Observer2010
Senior Member
- Oct 29, 2010
- 195
- 44
Tukiwa tunaelekea ule wakati ambao binafsi nauita ni peak ya michuano ya UCL, napenda kuwakumbusheni nusu fainali kali zaidi ambazo nimewahi kuziona live katika miaka ya karibuni. Hii ni kwa mujibu wangu binafsi nikiwa kama International Observer.
Manchester United vs Juventus Turin 1998/1999
Wakati Juventus Turin ikionekana ndio club bora zaidi kwa wakati huo ikiwa na viungo walio magwiji kabisa katika historia ya soka Zinedine Zidane na Edgar Davids, walikuwa wanapewa nafasi kubwa kusonga fainali na kuwa mabingwa. Game ya kwanza ilianzia Old Trafford, goli la Antonio Conte likatenganisha timu mbili, huku muda ukielekea ukingoni kabisa, Ryan Giggs akasawazisha dakika za majeruhi na kufanya matokeo kuwa 1-1.
Mechi ya marudiano Italia ilikuwa ni kama ishamalizika, huku timu za Uingereza zikiwa hazijawahi shinda katika ardhi ya Italia kwa miaka zaidi ya arobaini, magoli ya haraka ya Filipo Inzaghi yakawa ni kama yamemaliza mchezo. Roy Keane akafufua matumaini kwa header baada ya kona ya David Beckham, Dwight Yorke anaequalize kwa diving header kabla ya Andy Cole kupiga msumali wa mwisho na kufanya matokeo kuwa 2-3. Wonderful semi final. Man U wanasonga fainali kwa agg ya 4-3.
FC Bayern Munich vs Real Madrid 2000/2001
Real Madrid wakiwa ndio mabingwa watetezi, ilikuwa ni club inayotisha zaidi katika miaka hii. Ikiwa chini ya Vicente Del Bosque, ilikuwa ni club yenye kutandaza soka la hatari. Louis Figo akiwa ndio katoka kusajiriwa tokea Barca kwa rekodi ya dunia, Raul Gonzalez akiwa ndiye anaongoza mashambulizi hakika ilikuwa ni club bora sana. Game ya kwanza ndani ya Santiago Bernabeu, Giovanne Elber anawashangaza maelfu ya mashabiki wa Madrid kwa goli pekee la dakika ya 55. Dunia nzima ikiamini bado Madrid wana nafasi ya kusonga mbele wakikumbuka msimu wa 1999/2000 jinsi Madrid walivyoigaragaza Man U ndani ya Old Trafford. Game ya pili ndani ya Olimpiki Stadium Munich, Elber dakika ya 8 anafungua hesabu, dakika ya 18 Louis Figo anasawazisha na kurudisha matumaini kwa Mabingwa watetezi, dakika ya 34, Jens Jeremies akiwa yard 25, anaunganisha faulo ya Memet Scholl kwa a wonderful strike na kufanya matokeo kuwa hadi mwisho Bayern 2 Madrid 1. Hii hakika ilikuwa ni brilliant semi final.
FC Barcelona vs Chelsea FC 2008/2009
Huku dunia nzima ya wapenda soka ikijaribu kuaminishwa na maneno ya Morinho kuwa Barca inabebwa, CFC wanaenda Camp Nou wakiwa na matumaini ya kufuta makosa ya msimu uliopita ili waingie tena fainali na Man U. Game ya kwanza Camp Nou, Drogba anakosa nafasi za wazi kadhaa, Barca wakionekana wamebanwa na Chelsea, hadi dakika ya 90 matokeo yanakuwa 0-0.
Game ya pili ndani ya Stamford Bridge, Chelsea wanaanza na kasi, goli kali sana toka kwa Michael Essien, left footed long range strike inafanya matokeo yawe 1-0. Dakika 90 zikiwa zimeisha, na za nyongeza zikiwa zinaelekea kuisha, Dani Alves anakimbia kwa kasi wingi ya kulia, anapiga cross golini kwa Chelsea, Captain John Terry anapiga kichwa, mpira unadondoka miguuni mwa Samuel Etoo kwenye line ya upande wa kushoto ya 18 yard box, Etoo anacontrol mpira ila unakuwa km unamshinda unamkuta Michael Essien, anajaribu kuondoa hatari, anauparaza mpira unaenda mguuni mwa Messi, Messi anadrible kidogo na kumpelekea Andres Iniesta, sekunde zinakuwa zimeisha, huku refa akisubiri kumaliza mpira. A wonderful strike toka kwa Andres Iniesta, akiwa just nje ya 18, unafanya matokeo kuwa 1-1, CFC wanaondolewa kwa away goal. Hii ilikuwa ni a fantastic semi final.
Hapa sijazipanga kwa namba wala kwa ubora ila nimezipanga kwa miaka, ila wadau mnakaribishwa kwa maoni. Huu ni mtazamo wangu tukiwa tunaelekea kwenye nusu fainali ya UCL. Natumaini baada ya hapa nitatoa pia tathmini ya fainali 3 kali zaidi ktk UCL nilizowahi kuziona.
Cheerz !!!
Manchester United vs Juventus Turin 1998/1999
Wakati Juventus Turin ikionekana ndio club bora zaidi kwa wakati huo ikiwa na viungo walio magwiji kabisa katika historia ya soka Zinedine Zidane na Edgar Davids, walikuwa wanapewa nafasi kubwa kusonga fainali na kuwa mabingwa. Game ya kwanza ilianzia Old Trafford, goli la Antonio Conte likatenganisha timu mbili, huku muda ukielekea ukingoni kabisa, Ryan Giggs akasawazisha dakika za majeruhi na kufanya matokeo kuwa 1-1.
Mechi ya marudiano Italia ilikuwa ni kama ishamalizika, huku timu za Uingereza zikiwa hazijawahi shinda katika ardhi ya Italia kwa miaka zaidi ya arobaini, magoli ya haraka ya Filipo Inzaghi yakawa ni kama yamemaliza mchezo. Roy Keane akafufua matumaini kwa header baada ya kona ya David Beckham, Dwight Yorke anaequalize kwa diving header kabla ya Andy Cole kupiga msumali wa mwisho na kufanya matokeo kuwa 2-3. Wonderful semi final. Man U wanasonga fainali kwa agg ya 4-3.
FC Bayern Munich vs Real Madrid 2000/2001
Real Madrid wakiwa ndio mabingwa watetezi, ilikuwa ni club inayotisha zaidi katika miaka hii. Ikiwa chini ya Vicente Del Bosque, ilikuwa ni club yenye kutandaza soka la hatari. Louis Figo akiwa ndio katoka kusajiriwa tokea Barca kwa rekodi ya dunia, Raul Gonzalez akiwa ndiye anaongoza mashambulizi hakika ilikuwa ni club bora sana. Game ya kwanza ndani ya Santiago Bernabeu, Giovanne Elber anawashangaza maelfu ya mashabiki wa Madrid kwa goli pekee la dakika ya 55. Dunia nzima ikiamini bado Madrid wana nafasi ya kusonga mbele wakikumbuka msimu wa 1999/2000 jinsi Madrid walivyoigaragaza Man U ndani ya Old Trafford. Game ya pili ndani ya Olimpiki Stadium Munich, Elber dakika ya 8 anafungua hesabu, dakika ya 18 Louis Figo anasawazisha na kurudisha matumaini kwa Mabingwa watetezi, dakika ya 34, Jens Jeremies akiwa yard 25, anaunganisha faulo ya Memet Scholl kwa a wonderful strike na kufanya matokeo kuwa hadi mwisho Bayern 2 Madrid 1. Hii hakika ilikuwa ni brilliant semi final.
FC Barcelona vs Chelsea FC 2008/2009
Huku dunia nzima ya wapenda soka ikijaribu kuaminishwa na maneno ya Morinho kuwa Barca inabebwa, CFC wanaenda Camp Nou wakiwa na matumaini ya kufuta makosa ya msimu uliopita ili waingie tena fainali na Man U. Game ya kwanza Camp Nou, Drogba anakosa nafasi za wazi kadhaa, Barca wakionekana wamebanwa na Chelsea, hadi dakika ya 90 matokeo yanakuwa 0-0.
Game ya pili ndani ya Stamford Bridge, Chelsea wanaanza na kasi, goli kali sana toka kwa Michael Essien, left footed long range strike inafanya matokeo yawe 1-0. Dakika 90 zikiwa zimeisha, na za nyongeza zikiwa zinaelekea kuisha, Dani Alves anakimbia kwa kasi wingi ya kulia, anapiga cross golini kwa Chelsea, Captain John Terry anapiga kichwa, mpira unadondoka miguuni mwa Samuel Etoo kwenye line ya upande wa kushoto ya 18 yard box, Etoo anacontrol mpira ila unakuwa km unamshinda unamkuta Michael Essien, anajaribu kuondoa hatari, anauparaza mpira unaenda mguuni mwa Messi, Messi anadrible kidogo na kumpelekea Andres Iniesta, sekunde zinakuwa zimeisha, huku refa akisubiri kumaliza mpira. A wonderful strike toka kwa Andres Iniesta, akiwa just nje ya 18, unafanya matokeo kuwa 1-1, CFC wanaondolewa kwa away goal. Hii ilikuwa ni a fantastic semi final.
Hapa sijazipanga kwa namba wala kwa ubora ila nimezipanga kwa miaka, ila wadau mnakaribishwa kwa maoni. Huu ni mtazamo wangu tukiwa tunaelekea kwenye nusu fainali ya UCL. Natumaini baada ya hapa nitatoa pia tathmini ya fainali 3 kali zaidi ktk UCL nilizowahi kuziona.
Cheerz !!!