Hivi watanganyika hatuwezi kufanya waliyofanya wazanzibari....???

Sajenti

JF-Expert Member
Apr 24, 2008
3,651
412
Kupigwa kwa kura za maoni zanzibar juu ya kuwa na serikali ya umoja wa kitaifa kwa kiasi kikubwa ni jambo lililoleta faraja kwa wananchi wengi wa visiwa hivyo. Na huenda ikawa ni tiba ya matatizo yaliyokuwa yakitokea huko kwenye mfumo wa uongozi. Mabadiriko ya katiba ni wazi yatafungua njia kuelekea katika utulivu zaidi.

Swali langu, ni je kwa nini na sisi watanganyika tusidai kupigwa kura ya maoni juu ya kuwa na serikali ya umoja wa kitaifa Tanganyika? Kwa mtazamo wangu hii serikali ya CCM kwa kiasi kikubwa imekuwa ikifanya kazi kwa kusinzia na huenda inatokana na viongozi wake wana-CCM kuijisahau na kuona kuwa ni wao tu wenye uwezo wa kufanya kazi ya kiuongozi.

Tumeona ni jinsi gani mawaziri wa kikwete walivyovuruga mambo na bila kuchukuliwa hatua yoyote. Mifano michache ni Uvujaji uliokithiri wa mitihani kuanzia shule za msingi mpaka sekondari na waziri yupo tu anadunda,Matukio ya wananchi kupoteza maisha kwa kukosa maamuzi na utendaji thabiti wa wizara husika mfano wanafunzi waliokufa maji mto rufiji, wanafunzi waliokufa maji ziwa victoria.

Ujambazi wa kutumia silaha uliokithir utadhani nchi haina serikali. Napendekeza tuwe na kura ya maoni ambapo pia serikali itakayoongoza nchi uwe na wawakilishi kutoka vyama pinzani ili kuondoa uzembe wa wazi unaondelea.
 
Tatizo kubwa la Wadaganyika ni waoga sana wanafuata propaganda za chama kiasi kwamba wanaona ni vitu visivyowezekana,Ndugu zangu wadanganyika tuache woga tujiamulie na sisi mustakabali wetu.Sasa Wanzanzibari wanabadlisha kifungu kinachosema kuwa Zanzibar si sehemu ya Jamhuri ya Muungano je sisi wadanganyika tunasubiri nini kuidai Tanganyika.
MUNGU IBARIKI TANGANYIKA NA SIE TUWE NA SERIKALI YETU.
 
itasikitisha mtu kama dr.slaa asiwepo ktk siasa active za nchi kwa muda wa miaka kama mitano!
 
Kuna magonjwa ambayo yanaweza kutibiwa kwa vidonge na mengine ni lazima ifanyike operesheni. Kwa ugonjwa huu wa kwetu ambapo tuna uvimbe wa ndani ya ubongo unaoitwa CCM-UFISADI, ni lazima tukubali operesheni, vinginevyo hatutapona. Serikali ya kitaifa na CCM ni vidonge tu vitakavyotuliza maumivu kwa muda mfupi wakati uvimbe wenyewe ukiwa bado unaendelea kukua, ni kama ilivyotokea Zimbabwe. Kinachotakiwa kwetu ni operesheni kubwa na kuondoa uvimbe huo wa CCM-UFISADI for ever.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom