Hongera magufuli!!!

BONGOLALA

JF-Expert Member
Sep 14, 2009
16,508
11,881
Napenda kumpongeza mhe Magufuli kwa uamuzi wake wa kugawa samaki kwa wanaostahili bure.Amekaa akakumbuka kuwa serikali kazi yake si biashara!huo ndio utawala bora na mfano wa kuigwa katika maamuzi.Nakumbuka hata kazi za ukandarasi huyu bwana alikua akisaidia JKT kupata tenda nyingi za serikali.Hapo rushwa inakua zero maana.TOFAUTI NA MAFISADI TENDA HUWAPA WAHINDI NA MAKABURU hivyo pesa haimfikii mtanzania halisi.Mfano hai kwa nini TIPER haikupewa tenda ya kuleta mafuta ya IPTL na kustaajabisha mafuta hayo hayo yamehifadhiwa sasa kwenye tenki za TIPER baada ya deal kukamilika na TOTAL.SI WANGEHIFADHI HAO HAO TOTAL WALIOANDAA CHAKULA?Kisa Ukitaka kula muhimu ushirikiane na mfanyabiashara si taasisi ya umma cheque itatokaje!
 
Huh!...Unachoongea mkuu ni kweli tupu!
Nilifurahi sana kusikia kwamba hao samaki wanagawiwa bure kwa taasisi kama mashule, maana zingetumika njia za mnada, ni wachache ambao wangefaidi!
Bravol tena MAGUFULI, makeke yako bado tunayafeel!
 
Sijui kama tatizo ni waendesha mashtaka au ni mahakama, lakini muda iliochukua hadi kufikia uamuzi wa kugawa hao samaki umekuwa mrefu sana unnecessarily na kuligharimu taifa. Tunaweza kujifunza kitu hapa!
 
hata mimi pia nampongeza sana huyu jamaa, kwa kweli amefanya jambo la maana sana kwa kuchukua uamuzi wa kuwagawa hawa samaki. Maana sasa watanzania watafaidika na kuonja matunda ya nchi yao. Na hii imeleta historia kwa nchi na mpaka kuna mataifa kama Japan wanataka kuingia mkataba na tanzania kwa ajili ya uvuvi wa samaki kwa hiyo nchi itaingiza mapato mengi sana kutokana na mkataba huo. Lakini inasemekana kuwa hawa samaki wametumia gharama ya shilingi Bilioni 6 kuhifadhi toka siku waliyokamatwa lakini yeye mheshimiwa anasema tusiangalie gharama bali tuangalie nchi imefaidika vp na hili suala la kukamata wavuvi haramu. Heshima mbele wakuu
 
John Pombe Magufuli, you feel his vibration wherever he get placed. Hongera John, angalau umepooza machungu ya raia dhidi ya shaghalabaghala kibao za kiutendaji at different levels serikalini.
 
Huyu ndiye ilibidi awe waziri mkuu au Rais wa Tanzania lakini kwa ccm ilivyo watu kama hawa hawana nafasi
 
niliposikia nilifurahi sana alikuwa anahojiwa asubuhi na tbc yule dada kamkomalia eti hasara, ningemwona jasiri sana km angemfuata au angemwambia lowasa kaitia hasara nchii hii big up sana magufuli
 
Labda nielemishwe kimetokea nini mpaka samaki hawa wanagawiwa BURE. Ninachokumbuka, samaki waliwahi kupigwa mnada na Serikali hiyo hiyo na chini ya waziri huyohuyo. Walipigwa mnada na kampuni ya Mheshimiwa Yono, (Yono Auction Mart). Nikamsikia Mh. Yono akitamba TBC kuwa amewaalika wanunuzi wa kimataifa wa samaki, hivyo haitakuwa kazi kwake kuwauza. Siku ya mnada hakukuwa na mnunuzi wa kimataifa wala nini. Kama sijakosea aliuza sio zaidi ya tani moja. Hata alipogawa kwa mafungu ya tani kumikumi hakuna aliyeweza kununua. Mnada huo ukadoda. Hawakuuzika. Hata huo utaratibu wa kugawa bure utaborongwa tu. Wataishia kupelekwa Pugu Kinyamwezi.
Wakati mwingine ni kutumia muda mwingi kuzungumza. Hule dada aliyemhoji Magufuli TBC alikuwa sahihi kabisa.
 
Napenda kumpongeza mhe Magufuli kwa uamuzi wake wa kugawa samaki kwa wanaostahili bure.Amekaa akakumbuka kuwa serikali kazi yake si biashara!huo ndio utawala bora na mfano wa kuigwa katika maamuzi.Nakumbuka hata kazi za ukandarasi huyu bwana alikua akisaidia JKT kupata tenda nyingi za serikali.Hapo rushwa inakua zero maana.TOFAUTI NA MAFISADI TENDA HUWAPA WAHINDI NA MAKABURU hivyo pesa haimfikii mtanzania halisi.Mfano hai kwa nini TIPER haikupewa tenda ya kuleta mafuta ya IPTL na kustaajabisha mafuta hayo hayo yamehifadhiwa sasa kwenye tenki za TIPER baada ya deal kukamilika na TOTAL.SI WANGEHIFADHI HAO HAO TOTAL WALIOANDAA CHAKULA?Kisa Ukitaka kula muhimu ushirikiane na mfanyabiashara si taasisi ya umma cheque itatokaje!


Great!! ha ta mimi nili furahi!!...Magufuli kumbuka DODOMA SHINYANGA ARUSHA MTWARA>>
 
Ni sawa kabisa uamuzi aliochukua. Tena ningefurahi kusikia kuwa wamegawiwa taasisi kama za walemavu, watoto yatima, mashule hata magereza na hospitali.
Kujaribu kuwauza ilikuwa sahihi pia, na kama haikuwezekana basi uamuzi wa mwisho ndiyo huo. Na ninachoamini ni kwamba "to him there are big lessons learned" haswa kwa kuwa ameonyesha kufanya kitu kama hiki kwa mara ya kwanza. Hakika Magufuli alistahili kuwa Waziri Mkuu. Lakini bado hajakosa kabisa bado tunamatumaini ya yeye kufika hapo. Anaendelea kupata uzoefu na kukomaa maana tunamhitaji huko mbele tuendako.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom