Hamna cha wito wala nini hapo wanataka tu kuendeleza nidhamu ya uoga kwa watu na kuwapotezea malengo ya kudai haki zao za msingi kwa kusngizia wito. Kama serikali inajua habari za Wito kwa nini wasiuheshimu huo wito wao?
hakuna kazi ya wito kwani kama aingekuwa ni wito wasingekimbila/kuingiza suala la kodi kwa kile kidogo kinachopatikana kwa huo witowa mazingira magumu ya kazi..
Wito lazima uitwe, wameitwa na nani?
Hamna cha wito wala nini hapo wanataka tu kuendeleza nidhamu ya uoga kwa watu na kuwapotezea malengo ya kudai haki zao za msingi kwa kusngizia wito. Kama serikali inajua habari za Wito kwa nini wasiuheshimu huo wito wao?
Umenena mkuu... Kwanini wasiuheshimu basi huo wito? Yaani kwa kuwa imepewa jina (sijui lini na wapi),kuwa ni kazi ya wito,ndiyo huo wito umwelemee mfanyakazi?
Yaani kuwafanya wajute kwa kozi walizochukua?
Lazima tukubali kuwa si kila mtu anaweza kuwa Daktari jamani.. Ila si shida kwa Daktari kama akiamua,akahamia Msc ya Uhasibu,na fani nyingine yeyote..
Kuna watu wanaongea kwa kuwa hawaijui kazi yenyewe..
Kukutana madonda makubwa ya kutisha na mengine yana harufu mbaya..
Kufanya oparesheni ambazo wakati mwingine unalazimika kusimama muda mrefu hata saa 8 mfululizo!
Na mambo mengine mengi ya ajabuajabu...
Halafu mtu wa aina hiyo alaumiwe kwa kutokuwa na wito..
Na wangepewa kila kitu bule kama masister na mapadri
"Not everybody can be a Doctor" source: Dr. Riwa
Huwezi ukasomea kazi alafu ikawa wito. Ukishasomea hiyo ni taaluma. Mimi nadhani wito ni kuitwa kufanya kazi ambayo hukuwai kufikiria kufanya.