Hoja ya Kusimamisha mgombea urais wa kike Chadema ina mashiko.

Ng'wanangwa

JF-Expert Member
Aug 28, 2010
10,827
4,172
nimesoma vizuri moja ya makala za Tanzania Daima toleo la Jumapili ya leo. Makala hayo yanahusu propaganda mpya ambayo ccm wanaweza kuja nayo katika uchaguzi mkuu ujao ... propaganda ya ujinsia. Nafikiri wengi tuna taarifa zinazomuhusisha mwalimu Dr. MIGIRO, Asha Rose na urais wa Chama Cha Mabwepande mwaka 2015.

mwandishi wa makala yale amejikita katika kujenga hoja zake kwamba si dhambi mwana mama kuwa Rais wa taifa hili, lakini kwa kuwa wenzetu wapo kwenye siku zao za mwisho za kuongoza Taifa hili, watajaribu kupenyeza hoja za ujinsia, na kwa kufanya hivyo, wataukandia kwa nguvu zote mfumo-dume (na hii itapelekea chama changu kilichonilea, Chadema, kuzidiwa nguvu kwani ccm kwa sarakasi hawakamatiki). Ili kula nao sahani moja, naungana na hoja ya muandishi wa makala yale kwamba, kuna haja ya kusimamisha mwana-mama katika uchaguzi ujao ili tule nao sahani moja hawa magamba.

ujio wa mama Ellen Johnson, Rais wa Liberia ni dalili ya mvua. So Chadema, let's go neck in neck with magamba.

Vyuma mbona tunavyo jamani!? mikakati tu!

Kwa mtizamo wangu, kama hoja hii itapita (ni juu ya chama kuamua), Ms. Halima James Mdee ndiyo GHARIKA ya wanawake wote wanaojiita UWT na waume zao.
 
​maana halima mdee ni kijana na mabinti wote mamiss watampigia tu

hata wamama watu wazima wanaojiita uwt na wakati hawajui hata kirefu chake watampigia Halima aka Mwanamke Chuma.
 
Mabwepande wakisimamisha mwanamke watakunywa maji kwa karai haki ya nani! Mambo yako wazi kuwa huyo Asha kachemsha Umoja wa Mataifa (yaani ameprove incopetent) ndo maana wamemmwaga. Kufikira kumpa urais mwanamke CCM kunanipa taswira ya kuongozwa na Bi Kiroboto! Nitahama nchi!
 
Mabwepande wakisimamisha mwanamke watakunywa maji kwa karai haki ya nani! Mambo yako wazi kuwa huyo Asha kachemsha Umoja wa Mataifa (yaani ameprove incopetent) ndo maana wamemmwaga. Kufikira kumpa urais mwanamke CCM kunanipa taswira ya kuongozwa na Bi Kiroboto! Nitahama nchi!

wanaojuwa kama Mwalimu Dr. Migiro kachemka UN ni mimi na wewe tuliopitapita skuli. lakini kuna watu huko 'kwetu', leo akipita wa magamba wanarudisha kadi za chadema wanachukua za magamba; akipita wa chadema wanarudisha kadi za magamba wanachukua za chadema. hao ni changamoto kubwa sana, na ndiyo mtaji wa mabwepande. hao akipita mtu akawaambia mfumo-dume ni haram (japo tumekuwa tukiongozwa na marais wanamume tangu baada ya enzi za mkoloni mweupe), wao wataamini tu, provided umewagawia fulana kidogo, kofia, khanga na vilemba kwa wamama watakuamini. si unajuwa watanzania tunalaumiwa kwa kuwa wepesi wa kusahau!?
 
CCM ingawa wapo thick, at least they are smart kurealise kwamba kusimamisha mgombea mwenye jinsia ya kike ni risk ambayo hawapo tayari kuichukua. We will see though.....
 
CCM ingawa wapo thick, at least they are smart kurealise kwamba kusimamisha mgombea mwenye jinsia ya kike ni risk ambayo hawapo tayari kuichukua. We will see though.....


time will tell mkuu. mtu akiwa anakata roho anaweza akataka maji, na ukimpa hanywi. tusubiri. cha muhimu ni kwa intelijensia zetu kuwa macho na haya magamba. nyendo zao zote ziwe on record.
 
nimesoma vizuri moja ya makala za Tanzania Daima toleo la Jumapili ya leo. Makala hayo yanahusu propaganda mpya ambayo ccm wanaweza kuja nayo katika uchaguzi mkuu ujao ... propaganda ya ujinsia. Nafikiri wengi tuna taarifa zinazomuhusisha mwalimu Dr. MIGIRO, Asha Rose na urais wa Chama Cha Mabwepande mwaka 2015.

mwandishi wa makala yale amejikita katika kujenga hoja zake kwamba si dhambi mwana mama kuwa Rais wa taifa hili, lakini kwa kuwa wenzetu wapo kwenye siku zao za mwisho za kuongoza Taifa hili, watajaribu kupenyeza hoja za ujinsia, na kwa kufanya hivyo, wataukandia kwa nguvu zote mfumo-dume (na hii itapelekea chama changu kilichonilea, Chadema, kuzidiwa nguvu kwani ccm kwa sarakasi hawakamatiki). Ili kula nao sahani moja, naungana na hoja ya muandishi wa makala yale kwamba, kuna haja ya kusimamisha mwana-mama katika uchaguzi ujao ili tule nao sahani moja hawa magamba.

ujio wa mama Ellen Johnson, Rais wa Liberia ni dalili ya mvua. So Chadema, let's go neck in neck with magamba.

