Elections 2010 Hofu ya serikali ya CCM Kilimanjaro yazuia graduation Majengo Sec School

dm2000inter

Member
Oct 27, 2010
29
10
Ama kweli CHADEMA imeishika pabaya CCM. Msimamizi wa uchaguzi Jimbo la Moshi mjini,Bernadette Kinabo leo amepiga marufuku sherehe za mahafali ya sekondari ya Majengo inayomilikiwa na Kanisa Katoliki Jimbo la Moshi kwa sababu itaipa ujiko Chadema. Taarifa za maofisa usalama zinadai mkuu wa shule hiyo aliitwa leo saa 3:00 asubuhi na Kinabo na kuambiwa afute Graduation hiyo iliyokuwa ifanyike Jumamosi ya Tarehe 30.10.2010 hadi uchaguzi utakapomalizika. Inaelezwa kuwa mkuu wa shule hiyo alielezwa wazi kuwa maagizo hayo ni maelekezo toka ngazi za juu. Taarifa ni kwamba Academic Master wa shule hiyo, Pantaleo Minja anagombea Udiwani kata ya Majengo kwa tiketi ya Chadema na ndiye anayepewa nafasi kubwa ya kushinda. Shule hiyo ina wanafunzi zaidi ya 2,800 na wanafunzi 1,600 wamejiandikisha kupiga kura katika daftari la kudumu la wapiga kura. Uamuzi huu wa serikali umechochea hasira ya wazazi na wanafunzi kwa kuwa baadhi ya wazazi walishakodisha kumbi kwa ajili ya kuwapongeza watoto wao, kutoa order za cake na kadha wa kadha. Swali la kujiuliza ni je Uamuzi huu wa msimamizi umekisaidia CCM au ndio umekimaliza zaidi kisiasa?Jibu unalo kwa kichwa....:sad:
 
Ama kweli CHADEMA imeishika pabaya CCM. Msimamizi wa uchaguzi Jimbo la Moshi mjini,Bernadette Kinabo leo amepiga marufuku sherehe za mahafali ya sekondari ya Majengo inayomilikiwa na Kanisa Katoliki Jimbo la Moshi kwa sababu itaipa ujiko Chadema. Taarifa za maofisa usalama zinadai mkuu wa shule hiyo aliitwa leo saa 3:00 asubuhi na Kinabo na kuambiwa afute Graduation hiyo iliyokuwa ifanyike Jumamosi ya Tarehe 30.10.2010 hadi uchaguzi utakapomalizika. Inaelezwa kuwa mkuu wa shule hiyo alielezwa wazi kuwa maagizo hayo ni maelekezo toka ngazi za juu. Taarifa ni kwamba Academic Master wa shule hiyo, Pantaleo Minja anagombea Udiwani kata ya Majengo kwa tiketi ya Chadema na ndiye anayepewa nafasi kubwa ya kushinda. Shule hiyo ina wanafunzi zaidi ya 2,800 na wanafunzi 1,600 wamejiandikisha kupiga kura katika daftari la kudumu la wapiga kura. Uamuzi huu wa serikali umechochea hasira ya wazazi na wanafunzi kwa kuwa baadhi ya wazazi walishakodisha kumbi kwa ajili ya kuwapongeza watoto wao, kutoa order za cake na kadha wa kadha. Swali la kujiuliza ni je Uamuzi huu wa msimamizi umekisaidia CCM au ndio umekimaliza zaidi kisiasa?Jibu unalo kwa kichwa....:sad:
Msimamizi wa Uchaguzi hana mamlaka hayo kila shule ina haki ya kufanya sherehe zake na kwa kuwa siku hiyo ni sahihi. Ingekuwa kama sherehe imegeuzwa kuwa mkutano wa kampeni hapo sawa. Hivyo huyo Mkuu wa Shule anaweza kupuuza hayo mawazo ya huyo Mkurugenzi.
 
uchaguzi hauna maana ya kusimamisha kila kitu, waacheni watoto wafanya graduation yao
 
bado haizuii kuipeleka chadema ikulu duuuh huyo ni bogas kama mrs mkwere
 
Jamani angalieni! mwishoni mtakuja kuahirisha mazishi. Hofu yote ni ya nini? kumbe mambo ya CCM yamefikia hali hiyo. Kwa kweli tufanye maandalizi ya kuiaga CCM.

Watu walishatabiri huko nyuma kuwa CCM itakufa mikononi mwa Kikwete.
 
Jamani angalieni! mwishoni mtakuja kuahirisha mazishi. Hofu yote ni ya nini? kumbe mambo ya CCM yamefikia hali hiyo. Kwa kweli tufanye maandalizi ya kuiaga CCM.

Watu walishatabiri huko nyuma kuwa CCM itakufa mikononi mwa Kikwete.

Dah! Hii kali mkuu. Kuahirisha mpaka mazishi? In short it means hakuna kufanya event yoyote yenye mkusanyiko wa watu mpaka baada ya uchaguzi?
 
Kama hii taarifa ni ya kweli basi tujiande na vurugu za matokeo maana kwa mtaji huu sintashangaa wakivuruga matokeo
 
Back
Top Bottom