Hongera Askari wetu leo!

PSYCHOLOGY

Senior Member
Feb 10, 2011
177
14
habar JF!<br />
Muda wa saa kumi leo jioni nlipanda dala dala la kutokea mwenge kwenda Tandika DCM lenye usajili T 741 AEG (MOCHANA). Kumbe dereva kalewa kinoma...abiria wamelalamika kuhusu dereva mwendo na kutojali...alipofika maeneo ya karume kulikua foleni ..bahati askar wa njia wa kike akaelezwa na abiria tatizo hilo akamkemea dereva ili apaki pembeni..dereva kwa jeuri ya ulevi akamtukana huyo askari. Mwenendo na kutojali kama kawaida. Dereva akasema asimami popote na haipeleki gari kituo cha polis mpaka ifike mwisho (tandika). Mara askar wa bara baran wa kike akaomba msaada ili askari aliepo bara bara ya nyerere na kuingia veta asiruhusu gari kupita zitokeazo mwenge(karume)...ili akamatwe atolewe ndani ya gari...lakin dereva alikua mvishi sana hakukubali kuiachia gari ikawa vurugu japo aliingia askari wa bara bara wa kiume...kuanzia hapo ilikua tunasubiri lolote kutokea ..maana dereva huyo aliendelea kuendesha hovyo hovyo ndani ya gari...kelele ndani ya gari kwa akina mama na watoto za kuomba msaada zikiendelea! ''tunakufa jamani...tuokoeni dereva atatuua huyo...amelewa jamani!'' nawanukuu!
Nilipiga simu kwenye namba yao ya kuzuia uhalifu na taarifa mbali mbali nilipokelewa haraka na kuwapa maelezo na namba ya gari na mahali tulipo wakati huo.
Bahti nzuri njia alizozipita huyo dereva za ndan ndan mara akafika maduka mawili Chang'ombe hapo kulikua na foleni ..wakt dereva akijiandaa aipitishe pembezuni mwa bara bara ndipo abiria wakamvamia dereva kwa nguvu na kufanikiwa kumtoa nje ya gari huku askari wa Land cruiser wakiwa wameshafika eneo la hatari. Hapo niliamini askari wetu wapo makini ...maana gari zilifika tatu zikiwa na askari kwa kudhibiti hali yoyote ya hatari na kuizima. Walimchukua dereva ...mara na askari wa doria wa piki piki walikua wamefika. Hali ilikua ni shwari na abiria wote Tunamshukuru Mungi tulikua salama salimini. Baadhi ya abiria walishuka ilipopatikana nafasi ili waweke mawe kuizuia gari hawakufanikiwa.
Kwa hili nawapongeza sana askari wetu.
Nawakilisha!
 
Baada ya kumchukua kilichofatia? Isiwe yale yale wenye hatia wanajulikana hadi mahakamani wanapanda mwisho wa siku hakuna hatua zozote wanazochukuliwa madai hawana hatia. Kwa case itakuwa ngumu kupongeza.
 
kilichofuatia tulishuka kwa salama. Baada ya hapo nawaachia wana usalama.
Gari ilichukuliwa na askari kupelekwa kituoni. Umuhim tuliwaona nao askari kwenye tukio.
Kwa kua tulishuka salama sina jingine tena...labda wakiniita kutoa ushuhuda wangu mchache!.
 
Halafu ooohh< Kikwete hafanyi kitu! Hizi ni katika ahadi za kulboresha jeshi la polisi na tunaona linavyoboreka siku hadi siku. Hongera Kikwete, hongera Nahodha, hongera Mwema.
 
Halafu ooohh< Kikwete hafanyi kitu! Hizi ni katika ahadi za kulboresha jeshi la polisi na tunaona linavyoboreka siku hadi siku. Hongera Kikwete, hongera Nahodha, hongera Mwema.

Inshu ndogo sana hiyo kumpa heko mkuu wa kaya.
 
Halafu ooohh&lt; Kikwete hafanyi kitu! Hizi ni katika ahadi za kulboresha jeshi la polisi na tunaona linavyoboreka siku hadi siku. Hongera Kikwete, hongera Nahodha, hongera Mwema.
ingekuwa hivi:polisi njooni hapa magomeni mapipa kuna majambazi yamevamia yanauwa watu kama mende yana silaha nzito nzito kama:smg,rpg,lmg, na mabom ya mkono.pia majambazi yamesikika yakisema yoyote atakae leta pua yake tu.wanammaliza.jamani polisi njooni.!
 
Halafu ooohh&lt; Kikwete hafanyi kitu! Hizi ni katika ahadi za kulboresha jeshi la polisi na tunaona linavyoboreka siku hadi siku. Hongera Kikwete, hongera Nahodha, hongera Mwema.
<br />
<br />
Du!back again!?hongera jairo,hongera ngeleja.
 
Halafu ooohh&lt; Kikwete hafanyi kitu! Hizi ni katika ahadi za kulboresha jeshi la polisi na tunaona linavyoboreka siku hadi siku. Hongera Kikwete, hongera Nahodha, hongera Mwema.
<br />
<br />

Huu ni upuuzi mtupu! Jukumu kubwa la jeshi la polisi ni ulinzi wa raia na mali zao. Kama wametekeleza wajibu wao, pongezi ni za nini! Si wanalipwa kwaajili hiyo? Unapotekeleza wajibu wako kwa kiwango STAHIKI hustahili pongezi na mbwembwe za kisiasa zaidi ya kusubiri mwisho wa mwezi upewe stahili yako!
 
&lt;br /&gt;<br />
&lt;br /&gt;<br />
Umerudi lini toka Libya? Tena wapanda daladala? Jamani mitandaoni kuna vibweka, ukilegeza umeliwa.
<br />
<br />
Ulipowasiliana nami!
Jaman wa bongo mnachekesha kama naenda libya nkiwa Bongo siwezi kupanda dala dala?
Acheni hizo za kisha.m.b.a.
Kuna muda nilikua nakatisha jangwani nikienda kariakoo!
Kwani ananipunguzia nini?
Kuna muda natokea Morocco nakatisha kwa miguu hadi oysterbay! Inategemea na muda wa mtu!.
Nyie ndio wale wale!
Mungu awapunguzieni matatizo ili mjifariji.
Kutembea kwa mguu au kupanda dala dala ni mazoezi mazuri.
 
Halafu ooohh&lt; Kikwete hafanyi kitu! Hizi ni katika ahadi za kulboresha jeshi la polisi na tunaona linavyoboreka siku hadi siku. Hongera Kikwete, hongera Nahodha, hongera Mwema.
<br />
<br />
huyo nae n gamba.
 
Halafu ooohh< Kikwete hafanyi kitu! Hizi ni katika ahadi za kulboresha jeshi la polisi na tunaona linavyoboreka siku hadi siku. Hongera Kikwete, hongera Nahodha, hongera Mwema.

Ha ha ha LOL Haya dada FF kweli mkuu anafanya kazi kwa kujituma
 
[kilichofuatia tulishuka kwa salama. Baada ya hapo nawaachia wana usalama.
Gari ilichukuliwa na askari kupelekwa kituoni. Umuhim tuliwaona nao askari kwenye tukio.
Kwa kua tulishuka salama sina jingine tena...labda wakiniita kutoa ushuhuda wangu mchache!. [/]

Kuwaachia askari, huyo mtu ataachiwa huru kwa kuwa mashahidi hawakutokea. Polisi jamii na ulinzi shirikishi, inamtaka kila mtu kuchukia uhalifu na kuwa kitu kimoja kuzuia uhalifu.

Umefanya vizuri kutoa taariafa na mkasaidiwa kabla ajali haijawamaliza, hapo tayari umezuia uhalifu. Kinachotakiwa baada ya hapo, ni kutoa ushirikiano hasa kwa kufuatilia mpaka dreva apumzishwe gerezani.

ukikaa kimya tu, keshokutwa utamouna barabarani, na utaanza kulaumu bure kumbe wewe mwenyewe umechangia kwa kutotoa ushirikiano.

umoja wetu ndio utakaotufanya tuwe salama. na hii ndiyo polisi jamii na ulinzi shirikishi.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom