nickname
JF-Expert Member
- Dec 20, 2009
- 544
- 147
Uchaguzi mkuu wa Rais,wabunge na madiwani nchini Tanzania ulifanyika mwezi Oktoba,2010.Uchaguzi ulikwisha na kila chama kiliambulia chake.
Pamoja na CDM kulalamika kuwa matokeo ya Urais yalipikwa na kutotambua njia zilizotumika kumweka Rais madarakani lakini viongozi wa Chadema kwa busara hawakutumia nguvu ya umma kupinga matokeo ya Urais.Kwa hili nawapongeza sana.
Maandamano ya kupinga uchaguzi wa meya wa Arusha yalifanyika,nasikitika kwa vifo vya watu watatu kulikosababishwa na Polisi kutumia nguvu kupita kiasi.
Nikirudi kwenye mada kuu ni hivi baada ya uchaguzi mkuu kumalizika kumejitokeza kampeni zilizofanywa na CDM katika mikoa ya kanda ya ziwa,kampeni hizi zimekuwa zikianza kwa maandamano ya AMANI na baadae mikutano ya hadhara.Nashukuru kuwa lengo ni kupinga malipo kwa DOWANS,kuwatetea watanzania kuwanusuru na maisha magumu yaliyopo sasa.
CCM wameogopa sana wakisema kuwa CDM inafanya uchochezi wa kutaka kuipindua serikali ya JK.CCM hawajui kuwa wanachokifanya Chadema ni kazi mojawapo ya chama cha upinzani ya kuikosoa serikali iliyo madarakani.Kulingana na matamko ya viongozi wa CDM,CCM walipaswa kujibu hoja.Kwa hili safi sana kwa kuwa baada ya viongozi wa Chadema kulalamikia upandaji bei wa vitu hususani sukari serikali ikaamua kushusha bei ya sukari toka sh.2000 mpaka sh 1700.
Tumejionea nao CUF na NCCR baada ya kuipinga Chadema nao wameamua kufanya mikutano ya hadhara huku maudhui katika mikutano hiyo ikishahabiana na na kile kilichosemwa na Chadema.CUF wameanza mikutano yao katika mikoa ya Tanga,Mtwara,Lindi,Pemba,Unguja n.k huku NCCR wakifanya mikutano yao katika mkoa wa Kigoma.CCM wao wamekuwa wakifanya kampeni zao za kujibu mashambulizi ya Chadema kupitia vyombo vya habari hasa TBC1.
Tunachoendelea kujionea ni kampeni za kuwatetea wananchi na kuona kuwa maisha ya wananchi yanaboreka.Uzuri wa kampeni hizi ni kuwa hazina muda maalum na hakuna uchakachuaji wa kura na matokeo yake ni kwa serikali kuboresha maisha ya wananchi kwa msukumo wa wapiga kampeni.HOngera kwa walioanzisha kampeni hizi.HOngera Chadema.Alamsiki
Pamoja na CDM kulalamika kuwa matokeo ya Urais yalipikwa na kutotambua njia zilizotumika kumweka Rais madarakani lakini viongozi wa Chadema kwa busara hawakutumia nguvu ya umma kupinga matokeo ya Urais.Kwa hili nawapongeza sana.
Maandamano ya kupinga uchaguzi wa meya wa Arusha yalifanyika,nasikitika kwa vifo vya watu watatu kulikosababishwa na Polisi kutumia nguvu kupita kiasi.
Nikirudi kwenye mada kuu ni hivi baada ya uchaguzi mkuu kumalizika kumejitokeza kampeni zilizofanywa na CDM katika mikoa ya kanda ya ziwa,kampeni hizi zimekuwa zikianza kwa maandamano ya AMANI na baadae mikutano ya hadhara.Nashukuru kuwa lengo ni kupinga malipo kwa DOWANS,kuwatetea watanzania kuwanusuru na maisha magumu yaliyopo sasa.
CCM wameogopa sana wakisema kuwa CDM inafanya uchochezi wa kutaka kuipindua serikali ya JK.CCM hawajui kuwa wanachokifanya Chadema ni kazi mojawapo ya chama cha upinzani ya kuikosoa serikali iliyo madarakani.Kulingana na matamko ya viongozi wa CDM,CCM walipaswa kujibu hoja.Kwa hili safi sana kwa kuwa baada ya viongozi wa Chadema kulalamikia upandaji bei wa vitu hususani sukari serikali ikaamua kushusha bei ya sukari toka sh.2000 mpaka sh 1700.
Tumejionea nao CUF na NCCR baada ya kuipinga Chadema nao wameamua kufanya mikutano ya hadhara huku maudhui katika mikutano hiyo ikishahabiana na na kile kilichosemwa na Chadema.CUF wameanza mikutano yao katika mikoa ya Tanga,Mtwara,Lindi,Pemba,Unguja n.k huku NCCR wakifanya mikutano yao katika mkoa wa Kigoma.CCM wao wamekuwa wakifanya kampeni zao za kujibu mashambulizi ya Chadema kupitia vyombo vya habari hasa TBC1.
Tunachoendelea kujionea ni kampeni za kuwatetea wananchi na kuona kuwa maisha ya wananchi yanaboreka.Uzuri wa kampeni hizi ni kuwa hazina muda maalum na hakuna uchakachuaji wa kura na matokeo yake ni kwa serikali kuboresha maisha ya wananchi kwa msukumo wa wapiga kampeni.HOngera kwa walioanzisha kampeni hizi.HOngera Chadema.Alamsiki