Hoja kuu ya CCM ya kuwasemea wapinzani kuwa na 'vurugu' yaanza kupuuzwa na wapiga kura

Zak Malang

JF-Expert Member
Dec 30, 2008
5,404
233


Uchaguzi wa Igunga imedhihgbirisha bila shaka yoyote kwamba hoja kuu ya CCM katika kampeni zake za kukisemea chama kingine kuwa ni cha “vurugu” inaanza kupitwa na wakati na polepole inatokomea mbali.

Pamoja na kupandikiziwa kuwa CDM ni chama cha vurugu, wananchi wasikichague, bado CCM ndiyo ikajikuta inapoteza kura (ingawa si jimbo) na CDM kujilimbikizia kura.


Ni kawaida kwa chama kinachopoteza mvuto kukazania hoja ya ‘vurugu’ baada ya kushindwa kuwaelezea wapiga kura kipi kimekuwa kinawafanyia, na mara moja hukimbilia wamekuwa wanasimamia ‘amani’ utadhani ‘amani’ inaweza ikafanywa kuwa ni sera ya chama fulani.

Nani asiyetaka amanai? Na amani haiimbwi majukwaani, hujengwa kwa misingi imara ya haki na utawala bora, vitu ambavyo kwa CCM vimetoweka.

Kwa hiyo ni bora CCM wakaachana na hoja yao hii ya jutaja “vurugu” kuwaponda wapinzani wake, imeanza kutokuwa na mshiko wowote, maana wananchi sasa wameanza kun’amua vurugu zinaanza vipi.
 


Uchaguzi wa Igunga imedhihgbirisha bila shaka yoyote kwamba hoja kuu ya CCM katika kampeni zake za kukisemea chama kingine kuwa ni cha “vurugu” inaanza kupitwa na wakati na polepole inatokomea mbali.

Pamoja na kupandikiziwa kuwa CDM ni chama cha vurugu, wananchi wasikichague, bado CCM ndiyo ikajikuta inapoteza kura (ingawa si jimbo) na CDM kujilimbikizia kura.


Ni kawaida kwa chama kinachopoteza mvuto kukazania hoja ya ‘vurugu’ baada ya kushindwa kuwaelezea wapiga kura kipi kimekuwa kinawafanyia, na mara moja hukimbilia wamekuwa wanasimamia ‘amani’ utadhani ‘amani’ inaweza ikafanywa kuwa ni sera ya chama fulani.

Nani asiyetaka amanai? Na amani haiimbwi majukwaani, hujengwa kwa misingi imara ya haki na utawala bora, vitu ambavyo kwa CCM vimetoweka.

Kwa hiyo ni bora CCM wakaachana na hoja yao hii ya jutaja “vurugu” kuwaponda wapinzani wake, imeanza kutokuwa na mshiko wowote, maana wananchi sasa wameanza kun’amua vurugu zinaanza vipi.


Yote hayo ni kuanza kuishiwa sera wanakimbilia 'vurugu.' Polepole hoja hiyo inaanza kuwa siyo tena dili kwao na sijui sasa watatafuta nini mbadala. La mwisho watakalofanya nadhani litakuwa lile la Kivuitu - kutumia ubabe kubadilisaha matokeo na potelea mbali nendeni mkauane huko mitaani.
 
mkuu umenena, hata zile hoja za ukabila na udini naona zime bounce tena kwa kishindo, wananchi zaidi ya 23,000 walioipigia kura chadema pale igunga imeonyesha kwamba CDM inakubalika na yanayosemwa na sisiem ni fitina tupu
 
Mimi naomba Meli nyingine ipinduke kule Zanzibar itoweke na Wabunge kama watatu hivi wa kuchaguliwa ili tuanze mtanange mwingine huko Zenji, ndo watajua CDM ni chama cha kitaifa au la.
 
Mimi naomba Meli nyingine ipinduke kule Zanzibar itoweke na Wabunge kama watatu hivi wa kuchaguliwa ili tuanze mtanange mwingine huko Zenji, ndo watajua CDM ni chama cha kitaifa au la.

Samahani Ndugu - post yako ina mahusiano gani na mada? Bora ungeanzisha mada hiyo ya utaifa wa vyama ili ijadiliwe.
 
Back
Top Bottom