe lililopigwa na wenzake wanne aliokuwa ameongozana nao.
"Kelele za wenzake zilifanya watu wajitokeze haraka kwenye eneo la tukio na kuwakimbiza hadi walipowakamata watu hao waliotambulika kuwa wavuvi, wakiwa wamemjeruhi Martha sehemu ya juu na chini ya jicho la kulia," alisema Mashinge.
Alisema Martha si albino, isipokuwa rangi yake inashabihiana nao, hivyo kwa watu wasiomfahamu, hudhani kuwa ni albino.
Mashinge alisema waliouawa na wananchi wametajwa kwa jina moja la Seleman na Method, wanaokadiriwa kuwa na umri wa kati ya miaka 30 na 32.
Alisema kabla ya kuuawa kwa silaha za jadi, watu hao walipohojiwa na wananchi sababu za kumkamata mtoto huyo, walidai kutokana na rangi yake walidhani ni albino na kwamba, walikuwa wanataka viungo vyake.
Wakati huo huo, Suzana Sengerema (48), mkazi wa kata ya Katunguru, anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kukutwa na vipande vya mifupa inayosadikiwa kuwa ya binadamu.
Suzana alikamatwa Machi 15, mwaka huu saa nne usiku, katika mtaa wa Migombani, baada ya polisi kupata taarifa kutoka kwa raia mwema.
Taarifa za polisi zilisema baada ya kuhojiwa, Suzana alikiri kuwa mifupa hiyo ni ya binadamu na kwamba huisaga na kuitumia kwa matumizi mbalimbali, ikiwa ni pamoja na kuinywa.
Kaimu Kamanda Kalinga alisema mifupa hiyo itapelekwa kwa wataalamu kuthibitisha kama ni ya binadamu au la, kabla ya kumfikisha mahakamani.
My Take:
Niseme nini, hili lawezekana kuwa suluhisho la mauaji ya Albino. I think.
* Wavuvi waliomvamia wauawa na wananchi
* Mwingine anaswa na mifupa ya binadamu
NA PETER KATULANDA, MWANZA (Uhuru)
MWANAFUNZI wa darasa la kwanza, katika Shule ya Msingi Nyamatongo, wilayani Sengerema, Martha Hussein (10), amejeruhiwa kwa kukatwa panga sehemu ya jicho, baada ya kuvamiwa akidhani albino.
Mbali na hilo, polisi mkoani Mwanza wanamshikilia mwanamke anayetuhuma kukutwa na mifupa inayodhaniwa kuwa ya binadamu.
Martha alivamiwa Machi 12, mwaka huu, saa 12.00 asubuhi, ambapo waliomvamia waliuawa na wananchi.
Tukio hilo lilithibitishwa na serikali ya kijiji cha Nyamatongo na Kaimu Kamanda wa Polisi, Elias Kalinga.
Ofisa Mtendaji wa kijiji cha Nyamatongo, Lucas Mashinge, alisema Martha alikumbwa na mkasa huo, baada ya watu wawili waliodaiwa kuwa wavuvi kumvamia wakidhani ni albino kutokana na weupe wake.
Alisema wavuvi hao wakiwa na mapanga walimshambulia Martha alipokuwa akielekea shule.
Mashinge alisema Martha aliokolewa na yowe lililopigwa na wenzake wanne aliokuwa ameongozana nao.
"Kelele za wenzake zilifanya watu wajitokeze haraka kwenye eneo la tukio na kuwakimbiza hadi walipowakamata watu hao waliotambulika kuwa wavuvi, wakiwa wamemjeruhi Martha sehemu ya juu na chini ya jicho la kulia," alisema Mashinge.
Alisema Martha si albino, isipokuwa rangi yake inashabihiana nao, hivyo kwa watu wasiomfahamu, hudhani kuwa ni albino.
Mashinge alisema waliouawa na wananchi wametajwa kwa jina moja la Seleman na Method, wanaokadiriwa kuwa na umri wa kati ya miaka 30 na 32.
Alisema kabla ya kuuawa kwa silaha za jadi, watu hao walipohojiwa na wananchi sababu za kumkamata mtoto huyo, walidai kutokana na rangi yake walidhani ni albino na kwamba, walikuwa wanataka viungo vyake.
Wakati huo huo, Suzana Sengerema (48), mkazi wa kata ya Katunguru, anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kukutwa na vipande vya mifupa inayosadikiwa kuwa ya binadamu.
Suzana alikamatwa Machi 15, mwaka huu saa nne usiku, katika mtaa wa Migombani, baada ya polisi kupata taarifa kutoka kwa raia mwema.
Taarifa za polisi zilisema baada ya kuhojiwa, Suzana alikiri kuwa mifupa hiyo ni ya binadamu na kwamba huisaga na kuitumia kwa matumizi mbalimbali, ikiwa ni pamoja na kuinywa.
Kaimu Kamanda Kalinga alisema mifupa hiyo itapelekwa kwa wataalamu kuthibitisha kama ni ya binadamu au la, kabla ya kumfikisha mahakamani.
My Take:
Niseme nini, hili lawezekana kuwa suluhisho la mauaji ya Albino. I think.
Last edited by a moderator: