Waberoya
Platinum Member
- Aug 3, 2008
- 15,169
- 10,783
Matokeo ya kura yalionyesha dhahiri kuwa CDM ingepata wabunge 120. Na ikazuka hofu ya ghafla ikulu kuwa itakuwaje kuhusu matokeo ya rais? CDM ikiwa haina cha kushikiria wala uthibitisho kwani asilimia 9 ya vituo vyote vya kupiga kura hakukuwa na wakala wa CDM
Saa sita na dakika kumi siku tatu kabla ya matokeo taarifa rasmi ambayo haikuwa na kupingwa ilionyesha kuwa Slaa ameshinda. Na taarifa zingine za ndani kutoka source zingine nje ya election team zilionyesha Kikwete kashindwa
Kama kawaida kitu ambacho wengi hawakijui, ili Fulani awe rais lazima jeshi, kura na usalama wa taifa vikubaliane!! Bosi mkuu wa moja ya vyombo hivi alikataa kukubali upinzani kushika nchi!
What happened!
1. Kikwete alikubali kuwa acha upinzani ushike nchi na hayuko tayari kuona damu ikimwagika!
2. Mkutano mkali kwenye moja ya vyombo vya ulinzi, huku kimoja kikisema washike wapinzani, kingine kikasema haiwezekani chombo kimoja kikadai zitolewe sababu ya msingi ama sivyo kutasababisha tatizo.Sababu ya msingi na ambayo iliwamaliza wote ilitolewa na mtu ambaye aliitoa kwangu kuwaIli tujenge Tanzania kama nchi, basi lazima vyama vya upinzani vyote ( minimum viwili) viwe na nguvu ambayo inafanana, ilihofiwa kuwa endapo CCM itaondoka madarakani basi kitakufa tu! Halafu baada ya siku si nyingi CDM nayo itageuka kuwa CCM nyingine.
Uzuri ni kuwa vyombo vya usalama vyote vilikiri kuwa ccm imepoteza ule utamu wake!! Hoja hii si ya kwanza..wakati Kenya Odinga akiwa na ajenda ya siri ya kidini, usalama wa taifa ukalazimisha Kibaki awe rais, ili kulinda u-kenya. Same cases can be said in zimbabwe etcKikwete akaelezwa umuhimu wa kuibadili CCM na kuwa izaliwe upya a.k.a rebirth au kujivua gamba
Je hoja hii ambayo iliungwa mkono kwa nguvu zote na kuifanya ccm iendelee madarakani ina mashiko kiasi gani??
jadili