Hizi ni siasa mpya au ndio utabiri wa mwl nyerere unatimia?

maphie

Senior Member
Jul 28, 2011
174
47
Uchaguzi wa Arumeru umeisha; kuisha kwa uchaguzi kumeibua mambo mengi. Mosi ni uwezo wa ccm kupambana na nyama vya upinzani na hasa Chadema katika majukwaa; ccm walionekana kushindwa kabisa kisera na katika kuonyesha hilo walianzisha siasa za matusi tena hadharan kabisa! Je hii ni kuonyesha ccm imeshindwa kuendana na kizazi hiki hasa vijana?
Pili ni mwaamko mkumbwa wa wananchi kukiunga mkono chama cha CHADEMA na kuipa mgango ccm a.k.a magamba. Katika mikutanao yote ya CDM wananchi walionekana kukaa kimya na kusikiliza kwa masikini sera za chama hiki na pale ulifika mkutano wa ccm yalikuwa makelele tu! Moja ya nasaha za mwl Nyerere kwa ccm ni kwamba ikifika mahali wananchi wakakosa sera sahihi ndani ya CCM, watazifuta sera zinazowafaha nje ya CCM! Je, huundio wakati wa utabiri wa mwalimu kutimia? Na je, ccm ya leo hilo inaliona
?
 
Back
Top Bottom