Ni ukweli Usiopingika kuwa Mhe. Membe ndo Rais Ajaye Tanzania, ndio atamrithi JK maana historia inamlinda kila awaye Waziri Mambo ya Nje ndo Rais Ajaye toka 1995
mkuu yaani huyu alivyo dhaifu akiwa plez dah ntajiunga na maadui zake wale 11 kuhamia kenya.duuuh mkuu nahisi umekosa topic ya kupost kumsimamisha membe itakuwa bora hata arudi white hair
Ukiangalia sana kati ya viongozi wengi wa CCM na walioko serrikalini Membe ndiye anayeonekana kuja kuweza kumudu kuwa mgombea wa kiti cha Urais kupitia chama hicho.
Ukimlinganisha na wagombea wengine (hasa Lowassa aliyejiuzulu kwa kashfa) ni Membe tu ambaye anaonekana kulindwa na mlolongo mkubwa wa kashfa mbalimbali na japo - kama nilivyosema wiki kadhaa nyuma - hajajiandaa kuwa Rais ni wazi miaka hii miwili iliyobakia inaweza kumsaidia kujitengenezea na kuwa a true "presidential candidate"
CCM ikimsimamisha Membe kama mgombea wake inaweza kuwa na nafasi ya kushinda tena kiti cha Urais; wakimsimamisha mtu mwingine yeyote itakuwa ni mwisho wa utawala wa CCM.
Ni kweli?
Lowassa ana tatizo gani?