Hilo ndo jibu mkuu, ni mara chache sana wanakosea
hili ndilo tatizo la wabongo mkifaulu mnaona wenzenu vilaaza hata kama wameonewa lkn ukweli wote unaonekana vyuo mkikutana na waliopitia diploma wanawakimbiza kishenz mi najua bongo uonevu 2 watto wa wakubwa wakiappeal wanbadilishiwa na kupangiwa shule nzuri
Nimekuwa nikifuatilia kwa makini rufaa mbali mbali za wanafunzi wa kidato cha 4 na 6 pale NECTA. Lakini kwa miaka kadhaa naona matokeo yao ya rufaa kuwa vile vile (matokeo hayabadiliki). Ni kweli wako makini hivyo?
Kwani wanaosahihisha hizo rufaa ni wale wale wa;iosahihisha mwanzo?Una uhakika na usemacho????kwa taarifa yako mtu akiappeal na maks 5 zikaongezeka wale wote walio sahihisha hilo somo huandika barua ya maelezo kwanini walimkosesha. sasa nani hupenda kufanya hivyo??? na kwa nini wakukoseshe kwa makusudi???? Ukipata majibu ya maswali hayo ndo uje tena, nikupe taarifa zingine.
How possible on earth for a good number of students (some did essay qns) get the same marks after been re-marked?What is the basis of your doubts?
Kwani wanaosahihisha hizo rufaa ni wale wale wa;iosahihisha mwanzo?
Unategemea mwalimu alietoka kigoma aje asahihishe kwa hiyo buk20??? huchukua waalimu wale walio sahihisha na walio karibu.
Nimekuwa nikifuatilia kwa makini rufaa mbali mbali za wanafunzi wa kidato cha 4 na 6 pale NECTA. Lakini kwa miaka kadhaa naona matokeo yao ya rufaa kuwa vile vile (matokeo hayabadiliki). Ni kweli wako makini hivyo?
Wanajichanganya sana hao NECTA.. Majibu ya essay huwezi kusahihisha mara mbili na majibu yakawa ni yaleyale...!Maana yake wanawalia watu hera tu!
Tatizo unao uelewa mdogo kuhusu rufaa. Rufaa haina maana unapokata rufaa inatakiwa ibadilike. Aidha, unapokata rufaa unaonesha kutoridhika na usahihishaji wa awali. hivyo, basi NECTA utafuta wasahihishaji wapya waje wachunguze kwa makini usahihishaji wa awali. Anayekata rufaa ina maana anao uhakika wa alichokiandika bila error ya aina yoyote. umejibu maswali kwa ufasaha na kutetea hoja zote kwa lugha fasaha na inayoeleweka.
Kumbuka ni uchunguzi wa kina, kwa hiyo katika rufaa yoyote lazima wahusika watoe maamuzi yatakayoonesha umeonewa au haukuonewa. ikiwa umeonewa haki itafanyika.
hatakama wakikosea hawawezi kujikosoa...
Wangeacha kula hela ya watu ya ngama,maisha yanabana.
no, big no mate...hapa ni uelewa mdogo unaomsumbua mtoa hoja na baadhi ya wachangiaji. Ukweli ni kuwa mtahiniwa akikata rufaa, hutafutwa wasahihishaji wengine wasahihishe karatasi yake/zake na kutoa maamuzi ya kuonewa kwake au la. Kinachotokea ni kuwa vijana wengi huwa hawakufanya vizuri lakini kwa vile waliwaaminisha wazazi kuwa wao ndo wenyewe, ikitokea wameshindwa mitihani yao hulalama nyumbani kuwa wameonewa na kwamba lazima wakate rufaa!!! Na inapotokea rufaa imeshindwa, huwaaminisha wazazi na jamaa zao kuwa wameonewa. Lakini ukweli sivyo, huwa wamechemsha ile mbaya!!!