Kiby
JF-Expert Member
- Nov 16, 2009
- 6,899
- 4,623
ndugu pakajimmy,
hatukejeli wanaopata faraja huko kwa babu kutokana na magonjwa na madhaifu mbalimbali, la hasha. tunawashauri wapendwa wetu wasome na kufahamu ukweli juu ya nini yaliyo mapenzi na makusudi ya Mungu kama yalivyobainishwa ndani ya biblia na wapime na kujaribu kila roho kama inatokana na Mungu.
hivi kuna mtu huko samunge aliyepata majaribu kumshinda ayubu? mbona ayubu alikataa kumkufuru Mungu? iweje maelfu huko samunge wawe tayari kumdhihaki Mungu kwa sababu ya BP, cancer, ukimwi nk, eti kwa kupokea kikombe cha mchungaji mstaafu!
mwenye imani ya kweli na iliyojengwa kwenye neno (siyo iliyojengwa kwenye miujiza) atamtukuza Mungu hata apate mateso kiasi gani. atamtukuza Mungu hata katikati ya mateso, naam hata kama atamiminwa damu na kufa kama shahidi (martyr). imani yenu iko wapi sasa?
mimi niko tayri kuishi na majaribu ya ukimwi na mengineyo sugu lakini sio kumkufuru Mungu kiasi hicho cha samunge. ee Mwenyezi Mungu naomba nisaidie
Glory to God
.
Sii kweli hata kidogo kwamba uko radhi kufa shahidi. Kwani avatar yako inashuhudia umeanguka kwenye kamtihani kadogo tu ka Neno la Mungu la kuwataka wanawake wajifunike kwa mavazi ya staha. Ila wewe unahusudu mwanamke kujianika maumbile yake hadharani (ref U'r avatar)
Sembuse mtihani wa maradhi ya kifo.
Halafu hakuna mtu anaemwabudu babu, ni wewe tu kwa maslahi yako binafsi unataka kuaminisha watu ndivyo sivyo.
.