Vyuma mbona tunavyo jamani!? mikakati tu!

Kwa mtizamo wangu, kama hoja hii itapita (ni juu ya chama kuamua), Ms. Halima James Mdee ndiyo GHARIKA ya wanawake wote wanaojiita UWT na waume zao.

Kwanini na kuwa na Mawazo ya kuiiga CCM? CHADEMA ni CHADEMA na CCM ni CCM? Saa nyingine FIKRA za WANA

JAMII ZINATISHA... ELLEN JOHNSON aliwekwa hajashinda kihalali Chaguzi zote Mara mbili... she's just a figure head

Usilinganishe kuwa alichaguliwa kwahiyo ni DEMOKRASIA ni pressue toka Nje ya NCHI wapinzani wake wanajitoa
 
Mkuu JK ana uwezo wa kumchagua PM anaemtaka.. AG anaemtaka.. mawaziri anaowataka bt hana ubavu wa kuwachagulia ccm mgombea wao wa uraisi.. Kuna machui na masimba yanayoutaka uraisi kwa gharama zozote na ambao wana nguvu na uwezo wa kifedha ndani ya CCM na hapo ndipo utakaposhangaa JK atakavyokosewa adabu na wenzie.. So liciwatishe hilo kwa kuwa halipo..
 
Kwanini na kuwa na Mawazo ya kuiiga CCM? CHADEMA ni CHADEMA na CCM ni CCM? Saa nyingine FIKRA za WANA

JAMII ZINATISHA... ELLEN JOHNSON aliwekwa hajashinda kihalali Chaguzi zote Mara mbili... she's just a figure head

Usilinganishe kuwa alichaguliwa kwahiyo ni DEMOKRASIA ni pressue toka Nje ya NCHI wapinzani wake wanajitoa

hoja ni propaganda mkuu. ccm hawajambo kwa hili, na uzoefu unaonesha wamefanikiwa mara nyingi tu.

ili tusijekuanza ku-deal na propaganda badala ya kumwaga sera, ni bora kubalance nao kwenye ishu ya gender ili tuzungumze mambo ya msingi ya taifa badala ya uke na uume wa mifumo yetu ya kiutawala.

kimsingi aliyeandika makala yale ana hoja, na mimi nimenusa ukweli ndo maana nahisi kuna haja ya kumuunga mkono.
 
hoja hii ingepita vyema kwa watanzania kama spika angeongoza bunge vyema......

Lakini kwa style hiyo amewaangusha mamilioni ya wanawake tz...........
 
CCM wakimsimamisha Dk.Migiro kitakachowagharimu ni uwezo wake wa kujenga hoja kwa wapiga kura.
 
Hoja dhaifu, tunataka mpambanaji wa kweli atakayekuwa tayari kufanya maamuzi magumu, hatuhitaji aliye na experience ya kukaa Newyork au mwenye passport inayoonyesha kasafiri sana nje (Membe). Tunamhitaji atakayekuwa tayari kuweka mikabata yote ya madini mezani iwe reviewed. Mtu huyo lazima atoke nje CCM maana akitoka ndani yake lazima abebwe na hao hao Mafisadi kufika Ikulu na litakapofika suala la maamuzi mugumu atakutana na hao hao Mafisadi!!
 
Binafsi naona hoja ya ujinsia haina nguvu hasa kwa kuzingatia performance ya Speaker Anne Makinda! Cha muhimu wataalamu ya CDM waingie kazini mapema ili kufikia 2014 waje strategy inayouzika ya jinsi watakavyopunguza ukubwa wa bunge,namna bora ya uchaguzi ambayo hairuhusu mianya ya rushwa,udogo halisi wa baraza la mawaziri,kukomesha posho za wabunge,kubana matumizi holela ya serikali, nk! Kisha waonyeshe ni kiasi gani cha fedha kitakuwa kimeokolewa kwa njia hiyo na jinsi gani fedha hizo zitafanikisha sera ya kutoa elimu bure kwa vijana wetu mpaka chuo kikuu, kuboresha huduma za afya, namna gani zita subsidize bei ya cement+mabati ili wananchi wengi waweze kujijengea makazi bora etc
CDM kama "chama tawala mtarajiwa" ni muhimu kitoke kisayansi zaidi na sio kuiga iga kila kinachofanywa na ccm!!! Tafakari!!!
 
Back
Top Bottom