Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 92,216
- 113,510
Hata mitaala ikibadilishwa namna gani, kama miundo mbinu itaendelea kuwa yenye hali kama hiyo inayoonyeshwa kwenye hicho kipande cha taarifa ya habari hapo chini, mabadiliko hayo yatakuwa ni kazi bure.
Haya mazingira ni mabaya kupindukia. Si kwa wanafunzi tu bali hata walimu. Ni mtoto gani atakuwa na shauku ya kurudi shuleni kila asubuhi kujifunza mambo mapya? Ni mwalimu gani anapenda kufanya kazi kwenye mazingira kama hayo ambapo hata vyoo hakuna? Walimu na wanafunzi wanajisaidia vichakani. Daaaah!!!!!
Kwa mfano tu, ili kuandika wanafunzi inawabidi wapige magoti na wapindishe migongo. Hayo ni mateso.Hakuna kitakachoingia akilini na kubaki.
Halafu tunashangaa kwa nini wanafunzi wanafeli sana mitihani ya taifa wakati asilimia kubwa ya majibu tunayo. Hivi sisi ni nini tunachokiweza?
Haya mazingira ni mabaya kupindukia. Si kwa wanafunzi tu bali hata walimu. Ni mtoto gani atakuwa na shauku ya kurudi shuleni kila asubuhi kujifunza mambo mapya? Ni mwalimu gani anapenda kufanya kazi kwenye mazingira kama hayo ambapo hata vyoo hakuna? Walimu na wanafunzi wanajisaidia vichakani. Daaaah!!!!!
Kwa mfano tu, ili kuandika wanafunzi inawabidi wapige magoti na wapindishe migongo. Hayo ni mateso.Hakuna kitakachoingia akilini na kubaki.
Halafu tunashangaa kwa nini wanafunzi wanafeli sana mitihani ya taifa wakati asilimia kubwa ya majibu tunayo. Hivi sisi ni nini tunachokiweza?
Last edited by a moderator: