Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,890
- 6,896
Huduma zinazotelewa na baadhi ya wabunge kwa wapiga kura wao haziwezi kuhalalisha kwamba serikali iwaongezee wabunge posho za ziada kwa kuwa wanaishiwa kutokana na kutoa misaada kwa wapiga kura wao. Katiba ya Jamhuri ya Muungano haina kifungu kinachoainisha kwamba kazi za Mbunge ni kutoa misaada na huduma za jamii kwa wapiga kura wake, ila ni mwakilishi, msemaji na mtetezi wa wananchi wa jimbo lake kwa serikali pamoja na jukumu la kuwa katika jopo la nchi la kutunga sheria.
Kuna wabunge kadhaa ambao wamediriki kutoa misaada ya kiutu kwa wapiga kura wao ni kutokana na walicho nacho au mbinu wanazojua wenyewe kukokotoa misaada ambayo kama inasimamiwa kiufanisi inaweza kurudisha gharama hizo kwa vile huduma kama za magari ya kubeba wagonjwa si bure kwani wanalipia gharama hizo ili huduma hizo zijiendeshe.
Lakini kujenga hoja ya kuongeza posho kwa wabunge kwa ajili ya kuhudumia wapiga kura wao ni kufuru kwa vile serikali inazo wizara na idara husika kwa kazi hiyo kila kona ya nchi. hali kadhalika kuna mashirika kadhaa ya kiserikali, dini na kimataifa yanayofanya kazi hiyo, ni dhana potovu kuwamegea watu binafsi wabunge pesa hizo kwa kisingizio ambacho kinapingana na mfumo wa majukumu na utendaji wa mihimili mitatu ya nchi yetu.
Kwa upande mwingine serikali inatoa rushwa kwa wabunge na kuamsha ari ya wabunge kudai posho zaidi ili kuwa na akiba ya kutosha kuwarubuni wapiga kura wakati wa uchaguzi ujao. CCM kwa vile imezoea kushinda kura kwa kutumia pesa kuwahonga wapiga kura, hii ni mbinu ya kuwaandaalia mazingira wabunge wao kuwa na akiba ya kutosha kutoa rushwa uchaguzi mkuu ujao ili kujihakikishia viti vingi bungeni.