ZionTZ
JF-Expert Member
- Oct 6, 2009
- 1,283
- 538
Anajisikia kama kawaida kwa kuwa hiyo ni ajali hakuna mutu anayekusudia kufanya mambo Kama hayo.Hivi waziri kama Mwinyi anajiskiaje anapoona picha kama hii?? je kitendo cha yeye kuendelea kung`ang`ania madaraka tukitafsirije???? kwangu namuona zaidi ya muuaji...
Hakuna mankiti yoyote kwa waziri wa jeshi la wananchi na JKT kujiuzulu,wanaopaswa kufukuzwa kazi ni watendaji wa jeshi la wananchi kuanzia mkuu wao,wakuu wa vikosi wa mahali yalipotokea maafa na wengine wote watakaoonekana inafaa.
Kwa sasa serikali yetu haieleweki ilipo kwani mambo mengi yanayofanyiwa maamuzi hayana manufaa makubwa kwa wananchi,angalia suala la umeme,kupanda kwa petrol,kupanda kwa bei za vyakula na ujenzi,kupanda kwa nauli,ubovu wa miundombinu,uuzaji wa nyumba za serikali kiholela,kuvuruga mfumo wa elimu,michezo kutokuwa na mwelekeo,vijana kukosa mwelekeo kimaisha,nk.(hapa nani anayestahili kubakia serikalini?).
System nzima ni tatizo,huwezi kumwondoa waziri mwinyi wengine wakabaki,hata wao hawana sifa za kuendelea kuwepo walipo.Suala la mbagala ilikuwa fundisho hasa kwa mkuu wa nchi,si ndie tuyempigia kura,hao wengine si wamealikwa tu!