CCM wanavyohaha kuzima soo la RACHEL na kwa kauli ya Mkama nimeanza kuamini kweli RA ni rais.Pokea hongera zangu mheshimiwa rais kwa kufanya haya yafuatayo kwa ufanisi mkubwa.
1. Umepigana kufa na kupona na kuhakikisha Dr. Slaa hasikii harufu ya ikulu.
2. Hukulala usiku na mchana hadi ulipohakikisha Jakaya anaingia ikulu.
3. Umetumia kila linalowezekana kuhakikisha Sitta haukwai uspika.
4. Umepandikiza spika wako umpendae mama Makinda.
5. Umetumia hila za ajabu kuua upinzani rasmi bungeni - japo hujafanikiwa sana.
6. Umesaidia rafiki na wapambe wako kushika kamati nyeti za bunge.
7. Unajipanga kumsafishia njia swahiba wako Lowassa agombee 2015.
Kazi uliyofanya ni kubwa, tunakuzawadia kifuta jasho shilingi bilioni 94!