Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Mojawapo ya vitu ambavyo tumekuwa tukivisikia kwa muda wa wiki sasa na zaidi ni kuwa wananchi wanatakiwa "watii sheria". Kwamba wananchi wakitii sheria basi hawawezi kukutwa na matatizo mbele ya vyombo vya dola. Wapo ambao wanaamini kauli hii bila kuihoji sana. Na kauli hii inapewa uzito zaidi na ile kampeni ambayo tumeona mara nyingi kwenye luninga na matamasha ya kile kinachoitwa "Utii wa Sheria bila Shurti".
Kimsingi, hoja ya kutii sheria bila shurti inataka kupendekeza kwa wananchi kuwa watambue matakwa ya sheria na wakisha yatambua wakubali (assent) na kutii (obey). Kwa mfano, mahali ambapo sheria inasema "Usipite hapa" basi mtu asikutwe anapita kwani akiwa anapita atakuwa anavunja sheria na nguvu inaweza kutumika kumzuia asipite (shurti). Kwa kweli kwenye mazingira yenye nchi ambayo utawala wa sheria unatawala wananchi wangekuwa wanajikuta wanatii sheria bila haja ya kulazimishwa.
Hili ni kweli pia kwenye mambo ya kisiasa ambapo watu wanadaiwa kuwa wawatii polisi bila kushurtishwa. POlisi wakisema rudi nyuma unatakiwa kurudi, wakisema simama unatakiwa usimame na wakisema tawanyika basi unatakiwa kutawanyika. Siyio kusudio langu leo kugusia suala la haki ya mtu/raia kutotii amri halali (inshallah siku nyingine nitagusia hili). Hata hivyo, nataka kupendekeza tu kuwa wale wanaotaka wananchi watii sheria bila shurti wao wenyewe lazima wawe wa kwanza kutii sheria hizo bila kushurtishwa!!
Kumbe kushurtishwa kuko kwa pande mbili. Wakati polisi na vyombo vya dola vinaweza kuwashurtisha watu kutii sheria wananchi nao wanayo haki na uwezo wa kuwashurtisha watawala kutii sheria! Wananchi wanaweza kufanya hivyo kwa njia nyingi mojawapo ni kutumia Bunge, kuwaandikia watawala na pale inapobidi kuandamana dhidi ya watawala kuwalazimisha kutii sheria.
Kama watawala wanapata kazi kutii sheria zinazohusiana na manunuzi ya umma, wananchi wanayo haki ya kuwajia ju; kama watawala hawataki kuwakamata wahalifu na kusimamia sheria (fikiria Kagoda) basi wananchi wanayo haki ya kuishrutisha serikali kutii sheria. Ninachosema ni kuwa tunapotaka wananchi watii sheria tujue kuwa nao wanataka kuona serikali yao inatii sheria vile vile bila shurti. Kama serikali inafikiri inaweza kuwashurtisha wananchi kutii basi wananchi nao wana uwezo - na haki - ya kuweza kuwashurtisha watawala nao kutii sheria.
Hii ni kwa sababu hakuna aliye juu ya sheria. Tunaposema hivi tuna maana hata polisi, usalama wa taifa, JWTZ na hata rais hawako juu ya sheria. Wote wanatakiwa kutii sheria bila shurti. Lakini wasipotii wao basi wajue hawana haki ya kusimama kudai wengine (wananchi) watii sheria. Wanaweza vipi kudai wananchi watii sheria bila shurti wakati wao wenyewe wanaona sheria kwao ni kama "mapendekezo yasiyo na nguvu". Kama sheria inasema polisi wanatakiwa kutoa ulinzi kwa mikutano ya kisiasa bila upendeleo kwanini polisi wasitii takwa hilo la sheria? Kama sheria inasema na kuweka utaratibu wa kumkamata mtu asiye na silaha au asiye tishio kwa polisi au usalama wa wengine kwanini polisi wasitii sheria hiyo lakini wao wanataka wananchi watii sheria ya kutawanyika?
Utii wa sheria basi unahusu wote, popote na kwa vyovyote. Kama wao wanaonesha jinsi wasivyoweza kutii sheria inakuwaje wanashangaa wananchi wengine wanapoamua nao kutotii sheria? Wao watawala watii kwanza!!
MMM
Kimsingi, hoja ya kutii sheria bila shurti inataka kupendekeza kwa wananchi kuwa watambue matakwa ya sheria na wakisha yatambua wakubali (assent) na kutii (obey). Kwa mfano, mahali ambapo sheria inasema "Usipite hapa" basi mtu asikutwe anapita kwani akiwa anapita atakuwa anavunja sheria na nguvu inaweza kutumika kumzuia asipite (shurti). Kwa kweli kwenye mazingira yenye nchi ambayo utawala wa sheria unatawala wananchi wangekuwa wanajikuta wanatii sheria bila haja ya kulazimishwa.
Hili ni kweli pia kwenye mambo ya kisiasa ambapo watu wanadaiwa kuwa wawatii polisi bila kushurtishwa. POlisi wakisema rudi nyuma unatakiwa kurudi, wakisema simama unatakiwa usimame na wakisema tawanyika basi unatakiwa kutawanyika. Siyio kusudio langu leo kugusia suala la haki ya mtu/raia kutotii amri halali (inshallah siku nyingine nitagusia hili). Hata hivyo, nataka kupendekeza tu kuwa wale wanaotaka wananchi watii sheria bila shurti wao wenyewe lazima wawe wa kwanza kutii sheria hizo bila kushurtishwa!!
Kumbe kushurtishwa kuko kwa pande mbili. Wakati polisi na vyombo vya dola vinaweza kuwashurtisha watu kutii sheria wananchi nao wanayo haki na uwezo wa kuwashurtisha watawala kutii sheria! Wananchi wanaweza kufanya hivyo kwa njia nyingi mojawapo ni kutumia Bunge, kuwaandikia watawala na pale inapobidi kuandamana dhidi ya watawala kuwalazimisha kutii sheria.
Kama watawala wanapata kazi kutii sheria zinazohusiana na manunuzi ya umma, wananchi wanayo haki ya kuwajia ju; kama watawala hawataki kuwakamata wahalifu na kusimamia sheria (fikiria Kagoda) basi wananchi wanayo haki ya kuishrutisha serikali kutii sheria. Ninachosema ni kuwa tunapotaka wananchi watii sheria tujue kuwa nao wanataka kuona serikali yao inatii sheria vile vile bila shurti. Kama serikali inafikiri inaweza kuwashurtisha wananchi kutii basi wananchi nao wana uwezo - na haki - ya kuweza kuwashurtisha watawala nao kutii sheria.
Hii ni kwa sababu hakuna aliye juu ya sheria. Tunaposema hivi tuna maana hata polisi, usalama wa taifa, JWTZ na hata rais hawako juu ya sheria. Wote wanatakiwa kutii sheria bila shurti. Lakini wasipotii wao basi wajue hawana haki ya kusimama kudai wengine (wananchi) watii sheria. Wanaweza vipi kudai wananchi watii sheria bila shurti wakati wao wenyewe wanaona sheria kwao ni kama "mapendekezo yasiyo na nguvu". Kama sheria inasema polisi wanatakiwa kutoa ulinzi kwa mikutano ya kisiasa bila upendeleo kwanini polisi wasitii takwa hilo la sheria? Kama sheria inasema na kuweka utaratibu wa kumkamata mtu asiye na silaha au asiye tishio kwa polisi au usalama wa wengine kwanini polisi wasitii sheria hiyo lakini wao wanataka wananchi watii sheria ya kutawanyika?
Utii wa sheria basi unahusu wote, popote na kwa vyovyote. Kama wao wanaonesha jinsi wasivyoweza kutii sheria inakuwaje wanashangaa wananchi wengine wanapoamua nao kutotii sheria? Wao watawala watii kwanza!!
MMM