mama kubwa
JF-Expert Member
- Nov 3, 2010
- 5,412
- 8,398
Nimekuwa nikijiuliza sana sisi watanzania na hasa wanamageuzi nini hasa tunachokitaka nikakosa jibu. Tumeshuhudia kwa mara ya kwanza Bunge lililopita likiwa na mvuto wa hali ya juu pale ambapo kinyume na mategemeo ya wengi bunge lileta majibu ya faraja kuhusu mkataba wenye utata wa richmond.japokuwa mwisho wake haukuwa mzuri lakini angalau Watanzania walipunguziwa kiu ya kujua sual hilo.
kilichonifanya nitoe hoja hii ni pale nilipoona juhudi za wabunge wale kutufumbua macho kwenye mkataba wa richmond kuonekana ni unafiki bila kujali jambo hili limesaidia kiasi gani wananchi kuifahamu serekali yao inayowakebehi kuleta maisha bora kumbe inawanyonya kupitia mkataba huu na mingine feki.
Limejitokeza suala la mheshimiwa sitta kuonekana mnafiki anapozungumzia masuala la dowans eti kwa sababu anasemekana anatafuta uraisi 2015 na kufanya kuwaacha vita hiyo apigane peke yake na Mwakyembe aliyeko hospitalini ambapo wengine wanadiriki kusema unafiki wa kuficha uovu umemfikisha hapo.
Inawezekana ni kweli sitta anataka urais na je ni kosa? hivi yuko peke yake ? .Sitta huyu anatujulisha kwamba hizo hela za dowans ndizo zitakazotuchagulia rais 2015 sisi tunamjibu, mnafiki wewe! sitta huyohuyo anasema hizo hela tunalipa kundi dogo la wajanja sisi tunamjibu mnafiki wewe!.hivi wanamageuzi wenzagu kwa maneno hayo sitta anaisaidia ccm? au anatusaidia sisi ? si ndio jambo tulilokua tunalitaka? au tunataka nini?.walichokifanya pale bungeni ni kutupa mwanga (tip) ili sisi tuendelee mbele ilikuwa sio rahisi kwa tume ile kusema yote maana walikuwemo na bado wamo kwenye chama.
Maoni yangu tukiendelea kuwakatisha tamaa hivi hata waliozidiwa na joto la kwenye magamba watashindwa kuja huku maana wanaona vita anayopigana sitta isivyokuwa na wanaoiunga mkono.Tupigane vita hii kama sisi ni wana mageuzi kweli maana hicho naamini ndicho tunachokitaka
kilichonifanya nitoe hoja hii ni pale nilipoona juhudi za wabunge wale kutufumbua macho kwenye mkataba wa richmond kuonekana ni unafiki bila kujali jambo hili limesaidia kiasi gani wananchi kuifahamu serekali yao inayowakebehi kuleta maisha bora kumbe inawanyonya kupitia mkataba huu na mingine feki.
Limejitokeza suala la mheshimiwa sitta kuonekana mnafiki anapozungumzia masuala la dowans eti kwa sababu anasemekana anatafuta uraisi 2015 na kufanya kuwaacha vita hiyo apigane peke yake na Mwakyembe aliyeko hospitalini ambapo wengine wanadiriki kusema unafiki wa kuficha uovu umemfikisha hapo.
Inawezekana ni kweli sitta anataka urais na je ni kosa? hivi yuko peke yake ? .Sitta huyu anatujulisha kwamba hizo hela za dowans ndizo zitakazotuchagulia rais 2015 sisi tunamjibu, mnafiki wewe! sitta huyohuyo anasema hizo hela tunalipa kundi dogo la wajanja sisi tunamjibu mnafiki wewe!.hivi wanamageuzi wenzagu kwa maneno hayo sitta anaisaidia ccm? au anatusaidia sisi ? si ndio jambo tulilokua tunalitaka? au tunataka nini?.walichokifanya pale bungeni ni kutupa mwanga (tip) ili sisi tuendelee mbele ilikuwa sio rahisi kwa tume ile kusema yote maana walikuwemo na bado wamo kwenye chama.
Maoni yangu tukiendelea kuwakatisha tamaa hivi hata waliozidiwa na joto la kwenye magamba watashindwa kuja huku maana wanaona vita anayopigana sitta isivyokuwa na wanaoiunga mkono.Tupigane vita hii kama sisi ni wana mageuzi kweli maana hicho naamini ndicho tunachokitaka