Hoja binafsi: Zitto akabidhiwe jahazi??

Mimi ni mkristo na tangu awali nilijua kuwa ZK ni mwislam, nilimpenda sana kijana ZK hapo alipojitokeza kama kijana shujaa hadi hapo alipoanza kuyumba na kuonyesha tabia za kihuni katika CDM. Hata mleta hoja unajua kuwa zito kama ameonyesha udhaifu mkubwa huu akiwa ktk cheo cha unaibu katibu mkuu wa CDM na mbunge, hivi akiwa sasa ndo m/kiti wa chama mambo yatakuwaje!!!!! Na hapa tuondoe ushabiki wa kumchukia au kumpenda kijana ZK kwa namna yoyote ile.

Kijana wangu ZK ni nani aliye kuloga au umepatwa na nini? ulianza aktika kuaminika sana na unamalizia katika kutiliwa mashaka na umma mkubwa wa wapenda mageuzi. yanayojitokeza na yanayowekwa wazi juu yako yanatuhuzunisha sana kuwa sasa ZK umebadilika na umekuwa siye shujaa yule... angalia wapi umeanguka ukauacha upendo wa kwanza ukatubu na Mungu atakupa nguvu tena kama mwanzo na watanzania nikiwa mmoja wao huenda tutakuamini tena.

Safari ya mabadiliko mtoa hoja siyo ya nani awe m/kiti wa CDM ni zaidi ya hapo. Hata mimi naweza kuwa m/kti muhimu ni Watanzania kuelewa Haki zao na kuziendea kwa namna yoyote ile.

Kama wewe ni msomi kama unavyodai ebu mfanyie ZK na wewe menyewe SWOT analysis halafu uache kutaka nani ( au ZK) awe m/kti wa CDM maana siyo hoja kuu

Nimesikitishwa sana na mawazo finyu eti ndo ya great thinkers....!!!! ZK awe m/kti wa CDM!!!!

Suala siyo udini wala ukabila ni tamaa ya kutotaka kutulia na kujifunza na kujua kuwa kila jambo lina wakati wake chini ya jua.

Nikisoma vizuri between the lines naona kabisa husemi ukweli kuhusu ZT, unajidai tu..no evidence
 
Ndugu zangu, kwa mheshimiwa kabwe zitto kupewa uwenyekiti wa chama siyo sahihi kwa kuwa yeye bado ni limbukeni (kabla ya kupiga kura uchaguzi uliopita alisha jitangazia kule kigoma kuwa akirudi kule mwaka mwingine ataenda kuomba kura za urais swali la kujiuliza Dr. slaa wasinge mchakachua yeye angempokea urais 2015).
pia yeye ndiyo tatizo ndani ya chadema na anatafuta umaarufu wake badala ya chama ambalo ni tatizo kubwa katika chama!.
alishajitangaza kuwa yeye anakubalika majimbo mengi, je kule alikosema anaweza kwenda kuwa mbunge hawana watu wakushika wadhifa huo?.

kwasasa mimi naamini kabisa kuwa ni kibaraka wa Kikwete na CCM na pale yupo kuvuruga chama! na akipewa chama ndiyo itakuwa rahisi kukimaliza.
Amini usiamini Zitto kabwe hata kaa atulie mpaka chama kife na mwisho atajiunga na chama kingine ili akiue kabla ya kujiunga na chama chake (ccm). kwani si ndiyo walewale na akina lyatonga mrema?
zk anapenda chama wasifanye mambo ya mana badala yake wawe wanamjadili yeye na kutatua matatizo yanayosababishwa na yeye!
chanzo kikubwa ni ile kuonywa alipokiuka makubaliano ya kutaka nje ya ukumbi wa bunge kikwete alipokuwa anahutubia bunge naye hakwenda bungeni ili asiwemo kwenye mkumbo ambalo ni kosa!

Chonde chonde ZK Hafai kuwa rais wala uenyekiti!
 
