by default
JF-Expert Member
- Jul 11, 2011
- 839
- 215
Mi nipo ifakara kibaoni mbuge aonekani barabara kilometa 60 kutoka kidatu hadi kibaoni ni mbovu zimekuwa ahadi za kila chaguzi leo ndio unakuja kuanza kuwapelekesha wenzako! Shame on u nape
Huu ushindi wa CDM huko Arumeru na kwenye Kata tatu ni dalili mbaya kwa CCM.Pamoja na CCM kutumia majembe yake yote lakini imeshindwa. Mategemeo ya CCM kwa siku za karibuni imekuwa ni maeneo ya vijijini kwa kuwa sehemu za mijini imekuwa ngome ya CDM. Lakini sasa inaonekana kwamba moto wa CDM umeanza kuenea hadi vijijini na vitongojini. Sijui 2015 CCM itakuwa katika hali gani. Na kama chaguzi ndogo zitaendelea naona CCM itaendelea kumong'onyoka na kufikia 2015 itakuwa inaanguka.
Makundi yanaimung'unya CCM na bil kushughulikiwa hakika 2015 itakuwa ni kilio na kusaga meno.
Kushindwa huku iwe ndio chachu ya CCM kujiangaloa mara mbili yasije kuyakuta ya UNIP ama KANU.
Nawatakieni kila lakheri wote mliochaguliwa, nawatakieni utumishi uliotukakuka!
huyu jamaa amefurahi kwani anajua ni pigo kubwa kwa lowasa ambaye ni fisadi waliyembakiza ndo maana wakamwingiza ili akajimalize mwenyewe.
Kwa heshima nachukua nafasi hii kuwapongeza kwa dhati watani zetu, CHADEMA kwa ushindi walioupata Arumeru Mashariki na kwenye kata tatu(Kirumba, Kiwira na Lizabon). Lakini pia nawapongeza CUF kwa kushinda ile kata ya Tanga. Katika kata nane zilizokuwa zikifanya uchaguzi CCM tumeshinda kata nne. Tunawashukuru wananchi kule walikoendelea kutuamini na kutupa dhamana ya kata hizo nne. TUNAWAAHIDI KUWATUMIKIENI KWA MOYO WOTE.
Chama Cha Mapinduzi, kimeyapokea matokeo ya kura zilizopigwa na kutangazwa na tume ya Taifa ya uchaguzi kwa chaguzi ndogo zote, ule wa Arumeru Mashariki na zile za kata nane zilizofanyika jana nchini kwenye maeneo husika.
Kwa heshima nachukua nafasi hii kuwapongeza kwa dhati watani zetu, CHADEMA kwa ushindi walioupata Arumeru Mashariki na kwenye kata tatu(Kirumba, Kiwira na Lizabon). Lakini pia nawapongeza CUF kwa kushinda ile kata ya Tanga. Katika kata nane zilizokuwa zikifanya uchaguzi CCM tumeshinda kata nne. Tunawashukuru wananchi kule walikoendelea kutuamini na kutupa dhamana ya kata hizo nne. TUNAWAAHIDI KUWATUMIKIENI KWA MOYO WOTE.
Matokeo ya kura hizi kwa ujumla yameonyesha sauti ya wapiga kura kwenye maeneo husika, ndo maana tunaheshimu maamuzi yao. Tunatoa wito kwa vyama vilivyoshinda kwenye maeneo hayo kuhakikisha vinatumia muda na dhamana waliyopewa kutekeleza yale waliyowaahidi wapiga kura wao.
CCM tutatumia matokeo haya kufanya tathimini ya kina na kuangalia wapi tuliteleza ili tufanye marekebisho kuhakikisha makosa hayarudiwi tena. Kimsingi uchaguzi huu umeisha na tufunge mjadala wa uchaguzi tujikite katika kuwaletea maendeleo wale waliotuchagua.
Nawatakieni kila lakheri wote mliochaguliwa, nawatakieni utumishi uliotukakuka!