Hizi ndiyo shule zetu

Nyani Ngabu

Platinum Member
May 15, 2006
92,216
113,510
Hata mitaala ikibadilishwa namna gani, kama miundo mbinu itaendelea kuwa yenye hali kama hiyo inayoonyeshwa kwenye hicho kipande cha taarifa ya habari hapo chini, mabadiliko hayo yatakuwa ni kazi bure.

Haya mazingira ni mabaya kupindukia. Si kwa wanafunzi tu bali hata walimu. Ni mtoto gani atakuwa na shauku ya kurudi shuleni kila asubuhi kujifunza mambo mapya? Ni mwalimu gani anapenda kufanya kazi kwenye mazingira kama hayo ambapo hata vyoo hakuna? Walimu na wanafunzi wanajisaidia vichakani. Daaaah!!!!!

Kwa mfano tu, ili kuandika wanafunzi inawabidi wapige magoti na wapindishe migongo. Hayo ni mateso.Hakuna kitakachoingia akilini na kubaki.

Halafu tunashangaa kwa nini wanafunzi wanafeli sana mitihani ya taifa wakati asilimia kubwa ya majibu tunayo. Hivi sisi ni nini tunachokiweza?

 
Last edited by a moderator:
Hata mitaala ikibadilishwa namna gani, kama miundo mbinu itaendelea kuwa yenye hali kama hiyo inayoonyeshwa kwenye hicho kipande cha taarifa ya habari hapo chini, mabadiliko hayo yatakuwa ni kazi bure.

Haya mazingira ni mabaya kupindukia. Si kwa wanafunzi tu bali hata walimu. Ni mtoto gani atakuwa na shauku ya kurudi shuleni kila asubuhi kujifunza mambo mapya? Ni mwalimu gani anapenda kufanya kazi kwenye mazingira kama hayo ambapo hata vyoo hakuna? Walimu na wanafunzi wanajisaidia vichakani. Daaaah!!!!!

Kwa mfano tu, ili kuandika wanafunzi inawabidi wapige magoti na wapindishe migongo. Hayo ni mateso.Hakuna kitakachoingia akilini na kubaki.

Halafu tunashangaa kwa nini wanafunzi wanafeli sana mitihani ya taifa wakati asilimia kubwa ya majibu tunayo. Hivi sisi ni nini tunachokiweza?



Umesema kweli, hata tufanye kitu gani as long as tunaongozwa na watu wasiokuwa na nia ya dhati hatutakuwa na maendeleo. Inatia uchungu sana ukijaribu kujiweka katika adha wanazopata watoto hawa hapo ni shuleni tu bado hujafikiri mazingira ya nyumbani wanayoishi.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom