Hongera JK,CCM

Lole Gwakisa

JF-Expert Member
Nov 5, 2008
4,728
2,259
tz%7Dccm.gif

Matukio ya wiki hii, hasa hili la CCM "kujivua Gamba" linastahili pongezi .
Kwa muda mrefu sasa waanzishi wa malumbano ndani na nje ya JF wamekuwa wakiifuatilia kwa makini sana muelekeo wa CCM kama chama tawala na JK akiwa mweyekiti wake.

Wengi wamelaumu ufisadi wa waziwazi uliofanyika baada ya JK na "mtandao" kuingia madarakani.
Wengi zaidi wamelaumu kushindwa kwa CCM kuchukua hatua kudhibiti ufisadi baada ya JK kuingia madarakani mwaka 2005.
Na wengine wengi zaidi wamemlaumu JK binafsi kwa kutowachukulia hatua watuhumiwa wa ufisadi.
Wapo walio hoji ukaribu wa JK na watuhumiwa hawa, hasa Edward Lowassa, Rostam Aziz na Chenge.

Mara nyingi JK amekuwa akiwapoza wanachama wa CCM na wananchi kwa ujumla kuwa hakuna ushahidi wa kutosha kuwahukumu moja kwa moja watuhumiwa hawa wa ufisadi, na TAKUKURU pia imeshindwa kupata ushahidi juu ya hilo.

Wananchi hawakufanya ajizi, na hapa navipongeza vyama vya upinzani kwa elimu waliyoitoa kwa wananchi.

Ufisadi ni mbaya , ufisadi ni kuingiza umaskini katika nchi,ufisadi unahujumu uchumi wa nchi.
Tumeona mikataba inayoumiza nchi(Richmond na sekta ya madini), tumeona madeni yanayotokana na mikataba feki kama ya Dowans(94bil),tumeona ununuzi wa vifaa vibovu(radar).

Kwa ujumla wananchi wamejionea madhara ya ufisadi katika muda huu wa kipindi kisichozidi miaka 10.
Chama kilikuwa katika wakati mbovu pengine kuliko wakati wowote katika uhai wake kikiwa chini ya katibu Mkuu wake Makamba ambaye hakuwa na ubavu, upeo wala mbinu za kudhibiti ufisadi.
Kwa bahati mbaya sana wahusika wakuu ndio hao hao walioko katika ngazi za juu katika uongozi wa chama, na ni marafiki wa karibu wa mwenyekiti wa chama tawala CCM.
Kampeni na uchaguzi wa mwaka 2010 ni kama umekizindua chama kutoka katika usingizi mzito wa kufikiri kitatawala milele Tanzania.
Kupungua kwa kiwango kikubwa kwa watu wanao muunga mkono mkuu wa nchi kutoka 82% mwaka 2005 hadi 61% mwaka 2010 ni mstuko tosha kwa chama tawala.
Pongezi zangu kwa JK na CCM ni kuelewa maana ya mstuko huo na madhara yake kwa CCM.

Kitendo cha kudhibiti kundi lile la watu watatu(EL, RA na Mzee wa Vijisenti) si tu imeleta muamko mpya wa watu kuona kuwa chama hakijatekwa na mafisadi bali pia kuona kuwa chama bado kinawasikiliza wanachama wake na wananchi kwa ujumla.
Kwa staili ya kuwaengua hawa mafisadi katika nafasi za juu za chama, chama kimeonyesha uwezo mkubwa wa kujirekebisha-kitu ambacho vyama vingi vya upinzani haviwezi kukifanya kwa ufanisi.
Pongezi zangu kwa JK , CC na NEC yake kwa kuondoa kwa sasa mada za ufisadi zilizo wapa wapinzani nguvu ya kuishambulia CCM. Ni wazi kuwa wapinzani wa CCM sasa watachanganyikiwa kwa kukosa mada za kuwaunganisha.
Ilifika wakati mwana CCM wa kweli aliona aibu kusimama hadharani na kujitambulisha , kwa kuogopa kuzomewa!
Kukidumisha chama ni jambo la muhimu sana na tukumbuke kuwa hata Mao Tse Tung alihalalisha wanachama wake wa Communist Party kuishambulia Makao Makuu pale alipoona inaanza kutekwa na watu wachache wenye malengo yao binafsi.

Baada ya "kujivua gamba", pengine naweza kusema kuwa JK amejitengenezea uhalali wa kukumbukwa kwa kutoruhusu chama kutekwa myara na watu wenye malengo binafsi ya kujinuafaisha-kwa hili anastahili pongezi.
Kwa hili vile vile ameweka msimamo(precedence) ya kutambua kuwa chama kina wenyewe, nawenyewe ni wananchi na sio wafadhili.
Hongera CCM!
 
Thanks Lole kwa post yako...........

My question here is do you still hold even just a piece of trust in JK?

By my side i can say no! It can take years toi trust this man and what he says...In his time as a president i came to find that he act so wise, so concerned but doing contrary things

Ni nani aliesema anawajua wauza madawa ya kulevya na atadili nae? Amelifanya hili?

Nani aliewapa mafisadi uhuru wa kurudisha pesa kimyakimya wakati wanaendelea kuibuka kwa kashfa nyingine (Unaiba huku unalipa kule and the game goes on)

Nani aliewasafisha juzi kuwa ni wasafi?

Je kwa shinikizo la wanachama baada ya kuona wapinzani na watu wenye mapenzi mema na CCM wanalalamikia genge la wezi kujenga viota ndani ya CCM unadhani Kikwete amefanya maamuzi yote kwa nia moja juu ya wezi hawa? Je kun amazingira yoyote ya kuamini kauli zake?

Kama angekuwa anamaanisha anachofanya he would have put them all responsible na sio kusema wajipime wenyewe (Huu ni udhaifu mwingine ukichelea ni juzi tu amewasifia kuwa watu safi na wachapa kazi)

It will take time to believe what he meant.......BTW wanastahili pongezi maana hatua hii nayo itasaidia vyama vya upinzani (namaanisha UPINZANI) kuanza kujipanga upya kwa kuzingatia kuwa mkuu "katishia nyau" kuwashughulikia wezi na kusafisha chama....all in all,lets give them time and see
 
Ni post "nzuri"
Kwa maana, ni muendelezo uleule wa fikra nyepesi katika kujenga kataifa kadogo na kamasikini kuliko umasikini wenyewe (hasa kwa watu wake), haka kamchezo ka watu kuwa wepesi kuwa-carried away na events badala ya effects naona kanaendelea kushika kasi, mambo kama haya ndio kuna mjumbe akasema eti "...itachukua miaka 100 kuitoa ccm" sasa naona kwanini alisema hvyo, watu na akili zao wameendelea kujikita katika kuamini kuwa eti bila CCM hamna Tanzania.
Sawa kupongeza, lakini tupanue tafakari je hii ccm imechafuka saiv tu (kwenye uenyekiti wa Baba ridhwani)??? Mbona ya Mwalimu Nyerere kumshukia Mzee Mwinyi katika madudu yake kibao, tunajisahaulisha?? Ya Ndugu Kolimba je?? Ya Mzee Mkapa na kuuza mali (assets) zetu? Hayo yote yalisimamiwa na serikali za CCM na hayo ndio kiini cha umasikini wa watu wetu na ndio kiini cha ccm kupoteza maan, je kipindi hicho gamba alikuwa nani? nalo limevuka?.... CCM ivae au ivue Gamba, agenda yetu kubwa ni Tiafa kusonga mbele, tuje kuwa nchi kubwa duniani kama hizo zingine..(china n' tigerz etc), AGENDA ambayo haipo kwa ccm (baada ya mwl nyerere)....
 
Thanks Lole kwa post yako...........

My question here is do you still hold even just a piece of trust in JK?

By my side i can say no! It can take years toi trust this man and what he says...In his time as a president i came to find that he act so wise, so concerned but doing contrary things

Ni nani aliesema anawajua wauza madawa ya kulevya na atadili nae? Amelifanya hili?

Nani aliewapa mafisadi uhuru wa kurudisha pesa kimyakimya wakati wanaendelea kuibuka kwa kashfa nyingine (Unaiba huku unalipa kule and the game goes on)

Nani aliewasafisha juzi kuwa ni wasafi?

Je kwa shinikizo la wanachama baada ya kuona wapinzani na watu wenye mapenzi mema na CCM wanalalamikia genge la wezi kujenga viota ndani ya CCM unadhani Kikwete amefanya maamuzi yote kwa nia moja juu ya wezi hawa? Je kun amazingira yoyote ya kuamini kauli zake?

Kama angekuwa anamaanisha anachofanya he would have put them all responsible na sio kusema wajipime wenyewe (Huu ni udhaifu mwingine ukichelea ni juzi tu amewasifia kuwa watu safi na wachapa kazi)

It will take time to believe what he meant.......BTW wanastahili pongezi maana hatua hii nayo itasaidia vyama vya upinzani (namaanisha UPINZANI) kuanza kujipanga upya kwa kuzingatia kuwa mkuu "katishia nyau" kuwashughulikia wezi na kusafisha chama....all in all,lets give them time and see

Mkuu NewDawnTz I aacept your comments ambazo zimekuja with a pinch of salt.
Lazima tuya tazame haya mabadiliko with an open mind.
Kwamba this is a step in the right direction is beyond doubt.Mimi sikatai kwamba Mwenyekiti amechukua hatua hizi za "kujivua gamba" baada ya kupata shinikizo toka kwa wananchama na viongozi wenzake.
Matokeo ya uchaguzi mkuu vile vile ni shinikizo tosha.
Tukumbuke kuwa mmoja wa watuhumiwa wakuu,EL, alitamba hadharani kuwa hawakuonana na JK mitaani, hii ikimaanisha kuwa hakuna wa kumchukulia hatua yoyote ndani na nje ya chama.Huku ni kujisahau vibaya kwa kiongozi, mbaya zaidi Jk hakusema lolote juu ya hili.

Nini kimetokea?
Ni wazi kuwa shinikizo zilizowekwa na vyama, asasi na watu tofauti, pamoja na uchaguzi mkuu vimefanya kazi iliyotarajiwa-kumwamsha JK na CCM that it is not business as usual.
Kwa kutambua hilo na kuelewa maana yake na kuchukua hatua katika muda mfupi ndio msingi wa hongera zangu kwa JK na CCM, at least the CCM truck is not heading down hill!!
 
tz%7Dccm.gif

Matukio ya wiki hii, hasa hili la CCM "kujivua Gamba" linastahili pongezi .
Kwa muda mrefu sasa waanzishi wa malumbano ndani na nje ya JF wamekuwa wakiifuatilia kwa makini sana muelekeo wa CCM kama chama tawala na JK akiwa mweyekiti wake.

Wengi wamelaumu ufisadi wa waziwazi uliofanyika baada ya JK na "mtandao" kuingia madarakani.
Wengi zaidi wamelaumu kushindwa kwa CCM kuchukua hatua kudhibiti ufisadi baada ya JK kuingia madarakani mwaka 2005.
Na wengine wengi zaidi wamemlaumu JK binafsi kwa kutowachukulia hatua watuhumiwa wa ufisadi.
Wapo walio hoji ukaribu wa JK na watuhumiwa hawa, hasa Edward Lowassa, Rostam Aziz na Chenge.

Mara nyingi JK amekuwa akiwapoza wanachama wa CCM na wananchi kwa ujumla kuwa hakuna ushahidi wa kutosha kuwahukumu moja kwa moja watuhumiwa hawa wa ufisadi, na TAKUKURU pia imeshindwa kupata ushahidi juu ya hilo.

Wananchi hawakufanya ajizi, na hapa navipongeza vyama vya upinzani kwa elimu waliyoitoa kwa wananchi.

Ufisadi ni mbaya , ufisadi ni kuingiza umaskini katika nchi,ufisadi unahujumu uchumi wa nchi.
Tumeona mikataba inayoumiza nchi(Richmond na sekta ya madini), tumeona madeni yanayotokana na mikataba feki kama ya Dowans(94bil),tumeona ununuzi wa vifaa vibovu(radar).

Kwa ujumla wananchi wamejionea madhara ya ufisadi katika muda huu wa kipindi kisichozidi miaka 10.
Chama kilikuwa katika wakati mbovu pengine kuliko wakati wowote katika uhai wake kikiwa chini ya katibu Mkuu wake Makamba ambaye hakuwa na ubavu, upeo wala mbinu za kudhibiti ufisadi.
Kwa bahati mbaya sana wahusika wakuu ndio hao hao walioko katika ngazi za juu katika uongozi wa chama, na ni marafiki wa karibu wa mwenyekiti wa chama tawala CCM.
Kampeni na uchaguzi wa mwaka 2010 ni kama umekizindua chama kutoka katika usingizi mzito wa kufikiri kitatawala milele Tanzania.
Kupungua kwa kiwango kikubwa kwa watu wanao muunga mkono mkuu wa nchi kutoka 82% mwaka 2005 hadi 61% mwaka 2010 ni mstuko tosha kwa chama tawala.
Pongezi zangu kwa JK na CCM ni kuelewa maana ya mstuko huo na madhara yake kwa CCM.

Kitendo cha kudhibiti kundi lile la watu watatu(EL, RA na Mzee wa Vijisenti) si tu imeleta muamko mpya wa watu kuona kuwa chama hakijatekwa na mafisadi bali pia kuona kuwa chama bado kinawasikiliza wanachama wake na wananchi kwa ujumla.
Kwa staili ya kuwaengua hawa mafisadi katika nafasi za juu za chama, chama kimeonyesha uwezo mkubwa wa kujirekebisha-kitu ambacho vyama vingi vya upinzani haviwezi kukifanya kwa ufanisi.
Pongezi zangu kwa JK , CC na NEC yake kwa kuondoa kwa sasa mada za ufisadi zilizo wapa wapinzani nguvu ya kuishambulia CCM. Ni wazi kuwa wapinzani wa CCM sasa watachanganyikiwa kwa kukosa mada za kuwaunganisha.
Ilifika wakati mwana CCM wa kweli aliona aibu kusimama hadharani na kujitambulisha , kwa kuogopa kuzomewa!
Kukidumisha chama ni jambo la muhimu sana na tukumbuke kuwa hata Mao Tse Tung alihalalisha wanachama wake wa Communist Party kuishambulia Makao Makuu pale alipoona inaanza kutekwa na watu wachache wenye malengo yao binafsi.

Baada ya "kujivua gamba", pengine naweza kusema kuwa JK amejitengenezea uhalali wa kukumbukwa kwa kutoruhusu chama kutekwa myara na watu wenye malengo binafsi ya kujinuafaisha-kwa hili anastahili pongezi.
Kwa hili vile vile ameweka msimamo(precedence) ya kutambua kuwa chama kina wenyewe, nawenyewe ni wananchi na sio wafadhili.
Hongera CCM!

sawa mkuu lakini tatizo la ufisadi upo serikalini na siyo kwenye chama na huko ndiyo wananchi hasa wazalendo wanalalamika hizi deal za kuiba bado zitaendelea gamba lintakiwa litolewe serikalini ni kichekesho kutoa siku 90 kwa fisadi awe amejitoa kwenye chama na huo ufisadi alio ufanya serikalini inakuwaje? Chombo kinachoweza kusema wewe siyo fisadi ni mahakama leo hii watuhumiwa wote wanapaswa kufikishwa mahakamani na siyo kusema huyu fisadi lakini hakuna kumfikisha mahakamani.
 
sawa mkuu lakini tatizo la ufisadi upo serikalini na siyo kwenye chama na huko ndiyo wananchi hasa wazalendo wanalalamika hizi deal za kuiba bado zitaendelea gamba lintakiwa litolewe serikalini ni kichekesho kutoa siku 90 kwa fisadi awe amejitoa kwenye chama na huo ufisadi alio ufanya serikalini inakuwaje? Chombo kinachoweza kusema wewe siyo fisadi ni mahakama leo hii watuhumiwa wote wanapaswa kufikishwa mahakamani na siyo kusema huyu fisadi lakini hakuna kumfikisha mahakamani.

Nakubaliana na wewe Mkuu. lakini hata Mwalimu alisema chama kikiwa lege lege hata serikali yake itakuwa legelege.
Usafishaji wa hawa mafisadi lazima uanzie kwenye chama.
Hata fisadi anajua kuwa ili asikamatike lazima awe kwenye vyombo vile vinavyotoa maamuzi ya kisiasa.Wengi wetu tulishangaa sana kuona RA anapeta kwenye vikao vya juu vya CCM, haya tunayoyaona sasa tulijua yanakuja.
Wale waliopata utajiri kutokana na dili za kifisadi ndani ya serikali ni kama EL na Mzee wa Vijisenti-hawa wana matatizo ya kutotosheka na ulafi.
Wange kaa pembeni haya yasingewapata.
Hata hivyo nakubaliana kuwa ufisadi umepanda chati serikalini baada ya kuona wale waliofanikiwa na ufisadi na hakuna hatua yoyote inayochukuliwa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom