Hongera Dr. Bilal Kuutetea Muungano na kusimama kuhesabiwa; Wengine?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,476
39,995
Nimekuwa nikikosoa sana kuwa viongozi wetu wengi hawana ujasiri wa kuutetea Muungano wazo wamebakia kulalamika pembeni; na wale wanaosimama kuutetea wanautetea kwa minajili ya kisheria kuwa "ni uhaini kuvunja" au ni makosa na wengine wako tayari kusema "tuuvunje tu yaishe". Dr. Bilal amefanya utetezi japo kidogo lakini utetezi wa kwanza ambao binafsi unanipa matumaini kuwa wapo watu wenye kuthubutu kuutetea Muungano bila aibu au kuwaogopa watu. Je, nani mwingine atajitokeza kuutetea Muungano wetu? Je wataweza kusimama na kuutetea kwa hoja kweli na siyo vitisho au kejeli?

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Mohamed Gharib Bilal, amesema itatokea hasara kubwa iwapo Wazanzibari watakubali kuuvunja Muungano.
Akiwahutubia wananchi baada ya kuweka jiwe la msingi la tawi la CCM Mwera Misufini Wilaya ya Magharibi Unguja, alisema mabadiliko ya Katiba yasiwe chanzo cha kuzorotesha Muungano.
Alisema marekebisho hayo ya Katiba lengo lake kubwa ni kuimarisha Muungano ambao umeleta faida kubwa ikiwemo kujenga umoja wa kitaifa.
Aliongeza kuwa kuwepo kwa kasoro ndogo ndogo katika Muungano isiwe kigezo cha kutaka kuuvunja wakati Serikali za Muungano na Zanzibar zilidhamiria kumalizia kero zilizobakia baina ya pande mbili za Muungano.
“Hasara kubwa itatokea endapo wananchi wakikubali Muungano uliopo baina ya Tangayika na Zanzibar kama utavunjika,” alisema.
Alisema kwamba yapo mataifa mengi yamekuwa yakifika nchini kujifundisha Muungano ulioasisiwa na marehemu Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere na Rais wa Kwanza wa Zanzibar, Sheikh Abeid Amani Karume.
Dk. Bilal alisema sio vyema kuuchokonoa Muungano au kubeza kutokana na kasoro ndogo ndogo zilizopo na badala yake amewataka wananchi kutumia uhuru wa Kikatiba wa kutoa maoni wakati ukifika ili kuimarisha Muungano huo.
“Viongozi wetu waliopita waliona mbali na kuamua kuleta Muungano kutokana na kutambua faida zake na wananchi wa pande zote mbili wamekuwa wakinufaika na Muungano wetu,” alisema.
Aidha, alisema wakati huu si wa kufikiria kuukataa Muungano, wakati mataifa mengi duniani yameamua kila taifa litakuwa likijitegemea.
“Huu sio wakati wa kufikiria kuukataa Muungano, wakati mataifa mengi duniani wameamuwa kuungana kwa malengo ya kuunganisha nguvu za kiuchumi,” alisema.

Aahidi waliochomewa moto vibanda kuhudumiwa
Serikali ya Muungano itashirikiana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) kuhakikisha kuwa taratibu za umiliki wa ardhi zinafanywa haraka ili kuwawezesha wananchi waliochomewa moto vibanda vyao katika maeneo ya Pwani Mchangani, mkoa wa Kaskazini Unguja kupata sehemu ya kudumu ya kufanyia biashara.
Ahadi hiyo ilitolewa juzi na Makamu wa Rais, Dk. Mohamed Gharib Bilal, alipokuwa akizungumza na baadhi ya wananchi hao aliposimama kwa muda kwenye kambi yao iliyoko maeneo ya mpakani mwa Pwani Mchangani na Kiwengwa kuwapa pole.
Dk. Bilal alisema Serikali ya Mapinduzi Zanzibar inaelewa matatizo hayo na kwamba itafanya kila jitihada kuhakikisha wanapewa maeneo kwa ajili ya kuendeleza shughuli zao za biashara.
“Serikali inaendesha shughuli zake kwa kufuata Katiba. Hivyo, mtahudumiwa kwa mujibu wa Katiba na sheria za nchi,” alisema.
Hata hivyo, aliwataka wawe na subira wakati serikali ikifanya taratibu za kupata maeneo mengine.
Dk. Bilal alisema nchini Tanzania kuna uhuru wa kufanya kazi mahali popote pale mradi mtu havunji sheria na kusema hakuna atakayenyang’anywa uhuru huo.
Dk. Bilal alitoa ufafanuzi huo baada ya kupata taarifa kutoka kwa Mkuu wa wilaya ya Kaskazini B, Riziki Juma, kuwa wilaya imetenga maeneo hayo ya mpakani mwa Pwani Mchangani na Majeta kwa ajili ya wahanga wa moto lakini hawawezi kuyatoa mpaka Wizara ya Ardhi Zanzibar ikamilishe taratibu zake za umiliki wa ardhi katika maeneo hayo kwa kuogopa waisonekane wavamizi.
Kwa mujibu wa Mkuu wa wilaya ya Kaskazini B, tayari wametoa taarifa kwenye ofisi ya Maafa na Msalaba Mwekundu kuhusu tatizo hilo ili liweze kushughulikiwa.
Wananchi zaidi ya 50 ambao wengi wao ni wenye asili ya Tanzania Bara, walichomewa moto vibanda vyao vya biashara katika maeneo ya Pwani Mchangani na watu wasiojulikana mwanzoni mwa mwezi huu.
Wakati huo huo, Mahakama ya Mkoa Mfenesini Mkoa wa Kaskazini Unguja, imewaachia kwa dhamana washtakiwa wote wanaotuhumiwa kuchoma moto maduka na nyumba zilizokuwa zikimilikiwa na wafanyabiashara wenye asili ya Tanzania Bara.
Washtakiwa hao saba waliachiwa kwa dhamana na Hakimu Faraji Shomari Juma, baada ya kufikishwa kwa mara ya kwanza katika mahakama hiyo, mjini Zanzibar jana.
Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka, Omar Khalfan Sururu, alidai kuwa watuhumiwa walichoma moto mabanda katika kijiji cha Pwani Mchangani Zanzibar Mei 6, mwaka huu.
Hata hivyo, washtakiwa wote walikana mashtaka yote 17 waliosomewa.
Washtakiwa hao ni Haji Ame Iddi (45), Talib Faki Ame (60), Mohammed Haji Sheha (21), Mohammed Masoud Afadhali (21), Mwinyi Abdallah Msanifu (22), Hassan Makame Chande (21) na Thabit Muombwa Thabit, wakazi wa Pwani Mchangani Wilaya ya Kaskazini A Unguja.
CHANZO: NIPASHE
 
Inatia moyo! ila lakini mbona watuhumiwa wameachiwa huru?kuna kitu mbaya inanukia hapa! more tragedies to come! wait and see! its' a matter of time! ta!!
 
Mzee Mwanakijiji wanasiasa wa Zanzibar wanalugha mbili wana lugha za majukwaani na lugha za pembeni inakuwa ni vigumu sana kuwaelewa,
Dr. Bilal ameongea jukwaani vizuri sana sijui kama anamaanisha anachokisema. Muungano huu una faida kubwa hasa kwa ndugu zetu zaidi ya nusu ya wazanzibar wanaishi na kufanya shughuli zao bara leo muungano huu ukivunjika watawapeleka wapi? Umefikia wakati wa kuelezana ukweli tuache ubinafsi hayo mapungufu yaliyopo yafanyiwe kazi kwa faida ya muungano wenyewe.

Chama
Gongo la Mboto DSM.
 
Hoja ya msingi ni uwepo muungano utakaokubalika kwa pande zote za muungano. options ziko mbili serikali moja au shirikisho -serikali tatu. Huwezi kuunganisha nchi 2 ukapata nchi 2. That is a total confusion.
Hapa ndo inapokuja sera ya chadema ya nchi mbili ndani ya shirikisho la jamhuri ya muungano wa Tanzania. It means Tanganyika iwepo pia. Kuna suala la gharama. Changamoto ya uwepo wa gharama kubwa inajadilika kwani inategemea unaweka nafasi gani muhimu.
Kwa mfano Chadema wanasema kuwe na mawaziri wa muungano kama wanne au watano - mambo ya nje, ulinzi, fedha, elimu. Pia Ukifuta nafasi ya wakuu wa mikoa na wilaya ina maanisha kuwa pamoja na kuwepo kwa serikali tatu bado gharama haitaongezeka sana tofauti na ilivyo sasa.

Binafisi naona muungano uliopo kwa muundo wake unahitaji mabadiliko sana. Kero gani za muunganino zisizoisha zinatatuliwa miaka nenda rudi?
 
Nadhani kwa Bilal kusema hadharani hicho tu ndicho anachohukumiwa nacho siyo kile cha sirini kwani mtu yeyote anaweza kudaiwa kusema kitu fulani sirini. Swali langu ni watu kama kina Salim, Moyo (ambaye hakusema lolote la maana zaidi ya kushabikia), kina Vuai na wenzako na huku bara tuwasikie viongozi wetu nao waseme hadharani. Kinachconishangaza ni ukimya wa wabunge vijana ambao tuliambiwa wanaingia wakiwa na mawazo mapya - lakini wanakwepa kugusa suala la Muungano na mawazo yao yako wapi. Haitoshi kutuambia "kero zitatuliwe" n.k; Tunazungumzia the substance that is Muungano wao wanasimama wapi?

Ni swali ambalo linahitaji majibu kwa kadiri tunaelekea Katiba mpya.
 
Hakuna nafasi ya muungano ndani ya EAC............................wake-up guys and kill this nonsense...............
 
Kama muunagano unafaida nyingi na kama una kasoro kidogo na kama wazanzibar tutapata hasara kubwa pindipo tukikubali kuvunja muungano hayo ni maneno yake. Ila tunamwambia dr bilal kuwa kupima kama watu wamemfahamu na wamemtii na alete kura ya maoni zanzibar kuhusu muungano aone kitakachotokea.
 
Nadhani kwa Bilal kusema hadharani hicho tu ndicho anachohukumiwa nacho siyo kile cha sirini kwani mtu yeyote anaweza kudaiwa kusema kitu fulani sirini. Swali langu ni watu kama kina Salim, Moyo (ambaye hakusema lolote la maana zaidi ya kushabikia), kina Vuai na wenzako na huku bara tuwasikie viongozi wetu nao waseme hadharani. Kinachconishangaza ni ukimya wa wabunge vijana ambao tuliambiwa wanaingia wakiwa na mawazo mapya - lakini wanakwepa kugusa suala la Muungano na mawazo yao yako wapi. Haitoshi kutuambia "kero zitatuliwe" n.k; Tunazungumzia the substance that is Muungano wao wanasimama wapi?

Ni swali ambalo linahitaji majibu kwa kadiri tunaelekea Katiba mpya.

Mzee Mwanakijiji Bara hatuna tatizo la muungano pamoja kero zilizopo wananchi wa bara hatulalamiki hadharani kama ndugu zetu wa visiwani. Visiwani kuna matatizo mawili makubwa :
1. Ubaguzi wao wenyewe wanabaguana wapo wanajiona ni waarabu zaidi, wapo wanaodhalilishwa kwa sababu tu wanaasili ya bara, kuna ile dosari nyngine ya upemba na uunguja
2. Siasa za asili za Zanzibar zinafanya kazi hadi sasa. Vyama vya asili Zanzibar ASP, ZPPP, ZNP na vinginevyo. Siasa za Zanzibar hadi leo hii zimetawaliwa na chuki. Ukiwa na asili ya Hizbu hata ufanye mema gani hupati nafasi SMZ. Mfano hai ni Dr. Salim A. Salim pamoja na kuwa CCM wa dhati kwa vitendo hatambuliki kisiasa kisa Hizbu
Ni vyema kwa wazanzibar wawe na muafaka ili wamalize tofauti zao tuboreshe muungano ukweli hadi leo hii wapo wa unguja wanatamani leo hii warudi kutawaliwa na mwarabu, sasa pakiwa na ufinyu wa mawazo kama haya kweli muungano utadumu?

Chama
Gongo la Mboto DSM.
 
Hoja hizi zinazohusu masuala ya Taifa na umuhimu wa watu kuungana zinahitaji watu kufahamu tulipotoka na tunapokwenda. Mwanakijiji nakushukuru kuibua hoja hii, kusigana mawazo kuhusu muungano si hoja hatuwezi kuwa na hoja moja hayo tunayoyaita matatizo ama kero ni muhimu kuzipima lakini, Kuungana kwetu kunatufanya kuwa binadamu tulio na heshima na wenye utu wa kiwango cha juu. Kuna mafanikio mengi katika Muungano wetu lakini si rahisi kuyaona kwa kila mmoja. Nenda Unguja kisha tazama maana ya Muungano huu, lakini jiulize je, ni busara kutengana kwa kuwa kuna watu wana nia ya kufanikisha agenda zao za kisiasa. Nitarejea hapa baadaye kuunga mkono hoja ya kuulinda Muungano na pia kufafanua bayana nini ninachokiona kama Mtanzania wa kawaida kuhusu Muungano wetu.
 
Dr Bilal anajua Muungano ulivyomkosesha urais wa Zanzibar mara kadhaa. Kama ni Saulo anageuka kuwa Paulo sawa. Kwenye siasa hakuna marafiki au maadui wa kudumu. Na kwa siasa za Tanzania hakuna msimamo wa kudumu. Si unamwona hata Maalim Seif sasa anavyoisifu serikali ya mapinduzi?
 
Wanzanzibari tayari wamesha weka mipaka ya nchi yao ndani ya katiba yao. Sasa hii nchi tunayoiongelea kama Tanzania ni hipi? Je ni Tanganyika peke yake maana ndiyo ambayo mipaka yake haitambuliki na haina katiba yake? Ama kweli nchi yangu Tanganyika ni shamba la bibi hata wakenya sasa wanasema Samunge kwa babu wa Loliondo hiko Kenya.
 
Nadhani kwa Bilal kusema hadharani hicho tu ndicho anachohukumiwa nacho siyo kile cha sirini kwani mtu yeyote anaweza kudaiwa kusema kitu fulani sirini. Swali langu ni watu kama kina Salim, Moyo (ambaye hakusema lolote la maana zaidi ya kushabikia), kina Vuai na wenzako na huku bara tuwasikie viongozi wetu nao waseme hadharani. Kinachconishangaza ni ukimya wa wabunge vijana ambao tuliambiwa wanaingia wakiwa na mawazo mapya - lakini wanakwepa kugusa suala la Muungano na mawazo yao yako wapi. Haitoshi kutuambia "kero zitatuliwe" n.k; Tunazungumzia the substance that is Muungano wao wanasimama wapi?

Ni swali ambalo linahitaji majibu kwa kadiri tunaelekea Katiba mpya.

Mwanakijiji, achilia mbali wabunge vijana, wabunge wanaowakilisha Zanzibar ndani ya Bunge la Muungano wamukuwa kimya muda wote. Nasema muda wote kwa sababu matukio ya kuchoma moto biashara za watu wa asili ya Tz Bara, nyumba za ibada hayajaanza leo. Hata hapa ninapoondika wako waumini wanachunga makanisa (saa zote) just in case. Imebidi makanisa wajiwekee utaratibu huu wa ulinzi baada ya matukio ya moto kuzidi. Na muda wote huo wabunge wa Zanzibar sio Mh Rashid wala nani. kimya! Kwa kifupi wabara wamekuwa wanaishi kama yatima ni sasa tu baada ya mabanda kuchomwa kwa wingi kwa kipindi kimoja ndio wakubwa wanaanza kuongea.

Nategemea bunge la July walau mbunge mmoja atasimama KULAANI hiii hali.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom