Hoja hizi zijibiwe kabla ya kumtangaza nyerere mwenye kheri!!!!!!!!!!!

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,470
911,173



Viongozi wa kisiasa na kidini ambao kwa sababu binafsi au nyinginezo wamekuwa mstari wa mbele katika kumpigia debe mwasisi wa taifa hili awekwe kwenye njia ya kutangazwa mtakatifu kwa hatua ya awali ya kuitwa mwenye kheri.

Safari za Butiama na Kampala zikisindikizwa na misa si haba na shamra shamra za hotuba ndefu ndefu zinalenga kumtangaza Nyerere mwenye Kheri lakini kwenye Mathayo 6:5 Mtukufu Yesu Kristu alituaasa yafuatayo na ninanukuu:-

“6:5 And when you pray, you shall not be like the hypocrites: For they love to pray standing in the Synagogues and on the corners of the streets, that they may be seen by men. Assuredly I say to you, they have their reward.”


Katika Mathew 7 : 21-23 Mtukufu Yesu Kristu aliaagiza yafuatayo na ninamnukuu:-

“ 21: Not everyone who says to Me, ‘Lord, Lord’ shall enter the kingdom of heaven, but he who does the will of My Father in heaven.

“22: Many, will say to Me in that day, ‘Lord, Lord, have I not prophesised in Your name, cast out demons in Your name, and done many wonders in Your name?’

“23: And then I will declare to them, ‘ I never knew you; depart from Me, you who practice lawlessness!” Mwisho wa kunukuu.


Na kwenye Mark 12: 38 – 40 kuna maelekezo ya kiroho yafuatayo na ninanukuu:-

“38: Then He said to them in His teaching, “Beware of the scribes, who desire to go around in long robes, love greetings in the marketplaces,

“39: The best seats in the Synagogues, and the best places at feasts,

“40: Who devour widows’ houses, and for a pretense make long prayers. These will receive greater condemnations” Mwisho wa kunukuu.

Maudhui haya ya Mwana wa Mungu yanabainisha ya kuwa viongozi wa kanisa ni wa kuwaangalia angalia kwa mashaka mashaka tu kama kweli kauli zao na matendo yao yanawakilisha matakwa ya Mwenyezi Mungu au yanawakilisha matakwa yao binafsi.

Upo ushahidi wa kutosha kwenye Biblia ya kuwa hata viongozi wa dini mara nyingi hutafsiri visivyo maandiko matakatifu. Ukisoma Mathew 22: 29 – 30 yapo mafunzo yafuatayo na ninayanukuu:-

“Jesus answered and said to them, “You are mistaken, not knowing the Scriptures nor the power of God.

“For in the resurrection they neither marry nor are given in marriage, but are like angels of God in heaven.” Mwisho wa kunukuu



Lipo tatizo moja kubwa la kiimani kwa kunuia kumtangaza Nyerere kuwa mwenye kheri:-

a) Kipimo cha kumlinganisha Nyerere na viongozi wabovu kama akina Bokassa wa Afrika ya Kati, Idi Amin wa Uganda, Mobutu wa Seseko wa iliyokuwa Zaire ni kuchemsha katika maandiko matakatifu.

Kipimo sahihi cha kiroho ni kumlinganisha mlengwa mwenyewe kutokana na matendo yake kama yamekidhi mahitaji ya kiroho kulingana na Amri mbili ambazo alizotuasa Bw. Yesu Kristu.

Amri hizo ni umpende Bwana Mungu wako kuliko unavyoipenda nafsi yako na umpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe na kwa kuzitekeleza Amri tajwa Yesu Kristu alituahidi yafuatayo:-


i. Mark 14:15 “If you love Me, keep my commandments.”


ii. Mark 14:23 “Jesus answered and said to him, if anyone loves Me, he will keep My word; and My Father will love him, and We will come to him and make Our home with him,”


iii. Mark 14:14 “If you ask anything in my name, I will do it,”


Maandiko haya matakatifu yanatufunza ya kuwa ukaribu wetu na Mwenyezi Mungu ni kutimiza yale yote ambayo yapo kwenye Amri zake na kwa kufanya hivyo Yeye atahamia kwetu na cho chote tutakachoomba Mwenyezi Mungu atatutimizia.

Hiki ndicho kigezo kikuu katika kumfikiria yeyote kuwa mwenye Kheri na hatimaye mtakatifu: Kwenye uhai wake mwombea utkatifu lazima awe amefanya miujiza angalau mmoja au basi hata baada ya kifo chake.




b) Je, Nyerere anakidhi vigezo hivi?

Pamoja na ukweli ya kuwa kwenye Biblia takatifu Mathew 7:1 “Judge not, that you be not judged.” tumekatazwa tusipime mtu ili nasi tusije tukapimwa lakini ni ukweli usiopingika ya kuwa zoezi la kumtangaza yeyote yule kuwa mwenye kheri ni utaratibu unaohusisha kutoa hukumu.

Hivyo jibu la kama Nyerere anakidhi vigezo tajwa vya kutangazwa mwenye kheri kwa maoni yangu ni “hapana”

Na ninatoa mfano mmoja kuutetea msimamo huu. Mwaka 1997, Nyerere alipokuwa anasherehekea zaidi ya miaka mia moja ya kuzaliwa mama yake alitabiri juu ya yeye kumwona kwenye uhai wake Raisi wa CCM akimkabidhi Raisi mwingine na mwingine akimkabidhi mwingine kwenye uhai wake labda yeye “apondwe na gari afe” ndiyo tu itazuia utabiri wake kutotokea.

Bahati mbaya sana miaka miwili baadaye yaani tarehe 14th Oktoba 1999, aliaga dunia hii wala siyo kwa “kupondwa kwa gari” bali kwa maradhi ya saratani ya damu ambayo yeye mwenyewe hakujua kuwa yalikuwa mwilini mwake yakimpekecha pekecha polepole!!!!!!!!!!!!

Tatizo hapo ni kuwa utabiri wake ulikuwa wa uongo na manabii wa uongo Biblia takatifu inatuelekeza kuwa adhabu yao huwa ni kifo tu.


Soma “DEUTORONOMY 18:18

“When the prophet who presumes to speak a word in My name, which I have not commanded him to speak, or speaks in the name of other gods, that prophet shall die,

DEUTORONOMY 32: 39

“ Now see that I, even I, Am He, and there is no God besides Me; I kill and I make alive; I wound and I heal, nor is there any who can deliver from My hand” Mwisho wa kunukuu

Yawezekana kabisa ya kuwa Kanisa linalindwa na sheria nyingine za Mwenyezi Mungu katika hili zoezi linaloendelea lakini kutuelemisha waaumini litakuwa ni jambo la hekima ili isije ikadhaniwa ni viongozi tu ambo ufalme wa Mungu ni wao kinyume na matakwa ya Mwenyezi Mungu.
 
Hivi hii inaniusu nini mimi Almujaidina?
au wale wenzangu walokole?
au wale wazee wa kupanda ndege na biblia kama passport?

MIMI NAZANI INAWAHUSU SANA WENYE DHEHEBU LAO, ata kama wakiamua Lowasa/Rostam ni wenye heri huku wakiwa bado hai, SISI HAITUHUSU.
ni sawa na WANYAKYUSA WALIPOONA KWAO AMNA MWENYE UWEZO WA UCHIFU WAKA AMUA KUMPA MKWERE.

TAFADHALI TUIPOTEZEE!
 
Rutashubanyuma - waachie waumini wa kweli wa kikatoliki waendelee na mchakato wao kuhusu hiyo mada. Wewe hutalazimika kukubaliana na lolote watakalolifikia. Sana sana unaleta maudhi.
 
mkandara nadhani unakosea kwani nyerere si alikuwa mwanasiasa? Sasa kuna ubaya gani issue zake zikizungumzwa hapa?

Nyerere alikuwa Mwanasiasa, Mshairi, Mwanafalsafa, Mchunga ng'ombe etc. mada hii si ya Nyerere Mwanasiasa ni ya Nyerere Mkatoliki, Nadhani thread hii iende kwenye dini kama alivyopendekeza Mkandara, sioni sababu likitajwa jina la Nyerere basi tunaona kitu kimoja tu, siasa!
 
Hivi hii inaniusu nini mimi Almujaidina?
au wale wenzangu walokole?
au wale wazee wa kupanda ndege na biblia kama passport?

MIMI NAZANI INAWAHUSU SANA WENYE DHEHEBU LAO, ata kama wakiamua Lowasa/Rostam ni wenye heri huku wakiwa bado hai, SISI HAITUHUSU.
ni sawa na WANYAKYUSA WALIPOONA KWAO AMNA MWENYE UWEZO WA UCHIFU WAKA AMUA KUMPA MKWERE.

TAFADHALI TUIPOTEZEE!

Wewe Almujaidina? Au ni Mgalatia usiyekuwa na akili unayejaribu kupoteza lengo? :lol:
 
Back
Top Bottom