NEW NOEL
JF-Expert Member
- May 21, 2011
- 863
- 407
Hii imemtokea jamaa mmoja. Anasema alikuwa amesafiri kwenda mkoa mmoja huko kanda ya kusini. Alipofika huko kwa bahati mbaya akapoteza pochi yake ambayo ilikuwa na pesa taslimu pamoja na vitambulisho kadhaa. Lakini baada ya muda msamaria mwema akamtafuta,ili ampatie pochi yake. Cha ajabu alikuta kila kitu kipo ikiwemo pesa zake zote. Ila hakukuta kadi yake ya uanachama ya CCM. Sasa anajiuliza kwanini yule msamaria amemkabidhi vitu vyote isipokuwa ile kadi?