Kamarade,
Kwa kujibu swali langu umezua maswali mengi zaidi. Kwanza kuna Wachaga wangapi katika uongozi wa CHADEMA? Unasema kuwa kama uongozi wa Chadema utabadilishwa, mathalan, Zitto awe mwenyekiti badala ya Freeman "hata kina sisi wenye kuvutiwa na Chadema lakini wanaogopa kujihusisha ...watakuwa tayari kujiunga na kuwa mstari wa mbele katika kujenga chama.." Kama Chadema ina ukabila, kumwondoa Freeman na nafasi yake kuchukuliwa na Zitto haitaondoa ukabila huo, isipokuwa kama Zitto atawale kama dikteta. Kinachokuzuia kujiunga na Chadema si uongozi wa Freeman bali ukabila wako (sijui wewe ni kabila gani) kwa kuona kuwa kuna ukabila ndani ya Chadema.
Pili, umesema kuna Waislamu ndani ya CCM ambao wangependa kujiunga na Chadema lakini kwa kuwa kinaongozwa na Mkristo (Freeman) wanakwazwa na fikra kuwa CHADEMA ni chama chenye kulinda maslahi ya wakristo na ukristo nchini," maneno yako mwenyewe. Kwa hiyo, hawa ndugu zetu waislamu, watahakikishiwa maslahi yao yanalindwa ikiwa tu Zitto, au Muislamu mwengine ataongoza Chadema. Hebu niambie ndugu yangu kama huo si udini, ni nini? Kama hao Waislamu wanasukumizwa kubaki CCM kwa sababu ya udini wao wabaki huko huko.

Jasusi, Uko zako huko DC usidhani kuwa unaijua CDM kama tuijuavyo sisi viongozi na wanachama wa muda mrefu. Anachosema Kamarade ni kweli, CDM haina ajenda ya uchaga lakini ni wazi wachaga walio wengi wanaamini kuwa ndicho chama kinacholinda maslahi yao ambayo wanaamini kuwa CCM imewabana na hasa sasa wakati wa uongozi wa Kikwete. Hivi unajua ni wachaga wangapi ambao ni viongozi CCM lakini ni wachangiaji wakubwa wa CDM na wengine hata uanachama wa siri wanao? Hivi umepitia facebook ya Dr Slaa na ukaona wafuasi wake wengi wana majina ya kabila gani?

Kumondoa rafiki yako Freeman hakutaondoa ukabila lakini kutapunguza makali ya propaganda za CCM kuwa CDM ni chama cha wachaga. Propaganda ambayo imefanikiwa kwa kiasi kikubwa kutokana hasa na makosa mengi wanayoyafanya viongozi wetu ambao hawaoni umuhimu wa kuepuka matendo ambayo yanathibitisha ukabila huo. Hivi unajua ni kiasi gani cha bajeti ya Operesheni Sangara na Uchaguzi wa 2010 ambazo zimetumika katika majimbo ya uchagani ukilinganisha na majimbo mengine.

kuhusu uislamu sio kuwa Zitto atahakikisha maslahi ya waislamu yanalindwa isipokuwa itaondoa utando wa udini na kufungua milango kwa CDM kupata wafuasi wengi zaidi na kuthibitisha sura ya utaifa tofauti na ilivyo sasa. Na hili sio kutoka kwa kamarade tu lakini hata viongozi wa CDM akiwemo Mzee mtei analitambua ingawa inamlazimu kumbeba Mkwewe kiaina. Zitto mwenyewe huo uslamu ni asili tu maana hata maisha yake ni tofauti kabisa na itikadi za kiislamu. Lakini mimi najua kuwa kuna waislamu wengi katika CDM ambao hawakubaliana na hali ya kutokuwa na imani yao iliyojijenga miongoni mwa viongozi wa chama haswa wale wa sekretariat ambao karibia wote ni wafuasi wa rafiki yako Freeman Mbowe.

Haya yote naukichanganya na yaliyofanyika wakati wa uchaguzi uliopita ambayo tumeamua kuyanyamazia yanasababisha CDM kukosa wafuasi wengi muhimu hasa kutoka katikamakabila mengine makubwa na waislamu na bila ya kubadili hali hii tutaishia kuwa wapinzani wa kudumu hata CCM ikiendelea na madudu yake.
 
Wewe ZITTO ni mjinga,Mpumbavu na si msikivu kama mama yako mzazi alivyosema kwenye vyombo vya habari ni mbishi kama mshipa,watu wamekutahadhalisha kwamba hasira,visasi,uzandiki,unafiki haukufai umekuja kwa jina la Bwanyenye TZ ili ujisafishe huitaji mitandao kujisafisha itachukua muda jinsi ulivyo haribu jina lako hayo unayosema hapo juu inaweza kuwa kweli manake wewe ndio unajua picha halisi lakini sisi hatukuamini kabisa tunajua wewe ni msaliti na mvurugaji uliye pandikizwa umeshauliwa mara nyingi kuwafuata rafiki zako NCCR kwani unangoja nini badala ya kila siku kuendekeza beef lako na Mbowe na DrSlaa hufai kuwa kiongozi huwezi teamwork wala maamuzi ya pamoja,kama chama walikutetea ulipotakiwa kupigwa na wabunge wenzio na kuondoka usijifanye sasa kwamba wewe ndio mshindi kutaka kuvuruga chama una roho ya aina gani unaalika majeshi kuja kuanika mambo ya ndani ya chama chalo unajishusha hadhi mara 100 zaidi

