Jamani toka vuguvugu la uchaguzi lianze mpaka linaisha tumeshuhudia viongozi wetu wa dini wakijiingiza kwenye ushabiki wa siasa mambo ambayo me ninahisi hayawahusu, rejea uchaguzi wa meya arusha na kauli za mufti kuhusu chadema yani wanajipambanua waziwazi dini gani ni cdm na ipi ni ccm. Hivi hawajui waumini wao tupo wafuasi wa vyama tofauti? Mbona wanataka kutugawa? Eti wana jf wenzangu kwa nini vya kaisari wasimpe kaisari na vya Mungu wakamwachia navyo? Hebu nisaidieni kwa hili manake nashndwa kujua nimfate kiongozi wangu wa dini ambaye kwangu ni kioo na namtegemea kunifunza yalo mema au nishike hamsini zangu?