hongera chadema kwa kuwanyima usingizi ccm

andrews

JF-Expert Member
Mar 28, 2012
1,679
152
Hii ndiyo CCM! Huwa haishiwi propaganda chafu katika harakati zao za kutaka kuudhoofisha upinzani, ili kulinda kiti chake cha uongozi kisianguke (kisichukuliwe na upinzani). CCM wakati wote wanaihofia CHADEMA, na inasemekana kuwa, baadhi ya viongozi wake hata wakilala usiku huwa wanakurupuka katikati ya usingizi na kupiga mayowe ya CHADEMAaaa! Ni baada ya kuota ndoto ya kuona umati wa wafuasi wa CHADEMA (People's Power) wakiandamana kwa shangwe!
Hivyo basi, katika hali ya kutapatapa CCM kwa sasa wamechoka kisera. Sasa wameamua kuishambulia CHADEMA kwa chuki, na si kwa hoja. Na katika kuthibitisha hilo, tazama hata wabunge wake kule bungeni. Wengi wa wabunge wa CCM wameacha kuisimamia na kuishauri serikali, badala yake wamekuwa makini katika kuwakosoa na kuwakomoa wabunge wa CHADEMA ambao wamekuwa wakijaribu kujenga na kuwasilisha hoja muhimu kwa taifa.
Wabunge wa CCM hivi sasa wamegeuka kama watoto kule mtaani, ambao kwao umeme ukizimika wanafurahia 'Eeeeeeh!!’ Na Umeme ukiwaka utawaona wakifurahia pia 'Eeeeeeh!!’ Ni kama vile wabunge wa CCM, John Mnyika akisema CCM ni wadhaifu, utawasikia wakipiga kelele 'Aaaaaah!!’ Na Mnyika akitolewa nje ya bunge na Naibu Spika, utawasikia wakigonga meza kwa kelele huku wakisema 'Eeeeeeeh!!’ Ni kama vile watoto.
 
​http://www.youtube.com/watch?v=GAEpisZ3Cuk&feature=player_detailpage
 
​
tn+(16).jpg
WANAISHIA KUKODI BODABODA NDIO MAANA MUKAMA NA NAPE HAWAELEWANI
 
Back
Top Bottom