Hivi unadhani ni Zitto pekee anayoyaona mapungufu tuliyonayo ndani ya chama? Hivi mnadhani hizi chuki mnazozipandikiza dhidi ya Zitto ndio zitanyamazisha watu wasitoe mawazo mbadala ya Mbowe? Tumechoka na huu ujinga wenu wa kumsakama Zitto wakati mkijua wazi kuwa ni mwenyekiti wenu na timu yenu ndio chanzo cha ujinga unaoendelea katika chama. Kama wengine tulinyamaza sasa mtambue kuwa hata mkimaliza Zitto wengine mamia wataibuka kupambana na huu ujinga wenu. Tumechoka ujinga wenu..Na kama hamko tayari kubadilika basi hatutaacha kuwachoongea kwa watanzania ili labda wao watawafundisha na mkaaelewa kuwa ubinafsi wenu unamaliza ndoto ya CDM yetu. Ndiyo, CDM yetu sote hata kama hatutoki katika jamii zenu.
 
Jasusi, Uko zako huko DC usidhani kuwa unaijua CDM kama tuijuavyo sisi viongozi na wanachama wa muda mrefu. Anachosema Kamarade ni kweli, CDM haina ajenda ya uchaga lakini ni wazi wachaga walio wengi wanaamini kuwa ndicho chama kinacholinda maslahi yao ambayo wanaamini kuwa CCM imewabana na hasa sasa wakati wa uongozi wa Kikwete. Hivi unajua ni wachaga wangapi ambao ni viongozi CCM lakini ni wachangiaji wakubwa wa CDM na wengine hata uanachama wa siri wanao? Hivi umepitia facebook ya Dr Slaa na ukaona wafuasi wake wengi wana majina ya kabila gani?

Kumondoa rafiki yako Freeman hakutaondoa ukabila lakini kutapunguza makali ya propaganda za CCM kuwa CDM ni chama cha wachaga. Propaganda ambayo imefanikiwa kwa kiasi kikubwa kutokana hasa na makosa mengi wanayoyafanya viongozi wetu ambao hawaoni umuhimu wa kuepuka matendo ambayo yanathibitisha ukabila huo. Hivi unajua ni kiasi gani cha bajeti ya Operesheni Sangara na Uchaguzi wa 2010 ambazo zimetumika katika majimbo ya uchagani ukilinganisha na majimbo mengine.

kuhusu uislamu sio kuwa Zitto atahakikisha maslahi ya waislamu yanalindwa isipokuwa itaondoa utando wa udini na kufungua milango kwa CDM kupata wafuasi wengi zaidi na kuthibitisha sura ya utaifa tofauti na ilivyo sasa. Na hili sio kutoka kwa kamarade tu lakini hata viongozi wa CDM akiwemo Mzee mtei analitambua ingawa inamlazimu kumbeba Mkwewe kiaina. Zitto mwenyewe huo uslamu ni asili tu maana hata maisha yake ni tofauti kabisa na itikadi za kiislamu. Lakini mimi najua kuwa kuna waislamu wengi katika CDM ambao hawakubaliana na hali ya kutokuwa na imani yao iliyojijenga miongoni mwa viongozi wa chama haswa wale wa sekretariat ambao karibia wote ni wafuasi wa rafiki yako Freeman Mbowe.

Haya yote naukichanganya na yaliyofanyika wakati wa uchaguzi uliopita ambayo tumeamua kuyanyamazia yanasababisha CDM kukosa wafuasi wengi muhimu hasa kutoka katikamakabila mengine makubwa na waislamu na bila ya kubadili hali hii tutaishia kuwa wapinzani wa kudumu hata CCM ikiendelea na madudu yake.
Bwanyenye,
Haijalishi niko wapi. Naweza kuwa hata Greenland nikajua na kudadavua yanayoendelea nyumbani. Nafurahi umesema kuwa Chadema haina ajenda ya uchaga. That is well and good. Ukaongeza kuwa wachaga walio wengi wanaamini kuwa Chadema ndio chama kinacholinda maslahi yao. I have news for you. Hata pale Musoma ndugu zangu wanaamini kuwa Chadema ndiyo chama kinacholinda maslahi yao. Hiyo ya wafuasi wa CCM kuichangia Chadema hainishtui. Nilipokuwa nyumbani wakati wa uchaguzi nilikuwa "pleasantly surprised" kugundua kuwa marafiki zangu wengi wa CCM walimchangia na kumfanyia fundraising Halima Mdee. Hii inaeleweka. Kuna watu wengi CCM hivi sasa wamechoshwa na usanii wa chama chao. Hao nao wanatafuta chama mbadala. Tuwakaribishe Chadema. I have other news for you. CCM kinajijenga kwa propaganda. Kilianza na mapanga ya CUF wakati wa uchaguzi wa Zanzibar. Kikaja na Uarabu wa Salim katika uchaguzi wa 2005. Na mwaka huu tumeona propaganda za ukabila na udini wa Chadema. I assure you, hata Freeman akiondolewa uongozi CCM watatafuta propaganda nyingine dhidi ya Chadema. Tena itakuwa worse kama Zitto ndiye atakayekuwa mwenyekiti. Huyu wanasema kuwa ni lightweight. Wanajua "his achilles' heel ambayo wataitumia kudhoofisha Chadema hadi watajikuta wanapoteza idadi ya wabunge waliopata katika uchaguzi wa mwaka huu. Umeshasema Chadema haina ajenda ya ukabila. Tuanzie hapo kukiimarisha na pia kupambana na propaganda taka za CCM. Uongo ukirudiwa mara nyingi bila majibu watu wanaanza kuuamini.
 
Mtu kuwa kiongozi yoyote Makini ni lazima huhandaliwa katika itikadi na imani anayo lelewa.
Tangu unapata fahamu (utambuzi) unaelekezwa kuwa na Mtazamo, Msimamo, Mwonekano, Mwelekeo, Kwa manufaa ya waliokuandaa.
Na nikweli sana haiwezekani ubadili (utoke, uhame ) kwa waliokuandaa Na usiwe Mnafiki. Pale unapo hama itikadi iliyo kukuza, inawezakana Mtu huyo akaonekana au akafanya mambo yanayokubalika na wachache lakini wakawa na sauti ya kufanya wengi wayasikie,
lakini yeye hawi salama kwani dhamira yake humsuta, (hutenda kwa unafiki).
Kubadili imani siyo kitu rahisi,
Askofu kuwa Shehk ,
CCM kuwa Chadema n.k.
Zitto akabidhiwe jahazi??, wandugu semeni, Huyo kaandaliwa na nani?(katika imani na itikadi ipi?) au Mazingira ndiyo yaliyo muandaa?
 
Sikonge ni wazi ni mtu makini lakini ama ni chuki zako dhidi ya Zitto ama mapungufu yako katika imani ta demokrasia inakupelekea kuwa tayari kupotosha mambo.

Moja, Maana ya demokrasia ni pamoja na kutokubaliana na maamuzi ambayo kwako yanaweza kuwa sawa lakini kwa mwengine yasiwe sawa hata kama yana uhalali wa wengi. Zitto alipinga hoja ya kumtusi rais wa nchi kisiasa kwa kuondoka wakati anatoa hotuba muhimu kama ile kwa bunge na kwa taifa kwa ujumla. Lakini pia uamuzi ulipofikiwa Zitto hakuupinga bali alikataa kutii kwa kutokuingia kabisa katika ukumbi wa bunge akiungwa mkono na wabunge zaidi ya 15 wakiwemo wasomi kama Professor Kahigi, Naibu Mwenyekiti wa Chama Mzee Said Arfi na wanasiasa wazoefu kama Shibuda. Ukae ukijua hata Mnyika, Halima Mdee, Mzee Ndesamburo, Suzzane Lyimo, Lucy Owenya, Anna Komu wote hawakuunga mkono hoja ya kina Dr Slaa na hawakuhudhuria bungeni siku ile.Hao wengi waliojenga halali hoja hiyo ukitoa Grace Kihwelu wote ni freshaman MPs na wengi wao hata chadema hawaijui vilivyo.

Pili, Zitto hakukataa kutii uamuzi wa Chama kwani uamuzi huo haukuwa wa Chama bali ulikuwa ni wa wabunge wa CHADEMA. Lakini pia alikataa kupinga huku akiamini kuwa makubaliano ati yao kama viongozi wa chama yalikuwa ni kusubiri uamuzi wa Kamati Kuu kuhusu kumtambua ama kutomtambua Rais Kikwete na ni wnzake wakiongozwa na Mwenyekiti na Katibu Mkuu wake ndio waliongoza kuvunja makubaliana hayo. Hivyo basi huo haukuwa uamuzi wa Chama chake bali ulikuwa uamuzi wa viongozi wenzake uliokuwa na uungwaji mkono wa wabunge wenzake 21 ambao kwa mujibu wa idadi ya wabunge wa Chadema hawa hawajafikia hata nusu ya wabunge wote (absolute majority)

Tatu, Zitto hakuenda kulialia katika TV bali kueeleza hali halisi ya suala lile ambalo tayari wenzake walishaanza kulitumia kumnyooshea kidole huku wakijaribu kuficha ukweli wa kilichojiri. Naamini wewe ulikuwa muumimini mkubwa wa siasa za UWAZI na UKWELI na hivyo inanishangaza kuona una ni usaliti ama kulialia pale ambapo kiongozi kama Zitto nakuwa tayari kujiingiza katika msukosuko kisiasa ili kutekeleza spirit ya UWAZI na UKWELI ambayo ni muhimu katika kujenga demokrasia tunayo ltunayoitaka.

Nne, Ni Freeman Mbowe na sio Zitto mwenye siasa za hoja za kibabe na hata uadui pale anapozidiwa ama kutishiwa uthibiti wa nafasi yake. NI Freeman Mbowe ndiye mwenye histori ya kupiga watu, kuwatukana, kuwatukana, kuwachukia na hata kuwaangamiza kisiasa wale wote wanaothubutu kuhoji ama kupinga hoja zake lakini sio Zitto.



Hoja hii ninaiona ina mantiki hata kama nimekuwa natofautiana kiasi na style ya kisiasa ya Dr Slaa hivi karibuni....



Ni wapi ambako kuna ushahidi kuwa Zitto aliwafanyia kampeni hao unaowaita marafiki zake na ni kweli hao wabunge wote wa NCCR ni marafiki zake? Hivi ukiambiwa kuwa ukitoa Kafulila hao wengine Zitto hakuwa na uhusiano nao utaamini? Lakini vilivile huoni kuwa mtizamo wako unafanana na ule wa makada wa CCM ambao walitaminisha kuwa upinzani ni uadui na kushirikiana nao ni usaliti? Hivi kama wana CCM ama vyama vingine wakichukua huu mtizamo wabunge 47 wa Chadema wanaweza kufanya lolote la maana kwa watanzania? Hivi si MASLAHI YA TAIFA Kwanza ndio ilikuwa kauli mbiu iliyowezesha wabunge 11 wa CDM kuweza kushirikiana na wenzao wa CUF na CCM kuamsha na kushurutisha mabadilk kadhaa ambayo wote leo hii tunayasifia? Uma unaamini ni Ujasiri wa Dr Slaa tu ndio ulipelekea yote hayo?



Naamini Zitto ni mtu anayejaribu kuwa kiongozi katika uwanja wa wanasiasa. Kiongozi wa kweli ni pamoja na kusimamia kile unachoamini kuwa ni sawa na hata kama utaonekana ni msaliti kwa wengi. Lakini pia itakuwa vizuri kuonyesha ni wapi Zitto aliwahi kutoheshimu maamuzi ya chama ama ya wanachama kwa mantiki ya kuwa yametolewa na vikao rasmi vya maamuzi vya chama chake na sio maamuzi ya viongozi wenzake wachache waliotayari kutumia mapungufu ya kiasasi ya muundo wa chama ili kufanikisha ajenda zao binafsi?



Ina maana ni viongozi wa Chadema ama wanaCHADEMA tu ndio wanahaki ya kuzungumzia ama kutoa hoja zao kuhusu CDM?



Kwa hiyo unaamini kuwa kuficha siri za mapungufu ya CDM ndio kutasaidia CDM kufanikiwa zaidi na huku ukijua kuwa mafanikio ya sasa ni zaidi kutokana na mapungufu ya CCM na haswa kiongozi wake na sio imani ya watanzania kwa CDM? HUdani kuwa kuwa na kiongozi aliye tayari kuanika siri za mapungufu ya chama chake ni hatua mojawapo kubwa ya kujenga chama chenye kuweza kuaminika zaidi kutokana na umakini wake zaidi ya kuendelea kutegemea mapungufu ya CCM kama mtaji wa kufanikiwa kisiasa?




Kwa fikira kama hizi ni wazi tunakoelekea ni kubaya. Hupaswi kufurahia Tanzania inapoelekea kule ilipokuwa Pemba mradi tu itasaidia mafaniko kwa chama chako ama unachokishabikia. Kumbuka kuwa kule Pemba hakukuwa na mgawanyiko wa kikabila na Kidini lakini hapa kwetu haya yanaweza kugeuka kabisa kuwa ukabila ambapo kabila moja (ambalo linahusishwa na nguvu na ajenda za CDM) laweza kugeuka adui wa makabila mengine mengi na dini moja kuwa adui wa dini nyingine.

Wewe ZITTO ni mjinga,Mpumbavu na si msikivu kama mama yako mzazi alivyosema kwenye vyombo vya habari ni mbishi kama mshipa,watu wamekutahadhalisha kwamba hasira,visasi,uzandiki,unafiki haukufai umekuja kwa jina la Bwanyenye TZ ili ujisafishe huitaji mitandao kujisafisha itachukua muda jinsi ulivyo haribu jina lako hayo unayosema hapo juu inaweza kuwa kweli manake wewe ndio unajua picha halisi lakini sisi hatukuamini kabisa tunajua wewe ni msaliti na mvurugaji uliye pandikizwa umeshauliwa mara nyingi kuwafuata rafiki zako NCCR kwani unangoja nini badala ya kila siku kuendekeza beef lako na Mbowe na DrSlaa hufai kuwa kiongozi huwezi teamwork wala maamuzi ya pamoja,kama chama walikutetea ulipotakiwa kupigwa na wabunge wenzio na kuondoka usijifanye sasa kwamba wewe ndio mshindi kutaka kuvuruga chama una roho ya aina gani unaalika majeshi kuja kuanika mambo ya ndani ya chama chalo unajishusha hadhi mara 100 zaidi


BwanyenyeTZ

Junior Member

Join Date:Mon Dec 2010
Posts:5
Thanks:0
Thanked 0 Times in 0 Posts


Hahahahaha!! I Love JF.
 
Bwanyenye,
Haijalishi niko wapi. Naweza kuwa hata Greenland nikajua na kudadavua yanayoendelea nyumbani. Nafurahi umesema kuwa Chadema haina ajenda ya uchaga. That is well and good. Ukaongeza kuwa wachaga walio wengi wanaamini kuwa Chadema ndio chama kinacholinda maslahi yao. I have news for you. Hata pale Musoma ndugu zangu wanaamini kuwa Chadema ndiyo chama kinacholinda maslahi yao. Hiyo ya wafuasi wa CCM kuichangia Chadema hainishtui. Nilipokuwa nyumbani wakati wa uchaguzi nilikuwa "pleasantly surprised" kugundua kuwa marafiki zangu wengi wa CCM walimchangia na kumfanyia fundraising Halima Mdee. Hii inaeleweka. Kuna watu wengi CCM hivi sasa wamechoshwa na usanii wa chama chao. Hao nao wanatafuta chama mbadala. Tuwakaribishe Chadema. I have other news for you. CCM kinajijenga kwa propaganda. Kilianza na mapanga ya CUF wakati wa uchaguzi wa Zanzibar. Kikaja na Uarabu wa Salim katika uchaguzi wa 2005. Na mwaka huu tumeona propaganda za ukabila na udini wa Chadema. I assure you, hata Freeman akiondolewa uongozi CCM watatafuta propaganda nyingine dhidi ya Chadema. Tena itakuwa worse kama Zitto ndiye atakayekuwa mwenyekiti. Huyu wanasema kuwa ni lightweight. Wanajua "his achilles' heel ambayo wataitumia kudhoofisha Chadema hadi watajikuta wanapoteza idadi ya wabunge waliopata katika uchaguzi wa mwaka huu. Umeshasema Chadema haina ajenda ya ukabila. Tuanzie hapo kukiimarisha na pia kupambana na propaganda taka za CCM. Uongo ukirudiwa mara nyingi bila majibu watu wanaanza kuuamini.

Jasusi nadhani umeeleweka vema. Siamini kama kwa kumweka Kiongozi mwislam kutaua propaganda za CCM. Mara nyingi watu wenye akili wakianza kuitikia nyimbo za CCM huwa nasikitika.
Hivi kweli CDM ingekuwa ya wachaga tu kwa nini wana majimbo mawili tu kilimanjaro?? Halima Mdee kachaguliwa na wachaga jimbo la kawe?? Zitto amepigiwa kura na waislamu tu Kigoma?? Hivi unaweza kushinda urais kwa kura za wakristo/waislam pekee Tanzania.

Hebu tazama Central Commettee ya CCM, kama majina ya watu ni jambo la kushadidia basi tuseme CCM ina udini (waislamu). Kina Tambwe Hiza ndo watakwambia Zitto na Arfi wamewekwa kama pambo tu, sasa sijui the same applies kwa Msekwa!!
1. Ndugu Kakaya Mrisho Kikwete - Mwenyekiti
2.
Ndugu Pius Msekwa - Makamu Mwenyekiti (Bara)
3. Ndugu Amani Abeid Amani Karume
- Makamu Mwenyekiti(Zanzibar)
4. Ndugu Yussuf R. Makamba - Katibu Mkuu
5. Capt. (mst) George Huruma Mkuchika - Naibu Katibu Mkuu (Bara)
6. Ndugu Salehe Ramadhan Ferouz - Naibu Katibu Mkuu (Zanzibar)

7. Dr. Ali Mohamed Shein - Mjumbe
8. Ndugu Edward Ngoyai Lowassa - Mjumbe
9. Ndugu Shamsi Vuai Nahodha - Mjumbe
10. Alhaj Ali Hassan Mwinyi - Mjumbe

11. Ndugu Benjamin William Mkapa - Mjumbe
12. Mzee Rashid Mfaume Kawawa - Mjumbe
13. Dr. Salmin Amour - Mjumbe

14. Ndugu John Samwel Malecela - Mjumbe
15. Capt. (mst) John ZefaniaChiligati - Mjumbe
16. Ndugu Amos GabrielMakala - Mjumbe

17. Ndugu Bernard KamiliusMembe - Mjumbe
18. Ndugu Kidawa HamidSaleh - Mjumbe

19. Ndugu Samwel John Sitta - Mjumbe
20. Ndugu Pandu Ameir Kificho - Mjumbe
21. Ndugu Anna Abdallah - Mjumbe
22. Ndugu Rostum Aziz - Mjumbe

23.Dr. Mohamed Gharib Bilal - Mjumbe
24. Ndugu Pindi Hazara Chana - Mjumbe
25. Ndugu Andrew Chenge - Mjumbe
26. Dr. Maua Abeid Daftari - Mjumbe
27. Ndugu Samia Suluhu Hassan - Mjumbe
28. Ndugu Mohamed Seif Khatib - Mjumbe
29. Ndugu Haji Omar Kheri - Mjumbe
30 . Dr. Abdallah Omari Kigoda - Mjumbe
31 . Ndugu Abdurahman Kinana - Mjumbe
32 . Ndugu Anne Semamba Makinda - Mjumbe

33. Ndugu Fatuma Said Ali Mchumo - Mjumbe
34 . Ndugu Zakia Hamdan Meghji - Mjumbe

35. Ndugu Omar Yussuf Mzee - Mjumbe
36. Ndugu Emmanuel John Nchimbi - Mjumbe
37 . Ndugu Ali Ameir Mohamed - Mjumbe

38. Ndugu Yussuf Moh'd Yussuf - Mjumbe
NB: Pinda anaweza kuongezeka kwenye orodha kutokana na wadhifa wake
 
Ndugu zangu, kwa mheshimiwa kabwe zitto kupewa uwenyekiti wa chama siyo sahihi kwa kuwa yeye bado ni limbukeni (kabla ya kupiga kura uchaguzi uliopita alisha jitangazia kule kigoma kuwa akirudi kule mwaka mwingine ataenda kuomba kura za urais swali la kujiuliza Dr. slaa wasinge mchakachua yeye angempokea urais 2015).
pia yeye ndiyo tatizo ndani ya chadema na anatafuta umaarufu wake badala ya chama ambalo ni tatizo kubwa katika chama!.
alishajitangaza kuwa yeye anakubalika majimbo mengi, je kule alikosema anaweza kwenda kuwa mbunge hawana watu wakushika wadhifa huo?.

kwasasa mimi naamini kabisa kuwa ni kibaraka wa Kikwete na CCM na pale yupo kuvuruga chama! na akipewa chama ndiyo itakuwa rahisi kukimaliza.
Amini usiamini Zitto kabwe hata kaa atulie mpaka chama kife na mwisho atajiunga na chama kingine ili akiue kabla ya kujiunga na chama chake (ccm). kwani si ndiyo walewale na akina lyatonga mrema?
zk anapenda chama wasifanye mambo ya mana badala yake wawe wanamjadili yeye na kutatua matatizo yanayosababishwa na yeye!
chanzo kikubwa ni ile kuonywa alipokiuka makubaliano ya kutaka nje ya ukumbi wa bunge kikwete alipokuwa anahutubia bunge naye hakwenda bungeni ili asiwemo kwenye mkumbo ambalo ni kosa!

Chonde chonde ZK Hafai kuwa rais wala uenyekiti!

unaposema ni akina Lyatonga ina mana ZK Ni shushushu alipita usalama? Mana Mrema alikua usalama wa taifa
 
1. Ndugu Kakaya Mrisho Kikwete – Mwenyekiti (Tanzania Bara)
2.
Ndugu Pius Msekwa - Makamu Mwenyekiti (Bara)
3. Ndugu Amani Abeid Amani Karume - Makamu Mwenyekiti (Zanzibar)
4. Ndugu Yussuf R. Makamba - Katibu Mkuu (Tanzania Bara)

5. Capt. (mst) George Huruma Mkuchika - Naibu Katibu Mkuu (Bara)
6. Ndugu Salehe Ramadhan Ferouz - Naibu Katibu Mkuu (Zanzibar)
7. Dr. Ali Mohamed Shein – Mjumbe (Zanzibar)
8. Ndugu Edward Ngoyai Lowassa - Mjumbe
9. Ndugu Shamsi Vuai Nahodha – Mjumbe (Zanzibar)
10. Alhaj Ali Hassan Mwinyi - Mjumbe
(Zanzibar)
11. Ndugu Benjamin William Mkapa - Mjumbe
12. Mzee Rashid Mfaume Kawawa – Mjumbe (Tanzania Bara)
13. Dr. Salmin Amour – Mjumbe (Zanzibar)

14. Ndugu John Samwel Malecela - Mjumbe
15. Capt. (mst) John Zefania Chiligati - Mjumbe
16. Ndugu Amos GabrielMakala - Mjumbe

17. Ndugu Bernard Kamilius Membe - Mjumbe
18. Ndugu Kidawa HamidSaleh – Mjumbe (Zanzibar)

19. Ndugu Samwel John Sitta - Mjumbe
20. Ndugu Pandu Ameir Kificho – Mjumbe (Zanzibar)
21. Ndugu Anna Abdallah – Mjumbe
22. Ndugu Rostum Aziz – Mjumbe (Tanzania Bara)

23.Dr. Mohamed Gharib Bilal – Mjumbe (Zanzibar)
24. Ndugu Pindi Hazara Chana - Mjumbe
25. Ndugu Andrew Chenge - Mjumbe
26. Dr. Maua Abeid Daftari – Mjumbe (Zanzibar)
27. Ndugu Samia Suluhu Hassan – Mjumbe (Zanzibar)
28. Ndugu Mohamed Seif Khatib – Mjumbe (Zanzibar)
29. Ndugu Haji Omar Kheri – Mjumbe (Zanzibar)
30 . Dr. Abdallah Omari Kigoda – Mjumbe (Tanzania Bara)
31 . Ndugu Abdurahman Kinana – Mjumbe (Tanzania Bara)

32 . Ndugu Anne Semamba Makinda - Mjumbe
33. Ndugu Fatuma Said Ali Mchumo – Mjumbe (Zanzibar)
34 . Ndugu Zakia Hamdan Meghji – Mjumbe (Zanzibar)

35. Ndugu Omar Yussuf Mzee - Mjumbe (Zanzibar)
36. Ndugu Emmanuel John Nchimbi - Mjumbe
37 . Ndugu Ali Ameir Mohamed – Mjumbe (Zanzibar)

38. Ndugu Yussuf Moh'd Yussuf – Mjumbe (Zanzibar)



Jumla ya Wajumbe wa Kamati Kuu: 38
Jumla ya Waislamu: 24
Jumla ya Waislamu ukitoa Wazanzibari: 6
Jumla ya Wakristo: 14

Ina maana bila ya Zanzibar CCM wangelikuwa pabaya sana katika siasa hizi uwiano wa kidini.
 
Back
Top Bottom