Hivii kuoa/kuolewa...

Dr Lizzy

Platinum Member
May 25, 2009
30,801
59,273
.... ndo mwisho wa kua na marafiki wa jinsia tofauti???

Nauliza kwasababu naona watu hua wanalaani sana msichana mwenye “rafiki“ mwanaume aliyeoa au msichana aliyeolewa akiwa na “rafiki“ mwanaume.
Upande wa wanaume sijasikia malalamiko sana na nnadhani hii inatokana na zile fikra kuhusiana na “wanawake kua wepesi sana kushawishika pia kishawishi na bila kusahau wanawake kuwa wadhaifu.“

Naomba kusema kwamba binafsi sioni tatizo iwapo heshima stahili ipo kwa pande zote na kila mmoja anajua mipaka ya urafiki wao.Mimi nimewahi kua na rafiki aliyeoa na hatukua na matatizo yoyote.Japo sikupata bahati ya kukutana na mke wake ila tulitambulishwa na kujuliana hali mara kadhaa.
Nwy nachojaribu kuonyesha ni kwamba kama kuna urafiki wa kweli bila kua zaidi ya urafiki sioni tatizo la watu wa jinsia tofauti wenye wenza wao kua na marafiki wa jinsia tofauti!!
 
.... ndo mwisho wa kua na marafiki wa jinsia tofauti???

Nauliza kwasababu naona watu hua wanalaani sana msichana mwenye "rafiki" mwanaume aliyeoa au msichana aliyeolewa akiwa na "rafiki" mwanaume.
Upande wa wanaume sijasikia malalamiko sana na nnadhani hii inatokana na zile fikra kuhusiana na "wanawake kua wepesi sana kushawishika pia kishawishi na bila kusahau wanawake kuwa wadhaifu."

Naomba kusema kwamba binafsi sioni tatizo iwapo heshima stahili ipo kwa pande zote na kila mmoja anajua mipaka ya urafiki wao.Mimi nimewahi kua na rafiki aliyeoa na hatukua na matatizo yoyote.Japo sikupata bahati ya kukutana na mke wake ila tulitambulishwa na kujuliana hali mara kadhaa.
Nwy nachojaribu kuonyesha ni kwamba kama kuna urafiki wa kweli bila kua zaidi ya urafiki sioni tatizo la watu wa jinsia tofauti wenye wenza wao kua na marafiki wa jinsia tofauti!!

Lizzy
Niki-refer ulivyosema wewe ni mwanamke lakin una hisia za kiume naweza kuamini kuwa unaweza kusimamia ulichosema (65%)
Fahamu kwamba kila binadamu ni dhaifu, na udhaifu hauna mipaka.
Kutokana na huo udhaifu, binadamu anaweza kubadilika wakati wowote (throu ushawishi and so)
Nadhani umewahi kusikia mtu akisema " Wakati tunaanza kufahamiana ilikuwa kawaida tu, wala sikuwa na hisia zozote kwake. Ulikuwa urafiki wa kawaida tu, hata mke wake alijua.
Lakin nikajikuta naanza kumpenda, yaani hata sielewi imekuwaje. Najua ni mume wa mtu lakin nimeshindwa kujizuia, ananijali, ananiheshimu, ananipenda, ananisaidia . . . . najisikia kumpenda"

Wimbo wa wadada wawili waitwao Dataz unaosema Mume wa mtu umeongea mambo haya.
So urafiki unawezekanika lakin udhaifu hauzuiliki na wala haujali status ya mtu

Conclusion
Kujenga mazoea sana na mwanandoa wa mtu ni vyema lakin inaweza kuzaa usaliti
 
.... ndo mwisho wa kua na marafiki wa jinsia tofauti???

Nauliza kwasababu naona watu hua wanalaani sana msichana mwenye "rafiki" mwanaume aliyeoa au msichana aliyeolewa akiwa na "rafiki" mwanaume.
Upande wa wanaume sijasikia malalamiko sana na nnadhani hii inatokana na zile fikra kuhusiana na "wanawake kua wepesi sana kushawishika pia kishawishi na bila kusahau wanawake kuwa wadhaifu."

Naomba kusema kwamba binafsi sioni tatizo iwapo heshima stahili ipo kwa pande zote na kila mmoja anajua mipaka ya urafiki wao.Mimi nimewahi kua na rafiki aliyeoa na hatukua na matatizo yoyote.Japo sikupata bahati ya kukutana na mke wake ila tulitambulishwa na kujuliana hali mara kadhaa.
Nwy nachojaribu kuonyesha ni kwamba kama kuna urafiki wa kweli bila kua zaidi ya urafiki sioni tatizo la watu wa jinsia tofauti wenye wenza wao kua na marafiki wa jinsia tofauti!!

Swali lako lime-generalize watu wote bila kujali status zao
Ungeuliza "ndio mwisho wa kuwa na marafiki waume au wake za watu???"

Na kwanini ujizoeze kwa mwanandoa wa mtu??
Marafiki wema wameisha?
 
Conclusion
Kujenga mazoea sana na mwanandoa wa mtu ni vyema lakin inaweza kuzaa usaliti

Mimi nina mtazamo tofa na uti! Wazo la kujenga mazoea ama urafiki na mwanandoa wa mtu siafikiani nalo kihivyo hususan ukiwa ule urafiki wa jinsia tofa na uti. Amini usiamini mara nyingi hiyo huwaga chanzo cha migogoro mingi sana katika ndoa.

Hebu piga picha bwana CPU. Eti Ngabu na my waifu wako ni washikaji. Aahahahahahaa….daaah ebana eeh utaweza kweli ku-handle hiyo kitu? Utakuwa na amani kweli? Eniwei sijui, ila watu tumetofautiana sana na huenda labda wewe ikawa si ishu kwako. Lakini mara nyingi sana marafiki wa jinsia tofa na uti huwaga ni moja ya vyanzo vya migogoro kwa wanandoa. Binafsi sishauri hivyo. Ni mtazamo tu.
 
Swali lako lime-generalize watu wote bila kujali status zao
Ungeuliza "ndio mwisho wa kuwa na marafiki waume au wake za watu???"

Na kwanini ujizoeze kwa mwanandoa wa mtu??
Marafiki wema wameisha?

Swali limeanzia kwenye kichwa cha habari...unganisha!!

Khaaaa ina maana mtu aliyeoa/olewa sio/hawezi kua rafiki mwema???Aisee hii ni mpya kwangu!!
 
Ndo mchango wangu ndiyo. Kwa nini unashangaa? Kushangaa hakuruhusiwi hapa. Kama unataka kushangaa kashangae feri huko ambako shilingi inazama na meli inaelea. Ebo!

Haya nimekuelewa gubbe....
 
Mimi nina mtazamo tofa na uti! Wazo la kujenga mazoea ama urafiki na mwanandoa wa mtu siafikiani nalo kihivyo hususan ukiwa ule urafiki wa jinsia tofa na uti. Amini usiamini mara nyingi hiyo huwaga chanzo cha migogoro mingi sana katika ndoa.

Hebu piga picha bwana CPU. Eti Ngabu na my waifu wako ni washikaji. Aahahahahahaa….daaah ebana eeh utaweza kweli ku-handle hiyo kitu? Utakuwa na amani kweli? Eniwei sijui, ila watu tumetofautiana sana na huenda labda wewe ikawa si ishu kwako. Lakini mara nyingi sana marafiki wa jinsia tofa na uti huwaga ni moja ya vyanzo vya migogoro kwa wanandoa. Binafsi sishauri hivyo. Ni mtazamo tu.

Mkuu Ngabu
Kama nikioa
Kwa mimi CPU siwezi kwa kweli, nakiri wazi kabisaaaaa.
Hata waifu anihakikishie vipi kuwa hatatoa bado sitakuwa na amani
Likitokea tatizo dogo tu naweza kuanza kuhisi tatizo ni uhusiano wake na Ngabu (on first attempt)
Ila yeye Lizzy anajifanya ataliweza, labda apate mume ambaye hajampenda (yaani wivu is equal to zero)
Otherwise atakuwa anasababisha migogoro na mume wake bila kujijua, halafu akaona mumewe ana matatizo.
Then aanze kuja kupost ma-thread ya kuomba ushauri
:becky::becky:
 
Mkuu Ngabu
Kama nikioa
Kwa mimi CPU siwezi kwa kweli, nakiri wazi kabisaaaaa.
Hata waifu anihakikishie vipi kuwa hatatoa bado sitakuwa na amani
Likitokea tatizo dogo tu naweza kuanza kuhisi tatizo ni uhusiano wake na Ngabu (on first attempt)
Ila yeye Lizzy anajifanya ataliweza, labda apate mume ambaye hajampenda (yaani wivu is equal to zero)
Otherwise atakuwa anasababisha migogoro na mume wake bila kujijua, halafu akaona mumewe ana matatizo.
Then aanze kuja kupost ma-thread ya kuomba ushauri
:becky::becky:

Wow!! Super big ups my dude. That's what I call too much truth.

Yaani umekuwa mkweli na muwazi bila kumung'unya maneno. Mad respect.
 
  • Thanks
Reactions: CPU
Swali limeanzia kwenye kichwa cha habari...unganisha!!

Khaaaa ina maana mtu aliyeoa/olewa sio/hawezi kua rafiki mwema???Aisee hii ni mpya kwangu!!

Tatizo sio urafiki mwema, tatizo uhusiano na mume wa mtu unajenga picha mbaya kwa jamii na hata kwa mke wa mwanaume.
Wewe ulie nje ya ndoa unaweza ukaona poa tu, lakin wenzako wakikwaruzana kwenye ndoa yao wanaanza kukutajataja kama chanzo
Unaona ni mazuri hayo???
 
Hahahahhahahha
Owkey kille basi.....sifa hizo nakupa ujue!:majani7:

Sifa gani hizo unazonipa? Hilo neno "gubbe" limekaa kama tusi tusi flani hivi. Na sijui umeliokota wapi. Tafuta neno jingine bana…."gubbe" silitaki mimi.
 
Mkuu Ngabu
Kama nikioa
Kwa mimi CPU siwezi kwa kweli, nakiri wazi kabisaaaaa.
Hata waifu anihakikishie vipi kuwa hatatoa bado sitakuwa na amani
Likitokea tatizo dogo tu naweza kuanza kuhisi tatizo ni uhusiano wake na Ngabu (on first attempt)
Ila yeye Lizzy anajifanya ataliweza, labda apate mume ambaye hajampenda (yaani wivu is equal to zero)
Otherwise atakuwa anasababisha migogoro na mume wake bila kujijua, halafu akaona mumewe ana matatizo.
Then aanze kuja kupost ma-thread ya kuomba ushauri
:becky::becky:

Aiseee...sasa huo ndo ule wivu unaozidi mpaka kero.Yani mtu wa aina hiyo hata Sipiyu akinigongea Thanks na Like JF ananiuliza kwanini fulani kakugongea thanks?Embu kuweni na imani bwana....hata asipokua nao bado anaweza asiwe muaminifu vile vile.Kuwa mdanganyifu ni hulka ya mtu na sio swala la yeye kua na marafiki wa jinsia tofauti au la!!
 
Sifa gani hizo unazonipa? Hilo neno "gubbe" limekaa kama tusi tusi flani hivi. Na sijui umeliokota wapi. Tafuta neno jingine bana…."gubbe" silitaki mimi.

We nawe acha kudeka ...sinimeshabadilisha??Sasa hivi ni KILLE!!
 
Aiseee...sasa huo ndo ule wivu unaozidi mpaka kero.Yani mtu wa aina hiyo hata Sipiyu akinigongea Thanks na Like JF ananiuliza kwanini fulani kakugongea thanks?Embu kuweni na imani bwana....hata asipokua nao bado anaweza asiwe muaminifu vile vile.Kuwa mdanganyifu ni hulka ya mtu na sio swala la yeye kua na marafiki wa jinsia tofauti au la!!

Sawa, udanganyifu ni hulka ya mtu. Hilo mimi sikatai. Lakini kubali usikubali urafiki wa jinsia tofauti na mwanandoa ipo siku utaleta mzozo ndani ya ndoa.

Na haya mambo ya imani pofu mimi sikubaliani nayo. Cha muhimu ni wewe uliye kwenye ndoa kutokumpa mwenzako hata chembe ya sababu kukudhania kuwa unafanya mambo ambayo hutakiwi kufanya. Na kama kweli hufanyi jambo lolote baya basi na mwenzako naye wala hatakuwa na sababu ya kukushuku.
 
Back
Top Bottom