Ibrah
JF-Expert Member
- Mar 22, 2007
- 2,729
- 528
Wadau, hivi karibuni kumezuka kampeni za kuisifia Serikali ya awamu ya 4. Mwezi Desemba TRA walitoa makala kwenye gazeti wakisema "Mafanikio ya awamu ya 4 katika ukusanyaji wa kodi. Wakatoa na takwimu lukuki kuwa kwa mara ya kwanza Serikali ya awamu ya 4 kupitia TRA imefanikiwa kukusanya kodi kubwa zaidi kuliko ilivyowahi kutokea!
Mimi nakubaliana nao lakini mbona hatuoni matokeo ya ongezeko hilo kwa uchumi na maisha ya Watz? Au ni kama vile fedha hizo zaingia katika mifuko iliyotoboka? Pili, TRA watueleze ikiwa ongezeko hilo linatokana na kuongezeka kwa tax base au ndo hizo kodi tunazokamuliwa sisi walala hoi huku Wafanyabiashar wakubwaa na makampuni yakikwepa? Kwangu mimi haiingii akilini kwa Kampuni mfano ya Coca cola, Pepsi Cola na Bia (TBL) kutopandisha bei za vinywaji ikiwa wameongezewa kodi.Labda wachumi mniabie inawezekanaje Makampuni hayo kuongezewa kodi halafu bei za vinywaji zisiongezeke maana ongezeko la kodi linapandisha gharama za uzalishaji ambazo lazima zifidiwe kwa mtumiaji wa mwisho kuongezewa bei, vinginevyo kodi wanazoilipa TRA si sahihi, wanatuibia!
Pili, nnachokiona mimi ni TRA na Serikali kuendelea kutuumiza sisi Wafanyakazi kupitia PAYE maana kodi ya PAYE zimeongezeka na kwangu mimi kodi ninayokatwa inafikia karibu 25% ya mshahara! Sasa TRA watuambie ni mafanikio gani hayo ya kuzidi kutuumiza walipa kodi? Nadhani mafganikio halisi ni kama wangefanikiwa kuongeza idadi ya walipa kodi na si kuangalia kuwango cha ukusanyaji kwa kuwakamua walipa kodi ambao ni haohao waliotwisha mzigo wa mafanikio ya TRA. Wizi mtupu!
Wiki ilopita TANROADS nao wakatuchapia kwneye magazeti juu ya mafanikio ya Serikali ya awamu ya 4. Wakatoa na takwimu juu ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya barabara iliyokamilika,iliyosainiwa na ambayo uilitakiwa iwe imekamilika mwaka jana na ile ambayo itaanza mwaka huu; ajabu ni kuwa iliyokuwa ikamilike mwaka jana ilikuwa bado!.
Jana Waziri mmoja alikaririwa akisema Serikali ya awamu ya 4 imefanikkiwa kutoa ajira milioni moja! Yaani ni vioja; mbona hatuoni hayo ilia tunaaminishwa tu kwa kuambiwa na kulishwa takwimu ambazo hatajathibitisha?
Sipingi wala sikatai kuwa kuna mafanikio lakini kinachonishangaza ni hizi kampeni za magazetini kutuambia juu ya mafanikio ya Serikali ya awamu ya 4 ila kinachonishangaza ni jitihda za kampeni zinazofanywa na viongozi wetu kujaribu kuifagilia Serikali.
Msimamo wangu ni kuwa hawna sababu ya kutumia nguvu nyingi kutulisha takwimu na kutushawishi kwa habari na takwimu kwani MWENYE MACHO HAAMBIWI TAZAMA! Pia: CHEMA CHAJIUZA KIBAYA CHAJITEMBEZA! Watanzania tuna macho ya kuona na tunajua kilicho chema, hawana haja ya kupiga panda.
Mimi nakubaliana nao lakini mbona hatuoni matokeo ya ongezeko hilo kwa uchumi na maisha ya Watz? Au ni kama vile fedha hizo zaingia katika mifuko iliyotoboka? Pili, TRA watueleze ikiwa ongezeko hilo linatokana na kuongezeka kwa tax base au ndo hizo kodi tunazokamuliwa sisi walala hoi huku Wafanyabiashar wakubwaa na makampuni yakikwepa? Kwangu mimi haiingii akilini kwa Kampuni mfano ya Coca cola, Pepsi Cola na Bia (TBL) kutopandisha bei za vinywaji ikiwa wameongezewa kodi.Labda wachumi mniabie inawezekanaje Makampuni hayo kuongezewa kodi halafu bei za vinywaji zisiongezeke maana ongezeko la kodi linapandisha gharama za uzalishaji ambazo lazima zifidiwe kwa mtumiaji wa mwisho kuongezewa bei, vinginevyo kodi wanazoilipa TRA si sahihi, wanatuibia!
Pili, nnachokiona mimi ni TRA na Serikali kuendelea kutuumiza sisi Wafanyakazi kupitia PAYE maana kodi ya PAYE zimeongezeka na kwangu mimi kodi ninayokatwa inafikia karibu 25% ya mshahara! Sasa TRA watuambie ni mafanikio gani hayo ya kuzidi kutuumiza walipa kodi? Nadhani mafganikio halisi ni kama wangefanikiwa kuongeza idadi ya walipa kodi na si kuangalia kuwango cha ukusanyaji kwa kuwakamua walipa kodi ambao ni haohao waliotwisha mzigo wa mafanikio ya TRA. Wizi mtupu!
Wiki ilopita TANROADS nao wakatuchapia kwneye magazeti juu ya mafanikio ya Serikali ya awamu ya 4. Wakatoa na takwimu juu ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya barabara iliyokamilika,iliyosainiwa na ambayo uilitakiwa iwe imekamilika mwaka jana na ile ambayo itaanza mwaka huu; ajabu ni kuwa iliyokuwa ikamilike mwaka jana ilikuwa bado!.
Jana Waziri mmoja alikaririwa akisema Serikali ya awamu ya 4 imefanikkiwa kutoa ajira milioni moja! Yaani ni vioja; mbona hatuoni hayo ilia tunaaminishwa tu kwa kuambiwa na kulishwa takwimu ambazo hatajathibitisha?
Sipingi wala sikatai kuwa kuna mafanikio lakini kinachonishangaza ni hizi kampeni za magazetini kutuambia juu ya mafanikio ya Serikali ya awamu ya 4 ila kinachonishangaza ni jitihda za kampeni zinazofanywa na viongozi wetu kujaribu kuifagilia Serikali.
Msimamo wangu ni kuwa hawna sababu ya kutumia nguvu nyingi kutulisha takwimu na kutushawishi kwa habari na takwimu kwani MWENYE MACHO HAAMBIWI TAZAMA! Pia: CHEMA CHAJIUZA KIBAYA CHAJITEMBEZA! Watanzania tuna macho ya kuona na tunajua kilicho chema, hawana haja ya kupiga panda.